Kama sio Maaskofu wa Kanisa Katoliki, Watanzania tulikuwa tunapigwa na kitu kizito sana na DP World

Kama sio Maaskofu wa Kanisa Katoliki, Watanzania tulikuwa tunapigwa na kitu kizito sana na DP World

Waraka usomwe hadi Oktoba 2025

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)
Mwenye uchungu na bandari isiyowahusu...
Nenda TEC watakujibu
 
Wapi watu wamebishia uwekezaji? Ni vipengele vya kinyonyaji vya mkataba ndio vinaoigiwa kelele, sio uwekezaji..

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Nenda kwa Padri Slaa au TEC watakujibu. Humu wajifariji tu, hupati majibu
 
Aliyesaini mkataba ule kule Dubai ni mtaalam mbobezi wa sheria za mikataba ya kimataifa.

DP World anakwenda kupangishwa magati namba tano mpaka saba, namba nane mpaka kumi na moja ni mwekezaji mwingine.

Unapolaumu kilichoandikwa kwenye IGA ya serikali na DPW, umewahi kuiona mikataba mingine inayosimamia utekelezaji wa miradi mingi inayoendelea hivi sasa hapa nchini?, unajua nini kimeandikwa humo?.

Tupunguze ujuaji wetu.
Usijidai muhuni wewe, uhuni wenu hukohuko peleka
 
Aliyesaini mkataba ule kule Dubai ni mtaalam mbobezi wa sheria za mikataba ya kimataifa.

DP World anakwenda kupangishwa magati namba tano mpaka saba, namba nane mpaka kumi na moja ni mwekezaji mwingine.

Unapolaumu kilichoandikwa kwenye IGA ya serikali na DPW, umewahi kuiona mikataba mingine inayosimamia utekelezaji wa miradi mingi inayoendelea hivi sasa hapa nchini?, unajua nini kimeandikwa humo?.

Tupunguze ujuaji wetu.
We jamaa inaonekana una akili sana, kama si nusu!
Hebu tujuze, kwa nini DP Weldi walishinikiza hadi bunge likubali wanunue na rasilmali ardhi za nchi ndipo "ukodishaji" uwe mtamu?
 
Ndugu zangu Watanzania wale madingi wa Katoliki ni miamba sana, wamemaliza ujinga wa DPW.

Muda si mrefu Mama atatema bungo. Tender hiyo, wenye mbavu waipambanie. Ile sheria ya maliasili waliyotaka kubadilisha ili mikataba isipelekwe bungeni juzi nimeona kamati ya bunge ikipinga mapendekezo yote ya serikali. So far ile sheria haijaguswa.

Kama sio msuli wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC tungepigwa na kitu kizito vibaya sana.

Ahsanteni Maaskofu wa Katoliki.
Mungu amewatumia waziwazi kabisa, tulishaingizwa mjini.
 
Waraka wa TEC kwa serikali ni sawa na kikombe cha babu wa Loliondo kwa mgonjwa (hakuna impact yeyote).

Hizo sheria za 2017 zilikuwa hazibadilishwi kwa sababu ya DPW; kitendo cha kufanya ratification ya IGA inakuwa juu ya sheria yoyote ya nchi katika mambo yaliyomo mule.

Kitu pekee ambacho kipo juu ya IGA kisheria ndani ya Tanzania ni katiba ya jamuhuri ya muungano tu (that’s the whole point of ratifying something).

Sheria za mwaka 2017 zina mambo mabovu ambayo sio rafiki kwa uwekezaji generally speaking. Serikali kuzitoa wakati huu ni kwa sababu ya watu kuaminishana sababu ya IGA; hila vuguvugu la bandari likipoa hizo sheria zitabadilishwa tu mbeleni make no mistake. Sio kwa sababu ya uwekezaji bandarini bali zina ukakasi kwenye kuvutia uwekezaji in general.

Makelele ya IGA yamepelekea sasa kuiruhusu TPA kugawa Port yote ya Dar. Kitu ambacho sio sahihi kabisa kwa sababu serikali ilishafanya uwekezaji mkubwa tayari. Kuna justification ya uwekezaji wa DPW strategically lakini ni upuuzi wetu wenyewe ambao unapelekea serikali kwenda kugawa berth 8-11 bure bure huko sasa ndio mafisadi ya ndani yanaenda kupiga kweli.

Halafu wanaoumia kwenye upuuzi wa siasa za majungu na upotoshaji ni raia waliowengi ambao mlo wao wa siku tu kitendawili hela yenyewe ni ‘hand to mouth’.

Such a pathetic country
 
Ni waajiriwa wa Serikali hao.
Wanaogopa kufutwa kazi, si unajua Maprofesa wetu wanategemea ajira.

Kimaadili Mtumishi wa umma huruhusiwi kumkosoa Raisi wa Nchi hadharani.
Upo sawa mkuu sema wanaogopa ila kukosoa changamoto za mikataba kisomi ndio maadili na si kukaa kimya harafu vizazi vyao vinaangamia maana ya wao kupata shule ni nini sasa...yaani mikataba ya Nchi inazungumzwa na Wachungaji na Masheihk kweli ?.
 
Ukosahihj kwasababu Tanzania ni wajinga wasingeamini anachosema Lisu au mwabukusi kwa haraka au Dr slaa

Hivyo ,wangepuuzwa kama ulivoona tulia ackson kaazisha ujinga mbeya

Ccm ilikuwa ichague moja izikwe yote au ibakie japo kidogo
CCM wamechagua kuendelea na DP World pale bandarini na huo uchaguzi wa 2025 watashinda vile vile.
 
Kwanini msijitengenezee ufanisi nyie wenyewe? Mbona jeshi la Polisi hamjamuita mwekezaji alijengee ufanisi? Kwanini hao DPW hawawezi kuwa kama consultants wa kuwajengea ufanisi TPA?
Jeshi la polisi ni tofauti na shughuli zinazofanyika pale TPA. Uandishi na mawazo yako kwa ujumla ndio tatizo la uelewa wa nini kinachoendelea katika dunia ya sasa haswa kwenye suala zima la masuala ya bandari.
 
Jeshi la polisi ni tofauti na shughuli zinazofanyika pale TPA. Uandishi na mawazo yako kwa ujumla ndio tatizo la uelewa wa nini kinachoendelea katika dunia ya sasa haswa kwenye suala zima la masuala ya bandari.
Hao wataalam mnaowapeleka kusoma nje ya nchi kwa mabilioni ya pesa mnawatumiaje kama mnashindwa kuendesha bandari taasisi za umma kisasa??
 
Hao wataalam mnaowapeleka kusoma nje ya nchi kwa mabilioni ya pesa mnawatumiaje kama mnashindwa kuendesha bandari taasisi za umma kisasa??
Rahisi kuongea usichokifahamu. Muingereza na mtanzania nani kasomesha zaidi ya mwenzake?, DP World anaendesha bandari mbili pale Uingereza.

Belgium na Tanzania nani kasomesha kuliko mwenzake?, bandari ya Antwerp inaendeshwa na DP World.
 
Rahisi kuongea usichokifahamu. Muingereza na mtanzania nani kasomesha zaidi ya mwenzake?, DP World anaendesha bandari mbili pale Uingereza.

Belgium na Tanzania nani kasomesha kuliko mwenzake?, bandari ya Antwerp inaendeshwa na DP World.
Hiyo sio hoja mkuu, kwa maana nyie ndio mliodai ya kwamba sasa wageni waondoke na mjiendeshe wenyewe miaka ya 1960s ndio mkaita harakati za uhuru. Kiko wapi sasa?? Mliwafukuza ila sasa mnaomba warudi??

Alafu kwanini iwe bandari tu. Mbona hata TRA hakuna ufanisi na hamjampa mwekezaji??
 
Ndugu zangu Watanzania wale madingi wa Katoliki ni miamba sana, wamemaliza ujinga wa DPW.

Muda si mrefu Mama atatema bungo. Tender hiyo, wenye mbavu waipambanie. Ile sheria ya maliasili waliyotaka kubadilisha ili mikataba isipelekwe bungeni juzi nimeona kamati ya bunge ikipinga mapendekezo yote ya serikali. So far ile sheria haijaguswa.

Kama sio msuli wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC tungepigwa na kitu kizito vibaya sana.

Ahsanteni Maaskofu wa Katoliki.
Kwani wamefanyaje hao TEC? DP World Yuko pale pale
 
Back
Top Bottom