Kama mwalimu wa Rais Samia anapata uteuzi 2022, Vijana twafwa!

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Vijana wa nchi hii yatupasa tuungane pasipo kujali vyama vyetu tupiganie haki zetu kwa umoja wetu.

Pamoja na utofauti wa itikadi zetu lakini kuna masuala yafaa tupaze sauti kwa pamoja

Inakera na kuudhi kuona vijana tunakosa ajira halafu wastaafu wakiteuliwa kushika nyadhifa kila uchwao. Sitaki kutaja majina lakini kila mmoja wetu afuatilie.

Funga kazi ni uteuzi wa huyu mwalimu wa mhe Rais SSH. Kama Rais SSH ana miaka 62 vipi umri wa mwalimu wake?? Vijana ni lini tutateuliwa??

Mhe Samia alikuwa form 2 mwaka 1974

 
Hakuna kitu ambacho huwa sipendi kama vyeo vya kulipa fadhila, hivi ndio vinatuharibia Nchi yetu tulitawaliwa na watu wabovu na tutaendelea kutawaliwa na wabovu, Utasikia fulani Kikwete, mara Mwinyi, Karume, mara Nape, mara Makamba, mara Kinana.....etc
 
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Funga kazi ni uteuzi wa huyu mwalimu wa mhe rais SSH. Kama rais SSH ana miaka 61 vipi umri wa mwalimu wake?? Vijana ni lini tutateuliwa??
Pole yako mkuu, nasimama nawe, lakini nakusihi usiishie hapo pa kulalama tu! Jihoji ni kwa nini inakuwa hivi lakini; vijana ni sehemu ya tatizo?

Tazama huko kwa makini sana.

Lisingekuwa "sehemu ya tatizo", nina hakika nchi hii ingekuwa ni tofauti sana na ilivyo sasa.
 
Nina uhakika kwa asilimia zote kwamba kama aliyeteuliwa angekuwa baba yako au ndugu yako usingelalama hapa
 
Vijana wakipewa nafasi wanaaza kuteka na kutisha watu...
hii awamu ni ya wazee awamu yenu ilishapita, watu washa umwa na nyoka wakiona jani tu wanashtuka.
 
Niliwahi kufundishwa na kijana namzidi miaka 13. Ni Mwalimu wangu huyo.
Kwahiyo wewe umesoma form two ukiwa na miaka 30. Unajibu hoja tafakari kwanza mkuu.

Hatuongeli kufundishwa chuo kikuu .
 
Kichwa cha mwenda wazimu nasikia saiv power button ime toka, controller ana pata shida kuhamisha channel
 
Nina uhakika kwa asilimia zote kwamba kama aliyeteuliwa angekuwa baba yako au ndugu yako usingelalama hapa
Umeusemea moyo wako. Nina 100% kuwa wewe ni mbinafsi
 
Kwani Samia ana miaka mingapi Kama mwl ana 61?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…