Kaka wa Lissu aelezea masikitiko yao juu ya haki ya mdogo wake, adai watapambana hadi haki ipatikane

Kaka wa Lissu aelezea masikitiko yao juu ya haki ya mdogo wake, adai watapambana hadi haki ipatikane

20 May 2024
Ikungi, Singida

Ukoo pia wanakijiji wameamua baada ya kuligusa gari na yale matundu ya risasi watafanya tambiko la kijadi


View: https://m.youtube.com/watch?v=w8L0W7rtMX8

Msemaji wa familia ya ukoo na pia kaka wa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki Mh Tundu Lissu, advocate Bw Alute Simoni Lissu Mughway mjukuu wa Muro baada ya kumaliza shughuli za kijadi za kiukoo, mbele ya ukoo amesema suala la madai ya Tundu Lissu ...

Advocate Bw Alute Simoni Lissu Mughway mjukuu wa Muro azungumzia ujasiri uliopo katika ukoo wao na kutoa mfano babu yao alivyoua simba jike kwa mkuki akiwa pekee yake machungani .... na kama inavyofahamika simba jike ni mkali na mtata kuliko dume ...

Pia gari la Tundu Lissu limekaguliwa na ndugu kuona matundu zaidi ya 30 ya risasi za waovu wale waliotaka kuondoka na uhai wa Tundu Lissu na ukoo pia wanakijiji wameamua baada ya kuligusa gari na yale matundu ya risasi watafanya tambiko la kijadi ...

Advocate Bw Alute Simoni Lissu Mughway mjukuu wa Muro amesema tambiko ni muhimu na kumsifia Tundu Lissu kuweza kuendeleza msimamo wake pamoja na majeraha pia vitisho anavyopitia makamu mwenyekiti wa CHADEMA bara mheshimiwa Tundu Lissu ...

HAKI HUINUA TAIFA
 
Usichokijua ,kabudi hakufanya hayo kwasababu ya sheria za nchi

Ila kumbukeni tambiko lakwanza la lisu kilichotokea

Sasa ,inatambikwa gari tusubirie tuone

..Sheria gani?

..Unafikiri Adv.Alute Mughwai hajui sheria kiasi kwamba aombe msaada ambao ni batili kisheria toka kwa Waziri na Mwanasheria Mkuu?

..Na kama ombi la familia ya Lissu lilikuwa kinyume na sheria, kwanini Waziri, na Mwanasheria Mkuu, hawakujitokeza na kutoa taarifa kwamba wamelitupilia mbali kwasababu lipo kinyume na sheria?
 
..Sheria gani?

..Unafikiri Adv.Alute Mughwai hajui sheria kiasi kwamba aombe msaada ambao ni batili kisheria toka kwa Waziri na Mwanasheria Mkuu?

..Na kama ombi la familia ya Lissu lilikuwa kinyume na sheria, kwanini Waziri, na Mwanasheria Mkuu, hawakujitokeza na kutoa taarifa kwamba wamelitupilia mbali kwasababu lipo kinyume na sheria?
Kwamba,alichojibu kipindi kabudi mbele ya familia ya lisu ,hakikuwa sheria bali amri


Sasa,ndo lisu anashinda na mahakama ya jamii
 
Back
Top Bottom