Kama silaha zilizooneshwa ndio za Jeshi letu, bado tupo nyuma sana

Kama silaha zilizooneshwa ndio za Jeshi letu, bado tupo nyuma sana

Mbona unakua kama mshamba flani umeweka mwenyewe hapo imeandikwa since 1967 till now in service sasa unachoshangaa hapo ni nini? Wabongo kwa ujuaji bwana.
Wewe usiye mshamba ndio ushauri jeshi liwe na machuma yenye technology ya 1967!? Hata kwenye computer zipo Pentium 2. But is outdated technology.

Heshimu technology mwanangu na badili mtazamo.
 
Ombeni maji na umeme, acheni kutoa loopholes za majizi kuwaibia kwa kisingizio cha kununua silaha.
Fanyeni kazi mjenge taifa
Jeshi liko vizuri
 
Kuwa na silaha ya kisasa siyo ticket ya kushinda battle. Katika jeshi intelijensia ina 70% ya ushindi kwahiyo hilo la uganda hata usishangae.
Mzee nani amesema kushinda battle hapa. Kwani kuwa na computer ya kisasa ndio kujua programming!? Fungua ubongo wako acha kutetea outdated tools.
 
Magaidi wanastukiza na sio kuweza kupigana, Hakuna kundi lolote la kigaidi lenye kuweza kupigana na jeshi, Ingekuwa rahisi hivyo, serikali nyingi zingeshaanguka,gaidi ni SAwa na panyaroad wao uvizia na ushambulia
Moja ya mataifa ambayo yana teknolojia ya juu kabisa duniani ni ISRAEL ila kwa ishu ya ugaidi mpaka sasa bado inawapasua kichwa na wanatumia kiasi kingi cha fedha.

Kumbuka moja ya mataifa ambayo yanatumia akili nyingi saaaaana kujilinda duniani ni ISRAEL.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Onesha busara hata kama hukubaliani na kitu, unaongea as if kama una uwerewa na silaha kumbe ni hopeless. Military show off iko duniani kote sio Tanzania, kuhusu siraha outdated ni matangopori mnalishana hakuna mtu amkuja na pepa humu kuonesha kuwa tunameonesha siraha autdated. Maafisa sio wajinga harafu kuwa na akili basi kwenye uwanja wa medani hatugemei siraha tu bali morale, uhodari na ushapavu kwenye uwanja wa medani, rejea vita ya Kagera au vita ya Vietnam. Vijana mnatia kinyaa kujifanya kila kitu mnajua wakati hamjui siraha huwa zinaboreshwa na zingine zinazalishwa mpya. Kwa mfano rada nyingi kitambo zilizokuwa hazina uwezo ya kunasa wave za ndege zinazopita chinichini sasa hivi mifumo imebadilika. Sio lazima kila kitu uchangie mengine yaache yapite. Tujivunie nchi yetu kwenye makosa na mapungufu tuungane tuyasahihishe, kuikejeri nchi yako ni ujinga tu au elitism ya kishenzi tu
Nchi ambayo inawakejeli wananchi wake ni halali kukejeliwa pia
 
Vita na Uganda mlitumia maji kushinda?

Mababu zako kina Kinjeketile Ngwale walituma maji dhidi ya Wajerumani, leo hii na elimu yako bado unarudia mawazo ya mizimu yako. Kwani maji ndio mahitaji pekee katika nchi hii
Sijui kama anakumbuka zile Trilion 3 za mnadhimu wa jeshi awamu ya jk.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi nyie mnaish nchi gani, wakati TZ ikiingia kwenye mgogoro na umoja wa mataifa kwa kununua silaha north korea, mlikuwa huku dunian kweli? Muwe mnafuatilia mambo mnatia aibu asee
Ukweli ndo huo tokea magufur aingie madarakan hakuna gar Lolo la jesh alilo nunua magari yote unayo yaona Yana tembea barabarani yamenunuliwa awamu ya nne na mengi mabovu
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
Zile zilikuwa za kupendezesha sherehe tu, huwezi ukaonyesha silaha zako bora hadharani

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Taliban walitumia AK47 na mabomu ya kutega barabarani tuu na waliweza kumshinda Mwamerika mwenye kila aina ya silaha ambazo ziltengenezwa kwa matrilioni ya dola. Kuwa na silaha mpya siyo muhimu kama utayari wa kupigana.
 
Ulinzi ni pamoja na kuonesha uwezo ulionao. Kwa silaha zilizooneshwa kusema kweli ni hafifu. Zimepitwa ma wakati. Uganda na Kenya wana silaha bora kutuzidi.
We are weak compared to them.
Walikuonyesha ? Na jee wewe ndiye mboharia wa silaha zetu? Hapa tu silaha zinapoingia hata bandarini zinatolewaga usiku. Silaha ni jambo la siri.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Hivi nyie mnaish nchi gani, wakati TZ ikiingia kwenye mgogoro na umoja wa mataifa kwa kununua silaha north korea, mlikuwa huku dunian kweli? Muwe mnafuatilia mambo mnatia aibu asee
Wewe ndio umetia aibu kabisa.

Hao N. Korea tuliwaita waje kutupa spare parts na kufufua ndege zetu zilizochoka ambazo zimetengenezwa miaka ya 1960s. Zile ziko grounded na tuliagiza hizi J-7G kama iliyopita angani leo. North Korea ana vikwazo vya kutoa msaada wowote wa kijeshi, hata biashara nyingine hufanyi naye yuko under sanctions
 
Hizo helicopter zenye landing gear alinunua nani?

Uongo mbaya jamani
Zitakuwa zilinunuliwa awam ya 4 Una jua jeshi letu halina magar magari mengi yaliyopo yame choka ukitakujua we angalia plate namba utajua kwa mara ya mwisho jwtz limenunua magar mwaka gani
 
Sisi hatulaumu jeshi wala hatusemi ni dhaifu, wala hatulidharau. Sisi tunapaza sauti tuwe tiyari kila idara. Ni kama mtu akija kusema TANESCO wawe imara haambiwi anaidharau au hana uzalendo. Ingekuwa vyema tukajua ni jeshi la WANANCHI, sio jeshi la kikundi fulani wala wanajeshi wenyewe. Sisi wananchi tulipiganie liwe na nyenzo za kutulinda. Waliotakiwa kuhakikisha lina nyenzo ni hawa akina Musukuma na Babu Tale.
Hahaha yaani mpaka aibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom