Kama Saudi Arabia na Vatican wameweza kufanya ibada majumbani sisi tuliopokea dini toka kwao tunashindwa nini?

Kuna mahali popote pale katika andiko la mtoa mada aliposema kuwa Saudi Arabia wameanzisha dini?
Unajibu vitu visivyokuwepo kwenye hoja ya mtoa mada
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu shida kubwa nchini kwetu ni kiburi cha baadhi ya viongozi kutumia vibaya madaraka katika kulishugulikia gonjwa hili Covid-19. Na kama tungekuwa nchi ilioiva katika mfumo wa kidemokrasia, kama Korea ya kusini,Covid-19 ingekuwa kipimo cha uchaguzi mkuu October 2020
Lakini baya zaidi ni hao viongozi kutumia kivuli cha madhehebu kama kinga ya kuhadaa umma kukusanyika kusalia ndani ya nyumba za ibada wakati huu wa tishio la maambukizi ya Covid-19.
Kama uwezo wetu wa kupima maabukizi ya virusi vya Corona ni mdogo sana,je tunapata wapi nguvu ya kuwahamasisha watu kukusanyika katika nyumba za ibada bila vipimo?
 
Kwani huko waliofunga Makanisa kama USA,Kenya nk wagonjwa mbona wagonjwa wanaongezeka tu? Au uchunguzi umeona hao wagonjwa walioambukizwa wakiwa Msikitini au Kanisani? Hata hivyo wewe kama unaogopa kwenda Kanisani utaambukizwa baki kwako, sisi tukaenda kumlilia Mungu huenda akalirehemu Taifa.
 
Ninashauri hizi sentensi zako zingetumika kama Final Test Exam kwa wachungaji au wainjilisti au wafia dini woote ingefaa sana kuwa na watu sahihi sehemu sahihi na hasa kile kipengele cha kuwaombea wagonjwa wa Corona kwa kuwashika vichwani........
 
Tunaendeleza ujinga wetu wa kiafrika.

Kama kuna mtu ana jibu tofauti na hili anitag

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaribu kuficha ujinga wako na hizo stori zako za yesu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Basi ni vema mkaishi huko huko kanisani kama Walawi!
 

Dunia ya leo imejaa maasi, imani hazitponyi tena, kirusi kinaua hata makanisani tena kwa walokole, tumepewa hekima na Mungu tuitumie.
Kuna miaka ile, ilikua rahisi kuomba na miujiza inatokea, leo hii hao akina Gwajima video zao wakifanya porn zimezagaa kwenye internet, ndio unawategemea wakuombee.
 
Mungu ni zaidi ya utashi na uelewa wako , yeye haangalii eti kama fulani kafanya hivi kwa nini fulani . Litafute kusudi la Mungu dhidi ya Taifa lako ndipo utakapoacha kutumia neno Kama .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie mnaoshikilia misikiti na makanisa mnashangaza maana sababu yenu ni kwamba hiyo ni mikusanyiko isiyo ya lazima,watu wanaweza wasiswali misikitini na makanisani ila bado huku mitaani maisha yapo kama kawaida hakuna kilichobadilika. Na huku ndiyo tunachanganyika wote kuazia wanafunzi waliyozuiliwa kwenda shule,waumini mnaotakata kuzuia wasiabudu kwenye majumba ya ibada na hadi akina Kiranga pia tunakusanyika nao huku mitaani.

Kama kweli mmeona corona ni hatari na mna nia ya dhati ya kuzuia maambukizi basi yafanywe maamuzi ya kweli sio haya kutaka kuzuia wanafunzi wasisome na waumini kwenda kuabudu kwenye nyumba za ibada lakini watu hao hao wanakusanyika mitaani kama kawaida na hufanya mambo yao kama kawaida watu itakuwa ni kazi na bure tu.

Mie ndiyo maana nasema ikiwa bado hadi sasa tunatoleana mifano ya Italy na Spain kuonesha uhatari wa corona basi bado waafrika hatujaona huo uhatari wa corona hapa afrika na ndiyo maana maisha bado yanaendelea kama kawaida.
 
Uislamu ni mapokeo au si mapokeo? Kama ni mapokeo ni kutoka wapi? Huko ulipotoka wanaendelea kukusanyika kuswali misikitini pamoja na hii changamoto ya covid?
Uislam ni mfumo wa maisha na umetoka kwa Allah na Allah anatufahamisha katika Qur'an kuwa...

Qur'an 11:

36. Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani. Basi kati yao wapo alio waongoa MwenyeziMungu. Na kati yao wapo ambao ulio wathibitikia upotovu. Basi tembeeni katika ardhi, muangalie ulikuwaje mwisho wa wanao kanusha.
36
 
Mbona hamponyi corona sasa? Pamoja na kukusanyika kwa siku zote hizo idadi ya wagonjwa inazidi kuongezeka? Kuendelea na mikusanyiko ya ibada hali tunajua wazi ugonjwa unaambukiza sana kutokana na mikusanyiko ni kumjaribu Mungu wala haina tofauti na shetani alivyomtaka Yesu amjaribu Mungu. Majibu ya Yesu kwa jaribu kama lenu ni haya (Lugha Kiingereza na Kiswahili):-

Matthew 4:5-7
"[5]Then the devil taketh him up into the holy city, and setteth him on a pinnacle of the temple,
Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu,

[6]And saith unto him, If thou be the Son of God, cast thyself down: for it is written, He shall give his angels charge concerning thee: and in their hands they shall bear thee up, lest at any time thou dash thy foot against a stone.
akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

[7]Jesus said unto him, It is written again, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako."

Acheni kuwa mawakala wa shetani kwa kivuli cha Yesu.

Pia tambua kwamba Mungu yupo mahali popote na baadhi ya sifa zake ni hizi:-

1. God is omnipresent - Mungu yupo kila pahali.

2. God is omniscient - Has unlimited knowledge; Uelewa wa Mungu hauna mipaka (hakuna asichokijua).

3. God is omnipotent - God has unlimited power; Mungu ana nguvu/uweza usio na kikomo.

Ndiyo maana hata mkuu wa katoliki (Papa) anawaambia waamini wake Waungame popote pale walipo Mungu yupo na anawasikia badala ya kwenda kwa kasisi/padri kama wengi walivyozoea.
 
Maaskofu na Mapdri wanahusudu sadaka kuliko uhai wa kondoo wao....
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuelewa vema!
 
Ookey
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…