Kama ni kweli, basi comrade Kinana amepuuzwa!

Kama ni kweli, basi comrade Kinana amepuuzwa!

Mbona sioni tatizo lolote....

Mmeumbuka kwenye ndege na huyo mpiga picha wenu sasa mmeibuka na non issue kuhusu mzee Kinana....

Bado nacheka kuhusu mpiga picha Woody....😀
Hivi nyani ndege wameumbuka au mmeumbuliwa? Iweje mmetoa notification ya "correction" ikiwa wao ndio wameumbuka?
Mahaba usiniue ila nifanye kipofu na kiziwi kama nyani ngadu
 
Unajua saiv akina polepole wanaona watanzania ni waduwanzi na mapoyoyo kichwani kwamba hatuelewi kitu kwamba sisi ni viazi kwaio likisemwa lolote tunasema ndiyo mzee...
Ni kiazi tu na poyoyo atakayeamini kwamba kinana tena katibu mkuu wa chama alisafiri nje ya nchi na amerud kimya kimya ...
 
Dah kweli kila mtu ana bei nikiona comment za Nyani Ngabu kwenye huu uzi unaweza kuhisi wame hack account au amempa mtu akili amshikie kwa muda
 
Unajua saiv akina polepole wanaona watanzania ni waduwanzi na mapoyoyo kichwani kwamba hatuelewi kitu kwamba sisi ni viazi kwaio likisemwa lolote tunasema ndiyo mzee...
Ni kiazi tu na poyoyo atakayeamini kwamba kinana tena katibu mkuu wa chama alisafiri nje ya nchi na amerud kimya kimya ...
Ukisoma body language unagundua jambo moja kuwa Polepole alikuwa anatafuta maneno sahihi ya kusema ili maelezo yake yasiibue maswali mengi. Bahati mbaya ameleta maswali mengi kuliko majibu.
 
We mtoa mada ungetoka hospital hujarecover completely ungetaka makamera kwako?. Msipende kudandiadandia mambo bhana. Au basi mtumeni Woody akapige picha kwa juu pale kwa comrade
Mbona speaker watu Mzee wa kifimbo tulimjulia khali wakati hakiwa bado kabisa,yaani comrade wetu kweli kweli wacheni upuuzi
 
Mange kimambe anayomajibu,jamaa haumwi walichomfanyia ni kama alivyofanyiwa marehemu abdu jumbe baada ya sakata la nape

Mange Siku hizi ndio amemilikishwa Medula Oblangata yako?


Hujui alipo Fisadi wenu Ngoyai lakin hukitulizi unataka kujua alipo Comrade inakuhusu nini?
 
Unajua saiv akina polepole wanaona watanzania ni waduwanzi na mapoyoyo kichwani kwamba hatuelewi kitu kwamba sisi ni viazi kwaio likisemwa lolote tunasema ndiyo mzee...
Ni kiazi tu na poyoyo atakayeamini kwamba kinana tena katibu mkuu wa chama alisafiri nje ya nchi na amerud kimya kimya ...

Hizi sio kauli za Polepole (msemaji wa chama)
 
Sisi tuliambiwa na mwenyekiti wake kuwa ametumwa kutibiwa.Hivyo tunasubiri mwenyekiti wake atuambie kama ameshamwambia arudi.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Ngumu kumeza
Maana alilazwa maalim seif n Fr. Mbatia tuliona picha za viongozi walivoenda kumjulia hali
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Hii trick ya kusema "tumempa likizo" ilitumiwa na CDM wakati Slaa amegoma. Iweje CCM mnaiga tactic ambayo wenzenu walitumia ikafeli?
 
Mzee Kinana nikama vile psychologically hayuko vizuri. Kinana ni mtu aliyeamini kabisa kuwa kwa umri alionao na kwa kazi kubwa aliyoifanya na kuifanyia ccm huu ungekuwa muda mzuri kwake kupumzika.

Kupumzika ambako aliakutamani na kuona kazi aliyotumwa na kujituma ameikamilisha na ameweza kuandaa damu changa ambayo kwa mikono yake ameilea na kuipa uzoefu wakutosha. Hivyo ni muda sasa wakuiacha hiyo damu changa ifanye kazi na yeye na wengine waliowakongwe wawe washauri wa mipango na mikakati yakuendeleza chama.

Hata akafikia wakati kutaja kupumzika lakini ghafla akaambiwa hapana subiri kwanza. Hali hii imemstua sana. Pengine ndio chanzo cha kudhoofu kwa siha yake na 'kutumwa' kutibiwa huko alikotumwa.

Hii nikama hali ya mtu tajiri sana na aliyedumu katika maisha yake yote kuitengeneza familia yake kwa muda mrefu, akaiwekea misingi imara na madhubuti yakumudu maisha na maisha ya ushindani wakibiashara na miamalati ya maisha ya kawaida kwa hadhi ileile ya asili.

Lakini ghafla ikiwa umri umeenda sana, tajiri huyo akajikuta katika familia ile aliyoijenga na kuacha vijana wake wakiwa imara na akiwa na imani kuwa wataendeleza tunu za familia kwa pamoja na msikizano, anaiona familia inaanza kuparaganyika na kushikana mashati, pengine watoto wengine wanaambiwa hawahusiki na mali za mzee, tajiri yule anachanganyikiwa na pengine anaweza kuumwa ghafla na hata kupoteza maisha kwa hiyari au kwa kulazimishwa.

Watu waliopoteza umri wao mrefu katika kujenga jambo fulani nankuweka misingi bora ya aidha familia, kampuni, shirika, chama au hata nchi. Huwa wanapata huzuni sana pale wanapoona jitihada zao za miaka na miaka zinaweza kuharibiwa kwa sekunde tu na kuacha mvurugano usiokuwa na maana.

Hali hiyo pia ilimtokea baba wa taifa hili, mwalimu Nyerere pale alipoona misingi ya utawala bora na uchumi inaharibiwa na watu aliowaamini na kuwapeleka kwa jamii ili waaminiwe, wanaharibu nchi kwa sera za hovyo kama ubinafsishaji au utandawazi. Nyerere aliumizwa sana na kuona mashirika ya umma yakiuzwa kama njugu kwa bei za hovyo. Ilimuuma kwani alitumia umri wake wote kuyajenga mema hayo leo kufumba na kufumbua wanakuja watu wanaharibu machoni pake akiwa hai.

Mungu mbariki Mzee Kinana- zama zinabadilika.
 
Alienda kibinafsi au alitumwa na rais kwenda kwenye matibabu? Au alitumwa arudi kabla hajapona kwamaana bajeti ilikwisha kwahiyo anaugulia nyumbani?

JPM mwenyewe anajichanganya na inaonekana ana hofu na Kinana! Kusema amemtuma kwenda India kwa matibabu ni uongo!! Hivi mgonjwa anatumwa kwenda kwene matibabu au anapelekwa?
Vinginevo JPM atuambie kuwa alimlazimisha Kinana kwenda India ili asije akamwaga ugali!
Ni swala la muda tu! JPM lazima. ajue kuwa amekalia kuti kavu ndani ya CCM na serikali yake!
 
Mbona sioni tatizo lolote....

Mmeumbuka kwenye ndege na huyo mpiga picha wenu sasa mmeibuka na non issue kuhusu mzee Kinana....

Bado nacheka kuhusu mpiga picha Woody....😀
Ukweli utajulikana
 
Back
Top Bottom