Mwenye uchungu na bandari isiyowahusu...Waraka usomwe hadi Oktoba 2025
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa
1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)
Nenda kwa Padri Slaa au TEC watakujibu. Humu wajifariji tu, hupati majibuWapi watu wamebishia uwekezaji? Ni vipengele vya kinyonyaji vya mkataba ndio vinaoigiwa kelele, sio uwekezaji..
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa
1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)
2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?
3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?
4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!
6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Usijidai muhuni wewe, uhuni wenu hukohuko pelekaAliyesaini mkataba ule kule Dubai ni mtaalam mbobezi wa sheria za mikataba ya kimataifa.
DP World anakwenda kupangishwa magati namba tano mpaka saba, namba nane mpaka kumi na moja ni mwekezaji mwingine.
Unapolaumu kilichoandikwa kwenye IGA ya serikali na DPW, umewahi kuiona mikataba mingine inayosimamia utekelezaji wa miradi mingi inayoendelea hivi sasa hapa nchini?, unajua nini kimeandikwa humo?.
Tupunguze ujuaji wetu.
We jamaa inaonekana una akili sana, kama si nusu!Aliyesaini mkataba ule kule Dubai ni mtaalam mbobezi wa sheria za mikataba ya kimataifa.
DP World anakwenda kupangishwa magati namba tano mpaka saba, namba nane mpaka kumi na moja ni mwekezaji mwingine.
Unapolaumu kilichoandikwa kwenye IGA ya serikali na DPW, umewahi kuiona mikataba mingine inayosimamia utekelezaji wa miradi mingi inayoendelea hivi sasa hapa nchini?, unajua nini kimeandikwa humo?.
Tupunguze ujuaji wetu.
Mungu amewatumia waziwazi kabisa, tulishaingizwa mjini.Ndugu zangu Watanzania wale madingi wa Katoliki ni miamba sana, wamemaliza ujinga wa DPW.
Muda si mrefu Mama atatema bungo. Tender hiyo, wenye mbavu waipambanie. Ile sheria ya maliasili waliyotaka kubadilisha ili mikataba isipelekwe bungeni juzi nimeona kamati ya bunge ikipinga mapendekezo yote ya serikali. So far ile sheria haijaguswa.
Kama sio msuli wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC tungepigwa na kitu kizito vibaya sana.
Ahsanteni Maaskofu wa Katoliki.
Upo sawa mkuu sema wanaogopa ila kukosoa changamoto za mikataba kisomi ndio maadili na si kukaa kimya harafu vizazi vyao vinaangamia maana ya wao kupata shule ni nini sasa...yaani mikataba ya Nchi inazungumzwa na Wachungaji na Masheihk kweli ?.Ni waajiriwa wa Serikali hao.
Wanaogopa kufutwa kazi, si unajua Maprofesa wetu wanategemea ajira.
Kimaadili Mtumishi wa umma huruhusiwi kumkosoa Raisi wa Nchi hadharani.
Story za midomoni mwa watu, hakuna ushahidi wowote wa kina wa hiki ulichoandika.We jamaa inaonekana una akili sana, kama si nusu!
Hebu tujuze, kwa nini DP Weldi walishinikiza hadi bunge likubali wanunue na rasilmali ardhi za nchi ndipo "ukodishaji" uwe mtamu?
Wengi wanaoandika humu JF hawana biashara yoyote pale bandarini, hawajui wale wenye kusafirisha mizigo wanakutana na kero zipi katika michakato ya shughuli wanazofanya.Usijidai muhuni wewe, uhuni wenu hukohuko peleka
Kwanini msijitengenezee ufanisi nyie wenyewe? Mbona jeshi la Polisi hamjamuita mwekezaji alijengee ufanisi? Kwanini hao DPW hawawezi kuwa kama consultants wa kuwajengea ufanisi TPA?Bandari lazima irudi kwenye ufanisi. Dp World au mwengine lazima awekeze.
CCM wamechagua kuendelea na DP World pale bandarini na huo uchaguzi wa 2025 watashinda vile vile.Ukosahihj kwasababu Tanzania ni wajinga wasingeamini anachosema Lisu au mwabukusi kwa haraka au Dr slaa
Hivyo ,wangepuuzwa kama ulivoona tulia ackson kaazisha ujinga mbeya
Ccm ilikuwa ichague moja izikwe yote au ibakie japo kidogo
Jeshi la polisi ni tofauti na shughuli zinazofanyika pale TPA. Uandishi na mawazo yako kwa ujumla ndio tatizo la uelewa wa nini kinachoendelea katika dunia ya sasa haswa kwenye suala zima la masuala ya bandari.Kwanini msijitengenezee ufanisi nyie wenyewe? Mbona jeshi la Polisi hamjamuita mwekezaji alijengee ufanisi? Kwanini hao DPW hawawezi kuwa kama consultants wa kuwajengea ufanisi TPA?
Hao wataalam mnaowapeleka kusoma nje ya nchi kwa mabilioni ya pesa mnawatumiaje kama mnashindwa kuendesha bandari taasisi za umma kisasa??Jeshi la polisi ni tofauti na shughuli zinazofanyika pale TPA. Uandishi na mawazo yako kwa ujumla ndio tatizo la uelewa wa nini kinachoendelea katika dunia ya sasa haswa kwenye suala zima la masuala ya bandari.
Rahisi kuongea usichokifahamu. Muingereza na mtanzania nani kasomesha zaidi ya mwenzake?, DP World anaendesha bandari mbili pale Uingereza.Hao wataalam mnaowapeleka kusoma nje ya nchi kwa mabilioni ya pesa mnawatumiaje kama mnashindwa kuendesha bandari taasisi za umma kisasa??
Kimya KimyaVipi zile hela walizohonga dp world kwa wauza bandari, zinarudi kwa mfumo upi!
Hiyo sio hoja mkuu, kwa maana nyie ndio mliodai ya kwamba sasa wageni waondoke na mjiendeshe wenyewe miaka ya 1960s ndio mkaita harakati za uhuru. Kiko wapi sasa?? Mliwafukuza ila sasa mnaomba warudi??Rahisi kuongea usichokifahamu. Muingereza na mtanzania nani kasomesha zaidi ya mwenzake?, DP World anaendesha bandari mbili pale Uingereza.
Belgium na Tanzania nani kasomesha kuliko mwenzake?, bandari ya Antwerp inaendeshwa na DP World.
Wametutoa mbaliTEC waseme chochote sasa tutakuwa nao pamoja. Asante TEC kwa kuiokoa nchi.
Kwani wamefanyaje hao TEC? DP World Yuko pale paleNdugu zangu Watanzania wale madingi wa Katoliki ni miamba sana, wamemaliza ujinga wa DPW.
Muda si mrefu Mama atatema bungo. Tender hiyo, wenye mbavu waipambanie. Ile sheria ya maliasili waliyotaka kubadilisha ili mikataba isipelekwe bungeni juzi nimeona kamati ya bunge ikipinga mapendekezo yote ya serikali. So far ile sheria haijaguswa.
Kama sio msuli wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC tungepigwa na kitu kizito vibaya sana.
Ahsanteni Maaskofu wa Katoliki.