Kama ulianza kutumia Internet mapema miaka ya 1990 na 2000 njoo hapa tukumbushane Internet Cafe tulizoenda, Vimbwanga, Kero na Kumbukumbu

Kama ulianza kutumia Internet mapema miaka ya 1990 na 2000 njoo hapa tukumbushane Internet Cafe tulizoenda, Vimbwanga, Kero na Kumbukumbu

Matunda cafe Moro nilikuwa natoroka shule kwenda kujibu email za rafiki yangu aliyekuwa abroad 🤣🤣🤣
 
MUHIMU: UZI HUU SIO WA KUKUMBUSHANA COMPUTER GAMES

Binafsi nilianza kwenda Internet cafe 2002, computer zilikuwa zenye visogo 😂 .
View attachment 2648381


Mitanado maarufu kwa hapa bongo ilikuwa ni Marafiki.com na DarHotwire, baadae zikaja Jamboforums (kwa sasa jamiiforums), Hi5, Bongo 5,
View attachment 2654435


tulikuwa tunalipia kwa muda kuanzia nusu saa, Ukilipia wanawasha program ya kuhesabu muda, iliitwa time watcher muda ukiisha inaloki computer, Wajanja walikuja na mbinu za kuruka hiki kiunzi 😂
View attachment 2654432


Speed ilikuwa chini sana, kufungua ukurasa wenye picha unaweza subiri dakika nzima, ukitaka soeed nenda asubuhi sana.
View attachment 2654433


Kuwa na email ilikuwa ndio ujanja wa enzi hizo, Tulichat na kutumiana barua kwa email. katika watu 100 waweza jikuta pekeyako unayo basi unapata ka feeling flani ka v.i.p, email maaarufu ilikuwa hotmail, yahoo na msn.
View attachment 2654431


Enzi hizo tulitumia floppy disk kuhifadhi mafaili, ni kipindi ambacho bado cd na flash hazijawa common.
View attachment 2654434


Enzi hizo websites www.-----.com ilibidi uwe uzitunze kichwani ama uwe na ki diary maalum, Sio kama sasa google imerahisisha sana
View attachment 2654446


Waliokuwa hawana speed ya kutumia keyboard. walijifunza kwa kutumia program inaitwa mavis bacon
View attachment 2654448

///////////////////////////////////////

Hali imebadilika, kwa sasa unaweza kuwa na smartphone au laptop yako unaingia net, Hali haikuwa hivyo kwa miaka ya nyuma kabla ya 2010s, Kipindi hicho ilikuwa ni mwendo wa cafe.

Miaka ya 2007 angalau tulianza kutumia internet kwenye simu za Nokia batani na tovuti maarufu ilikuwa waptrick lakini hizi tobuti bado zilikuwa simple sana, bado tulilazimika kwenda internet cafes kupata mambo kamili,

2010s ndio Modems za kutumia kwenye laptops na simu za kisasa zaidi zenye uwezo mkubwa wa kuperuzi internet zilipoanza kujaa sokoni ndipo wengi tukaacha kwenda internet cafe na hii ikapelekea cafes nyingi kufungwa ama kugeuzwa kuwa stationery.
Sea boyz Magomeni, Kariakoo karibu na msikiti wa Manyema, Morogoro rd karibu na kituo cha mafuta opp na Mtendeni Pr Schoo, Posta Kisutu na mwisho kabisa Stambuli Cafe millenium tower Makumbusho. Nyingi ya hizi cafe zilimilikiwa ama na wahindi au waarabu. Mimi nilijifunzia kompyuta kitambo sana nj ya nchi, na niliporudi nilikuwa mwamba kweli kwani watu wachache sana ndio walikuwa wanajua kutumia kompyuta na hata pia waliokuwa na anuani za email walikuwa wachache sana.
 
Umenikumbusha mbali sana nilikuwa na dogde tuition naenda internet cafe kucheza need for speed,mortal combat,vice city,san andreas,project IGI na muda ukifika nami nageuka zangu kama nimetoka tution kumbe nimetok internet cafe....kuna siku game zilinoga mpaka nikasahau muda wa kurudi nyumbani kiza kikawa kinene mno.....kilichonikuta nitakuja kusimulia nikirudi🏃‍♀️
 
Internet nilikuwa na Access free, kwa rafiki yangu SALCOM internet Cafe.
 
Waptrick (Hapa ukitaka miziki ya zamani mingi utaikuta humu);

Wapdam (hii ilikuw kama substitute);

Redwap (Hapa nilikuw natafuta sana WARUMI ukitaka kuwaona unaingia humo);

Ikaja TUBIDY (hii kudownload videos za nyimbo etc)

Nakumbuka enzi hizo kulikuw hakuna kujiunga BANDWIDTH ya MB's ni kuweka VOCHA alafu iliwe mdg mdg...

Facebook ilikuja kutakeover nakumbuka mpk hii leo nimemiliki account si chini ya 5 kule😅.. ikaja whatsapp then instagram..

Pia kuna kipindi hapo kati kulikuw na mvumo wa movies za kihindi, na kinaijeria. Pia nyimbo za kihindi ktk simu za kichina ndio zikawa zinatrend hasa...

Aisee kitambo.. NOTE: simu nimeanza kutumia nikiwa na 7 yrs, sahiv nipo under 30 yrs.. account yangu ya JF ya kwanza nimefungua 2013..😅
 
Back
Top Bottom