Kaliba ya Ualimu lazima iheshimiwe

Kaliba ya Ualimu lazima iheshimiwe

Hao sio walimu kwa wito
Hao sio walimu waliopikwa wakaiva
Hao sio walimu waliokomaa kiakili na kifikra
Hao sio walimu waliosoma na kufaulu masomo ya haiba, misingi na falsafa
Kuna wale walimu wa Voda fasta, na wale waliopata mafunzo meaka mmoja. Wameteuliwa kuwa maafisa Elimu taaluma na takwimu wapo mikoani huko wanavaa vitenge. Na ni wakina mama na matacle makubwa ukimkuta utaamini tu lipo jambo. Wale waliomaliza Cuba watakuwa wamenielewa
 
Tatizo kubwa Sana la jamii forum ya Sasa ni wanajukwaa kukosa " facts" watu huongea au kuandika vitu wasivyovijua Kwa asilimia 100% .
Mfano mtu anasema serikali inawadharau walimu inawalipa laki 300,000 au 500,000!!
Hajui ni walimu Gani!? Wa level Gani!?
Halafu muulize kada nyingine wanalipwaje!? Mfano kilimo,afya,maendeleo ya jamii nk!! Hana jibu atakwambia hao wanalipwa zaidi!! Basi unamwangalia unamwacha!?
Mkuu hao waliopo kwenye kada zingine kuna mianya ya Rushwa,semina ,overtime allowance kwaio anaweza kulipwa Tsh 300,000/= lakini maisha yake yasifanane kabisa na Mwl.kwaio hapa point ni mwl aboreshewe maslahi kidogo ili asiishi kinyonge.Hili litampa motisha ya kufanya kazi kwa bidii zaidi na hatimae tutajenga taifa imara lenye watu wenye maarifa,maadili na uzalendo

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Ualimu ni kazi achana na bla bla za wito.

Pamoja na kufanga thread za Mpwayungu na wengine wako sahihi kabisa. Bila kelele kudai haki kamwe wasitegemee maboresho ya maana.
Wito ni karama .. Ile ni ajira kwahiyo hakuna niliposema kwakuwa ni wito basi wafanye kazi katika mazingira magumu
 
Kwanza uwalimu sio wito tuache kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa taaluma za watu tulizoshindwa kuziboresha kwa visingizio vya kishenzi kama hivyo.

WITO huwa haujali maslahi ya pesa wala aina ya mazingira ya kazi zaid ya kujali lengo la kazi tu.

Niwaambieni enyi walimu nyie hamna wito wowote bali mnatimiza wajibu wenu kwa serikali na kupata haki zenu za mishahara baada ya kuhitimisha kazi za kila mwezi, pia niwaambien nyie wanasiasa na raia achen kuwapotosha walimu kwa majina mengi ya kuwapamba, wao hawana uspecial wowote wa kuwapa hayo majina mnayotumia kuwadanganya ili muwanyonye, kuna kada nyingi ambazo ni muhimu kwa jamii kama vile Utabibu, ulinzi, na zinginezo za muhimu na mnaishi sababu ya uwepo wa hawo je kwann hamuwaiti na hawa kuwa wana Wito zaid ya kuwapamba walimu?

Kazi ya wito ni ile ambayo malipo yake ni sawa na = 0'' yaan mfanyakazi hatak malipo yoyote zaid ya kutimiza majukumu, hivyo basi tuhitimishe kwa kuwaita walimu wote ni wafanyakazi wa kawaida sana kama walivyo wafanyakazi wengine.

Wito hapa dunian ni kujitoa kwaajili ya manufaa na maendeleo ya wengine bila kujali maslahi ya kiuchumi,

Serikali ingekuwa makini walimu wangeheshimika kulko hata hao wabunge ambao hawana manufaa kwa taifa zaid ya kuharibu hii nchi kwa kukosa misimamo.
 
Kwanza uwalimu sio wito tuache kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa taaluma za watu tulizoshindwa kuziboresha kwa visingizio vya kishenzi kama hivyo.

WITO huwa haujali maslahi ya pesa wala aina ya mazingira ya kazi zaid ya kujali lengo la kazi tu.

Niwaambieni enyi walimu nyie hamna wito wowote bali mnatimiza wajibu wenu kwa serikali na kupata haki zenu za mishahara baada ya kuhitimisha kazi za kila mwezi, pia niwaambien nyie wanasiasa na raia achen kuwapotosha walimu kwa majina mengi ya kuwapamba, wao hawana uspecial wowote wa kuwapa hayo majina mnayotumia kuwadanganya ili muwanyonye, kuna kada nyingi ambazo ni muhimu kwa jamii kama vile Utabibu, ulinzi, na zinginezo za muhimu na mnaishi sababu ya uwepo wa hawo je kwann hamuwaiti na hawa kuwa wana Wito zaid ya kuwapamba walimu?

Kazi ya wito ni ile ambayo malipo yake ni sawa na = 0'' yaan mfanyakazi hatak malipo yoyote zaid ya kutimiza majukumu, hivyo basi tuhitimishe kwa kuwaita walimu wote ni wafanyakazi wa kawaida sana kama walivyo wafanyakazi wengine.

Wito hapa dunian ni kujitoa kwaajili ya manufaa na maendeleo ya wengine bila kujali maslahi ya kiuchumi,

Serikali ingekuwa makini walimu wangeheshimika kulko hata hao wabunge ambao hawana manufaa kwa taifa zaid ya kuharibu hii nchi kwa kukosa misimamo.
Wito ni karama .. Ualimu ni ajira kwahiyo hakuna niliposema kwakuwa ni wito basi wafanye kazi katika mazingira magumu
 
Kwanza uwalimu sio wito tuache kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa taaluma za watu tulizoshindwa kuziboresha kwa visingizio vya kishenzi kama hivyo.

WITO huwa haujali maslahi ya pesa wala aina ya mazingira ya kazi zaid ya kujali lengo la kazi tu.

Niwaambieni enyi walimu nyie hamna wito wowote bali mnatimiza wajibu wenu kwa serikali na kupata haki zenu za mishahara baada ya kuhitimisha kazi za kila mwezi, pia niwaambien nyie wanasiasa na raia achen kuwapotosha walimu kwa majina mengi ya kuwapamba, wao hawana uspecial wowote wa kuwapa hayo majina mnayotumia kuwadanganya ili muwanyonye, kuna kada nyingi ambazo ni muhimu kwa jamii kama vile Utabibu, ulinzi, na zinginezo za muhimu na mnaishi sababu ya uwepo wa hawo je kwann hamuwaiti na hawa kuwa wana Wito zaid ya kuwapamba walimu?

Kazi ya wito ni ile ambayo malipo yake ni sawa na = 0'' yaan mfanyakazi hatak malipo yoyote zaid ya kutimiza majukumu, hivyo basi tuhitimishe kwa kuwaita walimu wote ni wafanyakazi wa kawaida sana kama walivyo wafanyakazi wengine.

Wito hapa dunian ni kujitoa kwaajili ya manufaa na maendeleo ya wengine bila kujali maslahi ya kiuchumi,

Serikali ingekuwa makini walimu wangeheshimika kulko hata hao wabunge ambao hawana manufaa kwa taifa zaid ya kuharibu hii nchi kwa kukosa misimamo.
Umeongea maneno kuntu.

Ualimu siyo wito, "is a professional job" yenye kufuata kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Tukisema ualimu ni wito maana yake Mwalimu hapasi kusurutishwa na kanuni zozote zile (mtazamo wangu). Lakini, Mwalimu huyo huyo Kila kukicha maazimio na miongozo kede kede Kutoka Kwa Wakubwa/wanene inapelekwa kwake Kwa ajili ya kumsurutisha ktk kazi yake ya ualimu.

Changamoto ziko nyingi sana katika kada ya ualimu; hivyo, ni jukumu la Serikali kuwatazama walimu Kwa muktadha chanya na si kuwafanya wanyonge kila kukicha. Na ndiyo sababu ya jamii Pana ya Watanzania kuendelea kuwadharau/kutudharau.

Nampongeza mleta mada (Mshana Jr ) kaja na mada ya kuwapooza Walimu (Kwa maneno matamu) Kwa kuwa yeye kama yeye anatambua thamani ya ualimu na Walimu kiujumla (tumpongeze Kwa hili). Lakini bado ukweli uko pale pale Walimu wanakabiliwa na changamoto lukuki ambazo nyingine nyingi tu zinasababishwa na mabosi wa Walimu.

Nawasilisha. [emoji1812][emoji3578] Mwalimu Blue Bahari
 
Umeongea maneno kuntu.

Ualimu siyo wito, "is a professional job" yenye kufuata kanuni na taratibu za utumishi wa umma.

Tukisema ualimu ni wito maana yake Mwalimu hapasi kusurutishwa na kanuni zozote zile (mtazamo wangu). Lakini, Mwalimu huyo huyo Kila kukicha maazimio na miongozo kede kede Kutoka Kwa Wakubwa/wanene inapelekwa kwake Kwa ajili ya kumsurutisha ktk kazi yake ya ualimu.

Changamoto ziko nyingi sana katika kada ya ualimu; hivyo, ni jukumu la Serikali kuwatazama walimu Kwa muktadha chanya na si kuwafanya wanyonge kila kukicha. Na ndiyo sababu ya jamii Pana ya Watanzania kuendelea kuwadharau/kutudharau.

Nampongeza mleta mada (Mshana Jr ) kaja na mada ya kuwapooza Walimu (Kwa maneno matamu) Kwa kuwa yeye kama yeye anatambua thamani ya ualimu na Walimu kiujumla (tumpongeze Kwa hili). Lakini bado ukweli uko pale pale Walimu wanakabiliwa na changamoto lukuki ambazo nyingine nyingi tu zinasababishwa na mabosi wa Walimu.

Nawasilisha. [emoji1812][emoji3578] Mwalimu Blue Bahari
Asante Mwalimu Blue Bahari kwa uchambuzi mzuri[emoji1545][emoji1752]
 
Asante Mwalimu Blue Bahari kwa uchambuzi mzuri[emoji1545][emoji1752]
Nawe pia ubarikiwe [emoji120][emoji120][emoji120] Kwa kujaribu kutuheshimisha sisi Walimu. Ila Bahati mbaya tafsi ya heshima Kwa Mwalimu ni tofauti na jamii inavyotafsiri.

Kinachoheshimika siku hizi ni Pesa na si mtu au mtaalamu wa fani. Wewe mtaalamu wa fani flani, watu watakuuliza una nini?, Nazungumzia "material things".
Haujakosea kabisa kuleta uchambuzi murua wa thamani ya Mwalimu na ualimu kiujumla, ila tatizo ni nyakati.
 
Maslahi yangu: Mimi ni mwalimu kwa kusomea.

Nimefarijika na hatua zilizochukuliwa na uongozi wa JamiiForums kwa kuondoa/kufuta mada zote zinazowadhalilisha walimu na kada nzima ya ualimu na kuwapa adhabu stahiki wale wote waliokuwa vinara kwenye hilo.

Kuna mahali tuliyumba na tukakosea sana, tukakosea pakubwa napo ni pale tulipoipa siasa thamani kubwa kuliko taaluma. Kwamba mwanasiasa hohehahe wa elimu ana thamani kubwa na heshima stahiki kuliko mtu mwenye ujuzi wa elimu ya kusomea kama mwalimu, ama kama daktari. Haya yanayotokea sasa ni madhara ya matokeo ya kuwatukuza na kuwakweza wanasiasa.

Mwalimu ndio msingi wa maarifa yote ya ulimwengu na hapa nazungumzia walimu katika hatua ile ya awali/msingi ya kufundishwa kuumba herufi, kusoma, kuandika nk. Huko mbeleni hakuna changamoto kama hii hatua hii ya awali. Hivyo kumheshimu mwalimu sio jambo la hiari bali ni jambo la lazima.

Rais wa kwanza mweusi wa Tanganyika ni hayati Julius Kambarage Nyerere, lakini jina hilo halina ladha kabisa bila kutanguliza neno MWALIMU. Huyu alikuwa ni mwalimu kwa ujuzi na Marais wengine waliofuatia karibia wote walitokea kwenye ualimu. Ualimu ndio msingi wa maarifa yote.

Baada ya vita ya Kagera 1977-1979 nchi iliyumba kwenye nyanja nyingi na kaliba ya ualimu haikuachwa nyuma. Kufikia mwanzoni mwa miaka ya 80, Mwalimu katika kuhangaika huku na kule kutafuta usaidizi wa kielimu kiuchumi nk ndio akapata usaidizi wa UNESCO waliokuwa na program ya UPE (Universal Primary Education) Elimu ya Msingi kwa Wote.

Kufanikisha hili ikabidi kuwe na program ya kuwachukua watu wazima na kuwapiga brush ya elimu ya ualimu ili waweze kufidia nakisi ya walimu wa elimu ya awali kutokana na watoto kuandikishwa kwa wingi sana.

Program ya UPE kwa bahati mbaya ikapewa jina la dhihaka na waswahel waliooita Ualimu Pasipo Elimu.. Hili nalo lilikuwa kosa ambalo madhara yake yalikuja kuonekana baadae. Program ya UPE ilikuja kufutwa na Mzee Ruksa kama sio Mkapa.

Kiasili kaliba ya ualimu ni kaliba iliyokuwa inaheshimika sana. Maana mwalimu alichukuliwa kama kiumbe aliyeelimika kuliko wengine, mwenye maarifa mengi, ujuzi hekima, ufahamu mkubwa na jasiri muongoza njia. Mwalimu ndio aliaminiwa kwa kazi kubwa kubwa za kitaifa kama sensa, takwimu, chaguzi mbalimbali nkn.

Wakati huo kuitwa mwalimu ama kuwa mtoto wa mwalimu ilikuwa ni heshima sana kutokana na umuhimu wake kwenye jamii.

Vipaumbele na maono ya taifa ndio vilikuja kuitia doa kubwa kabila ya ualimu hasa pale walipoamua kuipa thamani kubwa siasa na kuisahau taaluma.. Kuteuliwa kwa wanasiasa kuongoza taasisi nyeti kama ELIMU ilikuwa kupigilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la walimu.

Zikaanza sarakasi kipindi cha Mkapa kuelekea Kikwete. Kukaletwa program kama za UPE lakini kipindi hiki wakiwachukua vijana waliofeli kidato cha nne, zile program zikapewa majina ya dhihaka kama voda fasta nk.

Kumpika mtu mpaka aje kuiva kuwa mwalimu si jambo dogo, sasa wale walimu wa miezi sita na mwaka mmoja tena waliofeli kidato cha nne sijui walifundishwa nini kwakuwa hata ukiwauliza haiba ni kitu gani ama misingi na falsafa ninini hawajui.

Kufikia hapa ndio kaliba ya ualimu ikawa imepoteza heshima, mvuto ustaarabu. Vijana barobaro wasioiva kihaiba ndio wakawa walimu, wanasiasa wakaanza kuwatumia kwa manufaa yao. Ualimu ikawa ni kichochoro cha kutumika na wanasiasa.. Wakaleta chama cha walimu na bank ya walimu. Yaliyofuatia yote ni msiba wa kuhuzunisha.

Hawa vijana wa sasa wanaokosoa na kudhihaki hii kaliba ni kizazi kile cha walimu wa mwendokasi na vodafasta. Ualimu ni Wito sio mbadala wa ajira. Hawa walienda kwenye ualimu kama mbadala baada ya kufeli na kukosa kaliba ya ndoto zao.

Hawa hawajapikwa wakaiva maana hata hivyo hawana wito ni makanjanja wa maisha wenye kinyongo kikubwa na kushindwa kwenye mengi. Wana nyongo za kutapika lakini wameshindwa kufanya hivyo kwenye mitandao mingine kwakuwa watatumia utambulisho binafsi na ni rahisi kujulikana.

Hawa walitaka kuitumia JF kama uchochoro wa kutoa hasira zao na kuidhalilisha kada ya ualimu kwa kutumia faida ya utambulisho bandia bila kujali kwamba kwa kufanya hivyo wanaishushia hadhi forum na kuwapa shida wamiliki wanaojulikana kwa majina, sura na hata mawasiliano yao.

Hata mitume wengi kwenye imani zetu walikuwa ni walimu. Ualimu ni kazi ya kiroho na ni kazi ya wito. Iheshimiwe, itambuliwe, ithaminiwe na kupewa hadhi inayostahili. Wanasiasa walione hili na kulifanyia kazi.

Mungu ibariki JamiiForums
Mungu ibariki Tanganyika
Mungu wabariki Walimu
 
Kwani "lofa" ni tusi? Mbona Marehemu Mkapa alituita watanzania wote malofa, ulofa ni sifa ya mtu asiyejielewa, ni kivumishi tu Kama ilivyo mjinga....sa mtu awe lofa umuite mjanja?
Mkapa hajawahi kutuita Watanzania wote Malofa.
 
Ukiruhusu uhuru wa kutoa maoni, kubali kusikia ukweli usioupenda....JF wamekosea..warudishe hizo nyuzi
Hapo ndio utafahamu kuwa democrasia huwa ni ngumu sana. Ukipenda democrasia na uhuru wa maoni ni lazima uwe tayari kusikia ukweli usio upenda au la sivyo ukubali kuitwa dictator.
 
Hapo ndio utafahamu kuwa democrasia huwa ni ngumu sana. Ukipenda democrasia na uhuru wa maoni ni lazima uwe tayari kusikia ukweli usio upenda au la sivyo ukubali kuitwa dictator.
Mimi nashangaa JF kuziacha zile nyuzi zinazomkashfu JPM mtu ambae hawezi kujitetea na kuzifuta za walimu ambao wanaweza kuja kukanusha kama yanayosemwa ni ukweli au uongo
 
Mkuu hao waliopo kwenye kada zingine kuna mianya ya Rushwa,semina ,overtime allowance kwaio anaweza kulipwa Tsh 300,000/= lakini maisha yake yasifanane kabisa na Mwl.kwaio hapa point ni mwl aboreshewe maslahi kidogo ili asiishi kinyonge.Hili litampa motisha ya kufanya kazi kwa bidii zaidi na hatimae tutajenga taifa imara lenye watu wenye maarifa,maadili na uzalendo

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
Waulize vizuri watakwambia ukweli !! Sisi tupo huko Hali haiko kama mnavyodhani!! Niambie mtu yupo maendeleo ya jamii Kuna rushwa Gani na shiling ngapi!??hizo simina ni lini na lini!? Overtime lini na lini!?allowance zipi!? Mara ngapi zipo!?! .
Nasema tena jamii forum uelewa wa watu ni finyu mno!?
 
Back
Top Bottom