Kama sio tajiri na huna asset, kusomesha watoto shule za gharama ni ujinga unaongeza umaskini kwenye ukoo

Kama sio tajiri na huna asset, kusomesha watoto shule za gharama ni ujinga unaongeza umaskini kwenye ukoo

Sehemu.tulipowezwa ni hapa..

Mtoto wako, anakuja kuishi Tanzania hiii hiii unahangaika awe mzungu..hahaha.. na anafundishwa matatizo ya kizungu, kwa lugha ya kizungu..akitoka huko ameshakuwa mzungu anakuja kwa watz mtaani anaanza moja.. 🙂

Na cha kufurahisha ni sisi wazazi ndio tunakuwa tumewanunulia watoto wetu hiyo delay huku mtaani. Elimu tuliyomnunulia ndio imekuwa kikwazo..

Bora kila mwaka ungekuwa unamnunulia mtoto ng'ombe nne ..anasoma shule ya laki tano kwa Temu.. akija kumaliza shule anakuwa na ng'ombe 68 ukiweka kuzaa na kufa hakosi ng'ombe 100 kwenye kipindi cha miaka 16 ya kusomea elimu.

Na elimu yenyewe ndio imekuwa uchuro uchoro mtupu

Dah, yaani umeongea kama wale jamaa wa kulima matikiti kwenye pdf.
 
Ukimsomesha mwanao kayumba mtaani unachekwa,kuna mother mtaani kapanga chumba kimoja halafu anamsomesha mwanae efemu akademia anachukuliwa na gari.......Ni maamuzi tu tuwaache mambo yakiwa magumu watawarudisha KAYUMBA.
Kuna wazazi wanapata stress ikifika kipindi cha kulipa ada mpaka wanatia huruma.
Kuna mtoto amekaa wiki tatu hajaenda shule tatizo ada.
Mwingine alikuwa analalamika hela imekuwa ngumu plus anadaiwa term ya nyuma hivo mtoto hatapokelewa atleast angekuwa anadaiwa mwaka huu mpya wa masomo wangemvumilia kidogo.
Mimi kwakweli nikija jaaliwa kama nikiona maisha yangu tia maji tia maji wala sitaki stress aende tu kayumba nitajitahidi asikose tution na kumsimamia.
Muda mwingine unakuta mtu anateseka na kumhamisha hawezi anawaza walimwengu watamuonaje.
Pata picha una watoto watatu halafu hela yenyew yamawazo lazima akili ikukae sawa.
 
Habari wadau..

January imeisha .. wazazi wengi walikuwa wanalalamika school fees tatizo.

Kwa maoni yangu kama mtu huna mali za kutosha, huna kampuni ya kueleweka wala huna mtaji wa kutosha... baba mzazi wewe mwenyewe unategemea ajira za laki nane ama milioni moja, kusomesha watoto wako shule za gharama sio jambo zuri.

Hakuna CEO Mtanzania ambaye ameajiriwa ambaye hayupo kwenye kampuni ya baba yake kama Mo, ambaye amesoma international schools, ama shule za bei nafuu za kiingereza ambazo tunaita english medium... tukumbuke english medium zipo Tanzania miaka kibao kama IST, Arusha school ama Olimpio.

Kuna CEO wengi wazawa kama Dada CEO wa NMB Ruth Zaipuna ama wa CRDB Majid Nsekela na wengine wengi hawajapita Olimpio wala Arusha schools enzi ambazo wanasoma msingi zilikuwepo tayari ila wamepata nafasi kubwa kwa uwezo wao binafsi wa kazi..

Mzazi ambaye huna hela za kutosha peleka mwanao shule za bei nafuu kisha msimamie mwanao vizuri kila siku mfatilie hela ya ada ya kulipa Tusiime nunua asset unazozimudu mwanao zitamsaidia kuliko kumlipia ada mamilioni.
Kwa laki nane hiyo hiyo,watoto wanasomeshwa shule za English medium,assets zinanunuliwa,na mipango mingine ya siku za usoni inajengwa,na unaposema shule za gharama ilibidi ufanunue,we wakati unaona millioni moja ni pesa kibao kulipa Ada,wenzio wanalipa millioni 3!na huyu wa millioni 3,akifikiri analipa ada kubwa,Kuna watoto wanalipiwa millioni 40! Kwa mwaka,Tanganyika international school!
La muhimu ni kulipa Ada kwa uwiano wa kipato chako,
Wakati mwingine,ada kubwa sio Elimu bora,shule yenye ada ya millioni moja,Dodoma,hapa Dar shule ya kiwango hicho na hadhi ni laki sita tu.
 
Hivi huu msemo Wa eti watoto wanaosoma shule za academics sijui private school eti wanaishia kujua lughatu,mi natofafautiama na we we mkuu,Kijana wangu yuko std seven hizo shule,sikifichi anawa challenge hata majamaa waliosoma hizo ma A level za kata.na wanamkubali mbaya.
Huu ni Uongo, mwanao ni Extra Ordinaly na Sio Sababu ya hizi Shule.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mada gongana....
Kuna wengine wanalazimika kutetea kayumba sababu ya hali za kiuchumi..

Kuna wengine hali za kiuchumi ni mbaya ila wamepeleka watoto shule za gharamaa, wanatetea uamuzi wao kumpiga mtoa mada.

Kuna ambao wanaangalia na Uwezo wa mtoto..

Kuna watu akiona mtoto yupo bright sana ndio anaamua kumpeleka shule za kayumba maana anaona haina haja kuumia ikiwa tayari ana uwezo ambao hauhitaji nguvu kubwa.(hapa ni kubeti, either uokoe pesa kweli au ndio ukamharibu).

Kuna wengine akiona mtoto yupo bright hampeleki mwanae kayumba asije akalemazwa hatimaye anaamua kumpeleka kwenye shule kubwa za private ili akatakate vizuri.

Mwingine atasema mwenye uwezo mdogo mpeleke kayumba asikupotezee hela, Mwingine atasema huyo ndio umpeleka Private ili wambadilishe.
Hapa napo ni kubeti, huko kayumba either ukampoteze zaidi au apate cha uwezo wake uokoe pesa zako,
Private nako either ukapoteze hela zako asibadilike kabisaaa, au kweli Akafanye mapinduzi.


Ni kweli watoto huathiliwa na mazingira kadiri anavyokua, ila hakuna ubishi kuna watoto unaweza kuwatambua uelekeo wao mapema,
Mwingine umempeleka kindergarten tuu ashaanza kufunguka akili anaaza kujitambua mapema.
Mwingine unalazimika kumpeleka mpaka STD 7, 4M4, 4M6 mwingine Chuo,
Ila kuna ambao mpaka anamaliza chuo Hajitambui,

Binafsi naona Hata kama huko mbeleni ataenda serikalini ila angalau mpaka darasa la saba aende english medium umwangalie.

Baada ya hapo kama unawaza kumpeleka serikali basi angalia vitu viwili, Nini umegundua kutoka kwake(japo hapa napo ni mtihani sababu mda mwingi hukua nae?) lakini pia angalia na hio shule pia.

Lakini pia kumpeleka shule za gharamaa mwanzo mwisho halafu chuo anagombania mkopo ambao haukua na lazima mwishowe anapata kazi mkopo unamtesa au anarudi mtaani kabisa, hapo lazima uwaze noti zako.

Binafsi naona kwa dunia ya sasa kila yule kupata elimu ni jambo la kawaida, Mtoto mwenye uwezo mkubwa hasa huyo ndio wa kumgharamikia hasa kwenye elimu,

Sio tuu mfano mwenye uwezo wa div 1, maana hii ni kawaida, hapa namaanisha unaona kabisa huyu ana cha ziada zaidi ya hapo.
 
Unafiki wa siasa za afrika wanaosema hiz shule ni nzuri Sana watoto wao hawasomi huko sasa utajiuliza huyu anasimamia hiz shule na kuzisifia kuwa zipo vizuri mbona hampeleki mwanae....Unafiki wa muafrika
 
Huu ni Uongo, mwanao ni Extra Ordinaly na Sio Sababu ya hizi Shule.....

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu baadhi ya shule za private zina makusudi sana,yani wanatafuta kuzipatia shule sifa katika ufaulu ili wapate wateja.

Ila mkuu usijali mi mwenyewe ni zao la shule za kata,kwa hivyo nimeona utofauti kwa kweli.ingawa sio shule zote ziko vizuri.
 
huyo kijana wako anakutana na A level vilaza mkuu, tena A level wa masomo ya Art. Lakini A level wanaosoma sayansi physics, chemistry, math, biology haya masomo hayahitaji ujue kiingereza ni kumeza kwako kanuni, michoro, kukokotoa hesabu, na kuzikuma projectile, hapo kama huna akili ya kuzaliwa hata uwe ujue kiinglish kichwa kinagoma tu.
Anakutana na A level waliosoma kuanzia la kwanza hadi form six shule za kata,ila wale waliotoka shule za private wakaenda A level shule za sirikali hao nadhani hajakutana nao maana watakuwa vizuri mkuu.
 
Hivi huu msemo Wa eti watoto wanaosoma shule za academics sijui private school eti wanaishia kujua lugha tu, mi natofautiana na wewe mkuu, Kijana wangu yuko std seven hizo shule, sikifichi anawa challenge hata majamaa waliosoma hizo ma A level za kata na wanamkubali mbaya.
Angalia huyu mshamba mwingine huku duniani, watu wanamaanisha maisha ya mtu baadae pamoja na kusoma hizo english school na mtu aliyesoma kayumba,ukweli ni kwamba watu wa kayumba wengi ndo utakuta wanatoboa maisha, hawa wa kwenu ambo unakuta wanasoma wengine mihula ya uingereza huishiaga kwenye ubishoo tu na wanatafuta kwenda kufanya kazi nje, kule ukubwani au uzeeni wanarudi na mikogo tu ya kutembea wametanua mikono na miwani ya jua machoni huku wameacha kizazi chao kikiishi utumwani ugenini na kua wamekimbia aridhi ya uzao wao,endelea kumsifia wa kwako bado yuko darasa la 7, huyo siyo jiwe anakua, akikua utaona kitakacho tokea labda tu awe amezaliwa na utashi wa asili, vinginevyo utajuta tu maana tumewaona wengi kwenye familia na majirani
 
Uhakika wa kufaulu upo kwenye private schools. Pitia matokeo shule za serikali. Hali ni mbaya.
hayo maneno ya "ufaulu umeongezeka" yasikie hivyo hivyo
Kufaulu maisha?
 
Mimi namtazamo mwingine japo sitofauti sana na wewe, mimi naona ni vyema kipindi hichi wazazi wenye kipato cha kawaida wakawa na malengo ya kuja kuwekeza zaidi kwa watoto wao kwenye elimu ya juu huku chini hakuna haja sana sababu watoto wanaishia kujua lugha tu.
Hata kiingereza chenyewe wanachokijua si kwa kiwango hicho kwani hata Waalimu wanaowafundisha wanababaisha tu. Mi nazani wazazi wengi wanafuata mkumbo tu ila sizani km wanafanya tathmini ya gharama za huo uwekezaji.

Mbaya zaidi mfumo wetu wa ajira unaangalia sana ufauru wa kwenye cheti bila kujali kujua au kutokujua kiingereza.
 
Angalia huyu mshamba mwingine huku duniani, watu wanamaanisha maisha ya mtu baadae pamoja na kusoma hizo english school na mtu aliyesoma kayumba,ukweli ni kwamba watu wa kayumba wengi ndo utakuta wanatoboa maisha, hawa wa kwenu ambo unakuta wanasoma wengine mihula ya uingereza huishiaga kwenye ubishoo tu na wanatafuta kwenda kufanya kazi nje, kule ukubwani au uzeeni wanarudi na mikogo tu ya kutembea wametanua mikono na miwani ya jua machoni huku wameacha kizazi chao kikiishi utumwani ugenini na kua wamekimbia aridhi ya uzao wao,endelea kumsifia wa kwako bado yuko darasa la 7, huyo siyo jiwe anakua, akikua utaona kitakacho tokea labda tu awe amezaliwa na utashi wa asili, vinginevyo utajuta tu maana tumewaona wengi kwenye familia na majirani
OK.
Ndio wanatoboa maisha,na wanakua viongozi kweli hebu angalia wanakotupeleka kama taifa kimataifa yani ni aibu tupu.

Hii nchi sa hivi hata wewe ukitoka nje ya nchi huwezi tembea kifua mberee kuwa unajivunia utanzania,katika east Africa sa hivi Rwanda wanatupita.
 
Hivi huu msemo Wa eti watoto wanaosoma shule za academics sijui private school eti wanaishia kujua lugha tu, mi natofautiana na wewe mkuu, Kijana wangu yuko std seven hizo shule, sikifichi anawa challenge hata majamaa waliosoma hizo ma A level za kata na wanamkubali mbaya.

Sikuelewi unaposema mtoto wako wa Std 7 medium School Ana m Challenge Mtu wa A Level za Kata !!!
Mtu wa Combination gani ipi hasa.
Kweli?
 
Back
Top Bottom