Kama Diamond anashindwa kumsitiri baba yake kwenye ukata utajiri wake una faida gani?

Mkuu humu zaidi wapo upande wa Mond kwasababu ya mahaba waliyonayo juu yke hivyo hawaangalii uzito wa hili jambo...! Huwezi kutoa msaada nje wakati kwako kunateketea..kuhusu kuumwa huyo mzee keshaumwa mara nyingi na hatujawahi kuona akipewa uzito si na Mond wala Mwajuma...! Akifa watamuweka kwenye kurasa zao Instagram na kwingineko wakijutia maamuzi yao (,japo kiunafki)...Dunia tunapita yatupasa kutengeneza mema na kuyaishi kuliko visasi.
 
Kuna wakati unaweza msaidia adui yako apate nguvu za kukumaliza kabisa.Binafsi simuamini baba diamond kama ana mapenzi ya dhati na diamond.

Sidhani kama akitokea mtu(adui) wa diamond na kuamua kumtumia mzee abduli kifedha kummaliza diamond atashindwa kufanikiwa.Sidhani

Sent from my HUAWEI CUN-L01 using JamiiForums mobile app
 
Huyu mzee anasaidiwa sana,nilisikikiza intvw ya Queen aliyofanyiwa na Soudy miaka kama minne iliyopita ila tatizo lake anapenda sana kamera,manake siku hiyo mpaka Queen Darleen alimtukana sana baba yake,sijui alikuwa yupo mtungi au kala kijiti.



Ila yote kwa yote sisi wanaume tuwajibike kwa matendo yetu,tunajua wengi hatuliziki na mwanamke mmoja sasa ikitokea umetia mimba we lea tu hata kisirisiri mkeo asijue,huku uswahilini kuna watoto lukuki ambao wapo tu wanasoma St Kayumba wakati baba zao wana hela nishamshudia mmoja,mama yake anauza supu ya kuku asubuhi mara nyingi huwa nanunuaga na mchana anakaanga kiepe,yule mama ana strugle sana kulea mtoto peke yake wakati baba yake yupo na anauwezo mkubwa tu.

Na hata ikitokea mmekorofishana na mke wako,haina haja ya kuhamishia hasira mpaka kwa watoto,timiza wajibu wako kwa watoto wako kama mwanaume,mengine muachie Mungu atakulipia kwani mwanaume hasusi so husiisusie familia yako,kesho watoto wanaweza wakatoboa ukapata aibu kama huyo mzee,manake wanaweza wakakuliza kama tusingefanikiwa ungetutafuta?.
 
Siyo yeye Diamond bali huo ni mkwara wa mama yake, yaani dogo kanunua ugomvi wa wanandoa. Pia unaweza kuta financials zote mama ndiye muamuzi, so kijana hapaswi kulaumiwa, baba anapaswa akapige magoti kwa mkewe ili yaishe asaidiwe.
Mtamsingizia sana mama. Diamond ni mtu mzima, hata kama anamheshimu mama, ana maamuzi yake mwenyewe kama mtu mzima. Na radhi ya baba haiwezi kwenda kwa mama bali ataibeba mwenyewe.
 
Ila mtoa mada sio diamond tu kuna Ommy dimpoz,mwana fa,barnaba nk.

Usihukumu kwa kuangalia muhimu muombe tu kijana mwenzio moyo wa upendo na uvumilivu ayasahau afanye kitu kwa mtu wake wa karibu.
 
Diamond ana moyo wa huruma kwa kweli hata kujitoa kumsaidia kiasi fulani.......ingekuwa ni mimi huyo mzee angetamani hata afe maana asingeonja hata sumni yangu.
Siwezi kumjali mtu aliyenitelekeza na kuniona taka taka
 
Mkuu kajengee kwanza kaburi la Baba yako,ikishindikana kiwango cha tiles,jaribu hata cha cement ndo uwezo wako huo.mambo ya familia hayo waachie wenyewe,hujamalizana na familia yako.kias cha kuzodoa familia nyengine.
Kila famila au ukoo una matatzo ya kifamilia au ukoo au mtu mwenye tatzo au masumbufu ya hapa na pale.
Hatuko perfect.
 
Sema yule Uncle Shamte atawapiga pesa hawatoamini. Anawalia tu timing. Naskia Mama Dangote ndo mshika mali za mwanane.
 
Hilo hutanishawishi hata uongee maneno gani, Huyo mzee alipotumia ugomvi wake na mkewe kumuadhibu Nassibu alikuwa hajui kesho yanaweza kumgeuka?
alimuadhibu adhabu gani!!!

maana inawezekana kuna mengi mnajua wana jf ila hamtaki kitushirikisha.
 
huu utajiri tunaoambiwa nao umejaa karata nyingi mno,ukitoboa kiukweli ukweli huwezi mwacha mzazi wako anasugua aisee.
 
Una faida kwake na kwa watoto wake.
 
Unajua alichofanya baba yake?
Unajua kama Mond hana ugomvi na baba yake?
Kuna watu wengi sana hawakukanya kwenye mazishi ya wazazi wao,hakuna jambo la ajabu hilo likitokea.
 
Tuambie sababu alizozipata kwa mama yake ni zipi ili tupime kama zinafaa kutomtunza baba yake.
Hakuna sababu yoyote ile chini ya jua ambayo inaweza kuhalalisha yeye kutomtunza baba yake,maana ni wazi sababu kazipata kwa mama yake.
 
Ugomvi unamuhusu mtoto pia kama baba alitelekeza familia kwa sababu mtoto pia atakuwa aliathirikia kwa kuishi kwenye maisha ya shida na kukosa uangalizi wa baba.
Hili nalo ni gumu kuelewa?
 
Hakuna cha radhi wala nyenye yoyote
Mtamsingizia sana mama. Diamond ni mtu mzima, hata kama anamheshimu mama, ana maamuzi yake mwenyewe kama mtu mzima. Na radhi ya baba haiwezi kwenda kwa mama bali ataibeba mwenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…