Kama kweli Mungu yupo, basi hana nguvu

Kama kweli Mungu yupo, basi hana nguvu

Inategemea na asili yenu, asili zingine sio nzuri na sio za kupata mafanikio unayoyataka. Lakini jaribu kua na imani, usiwe vuguvugu, chagua moja
Una experience na mambo ya asili?
 
Ili Mungu akusikie na kukupa yale unayomuomba, kuna vigezo na masharti. Baadhi ya vigezo vipo katika Andiko hili:
:Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, wakijinyenyekeza na kuomba na kunitafuta uso wangu, na kuziacha njia zao mbaya, ndipo nitawasikia kutoka mbinguni, na kuwasamehe dhambi zao, na kuiponya nchi yao.” (2 Mambo ya Nyakati 7:14)
Nimefanya hayo yote ila nimeambulia patupu.
 
Usimuombe Mungu moja kwa moja huwa yupo bize na mambo mengi

Watumie Malaika, wajulishe Malaika shida zako watamfikishia ujumbe

Hata mkuu wa mkoa tu huwezi kumuona kirahisi rahisi bila kupita kwa wasaidizi wake kwanza

Pia Mungu alishakupa kila kitu ni wewe tu kwenda kuchukua
Aisee!!!
 
Kuto kupata majibu ya maombi wala usimlaumu Mungu wala dini wala mtu yeyote, changamoto ni wewe mwenyewe,

IMANI Mkuu hauna imani... full stop 🛑

Mbona wenzako wanajibiwa... Mkuu inabidi ujiulize kwanini mimi!?
Akina nani hao wamejibiwa?
 
Kuto kupata majibu ya maombi wala usimlaumu Mungu wala dini wala mtu yeyote, changamoto ni wewe mwenyewe,

IMANI Mkuu hauna imani... full stop 🛑

Mbona wenzako wanajibiwa... Mkuu inabidi ujiulize kwanini mimi!?
Wanaojibiwa ni wale wenye matatizo feki
 
Pole Sana .
God exist

Isipokuwa njia nyepesi na ya uhakika uwe na IMANI na kile unachokiomba.


Mfano ukisema nataka nipate Kazi basi Amini kuwa utapata kweli na uwe positive.

.
 
Habari zenu Wanajamiiforums.
Kwa mda niliotumia kumuomba Mungu na kutokupata majibu yoyote, nahitimisha kuwa nguvu za Mungu si nyingi kama tulivyoaminishwa.

Aisee nataka kuamia Mizimuni, Anayejua namna ya kutambikia Mizimu anielekeze, Mungu aliyeletwa na meli kwenye maisha yangu amefeli (Hana impact yoyote).

Am done.
Unenda kumuomba Mungu hela unafikiri ni mwanadamu? Kumuomba Mungu ni kumwabudu/kumcha siyo kuomba kama akina matonya.
 
1. Mtu hujatubu madhambi yako ila unataka Mungu akutendee. ...Hilo sahau.
2. Mtu hutoi sadaka,zaka,malimbuko nk..bado unataka Mungu akuonekanie....Hilo sahau.
3.Mtu huna mahusiano mazuri na wenzako,ndugu zako na jamaa zako ..bado unataka Mungu akufanyie wepesi..Hilo sahau.
4. Mtu hujitoi Kwa kazi za Mungu,familia,jamii ..bado unataka Mungu ajibu maombi .Hilo sahau.
5.mtu unaishi Kwa kibri,unajisikia,si msikivu,hutaki ushauri,Wala huna chembe ya Huruma Kwa wenzako na Tabia ya wizi huachi...bado unataka Mungu akupe miujiza Hilo sahau..
6.mtu husomi neno la Mungu,hufungi..ukioomba Mungu unaomba Kwa kumshurutisha na malalamiko mengi..bado unataka MUNGU AKupende na kukutendea..Hilo sahau...
7.Mungu ana vigezo vyake..kama hutaki kuvijua ila unajiendea kama nyumbu...hakika sahau kupata majibu ...
8.mtu umekaa tu,hujaribu,huonyeshi jitihada Ili Mungu atie Kudra zake..wewe unataka maombi yashushe majibu kama Mana ..huna pa kushika Wala kuanzia huna connection...halafu eti Mungu mbona umeniachia...atakuacha kweli..

Kwa hiyo rekebisha njia zako...Mungu Hana sikio zito asisikie Maombi yako...
 
1. Mtu hujatubu madhambi yako ila unataka Mungu akutendee. ...Hilo sahau.
2. Mtu hutoi sadaka,zaka,malimbuko nk..bado unataka Mungu akuonekanie....Hilo sahau.
3.Mtu huna mahusiano mazuri na wenzako,ndugu zako na jamaa zako ..bado unataka Mungu akufanyie wepesi..Hilo sahau.
4. Mtu hujitoi Kwa kazi za Mungu,familia,jamii ..bado unataka Mungu ajibu maombi .Hilo sahau.
5.mtu unaishi Kwa kibri,unajisikia,si msikivu,hutaki ushauri,Wala huna chembe ya Huruma Kwa wenzako na Tabia ya wizi huachi...bado unataka Mungu akupe miujiza Hilo sahau..
6.mtu husomi neno la Mungu,hufungi..ukioomba Mungu unaomba Kwa kumshurutisha na malalamiko mengi..bado unataka MUNGU AKupende na kukutendea..Hilo sahau...
7.Mungu ana vigezo vyake..kama hutaki kuvijua ila unajiendea kama nyumbu...hakika sahau kupata majibu ...
8.mtu umekaa tu,hujaribu,huonyeshi jitihada Ili Mungu atie Kudra zake..wewe unataka maombi yashushe majibu kama Mana ..huna pa kushika Wala kuanzia huna connection...halafu eti Mungu mbona umeniachia...atakuacha kweli..

Kwa hiyo rekebisha njia zako...Mungu Hana sikio zito asisikie Maombi yako...
Apo umenena aise Mungu anatenda na anajibu kwa wakati
 
Wanaojibiwa ni wale wenye matatizo feki
Narudia tena, jiulize mwenyewe unakwama wapi kwenye hayo maombi yako.

Kwasababu swala la watu kujibiwa maombi, ni uhakika wala halina mjadala, sasa kwanini wewe hujibiwi?

Usifikili naongea kwa kusikia habari kwa watu... Ninauhakika na ninachokisema.

Kwa sababu tayari ulikua na option B
Kama alivyosema madam hapo, nimepitia comment zako. Inaonekana ulikua unaomba huku ukiwa dought/wasiwasi mashaka na unaemuomba. ((ulikua unaomba Ukimaliza kuna fikra zamashaka zinakuingia juu ya yale uliyoyaomba))

Mwandiko wako unazungumza mengi sana, kwanza msingi hauna, unyenyekevu (ego bado iko juu sana mkuu).
 
Free will; una uhuru wakufanya chochote na kwa chochote utakacho ukifanya uwe tayari kuwajibika kwa matokeo yake kiwe kibaya ama kizuri.
Freewill haipo.

Huna freewill.

Kwa mfano, Huna uhuru wa kurudi mwaka 1980.

Hukuwa na freewill ya kuchagua uzaliwe ama usizaliwe, Umeshtukia tu umesha zaliwa bila kuamua mwenyewe.

Hivyo hakuna freewill.
Kuhusu hao watoto, We ndio unawaona wanateseka, unajilinganisha na hali yako ila wao katika dunia yao wako normal...
Watoto wanakufa kwa njaa, vita, magonjwa halafu unasema wako normal?

Una utimamu huko kichwani kweli wewe?

Nenda Ethiopia huko Tigray, Cabo Delgado Msumbiji, Sudan kusini, Somalia Uone jinsi watoto wanavyo kufa kwa njaa na ukame!

Halafu wewe unakula na kushiba unasema eti hawateseki!!

Gentleman, Do you have common sense?

Ebu tembea uone!

FB_IMG_1710533066467.jpg

Wazazi wao ndio wanajisikia vibaya ila ni wajibu wao kwasababu waliamua kufanya hivyo.

Kuna kitu kinaitwa matumaini faraja(usawa kati ya furaha na huzuni) katika hili binadamu wote tupo sawa haijalishi unamali au hauna, kihisia wote tipo sawa ndio maana wote tunakuwa na matumaini ya kuendelea kuishi.

Pia material things vitu kama pesa ardhi magari nyumba ni vitu vya kumiliki tu, lakini sio utajili au vina thamani, huo uthamani wake tunaouona ni mtizamo tu, fikra(just perception) , tuliojengewa na mfumo wa maisha umeundwa katika namna ya kutufubaza, (illusion), mfano pesa ni number katika sarafu au karatasi.
Kuna watu kupata basic needs tu ni shida achilia mbali magari, nyumba na pesa.

Kuna watu hata mlo mmoja tu kwa siku hawapati.

Maji hawapati.

Makazi na malazi hawana.
 
kila nikiona kichwa cha huu uzi nacheka!..
jamaa kachapa bila mbwembwe kikatili sana halafu hapohapo anatafuta mizimu!.. aangalie isijekufika mwisho wa mwaka yeye ndo akageuka kuwa huyo mzimu!..🤣
NIwe mkweli mshikaj kanichekesha kabla sijasoma uzi wenyewe
 
Habari zenu Wanajamiiforums.
Kwa mda niliotumia kumuomba Mungu na kutokupata majibu yoyote, nahitimisha kuwa nguvu za Mungu si nyingi kama tulivyoaminishwa.

Aisee nataka kuamia Mizimuni, Anayejua namna ya kutambikia Mizimu anielekeze, Mungu aliyeletwa na meli kwenye maisha yangu amefeli (Hana impact yoyote).

Am done.
Wee jamaa acha kumdhihak MUNGUau utapata balaa!!
 
Back
Top Bottom