Kama Mwanaume haupaswi kula chakula kingi nyumbani heshima yako itashuka

Kama Mwanaume haupaswi kula chakula kingi nyumbani heshima yako itashuka

Hiyo ya kuachiwa sio makombo wala familia maskini. Kwa zamani, huo ulikuwa utaratibu tu wa wazee wetu. Baba alikuwa mfanyakazi na alikuwa anajiweza ila ni raha Baba unapoachia chakula kwa watoto hata kama walikuwa na kushiba. Wengi wetu tumekuwa hivyo toka zamani.
Kwetu sie huu utaratibu haukuwepo ndio maana nashangaa.
 
Au na mzee wangu atakuwa hivyo make ana mwili mkubwa ila anakula chakula hakiendani na mwili wake yaani maswala ya kula hayazingatii na akiwa home hawezi kula peke yake kama sio mkewe basi sie vihelehere tunaenda kumlisha baba chakula

[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Kwetu sie huu utaratibu haukuwepo ndio maana nashangaa.
Huo ni utaratibu wa familia za WAPUMBAVU zilizokuwa zinaongozwa na wazee WAPUMBAVU. Ni ujinga sana kusifia haya mambo. Ni mambo ya aibu watu wanatakiwa wawe wanaficha maana hapa conclusion tunayopata ni kuwa chakula kilikuwa hakitoshi. UMASIKINI MZIGO
 
Nyie ndio wale nyumbani umeacha hela ya mchicha huko umekula nyama choma na bia au vizuri vizuri.
Halafu akitengewa anaonja onja anasema ameshiba kumbe keshajilia vinono huko atokako.
Sasa unajiuliza hiyo hela aliyoenda kutapanya huko si angeacha tu kwa familia wakala vizuri kwa pamoja.
 
Huo ni utaratibu wa familia za WAPUMBAVU zilizokuwa zinaongozwa na wazee WAPUMBAVU. Ni ujinga sana kusifia haya mambo. Ni mambo ya aibu watu wanatakiwa wawe wanaficha maana hapa conclusion tunayopata ni kuwa chakula kilikuwa hakitoshi. UMASIKINI MZIGO
Kweli kabisa mkuu
 
Yawezekana hii ni sababu nyingine ya wanaume kufa mapema.Kujitwisha huruma na kufanya maigizo yanayoumiza aka "fujo inayoumiza/ua/tesa/kondesha.
Unafikiri hawali basi
Wengine wanakula huko watokapo wanakuja nyumbani wamejishibia na kama kumepikwa chakula sio kizuri ndo kabisaa anaishia kuonja.
Halafu wangine wana tabia mbaya nyumbani wanaacha hela ya mawazo halafu huko mtaani wanajilia vinono.
Mtoto hajui alikula kuku lini au samaki ila baba hamalizi wiki hajala hivo vitu.
 
Mzee alikua mjanja alikua anakwepa kulishwa sumu au kuwekewa limbwata.

Ndio maana anaonja halafu anawaachia na nyie ili kama ni madhara mpate wote au mhusika aogope kufanya hivyo kwani madhara yangekua makubwa.
 
Unakuta Zee lishatandika kilo nzima ya mbuzi,ndizi 5 na likashushia na konyagi huko lilikotoka.hiyo hamu ya kula home itatoka wapi?
Afu yaelekea humu jf watu wengi mmetoka kwenye familia zenye dhiki ya chakula?how comes mtu ale abakize then ndio akupasishie wewe makombo?kwetu sisi chakula kilikua kingi tu hakukuwa na mtu ana time sijui ya kuvizia mshua abakize msosi.
Siyo kuvizia msosi maana sio kila wakati unapasishiwa chakula kuna time chakula kinamwaga pointi ni kuwa mwanaume hupaswi kula sana ili kujijengea heshima yako.
 
Ni sijaona mantiki ya mtoa mada. Mimi ni Baba wa Familia nina watoto 5. Chakula kipo kinginhuku kijijini kwetu na mimi kama Baba najitahidi kuhakikisha msosi ni wa kusaza kwa watoto na sina utaratibu wa kula mtaani labda nisafiri kikazi. Sasa nishindwe kula kwangu eti naogopa watoto hawataniheshimu ila nikale Barabarani vyakula vinavyowekwa hamila?

Hiyo ni kwa ajili ya familia zenye uwezo wa chini. Nyumbani kwangu najiachia bwana, na watoto nao wanapiga sima lao tena huwa tunakula pamoja. Mara nyingi ikiwa usiku, namwambia mama yao weka kwenye sinia tule na watoto wetu kwa kushare chakula na mboga pamoja.
Heshima sio kwa watoto pekee ni kwa familia nzima hususani mama mtu inabidi awe na hofu ya kukupoteza wabaki na imani maisha yao bila wewe ni kipengele lakini ya kwako bila yao still yataendelea tena comfortable kabisa.
 
Yaani ule afu ubakishe ndo uwape watoto? Huo ni upendo wa wapi? Mzee wako alikuwa ni MPUMBAVU
Wewe mzee wako atakuwa mchoyo unakulaje bila ya kuwa na uhakika ya kuwa watoto wako wameshiba
 
Huo ni utaratibu wa familia za WAPUMBAVU zilizokuwa zinaongozwa na wazee WAPUMBAVU. Ni ujinga sana kusifia haya mambo. Ni mambo ya aibu watu wanatakiwa wawe wanaficha maana hapa conclusion tunayopata ni kuwa chakula kilikuwa hakitoshi. UMASIKINI MZIGO
sio rahisi kutenganisha familia za kitanzania na umasikini hata kama wewe kwenu zilikuwa zipo ila kuna mjomba, shangazi, baba yako mkubwa alikuwa masikini.

Huo ni utaratibu wa kawaida kabisa baba kuhakikisha familia yake sio imekula tu bali imekula na kushiba somo kubwa ni kuwa unapokuwa kiongozi wa familia lazima uhakikishe wategemezi wako wanapata basic needs hususani chakula ili kujenga heshima ndani ya familia.
 
Siku hizi hayo yamepitwa na wakati familia nzima inakula msosi heavy kwahiyo baba huna cha kuwapa watoto maana ulichokula ndicho wamekula muda mwingine wamekula na mengine extra zaidi yako.
Siku hizi watoto wanapewa sana priority ya kula misosi heavy kuliko hata baba. Au familia nzima kula vitu heavy. Enzi za baba anakula vilivyonona wengone wanakula vichwa vya samaki zishapita.
Mtoto akila heavy inamsaidia sana kukua. Baba akila heavy, sababu tayari amekuwa anapata obesity. Na kama mtu ulidumaa utotoni halafu ukaanza kula heavy ukubwani ni hatari sana.
 
Back
Top Bottom