Kama ulianza kutumia Internet mapema miaka ya 1990 na 2000 njoo hapa tukumbushane Internet Cafe tulizoenda, Vimbwanga, Kero na Kumbukumbu

Kama ulianza kutumia Internet mapema miaka ya 1990 na 2000 njoo hapa tukumbushane Internet Cafe tulizoenda, Vimbwanga, Kero na Kumbukumbu

Nilifanya utundu kwenye time watcher mhindi akanishtukia akasema usije tena hapa, wewe itafundisha na nyingine.
 
MUHIMU: UZI HUU SIO WA KUKUMBUSHANA COMPUTER GAMES

Binafsi nilianza kwenda Internet cafe 2002, computer zilikuwa zenye visogo 😂 .
View attachment 2648381


Mitanado maarufu kwa hapa bongo ilikuwa ni Marafiki.com na DarHotwire, baadae zikaja Jamboforums (kwa sasa jamiiforums), Hi5, Bongo 5,
View attachment 2654435


tulikuwa tunalipia kwa muda kuanzia nusu saa, Ukilipia wanawasha program ya kuhesabu muda, iliitwa time watcher muda ukiisha inaloki computer, Wajanja walikuja na mbinu za kuruka hiki kiunzi 😂
View attachment 2654432


Speed ilikuwa chini sana, kufungua ukurasa wenye picha unaweza subiri dakika nzima, ukitaka soeed nenda asubuhi sana.
View attachment 2654433


Kuwa na email ilikuwa ndio ujanja wa enzi hizo, Tulichat na kutumiana barua kwa email. katika watu 100 waweza jikuta pekeyako unayo basi unapata ka feeling flani ka v.i.p, email maaarufu ilikuwa hotmail, yahoo na msn.
View attachment 2654431


Enzi hizo tulitumia floppy disk kuhifadhi mafaili, ni kipindi ambacho bado cd na flash hazijawa common.
View attachment 2654434


Enzi hizo websites www.-----.com ilibidi uwe uzitunze kichwani ama uwe na ki diary maalum, Sio kama sasa google imerahisisha sana
View attachment 2654446


Waliokuwa hawana speed ya kutumia keyboard. walijifunza kwa kutumia program inaitwa mavis bacon
View attachment 2654448

///////////////////////////////////////

Hali imebadilika, kwa sasa unaweza kuwa na smartphone au laptop yako unaingia net, Hali haikuwa hivyo kwa miaka ya nyuma kabla ya 2010s, Kipindi hicho ilikuwa ni mwendo wa cafe.

Miaka ya 2007 angalau tulianza kutumia internet kwenye simu za Nokia batani na tovuti maarufu ilikuwa waptrick lakini hizi tobuti bado zilikuwa simple sana, bado tulilazimika kwenda internet cafes kupata mambo kamili,

2010s ndio Modems za kutumia kwenye laptops na simu za kisasa zaidi zenye uwezo mkubwa wa kuperuzi internet zilipoanza kujaa sokoni ndipo wengi tukaacha kwenda internet cafe na hii ikapelekea cafes nyingi kufungwa ama kugeuzwa kuwa stationery.
Mhudumu anakwambia marufuku kuangalia pono!
 
A
MUHIMU: UZI HUU SIO WA KUKUMBUSHANA COMPUTER GAMES

Binafsi nilianza kwenda Internet cafe 2002, computer zilikuwa zenye visogo 😂 .
View attachment 2648381


Mitanado maarufu kwa hapa bongo ilikuwa ni Marafiki.com na DarHotwire, baadae zikaja Jamboforums (kwa sasa jamiiforums), Hi5, Bongo 5,
View attachment 2654435


tulikuwa tunalipia kwa muda kuanzia nusu saa, Ukilipia wanawasha program ya kuhesabu muda, iliitwa time watcher muda ukiisha inaloki computer, Wajanja walikuja na mbinu za kuruka hiki kiunzi 😂
View attachment 2654432


Speed ilikuwa chini sana, kufungua ukurasa wenye picha unaweza subiri dakika nzima, ukitaka soeed nenda asubuhi sana.
View attachment 2654433


Kuwa na email ilikuwa ndio ujanja wa enzi hizo, Tulichat na kutumiana barua kwa email. katika watu 100 waweza jikuta pekeyako unayo basi unapata ka feeling flani ka v.i.p, email maaarufu ilikuwa hotmail, yahoo na msn.
View attachment 2654431


Enzi hizo tulitumia floppy disk kuhifadhi mafaili, ni kipindi ambacho bado cd na flash hazijawa common.
View attachment 2654434


Enzi hizo websites www.-----.com ilibidi uwe uzitunze kichwani ama uwe na ki diary maalum, Sio kama sasa google imerahisisha sana
View attachment 2654446


Waliokuwa hawana speed ya kutumia keyboard. walijifunza kwa kutumia program inaitwa mavis bacon
View attachment 2654448

///////////////////////////////////////

Hali imebadilika, kwa sasa unaweza kuwa na smartphone au laptop yako unaingia net, Hali haikuwa hivyo kwa miaka ya nyuma kabla ya 2010s, Kipindi hicho ilikuwa ni mwendo wa cafe.

Miaka ya 2007 angalau tulianza kutumia internet kwenye simu za Nokia batani na tovuti maarufu ilikuwa waptrick lakini hizi tobuti bado zilikuwa simple sana, bado tulilazimika kwenda internet cafes kupata mambo kamili,

2010s ndio Modems za kutumia kwenye laptops na simu za kisasa zaidi zenye uwezo mkubwa wa kuperuzi internet zilipoanza kujaa sokoni ndipo wengi tukaacha kwenda internet cafe na hii ikapelekea cafes nyingi kufungwa ama kugeuzwa kuwa stationeryh
A-Tech Njombe
 
Marafiki com
Ku chat na wajuba

Wote mnaondikaga chart badala ya chat mlaaniwe.
 
Dah nimetumia sana Cafe, enzi hizo ni dialup, Raha Tower, pale Samora na Mission Street, Bibi Titi x Morogoro sasa hivi ni City Mall kulikuwa na shule ya computer pale, Cafe kibao uindini na floppy zangua za 1.4 MB ukitaka kudownload game inabidi uigawanye vipande kumi kila moja na floppy yake, ukifika home floppy ya 5 imekufa! Siku mambo yakawa yes nikanunua Zip Drive kitu kilikuwa kinabeba 100MB, kama mfalme mjini!
 
Enzi za Computer Window 95. ndio atleast ilikuwa speed nafuu.. Window 486 ilikuwa Jau sana Cafe' ni kusubiri tu Game ifunguke ucheze.

Nakumbuka kuna uvumi wa kupata kazi New Caledonian Offshore na website yao so lazima ujisajili and ukimaliza wanakutumia na barua na documantations zote Mshahara mnono kuvuna mafuta na Gas maisha ya baharini..

Yahoo,MSN Messenger,Darhotwire,IPP Media,Darchat,Jambonet,Marafiki dotcom,Zanzibar chat, ESPN, NBA ,Livescore kila siku baadae huko ZEUtamu dot com wakaja kuharibu na edit photo ya jk.. somebody mtoto wa kigogo alikuja kamatwa .

Email zote nilifungua chache niliziacha

Hivi yule jamaa wa Jambo Mod alijiita Invisible aliishia wapi. mkuda yule
 
Daah,nimekumbuka mbali sana, nilianzia TipTop manzese 2002, nikahania Seaboys Magomeni Mapipa, baadaye nikahania cafe ya UDSM block 7, tatizo la hii cafe ya UDSM ni comp nyingine kutokuwa na mouse,unakomaa na keyboard tu ila ilikuwa na speed nzuri.
 
Daah,nimekumbuka mbali sana, nilianzia TipTop manzese 2002, nikahania Seaboys Magomeni Mapipa, baadaye nikahania cafe ya UDSM block 7, tatizo la hii cafe ya UDSM ni comp nyingine kutokuwa na mouse,unakomaa na keyboard tu ila ilikuwa na speed nzuri.
Cafèe ya UDSM mizinguo. Haina privacy wa kunicheki 'MIPICHA' yetu.
Pale Seaboys na ile nyinge upande wa pili Magomeni zilikuwa na Privacy partition ya Internet.
Hatari sana.
'MZIBO'.net ilikuwa hatari sana na DarhotWire..!
 
Back
Top Bottom