Kaliba ya Ualimu lazima iheshimiwe

Kaliba ya Ualimu lazima iheshimiwe

Kwa kusema hivi ndo wengine wanasema UALIMU umegeuka kuwa laana (japo mimi sikubaliani na dhana hii) ila sio mwalimu kama mwalimu. Na kwa mtizamo wako mwanasiasa ameharibu UALIMU wa mwalimu! Maana amefikiri kujenga majengo mapya nchi nzima na kuyaita shule/madarasa, lakini hakuna anayewaza shule mpya ngapi zinahitaji walimu wapya wangapi? Madarasa mapya mangapi yanahitaji walimu wapya wangapi? Lakini inaonekana mwalimu yule yule aliyelemewa na mzigo wa wanafunzi ataongezewa mzigo tena (na kwa kuwa ni ualimu ni WITO) basi hawezi kutusumbua atakubali tu. (Kumbuka mimi ni mwalimu na moja kati ya maudhi nifundishayo kwa wanafunzi wangu ktk somo langu ni kupinga uonevu 'protesting'), hapa wakija hawa kina village sijui wakisema mwalimu mwenye kukubali kufanyiwa haya basi ana laana tunawashindaje ktk hali hii?
Uko sahihi kabisa.. Mwanasiasa mpungukiwa wa taaluma na maarifa mengi yeye ni mtafuta sifa za kisiasa kwa manufaa binafsi. Bado nalia na wote walioamua kuipa siasa thamani kubwa kuliko taaluma
Leo hii mwanasiasa anachojua ni idadi ya vitu kwakuwa hapa ndio kikomo cha maarifa yake
Atakupa idadi ya madarasa yaliyojengwa
Atakupa idadi ya vyumba vya hospital nknk
Lakini kamwe hawezi kukupa idadi ya vyuo vya ualimu vilivyojengwa ama kuboteshwa
Hawezi kukupa idadi ya walimu walioenda kuongeza maarifa
Huwezi kukupa mipango endelevu ya kuboresha maslahi ya mwalimu na mazingira yake

Nina heshima kubwa kwa mwalimu fukara kuliko mwanasiasa maana hawa wamejaa ufedhuli, ujivuni ni wezi wapiga dili, wanyonyaji na wahujumu uchumi wakubwa
 
Habari mwl mshana. Sijui niseme nini ila, wapo wanaowaza wajenge madarasa wapeleke watoto humo ila hawawazi wapeleke ofisi mwl akajipange humo.
Kifupi ni kuwa mwalimu ni wa muhimu sana ila UALIMU umeepuuzwa mno ndo maana kila siku siku hizi hayaishi MAELEKEZO kwa hao walimu. Mwalimu asimamie majengo (sijui ndo haiba yenyewe?), Mwl apangiwe cha kufundisha( rejea ratiba mpya toka TAMISEMI) mwaka jana. Mwalimu aelekezwe namna ya kumtathimini mwanafunzi wake (rejea mtihani wa ku assess kidato cha kwanza mwaka huu), mwalimu anafungiwa mkataba mpya kazini afaulishe kila mwanafunzi ( sijui ndo somo la falsafa au maadili?) nk. Hata baada ya pasaka hii huenda kuna MAELEKEZO mapya tena.
HATA TUSEMEJE, UALIMU SIKU HIZI UPO HUKO TAMISEMI NA HUKU CHINI WALIMU NI KAMA VIRANJA TU.
Walimu wanawekewa makorokoro mengi sana na kila mkubwa akiwatembelea anataka matokeo mazuri kwa Mwl. ambaye anamadai yake kibao na mshahara duni sasa hapo unategemea Mwl. atafanya kazi kwa moyo?
 
Walimu waache kutumika na Serikali

Walimu wajitambue, wajiheshimu
 
Maslahi yangu: Mimi ni mwalimu kwa kusomea.

Nimefarijika na hatua zilizochukuliwa na uongozi wa JamiiForums kwa kuondoa/kufuta mada zote zinazowadhalilisha walimu na kada nzima ya ualimu na kuwapa adhabu stahiki wale wote waliokuwa vinara kwenye hilo.

Kuna mahali tuliyumba na tukakosea sana, tukakosea pakubwa napo ni pale tulipoipa siasa thamani kubwa kuliko taaluma. Kwamba mwanasiasa hohehahe wa elimu ana thamani kubwa na heshima stahiki kuliko mtu mwenye ujuzi wa elimu ya kusomea kama mwalimu, ama kama daktari. Haya yanayotokea sasa ni madhara ya matokeo ya kuwatukuza na kuwakweza wanasiasa.

Mwalimu ndio msingi wa maarifa yote ya ulimwengu na hapa nazungumzia walimu katika hatua ile ya awali/msingi ya kufundishwa kuumba herufi, kusoma, kuandika nk. Huko mbeleni hakuna changamoto kama hii hatua hii ya awali. Hivyo kumheshimu mwalimu sio jambo la hiari bali ni jambo la lazima.

Rais wa kwanza mweusi wa Tanganyika ni hayati Julius Kambarage Nyerere, lakini jina hilo halina ladha kabisa bila kutanguliza neno MWALIMU. Huyu alikuwa ni mwalimu kwa ujuzi na Marais wengine waliofuatia karibia wote walitokea kwenye ualimu. Ualimu ndio msingi wa maarifa yote.

Baada ya vita ya Kagera 1977-1979 nchi iliyumba kwenye nyanja nyingi na kaliba ya ualimu haikuachwa nyuma. Kufikia mwanzoni mwa miaka ya 80, Mwalimu katika kuhangaika huku na kule kutafuta usaidizi wa kielimu kiuchumi nk ndio akapata usaidizi wa UNESCO waliokuwa na program ya UPE (Universal Primary Education) Elimu ya Msingi kwa Wote.

Kufanikisha hili ikabidi kuwe na program ya kuwachukua watu wazima na kuwapiga brush ya elimu ya ualimu ili waweze kufidia nakisi ya walimu wa elimu ya awali kutokana na watoto kuandikishwa kwa wingi sana.

Program ya UPE kwa bahati mbaya ikapewa jina la dhihaka na waswahel waliooita Ualimu Pasipo Elimu.. Hili nalo lilikuwa kosa ambalo madhara yake yalikuja kuonekana baadae. Program ya UPE ilikuja kufutwa na Mzee Ruksa kama sio Mkapa.

Kiasili kaliba ya ualimu ni kaliba iliyokuwa inaheshimika sana. Maana mwalimu alichukuliwa kama kiumbe aliyeelimika kuliko wengine, mwenye maarifa mengi, ujuzi hekima, ufahamu mkubwa na jasiri muongoza njia. Mwalimu ndio aliaminiwa kwa kazi kubwa kubwa za kitaifa kama sensa, takwimu, chaguzi mbalimbali nkn.

Wakati huo kuitwa mwalimu ama kuwa mtoto wa mwalimu ilikuwa ni heshima sana kutokana na umuhimu wake kwenye jamii.

Vipaumbele na maono ya taifa ndio vilikuja kuitia doa kubwa kabila ya ualimu hasa pale walipoamua kuipa thamani kubwa siasa na kuisahau taaluma.. Kuteuliwa kwa wanasiasa kuongoza taasisi nyeti kama ELIMU ilikuwa kupigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la walimu.

Zikaanza sarakasi kipindi cha Mkapa kuelekea Kikwete. Kukaletwa program kama za UPE lakini kipindi hiki wakiwachukua vijana waliofeli kidato cha nne, zile program zikapewa majina ya dhihaka kama voda fasta nk.

Kumpika mtu mpaka aje kuiva kuwa mwalimu si jambo dogo, sasa wale walimu wa miezi sita na mwaka mmoja tena waliofeli kidato cha nne sijui walifundishwa nini kwakuwa hata ukiwauliza haiba ni kitu gani ama misingi na falsafa ninini hawajui.

Kufikia hapa ndio kaliba ya ualimu ikawa imepoteza heshima, mvuto ustaarabu. Vijana barobaro wasioiva kihaiba ndio wakawa walimu, wanasiasa wakaanza kuwatumia kwa manufaa yao. Ualimu ikawa ni kichochoro cha kutumika na wanasiasa.. Wakaleta chama cha walimu na bank ya walimu. Yaliyofuatia yote ni msiba wa kuhuzunisha.

Hawa vijana wa sasa wanaokosoa na kudhihaki hii kaliba ni kizazi kile cha walimu wa mwendokasi na vodafasta. Ualimu ni Wito sio mbadala wa ajira. Hawa walienda kwenye ualimu kama mbadala baada ya kufeli na kukosa kaliba ya ndoto zao.

Hawa hawajapikwa wakaiva maana hata hivyo hawana wito ni makanjanja wa maisha wenye kinyongo kikubwa na kushindwa kwenye mengi. Wana nyongo za kutapika lakini wameshindwa kufanya hivyo kwenye mitandao mingine kwakuwa watatumia utambulisho binafsi na ni rahisi kujulikana.

Hawa walitaka kuitumia JF kama uchochoro wa kutoa hasira zao na kuidhalilisha kada ya ualimu kwa kutumia faida ya utambulisho bandia bila kujali kwamba kwa kufanya hivyo wanaishushia hadhi forum na kuwapa shida wamiliki wanaojulikana kwa majina, sura na hata mawasiliano yao.

Hata mitume wengi kwenye imani zetu walikuwa ni walimu. Ualimu ni kazi ya kiroho na ni kazi ya wito. Iheshimiwe, itambuliwe, ithaminiwe na kupewa hadhi inayostahili. Wanasiasa walione hili na kulifanyia kazi.

Mungu ibariki JamiiForums
Mungu ibariki Tanganyika
Mungu wabariki Walimu
Nakuheshimu sana bro, ila unadhani ni uongo katika yote yaliyoongelewa? Sema mada ziliwasilishwa katika lugha zisizo za staha. Lakini ni ukweli asilimia 100 waalimu wetu wana changamoto nyingi na hata wewe hujataja hata moja, zaidi umezunguuka tu.
 
Nakuheshimu sana bro, ila unadhani ni uongo katika yote yaliyoongelewa? Sema mada ziliwasilishwa katika lugha zisizo za staha. Lakini ni ukweli asilimia 100 waalimu wetu wana changamoto nyingi na hata wewe hujataja hata moja, zaidi umezunguuka tu.
Asante kwa heshima[emoji1545][emoji1752]
 
Acheni Mpwayungu aseme ukweli halisi, hao wanasiasa na viongozi wamefumbia macho madhila ya walimu, hebu Fikiria kila siku wanakuja na mpango ya ujenzi wa madarasa lakini ujenzi wa nyumba za walimu ni mwendo wa jongoo.....hawana haja hata ya kujua hao walimu wanaishi wapi, ukizingatia hawana house allowance.
Uzuri mama kasema anapitiaga humu, Kina Tulia wanapita humu.....hebu waone hali halisi.
Halafu mtu akisema ukweli mnafuta uzi wake. Hao jamiiforums wenyewe nao ni walewale tu. Hivi unadhani utakwenda twitter ukatoe mawazo huru? Fanyieni kazi mawazo ya mtu, angalieni je yasemwayo yapo? Siyo kumuwajibisha mtu.
Mpwayungu nilikuwa sipendi uwasilishaji wake lakini ni kweli alikuwa na hoja, tena za msingi kabisa.
 
Halafu mtu akisema ukweli mnafuta uzi wake. Hao jamiiforums wenyewe nao ni walewale tu. Hivi unadhani utakwenda twitter ukatoe mawazo huru? Fanyieni kazi mawazo ya mtu, angalieni je yasemwayo yapo? Siyo kumuwajibisha mtu.
Mpwayungu nilikuwa sipendi uwasilishaji wake lakini ni kweli alikuwa na hoja, tena za msingi kabisa.
Nasikitika kama kuita Walimu Malofa' nao ni Ukweli.
 
[mention]Mshana Jr [/mention] uzi wako umeuandika vizuri sana.

Ila kitu ambacho sikubaliani na wewe ni kuwa umeongea sweet talk ambayo imekuwa ikiongelewa miaka yote, nadhani ni muda wa hard talk, bila kuvaa buti hao wanasiasa na wachumia tumbo hawawez kuthamini ualimu.

Ni heri tusemwe ili walimu tuamke na hata KUGOMA mbeleni huko ili haki zetu zizingatiwe
 
Mshana utakuwa ni miongoni mwa wale walokomba mamilioni benk ya walimu[emoji1787][emoji1787] (natania)
Kuna muda people must learn in a hard way, haya mambo ya kurembana rembana na kukosoana Kwa staha ndo yametufikisha hapa tulipo, Hadi Leo ripoti ya CAG ni kichefu chefu, watu wanajipigia tu.

Sasa ina maana gani kumsifia mwalimu na kumremba huku maslahi yake ni duni na hamna mpango wa kumboreshea....hayo mambo ya ualimu ni wito yalikuwa enzi ya ujamaa, sasa ni ubepari, capital ndo kila kitu....Mwalimu alipwe vizuri kuendana na hali ya maisha....sifa hazipeleki chakula mezani.

Katika ulimwengu wa kibepari pesa ndiyo kila kitu, lipa walimu vizuri heshima irudi, nidhamu ya wanafunzi irudi, watoto wafaulu taifa lisonge mbele.....Nani atamuheshimu mwalimu anayevaa suruali ya njano, mkanda uliopauka na Shati la kitenge mpauko?
True

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
[mention]Mshana Jr [/mention] uzi wako umeuandika vizuri sana.

Ila kitu ambacho sikubaliani na wewe ni kuwa umeongea sweet talk ambayo imekuwa ikiongelewa miaka yote, nadhani ni muda wa hard talk, bila kuvaa buti hao wanasiasa na wachumia tumbo hawawez kuthamini ualimu.

Ni heri tusemwe ili walimu tuamke na hata KUGOMA mbeleni huko ili haki zetu zizingatiwe
Msifanye hayo gizani na nyuma ya pazia.. Jitokezeni live tuwaunge mkono
 
Acheni Mpwayungu aseme ukweli halisi, hao wanasiasa na viongozi wamefumbia macho madhila ya walimu, hebu Fikiria kila siku wanakuja na mpango ya ujenzi wa madarasa lakini ujenzi wa nyumba za walimu ni mwendo wa jongoo.....hawana haja hata ya kujua hao walimu wanaishi wapi, ukizingatia hawana house allowance.
Uzuri mama kasema anapitiaga humu, Kina Tulia wanapita humu.....hebu waone hali halisi.
Walimu wanahitaji kuboreshewa maslahi yao ili waondokane na fedheha pamoja na frustration mbalimbali zinazopelekea wakose matumaini katika maisha yao.
MUHIMU
serikali iweke teaching allowance teaching allowance

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
[mention]Mshana Jr [/mention] uzi wako umeuandika vizuri sana.

Ila kitu ambacho sikubaliani na wewe ni kuwa umeongea sweet talk ambayo imekuwa ikiongelewa miaka yote, nadhani ni muda wa hard talk, bila kuvaa buti hao wanasiasa na wachumia tumbo hawawez kuthamini ualimu.

Ni heri tusemwe ili walimu tuamke na hata KUGOMA mbeleni huko ili haki zetu zizingatiwe
Mshahara mdogo kazi kama zote, kwa kipindi hiki ukinunua mchele kilo ishirini, korie litre 5 unga, maharage mshahara wote umekwisha...unaanza kuzihesabu siku.... Kiukweli Kuna kitu kipo moyoni mwangu Mungu azidi kunipa utulivu na uvumilivu....nimepanga kutokomea mashambani huko nikachimbe visima yawe maisha yangu kwa uhuru.
 
Mpwayungu hakua na Maana ya kuwatukana au kuwadhalilisha, Mpwayungu alikua anawatia Hasira ili muamke, mjue mnachotaka maishani .

Wee ukiwa Masikin, mtu akikutukana, Masikin mkubwa weee..,..... Hajakuonea na Wala wewe kukataa kua sio Masikin ,hakukufanyi uwe mwenye Kipato !!.



Msijifariji Walimu !!!!

Nadhan mnahaja ya kuungana kudai Masilahi yenu.


Hamna watu wenye Maisha magumu Tanzania hii kama Walimu, Wana Maisha magumu mnoo kwelikweli.


Hii mitandao na ID fake, zisiwaondoe kwenye uhalisia wa Maisha, tunaishi nanyinyi huku mitaani na tunawaona mnavyoishi.


Kujifanya mmeridhika na hali zenu, ni kujilisha upepo.

Mimi Binafsi, Haitokaa kamwe itokee Mwanangu asome Ualimu Kwa hali hii nayoiona na kama itaendelea hivi.
 
Back
Top Bottom