Kama kweli, basi Magufuli kwa hili atakuwa ameibua makubwa, Kenya hebu tuliangalie

Kama kweli, basi Magufuli kwa hili atakuwa ameibua makubwa, Kenya hebu tuliangalie

Yaleyale ya MDRT (huna Malaria) kwenye Darubini tena maabara za mtaani (una Malaria) wakati huo smytoms zote za kuumwa unazo.... Changamoto ya vifaa tiba na vipimo vya Afya TZ ni changamoto....
 
Ndio. Usisahau uchaguzi mkuu Tanzania ni mwaka huu. Kwa hivyo Magufuli lazima aonyeshe kuwa Corona sio tishio ili achaguliwe tena. Trump pia uchaguzi wake ni mwaka huu ndio maana hata yeye ana underplay the seriousness of corona ili achaguliwe tena. Hawa wanasiasa lazima waonyeshe kuwa corona sio tatizo for their own political survival.
Angalao Trump ana upinzani, huku Tanzania sitegemei kama kuna mgombea yeyote toka vyama vya upinzani atakayechukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais zaidi ya Magufuli, kama wewe unamjua tafadhali mtaje, Mbowe alishasema hatogombea Urais.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
ufiche ili iweje lazima uuweke ukweli wazi ili wahusika wajitafakari


Sent using Jamii Forums mobile app


It is not in such style the president exposed, as the so called "truth" is a typical crime when those concerned are found guilty, by exposing the "truth" is just as alerting them, in that case how can you then reprimand them with clear evidence to take them to a court?? !!.

The "truth" should have been exposed just after thorough investigation rather than letting the cat out of bag.
 
MK254,
Kwani hujasikia huko India, South Korea pia wameshalalamika Test Kit za Uchina? Hamfuatilii mambo mmebaki hapa tu JF kwenye udaku.
 
Magufuli has messed up. Anatafuta pa kutokea lakini this time mtego wa panya umenasa panya. Hamna pa kutokea. Hata WHO wamekashifu magufuli for lacklustre performance.
Wewe hangaika na Kenya yako na hao WHO sisi hatuwaogopi tunawapa za kichwa wakileta cha kuleta!
 
MK254,

Ulipaswa kumsikiliza kwa umakini, kila neno na sentesi kabla ya hitimisho lako hilo.

Mwanasayansi yeyote, makini na aliyebobea kwenye taaluma yake, kama Rais Magufuli, tofauti na wa sayansi ya jamii, tafiti zao hufanywa kutokana na nadharia (hypothesis) na si maswali "research questions". Ili kupata jibu sahihi la " hypothesis" inabidi mtafiti atayarishe mazingira ya kisayansi kukusanya takwimu, kuzichambua kabla ya kuhitimisha matokeo (hypothesis, data collection, data analysis, conclusion, recommendations).

Alichokisema Rais Magufuli ni nadharia kuhusu jinsi ya kupima na aina ya vipimo vya COVID-19 kama vinakidhi matakwa ya kisayansi (Generalisation + Replication). Nadharia yake hiyo aliifanyia majaribio uliyoyataja akahitimisha kwa nadharia mpya kama ulivyozianisha. Nadharia mpya ameagiza taasisi na vyombo husika kuzifanyia kazi kupata majibu sahihi.

Madai yako kwamba Hiyo hotuba itaibua mengi sana, na inaweza ikajadiliwa mpaka Ulaya, maana leo hii tunaambiwa na kuona watu wanakufa kona zote za dunia..., ametoa jibu. Baadhi ya watu wanakufa kwa sababu ya hofu, "stress", tiba isiyo sahihi, nk. Na wala hajasema COVID-19 siyo ugonjwa hatari.

Nakudhauri uisikilize vizuri kwani imeibua maswali mengi. Hakika Rais Magufuli atakuja kukumbukwa kwa mambo mengi Tanzania na dunia nzima.
 
Kwani hujasikia huko India, South Korea pia wameshalalamika Test Kit za Uchina? Hamfuatilii mambo mmebaki hapa tu JF kwenye udaku.

Usikimbilie kusema walikataa kits, pia fuatilia kujua walizikataa kwanini, elewa kwamba India walizikataa maana zinatoa false negative, kwamba watu wenye corona na wanafahamika, zinaonyesha hawana. Hivyo hazina uwezo wa kupata kirusi.
 
Mkuu ameibua mjadala mkubwa sana, nina amini asemacho ni kweli.
Hisia zangu zinaniambia sample zinakuwa contaminated wakati wa kuchukua, kusafirisha, au huko maabara.

Au reagent zina tatizo na hii ilitokea hata marekani walitupa na kuagiza mpya.
Mwisho inaweza kuwa kweli kuna hujuma ya ndani au toka nje ya nchi.

Mjadala mzuri sana huu maana mimi nimewahi kuambiwa nina damu group flani na kukapita miaka nikaenda kupima benki ya damu salama nikaambiwa nina group jingine tofauti na la mwazo na zote ni taasisi kubwa za serikali.
Aise

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijasema ufiche. Nimesema ufanye uchunguzi ujue ukweli unavokuja kutangaza uwe na suluhu.

Kuja kutulalamikia sisi wananchi kuhusu failures za taasisi zako zinasaidia nini kama huji na suluhisho?

Kama vifaa vinaingia tayari vina wadudu na TBS wanapitisha coz labda hawana uwezo (vifaa, nguvu kazi n.k) wa kupima, njoo utuambie hatua ulizochukua, i.e ulivyowawezesha kuhakikisha haitokei tena.
Naunga mkono asilimia 100%.. hii tendency italeta shida zaidi badala ya kutupa suluhisho.

Kwa sasa kuna information nyingi mitaani na walau wataalamu walisaidia kutoa clarification pale ilipohitajika.

Leo hii wataalamu wanapoteza credibility, Barakoa na vifaa vingine imported havifai. Tunachopokea ni confusion zaidi kuliko njia sahihi ya kufuata na hii itafanya situation iwe worse
 
This is ludacris!
You shouldn't discredit your institutions in public like that before a comprehensive and conclusive investigation.
Wewe ni mmoja wa watu wanaodai takwimu za COVID-19 zinapikwa au zibafichwa, leo unakuja na hilo jipya ukilaumu! Tuelewe na kukubali lipi?
 
This is ludacris!
You shouldn't discredit your institutions in public like that before a comprehensive and conclusive investigation.
Tunapenda kuficha ili nini kitokee, walikuwa wanaficha wakat huo..ila wakat huu ni mwingine, na mm nampenda rais muwaz, hii ni nchi, sio kama wewe uwapo ofisin na boss wako pamoja na wafuas wengine....yeye ni rais namba 1, zama za kuficha ficha zipitwe na wakat comrade
 
Ulipaswa kumsikiliza kwa umakini, kila neno na sentesi kabla ya hitimisho lako hilo.

Mwanasayansi yeyote, makini na aliyebobea kwenye taaluma yake, kama Rais Magufuli, tofauti na wa sayansi ya jamii, tafiti zao hufanywa kutokana na nadharia (hypothesis) na si maswali "research questions". Ili kupata jibu sahihi la " hypothesis" inabidi mtafiti atayarishe mazingira ya kisayansi kukusanya takwimu, kuzichambua kabla ya kuhitimisha matokeo (hypothesis, data collection, data analysis, conclusion, recommendations).

Alichokisema Rais Magufuli ni nadharia kuhusu jinsi ya kupima na aina ya vipimo vya COVID-19 kama vinakidhi matakwa ya kisayansi (Generalisation + Replication). Nadharia yake hiyo aliifanyia majaribio uliyoyataja akahitimisha kwa nadharia mpya kama ulivyozianisha. Nadharia mpya ameagiza taasisi na vyombo husika kuzifanyia kazi kupata majibu sahihi.

Madai yako kwamba Hiyo hotuba itaibua mengi sana, na inaweza ikajadiliwa mpaka Ulaya, maana leo hii tunaambiwa na kuona watu wanakufa kona zote za dunia..., ametoa jibu. Baadhi ya watu wanakufa kwa sababu ya hofu, "stress", tiba isiyo sahihi, nk. Na wala hajasema COVID-19 siyo ugonjwa hatari.

Nakudhauri uisikilize vizuri kwani imeibua maswali mengi. Hakika Rais Magufuli atakuja kukumbukwa kwa mambo mengi Tanzania na dunia nzima.

Umeweka sawa maeneo kadhaa lakini hilo la kusema watu wanakufa kisa hofu ondokana nalo kabisa, Corona inaua na wengi wa wanaokufa wakipimwa mapafu yanakutwa yamethurika mpaka yanabadilika rangi, acheni hizo propaganda za kuwafanya watu wachukulie hiki kitu poa, kipo na kinaua.

Ninaweza nikakubaliana na ubovu wa vifaa vinavyopima, au uzembe wa wahudumu kwenye maabara, lakini mengine hayo yaacheni, mnaharibu.

Ubovu wa vifaa umetajwa hata India, ila kule walisema vinashindwa kugundua Corona, sio kwamba vinaonyesha ipo.
 
Usikimbilie kusema walikataa kits, pia fuatilia kujua walizikataa kwanini, elewa kwamba India walizikataa maana zinatoa false negative, kwamba watu wenye corona na wanafahamika, zinaonyesha hawana. Hivyo hazina uwezo wa kupata kirusi.
Hapo kwenye comment yangu kuna neno 'walikataa kits'? Au nimesama walizilalamikia hizo test kits? Tuliza akili unaposoma. Kwani zikiwa zinatoa false results/negative maana yake haziko sawa zinaweza pia toa false positive pia! Tumia IQ na EQ zako vizuri mkuu!!
 
Tunapenda kuficha ili nini kitokee, walikuwa wanaficha wakat huo..ila wakat huu ni mwingine, na mm nampenda rais muwaz, hii ni nchi, sio kama wewe uwapo ofisin na boss wako pamoja na wafuas wengine....yeye ni rais namba 1, zama za kuficha ficha zipitwe na wakat comrade
Umeelewa ulichoki-quote?!
 
Umeweka sawa maeneo kadhaa lakini hilo la kusema watu wanakufa kisa hofu ondokana nalo kabisa, Corona inaua na wengi wa wanaokufa wakipimwa mapafu yanakutwa yamethurika mpaka yanabadilika rangi, acheni hizo propaganda za kuwafanya watu wachukulie hiki kitu poa, kipo na kinaua.

Ninaweza nikakubaliana na ubovu wa vifaa vinavyopima, au uzembe wa wahudumu kwenye maabara, lakini mengine hayo yaacheni, mnaharibu.

Ubovu wa vifaa umetajwa hata India, ila kule walisema vinashindwa kugundua Corona, sio kwamba vinaonyesha ipo.
Kwani kuna mtu amekataa kuwa corona haipo? Lakini ni ukweli usio pingiga kuwa hofu pia huua!
 
Mkuu ndio hivyo hapa nilivyo sina hakika damu yangu group gani.
Najiuliza alikosea mpimaji wa kwanza wa ile hospital kubwa ya serikali?
Alikosea mpimaji wa pili wa hifadhi ya taifa ya damu salama pale makao makuu yao?

Je, aliye kosea alikosea katika upimaji au alisoma majibu ya mtu mwingine?
Je alikosea yule mhudumu wa hifadhi ya taifa ya damu salama alikosea kusoma majibu kwenye mfumo wa computer?

Nitakwenda kupima tena safari hii naenda hospital au maabara nyingine kubwa ya taasisi binafsi maana ukipata dharula wakataka kuokoa maisha yako kwa kukuongezea damu haraka bila kupima kundi la damu yako inaweza kuwa shida. majibu wakati fulani yanachelewa na hali inaweza kuwa mbaya.
 
[QUOTE="hydrogen, post: 7 kuhusu failures za taasisi zako zinasaidia nini kama huji na suluhisho?!
Kama vifaa vinaingia tayari vina wadudu na TBS wanapitisha coz labda hawana uwezo (vifaa, nguvu kazi n.k) wa kupima, njoo utuambie hatua ulizochukua, i.e ulivyowawezesha kuhakikisha haitokei tena.[/QUOTE]

Rais kalalamika au wewe ndiye unalalamika?

Suluhisho gani ulitegemea atoe zaidi ya kuagiza taasisi na vyombo vinavyohusika kuchunguza zaidi, baada ya kutoa hadharani matokeo ya "rapid test" ya jinsi COVID-19 inavyopimwa nchini?

Pole sana kama wewe ni mmoja wa wana mahabara, imekula kwako, maana umeumbuliwa hadhari michezo yako na wenzio. Km mkojo wangu ulipimwa nikaambiwa nina mimba wakati mimi ni "me"
 
Hapo kwenye comment yangu kuna neno 'walikataa kits'? Au nimesama walizilalamikia hizo test kits? Tuliza akili unaposoma. Kwani zikiwa zinatoa false results/negative maana yake haziko sawa zinaweza pia toa false positive pia! Tumia IQ na EQ zako vizuri mkuu!!

Cha msingi acheni kutumia malalamiko ya wahindi kuendesha hoja zenu maana wale walilalamika kwamba vifaa vinashindwa kuona corona, vinakosa uwezo huo.
 
Hii Ni wake-up call. Sasa ziandaliwe sample za mananasi,mbuzi etc kea uangalifu mkubwa zisiwe contaminated ili ziipimwe rasmi ili kupata uhakika wa hivi vipimo.

Hiyo mbinu iliyotumika Ni Bab kubwa
 
Back
Top Bottom