Kama sio Maaskofu wa Kanisa Katoliki, Watanzania tulikuwa tunapigwa na kitu kizito sana na DP World

Awamu ya sita imeongoza kuwa na viongozi wasio wazalendo kwa taifa lao. Laiti wangejuwa wajibu wao kwa taifa ili leo tungepiga hatua kubwa baada ya Hayati Rais Magufuli kuandaa Njia.
Yaani wanatengeneza mkataba wa Kimangungo kwamba Tanzania inapotaka kuweka mwekezaji mwingine maeneo mengine ya bandari inatakiwa iende Dubai kuomba ridhaa, Dubai wakikataa kutoa idhini ndio basi,.....Lahaulah, tukaombe idhini Dubai kwa Mali zetu? Huu ujinga ubaki CCM na Dubai.
 
Asanteni TEC nawatakia sabato njema.
 
kaka uko nchi gani? mbona dpw kashapewa bandari na utekelezaji wa awali umeshaanza. ccm wameziba masikio na kuvaa miwani ya mbao, wanachojali wao ni matumbo yao na uchaguzi 2025
 
Mbona sioni uthibitisho wa kinachoongelewa zaidi ya watu kufarijiana humu?

Hivi kabisa hii serikali yetu isitishe mipango yake hata kama ni ya kula wao wenyewe kisa kelele zetu?

Mimi nataka nisubiri nije nijionee kama kweli
 
Mwezi wa kumi mwishoni DP World wanaanza kazi pale bandarini, jiandae kisaikolojia kuumia nafsi yako.

Magati namba tano mpaka namba saba yatahudumiwa na wao, magati namba nane mpaka kumi na moja watahudumia waendeshaji wengine.

Hao maaskofu wa TEC hawakuelewa kwa kina mipango ya serikali ndio maana wakaja na waraka wakihofia mwarabu amekwisha kuchukua bandari yote.

Tangazo la TPA likitafuta mwekezaji wa magati hayo ni jibu kwamba DPW hana mamlaka ya kuipangia serikali kipi cha kufanya na kipi sio cha kufanya, uoga wetu ukiwemo wewe mleta mada ni wa bure tu.
 
Kanisa Katoliki lianze kulipa kodi kwa taasisi zake zote, ili tuende sawa sasa, Kanisa lina ma trilioni ya miradi na investments yote Tax free, kiukweli Kanisa Katoliki Tanzania halijawahi saidia Serikali hata kidogo, tena Serikali ndio inaisaidia sana kupitia kutolipa kodi kwa kila kitu chao, Kanisa kazi kukusanya mabilioni kwa wananchi maskini na kuwanyonya wanyonge bila hata kuwainua kiuchumi, kanisa limekuwa cancer kuwanyonya wananchi waumini wake
 
Sijui TEC walikuwa wapi enzi za wasiojulikana
 
Ukosahihj kwasababu Tanzania ni wajinga wasingeamini anachosema Lisu au mwabukusi kwa haraka au Dr slaa

Hivyo ,wangepuuzwa kama ulivoona tulia ackson kaazisha ujinga mbeya

Ccm ilikuwa ichague moja izikwe yote au ibakie japo kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…