Kama misikiti inaweza kujengwa mitaani kwa uhuru, kwanini kujengwa kwa makanisa kuwe kero Zanzibar?

Kama misikiti inaweza kujengwa mitaani kwa uhuru, kwanini kujengwa kwa makanisa kuwe kero Zanzibar?

Duh Kwa kweli kama tumefika huko hii itakua chuki kubwa Sana mama Samia amiri jeshi mkuu kemea hili lisizae mizizi
Ninakumbuka yule aliykanyaga quruan Kilosa alishughulikiwa haraka sana. Ila kubomolewa kwa kanisa si tatizo.

Makanisa yanapiga kelele ila yale mavipasa sauti ya msikitini siyo tatizo.

Iko siku kisasi kitalipwa.
 
Hili suala la wazanzibari kutotaka ukristo visiwani humo iingia rasmi kama Kero jipya ya Muungano.
 
Aliekwambia serekali haina dini nani ? Zanzibar wakaazi wake wa kiislamu lakini skuli zinafuata kalenda ya kikristo na wala hawajalalmika miaka yote wakati wao ndio majority....
Hapo ndio kutakua na shida zaidi na hujafikiria sawasawa.

Una maana sehemu ambazo huku bara Kuna wakristo wengi mtaani , hakupaswi kujengwa msikiti?
 
Aliyewaambia wazanzibari wanahitaji makanisa ni nani?

Wazanzibar 99% ni waislamu hata hiyo misikiti iliyopo sasa haitoshi..

Hivyo anayehitaji kujenga nyumba ya ibada Zenji ajenge Msikiti ili kuCover mahitaji sahihi.

Unajenga kanisa la Tsh mil 100 halafu waumini wawili hiyo ni wastage of resources..

Eboo..!
 
S

Hatuogopi competition ya imani, hatutaki kupotoshwa na hatutaki kupoteshewa watoto wetu. Ikiwa unasema kuwa tunaogopa kupotoshwa, then yes sawa na wala hatuoni aibu kwa hilo tunaogopa kupoteshewa familia zetu, tunaogopa adhabu ya Mola wetu siku tukirudi kwake.
Wanapotoshaje? Wewe si ushike Imani yako? Nyie huwa sijui mnawazaga vipi wenzetu
Ndio maana mkifunga ramadhani hamtaki watu wengine wale mchana, eti watawatamanisha. Wtf......??
 
Hili Swala inabidi tuliendee bila kutumia hisia,nani hajui KERO ya makanisa ya kilokole yaliyotapakaa kila Kona ya nchi hii,kwa wakazi wa Dar,pale kawe Kuna makanisa kila Kona...
Tafakari pia haya;
-Hivi vile vipaza sauti vya misikiti vinavyopiga adhana alfajiri, adhuhuri, Alasiri, jioni na usiku huwa waviwapi kero wakristo au wapagani?

-Hivi ni misikiti mingapi huku kwenye mitaa ya Zanzibar ilijengwa kwa kibali?

-Hivi ni mamlaka gani ya SMZ itakupa kibali ujenge kanisa mitaani?

-Ni mamlaka gani iliyotoa kuvunjwa kwa hilo kanisa kwa sababu limejengwa bila kibali?
 
Mimi naona huyo jamaa aliyejenga kanisa hapo hakufanya sawa. Kwasababu asilimia 98 ya wazanzibar ni waislam. Ni hatari hata kwa maisha yake japo gharama ya ukristo ni zaidi ya uhai na mali. Kuna vitu vingine unatumia tu common sense na kupotezea.
Bado sijapata mantiki ya hoja yako.

Kosa ni kujenga kanisa kwenye waislamu wengi? How?

Wewe ulitaka ajenge wapi kanisa hapa Zanzibar?

Ni vipi uislamu uhatarishe maisha ya waumini wa kikristo hapa Zanzibar?

Nini mantiki ya kuwa na Uhuru wa kuabudu na uvumilivu wa kiimani unaotaja na kutafsiriwa katika katiba?
 
Nimeshuhudia taarifa na video mtandaoni ikionyesha kanisa dogo la TAG maeneo ya Zanzibar likivunjwa na greda kwa amri ya wakuu fulani wa serikali wa Zanzibar.

Sababu za kimsingi za hayo kutokea ni kukosekana kwa uvumilivu wa kidini kwa baadhi ya wakazi wa Zanzibar dhidi ya imani zingine, jambo ambalo linalindwa na watawala wa Zanzibar kwa miongo yote. Japokuwa wakuu wa serikali huko Zanzibar wamekuja na sababu nyingine duni na kijinga (wanadai wamevunja kanisa hilo kwa sababu za taarifa za kitisho cha hali ya hewa kuhusu mvua inayoweza kuleta mafuriko maeneo hayo!)

Tunapaswa kutambua haya.
1. Karibu mitaa yote ya Zanzibar kuna misikiti mikubwa au midogo.

2. Karibu misikiti yote ya Zanzibar ina vipaza sauti (horn speaker) zinazopiga adhana kila siku kutwa mara tano.

3. Karibu misikiti yote ya Zanzibar imejengwa kwenye makazi ya watu au jirani kabisa na makazi ya watu.

4. Mpaka sasa Zanzibar haina maeneo rasmi ya wazi yaliyotengwa mahususi kujenga nyumba za Ibada tu na kujulikana kwa watu wote.

5. Serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanzania kikatiba zote hazina dini na hazipaswi kufuata mlengo wa imani yoyote ya kidini zaidi ya kuheshimu na kulinda uhuru wa imani zote.

MAMBO MUHIMU YA KUTAFAKARI
-Kwanini kuwe na shida kila mara dhidi ya taasisi za kikristo zinapotaka kujenga makanisa, kuabudu kwa uhuru au kueneza imani yao maeneo ya Zanzibar?

-Kwanini Serikali ya mapinduzi Zanzibar na serikali ya muungano zinashindwa kulinda uhuru wa kuabudu kwa wakristo waliopo Zanzibar?

-Kwanini jamii za imani ya kikristo zionekane kama ni wavamizi, wapitaji na wageni waliokosa mwenyeji kila mara huko Zanzibar?

TAFAKARI
hawa wazanzibar ni wapuuzi Sana, 2010 niliwahi kushushwa kwenye gari zao za chai maharage bila sababu yoyote kisa tuu nimemuongelesha msichana aliyekuwa ameketi kando yangu kumuulizia kitu ninachoenda kushukia.


pia sokoni hapo darajani lijamaa limoja lilikataa kuniuzia mashine ya kukamua juisi ya miwa, mpaka nilitafuta mzanzibar akanisaidia kununua Kwa niaba yangu.
 
Wazanzibari wameukataa huu uhayawani wa makanisa haya feki.
Inashangaza huku Bara mtaa mmoja kuna makanisa matano!
Makanisa ni mengi kuliko waumini,matokeo yake ni makelele tu mitaani.
Kingine majority ya Wazanzibari ni waislam na huu ni ukweli ulio wazi.Hatuwezi kulazimisha Wazanzibari waishi kinyume na Utamaduni wao.

Jambo linalonishangaza Zanzibar,Sheria hizi na tofauti za Utamaduni haziwabani WAZUNGU kufanya watakavyo.
Mwezi mtukufu ukiwa na Ngozi nyeusi huwezi kula mahala popote Zanzibar,hata hoteli za nyota tatu au nne nilizowahi kutembelea nilinyimwa hata kuuziwa soda tu!
Lakini wazungu wanapata ulabu bila wasiwasi!.This is tantamount to slavery!

Tupo kwenye “Nchi” yetu lakini unabaguliwa na Mzungu wanamtukuza!
Beach wazungu wanakaa uchi lakini mtaani Mwanamke aliyeumbika akivaa nguo wao wanayoiona sio sahihi wanampiga na kumdhalilisha!
Sielewi mantiki yake!!.
Wazanzibari wana mambo ya ajabu sana,inahitaji moyo kuishi nao vizuri,unahitaji kuwa zaidi ya bwege ili uende nao sawa.
Ni ngumu kujifanya bwege kama wewe sio bwege,hasa ukiwa katikati ya mabwege.Bora uwe bwege kwa wenye akili.
Cha msingi tuwaache na Maisha yao.
 
OK OK OK enough! naona engi wanakuja hapa na kelele za kutaka Samia aingilie kati etc etc. Kwanza niwajuze suali la ardhi na majenzi haliko katika muungano kwa hivyo Samia hana ubavu katika suali la serikali ya zanzibar. Mkitaka mabadiliko kwanzabadilini katiba, muingize suali la ardhi na majenzi katika muungano, jambo ambalo hatutolikubali NG'O!!!!!

Pili duniani kote huibuki tu ukanunua kiwanja na kujenga unachotaka, ni lazima upate kibali. Kadhalika duniani kote wakaazi wa sehemu huwa wana haki ya kupinga ujenzi wa aina yeyote ile katika sehemu zao wanazoishi. Ndio maana daima kunakuwepo uwasilishwaji wa maombi na kufuatiwa consultationust kabla ya kukubaliwa ua kukataliwa kwa project yeyote ile. Just because tanzania na nchi nyingi za afrika serikali hutumia ubavu na kufanya walitakalo, haimaanishi ni kosa kwa serikali kusikiliza na kukubaliana na pingamizi za wananchi wake.

Zanzibar wananchi wake wengi ni waisilamu na hatuhitaji makanisa kila mahali. hatupingi kujengwa kwa makanisa tu, bali pia tunapinga kujengwa kwa bars na night clubs katika kila pembe ya visiwa vyetu. Kubaliana nasi au usikubaiane nasi, huo ndio msimamo wetu. Mna hiari zenu huko kwenu lakini sio kwetu.
 
Aliekwambia serekali haina dini nani ? Zanzibar wakaazi wake wa kiislamu lakini skuli zinafuata kalenda ya kikristo na wala hawajalalmika miaka yote wakati wao ndio majority.

Tumeondoshewa lugha ya kiarabu ambayo inaendana na uislamu sasa imekuwa kiengereza ili watu wafahamu biblia vizuri. Bado waislamu wa Zanzibar wamekaa kimya.

Mie nadhani huo uvumilivu unaotaka wewe utakuwa labda ni woga. Serekali lazima ina dini kwa maana serekali ni watu. Na watu wote wana dini zao!

Wacha wakristo wajaze hayo makanisa walioyo nayo kwanza kabla hawajajenga mengine!

Maasalaam,
Mjomba unatakiwa urudi shule..maana unaonkana hata elimu huna na hujaelemika sasa mtu akifundishwa kiingereza ndo anakua amejua biblia..?
 
Wanapotoshaje? Wewe si ushike Imani yako? Nyie huwa sijui mnawazaga vipi wenzetu
Ndio maana mkifunga ramadhani hamtaki watu wengine wale mchana, eti watawatamanisha. Wtf......?

Ni shida sana kujaribu kumfahamisha mtu ambae hafahamu dini yetu na ni vigumu zaidi ikiwa anaeuliza hataki kufahamishwa bali anataka kubishana.
 
Back
Top Bottom