Kama Biblia na Quran zingeletwa Mahakamani zithibitishe yaliyomo ndani yake, Quran ingeangukia pua

Hapana Mkuu.
Labda unahitaji kidogo kuijua vizuri DUNIA.
Hiyo tutajadili siku nyingine
Dunia hamna anaye ijua kila mtu hujaribu kutoa kile anacho elewa kuhusu Dunia..Hata wewe kuna vingi hujui kuhusu dunia... Only a fool knows everything.
 
Kaka kwanza Bible haiwezi kuipinga Qur'an Bible sio miongoni mwa vitabu vya M mungu . Wangeleta Injili na Qur'an sawa ila sio Bible
 

Nakupa mfano;
Msikilize Danieli hapa anaandika yeye mwenyewe kitu kinachotokea katika maisha yake Kwa wakati sahihi, akwia. Huko Babeli, na Mtawala anamtaja, na wakati anataja.
Danieli 10:1
Katika mwaka wa tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni vita vikubwa; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo.

Danieli 10:2
Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.

Danieli 10:3
Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia.

Danieli 10:4
Na siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa kando ya ule mto mkubwa, Hidekeli;

Danieli 10:5
naliinua macho yangu, nikatazama, na kumbe, mtu aliyevikwa nguo za kitani, viuno vyake vimefungwa dhahabu safi ya Ufazi;

Danieli 10:6
mwili wake pia ulikuwa kama zabarajadi safi, na uso wake mfano wa umeme, na macho yake kama taa za moto, na mikono yake na miguu yake rangi yake kama shaba iliyosuguliwa sana, na sauti ya maneno yake kama sauti ya umati wa watu.

Danieli 10:7
Nami, Danieli, nikaona maono haya peke yangu; maana wale watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona maono haya; lakini tetemeko kuu liliwashika, hata wakakimbia ili kujificha.

Danieli 10:8
Basi nikaachwa peke yangu, nikaona maono haya makubwa, wala hazikubaki nguvu ndani yangu; maana uzuri wangu uligeuzwa ndani yangu kuwa uharibifu, wala sikusaziwa nguvu.
 
Mathayo, Yohana wote walioandika Injili walikuwa wanafunzi wa Yesu.
Walimshuhudia wakasimulia.
Hiyo mathayo alikuwa msomi WA mahesabu ya ushuru na tozo.
Safi kabisa hapa ndipo napopataka. Nimecheka sana, tuwekee uthibitishe unao onyesha ya kuwa Matayo na Yohana walimshubudia Yesu na hizi Injili zao waliziandika lini ? Sababu Historian inaonyesha ya kuwa Wanafunzi wa Yesu walikuwa wanaishi kwa dhiki na kujificha na ilifikia kipindi wakawa hawawafundishi watu ufunuo kwa kuchelea kuuwawa. Sasa hizi habari walizipata wapi ?

Safi kabisa, Sasa habari za Matayo na Yohana ziliwafikia vipi nyinyi ? Mnayo chain inayofika mpaka kwa Matayo au Yohana ? Kipi kitatujulisha ya kuwa hizi habari wameziandika wao ?

Vipi kuhusu Luka na Marko ?
Unaposema hakuna ushahidi wao ndio waliandika hiyo Injili lakini muda huohuo unamuamini Muhammad ambaye anasimulia Stori ambazo hazimuhusu Kwa namna yoyote Ile.
Sio myahudi lakini anasimulia habari za Wayahudi.
Safi kabisa, tunamuamini sababu yeye alikuwa Mtume, na walio mshuhudia walikubali hilo. Yaani alikuwa haongei kwa matamanio yake. Kama ilivyo kwa Yesu alivyokuwa anashushiwa Injili.

Swali, rahisi sana unafikiri yeye hizo habari alikuwa anazitunga ? Alipokuwa anawasimulia mbona Mayahudi walizikubali na kujua ni za kweli ?
Hajawahi kuishi uyahudini lakini anaandika mambo ya nchi ambayo hajawahi kuiona.
Yaani Wewe ni hao Wakristo Nani mwenye matatizo ya kufikiri?
Mitume ndiyo jambo hilo, na halishangazi sababu walikuwa wanafunuliwa na Mola wao, hili kwa Allah ni jepesi sana.

Wakristo katika suala la dini hamna akili kabisa, hapa siwatukani, kwanza kitendo tu Cha nyinyi kukubali kutarujumiwa vitabu vyenu kwa lugha yenu ya Kiswahili na hamna matini husika wala lugha ya Yesu au hao mitume wengine hamzijui ni kutokuwa na akili kabisa. Hili tuache kwanza.
Kuanzia kitabu cha Mathayo mpaka kitabu ufunuo wa Yesu Kwa Yohana vitabu vyote vimeandikwa na wanafunzi wa Yesu.
Sasa usilete stori nachotaka Mimi unipe ushahidi. Haya madai tu, hata wengine wanaweza kuandika hivi unavyoandika wewe. Marko alikuwa Mwanafunzi wa Yesu ? Luka alikuwa Mwanafunzi wa Yesu ?


Kitabu Cha Ufunuo kimeandikwa na nani katika Wanafunzi wa Yesu ?
Huyo Paulo ambaye Waislam walimpinga Hakuwa mwanafunzi WA Kwanza wa Yesu(yaani wale 12 wa awali) lakini Paulo alifanya kazi na wanafunzi waliomshuhudia Yesu, hao kina Petro.
Wanafunzi walio mshuhudia Yesu unaweza kututhibitishia walimpa habari za Yesu ?
Barua za Paulo zote zimebeba Majina ya wakati huo WA Maeneo ya Uturuki, ugiriki, n.k.

Haya embu jadili hoja zilizopo kwenye Uzi
Hoja zilikuwepo kwenye Uzi zimeshajibiwa na wengine na haziwezi kuwa na nguvu mpaka tujue ukweli wa Biblia yaani sisi tunajadili msingi ili tuone jengo lenu ni imara au la ?
 
Napenda kupita kimya kimya kwenye hii Mijadala. Maana mm sijui chochote kwenye haya mambo..
 
Ndiyo maana nikasema hivi Wakristo Elimu ya uhakiki wa Habari hamna. Mmeshawahi kuthibitisha ya kuwa hizi habari ni za kweli ?

Unajua hiki hata wewe unaweza kukaa ukakisimulia. Mimi sipo kwenye matini, Mimi nipo katika kuhakiki kiini Cha habari zilipo Toka.

Hii ni stori kama stori nyingine, kumbuka hapa tunaongelea habari za ufunuo

Daniel I alikuwa nani na hizi habari nani amewanukulia mpaka zimewafikia nyinyi ?
 
Hakuna mtu yeyote mwenye akili nzuri anayeweza kufurahia nchi kuongozwa kidini.
Binadamu wa karne ya 21 anatakiwa kuishi kwenye mataifa yasiyo ya udikteta wa kidini(secular). Dini inapaswa kuwa ya watu binafsi sio suala la kitaifa au umma.
 

Kitabu cha Yohana, kimeandikwa na Mwanafunzi wa Yesu aitwaye Yohana.
Huyu ndio mwanafunzi WA mwisho wa Yesu kufa, kitabu kingine alichoandika ni kitabu cha Ufunuo,

Msikilize Yohana;
Ufunuo wa Yohana 1:9
Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.

Ufunuo wa Yohana 1:10
Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,

Ufunuo wa Yohana 1:11
ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.

Ufunuo wa Yohana 1:12
Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu;

Ufunuo wa Yohana 1:13
na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini.

Yupo mathayo;

Yupo Petro;
Msikilize Petro
1 Petro 3:18
Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,

1 Petro 2:21
Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

1 Petro 2:22
Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.

1 Petro 2:23
Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.

1 Petro 2:24
Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.

1 Petro 2:25
Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.

Huyo ni Petro mwanafunzi namba moja WA Yesu. Anashuhudia.

Hata jibu hoja za andiko alafu Kama unataka kuanzisha hoja mpya tutafanya hivyo baadaye.

Alafu ingekuwa vizuri hiyo hofu uliyonayo kuhusu Biblia ndio ingetakiwa maradufu kwenye Quran ambayo inasimulia habari za Wayahudi ilhali muandishi ni muarabu ambaye hajui waisrael hata mmoja anayemsimulia, hajawahi kufika Israel, hajakuwepo wakati hayo yanatokea hata Kwa ukaribu wa miaka 100 tuu.

Hizo ndio hoja, naona unataka kuanzisha mjadala mpya
 
Ninaanza kupata mashaka:

Leo hii practically Qur'an inaweza kuendesha nchi na ikatoa maelezo/sheria juu ya fields mbalimbali kuanzia biashara, maisha ya kijamii, military, general laws, miradhi n.k

Naomba nipe mfano wa nchi yoyote duniani iliyowahi kuendeshwa na watu wakahukumiana kwa BIBILIA!!!!

Bibilia ni muunganiko wa masimulizi ya watu na sehemu ya maneno ya mitume ambayo kimsingi hayawi kuendesha maisha ya WATU KAMA MWONGOZO!!!

Qur'an 8mehifadhiwa kwenye uasili wake na legal TRANSITION ili kuhakikisha inabaki katika uasili wake... LAKINI BIBILIA HATA UASILI WAKE UMESHAPOTEA Maana imesjapitia masaibu ya kutosha ikiwemo kuhamishwa kutoka kwenye lugha ya asili ARAMAIC, KIGIRIKI, KIYAHUDI mpaka kufikia hapa hata UASILI HAUPO TENA.

Huwezi kulinganisha vitabu hivi viwili...
 

Kwa hiyo Mimi ninayoitumia Quran kwenye mambo yangu ni Muislam? Kwa Uelewa wako.

Au Waislam wanaotumia Biblia ni Wakristo au Wayahudi?

Tumia akili zaidi kwenye hoja kuliko Imani katika mjadala. Ninawafahamu Babu zangu wawili hawakuwa Wakristo wala Waislam lakini nyumbani kuliko na Biblia na Quran na vyote wanavisoma
 
Reactions: PNC
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

Hiyo inaitwa "Royal We" yaani respect and glorification na sii PLURAL au UWINGI.....

Majestically Allah anaposema "Tume.." au "We" ni respect and glorification of the CREATOR na wala siyo UWINGI....
 
 

Mtume Muhammad anafunuliwa mambo ambayo Padri walaga jirani yake anayo?

Yaani ni Sawa atokee mtu sasa hivi ajifanye anafunuliwa habari za Quran ilhali Waislam mpo na mnajua habari zote za Quran.
Mtu huyo mtamchukuliaje?

Yaani Muhammad anafunuliwa Stori za kina Musa, sijui Ibrahimu, sijui Yusufu ilhali tayari wapo Wakristo kina Padri Walaga wanazo alafu mnaita ufunuo😀😀.

Yaani majaji/wasomaji ambao hawana ushabiki wataelewa na kuamua wenyewe Kwa hoja unazozitoa.

Muhammad anafunuliwa ati Suleiman alikuwa anafuga majini.
Hajui hata Utamaduni wa Suleiman ukoje, hajui Mungu WA Suleiman/Wayahudi aitwaye Yahwe anakataza kutumia maruhani/majini,
Muhammad hajui kuwa Suleiman hajawahi kumjua Allah mungu wa waarabu.

Hivi kweli bado unaona Quran iko makini?
Ni akheri wakati ina-copy wahusika wakiyahudi inge-copy na Mungu WA kiyahudi ingekuwa angalau kuna Ukweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…