Kama ulianza kutumia Internet mapema miaka ya 1990 na 2000 njoo hapa tukumbushane Internet Cafe tulizoenda, Vimbwanga, Kero na Kumbukumbu

Kama ulianza kutumia Internet mapema miaka ya 1990 na 2000 njoo hapa tukumbushane Internet Cafe tulizoenda, Vimbwanga, Kero na Kumbukumbu

sea boyz na sinza pale moli

facebook na yahoo ndiyo ilipiga pesa za cafe.
 
Enzi hizo tulikuwa tukizima au kureset timewatcher na Task manager mpaka tukawa tunatimuliwa café. Ilikuwa ni mwendo wa miniclip.com facebook na gmail. Ukiwa kwenye simu ni waptrick au phonerotica 😄😄😄😄. Kipindi cha 2010's bando la 500 unlimited tunatoboa nalo kwenye torrents na porn
 
Mleta mada kasema 1990 to 2000. Sasa wengine wanakuna na 2007.
1990 ulitumia INTERNET computer wapi
Even MAREKANI internet ilikuwa PUBLIC kuanzia miaka 1995
TANZANIA internet zilipamba moto baada ya Y2K 2000 ndo cafe nyingi ,Zikamwagika mtaan na mikoani
Chini ya hapo Cafe ilikuwa POSTA na kipande Cha MNAZI MMOJA even kkoo yenyewe ilikuwa hakuna INTERNET CAFE mpk kuanzia MNAZI mmoja
 
Enzi hizo tulikuwa tukizima au kureset timewatcher na Task manager mpaka tukawa tunatimuliwa café. Ilikuwa ni mwendo wa miniclip.com facebook na gmail. Ukiwa kwenye simu ni waptrick au phonerotica [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]. Kipindi cha 2010's bando la 500 unlimited tunatoboa nalo kwenye torrents na porn
Hivi phonerotica imefia wapi
 
Kuna mtu ali chat kwa ICQ hapa ??

Hiii ni ya wachache - ogopaaaa.
 
2010s ndio Modems za kutumia kwenye laptops na simu za kisasa zaidi zenye uwezo mkubwa wa kuperuzi internet zilipoanza kujaa sokoni ndipo wengi tukaacha kwenda internet cafe na hii ikapelekea cafes nyingi kufungwa ama kugeuzwa kuwa stationery.
Usisahau sheria mpya ngumu za makosa ya mitandaoni na sheria ya Posta zilikuja kuuwa internet cafe.
Mfano kuweka CCTV camera ndani ya cafe kila kwenye workstation ya computer.
Kulipia pesa ndefu na kuwajibika kwa baadhi ya makosa kwa mmiliki.
Fikiria mtu amepoteza SIM Card yupo mjini anataka kufanya mawasiliano au kuchukua copy ya documents zake zilizo kwenye Google drive au cloud yoyote.
Au mgeni amekuja tu hajasajili SIM card atahitaji internet cafe.
 
UCC UDSM Mlimani, Ubungo Hostel karibu na RUBADA nilipata girlfriend sababu ya internet surfing.
 
1990 ulitumia INTERNET computer wapi
Even MAREKANI internet ilikuwa PUBLIC kuanzia miaka 1995
TANZANIA internet zilipamba moto baada ya Y2K 2000 ndo cafe nyingi ,Zikamwagika mtaan na mikoani
Chini ya hapo Cafe ilikuwa POSTA na kipande Cha MNAZI MMOJA even kkoo yenyewe ilikuwa hakuna INTERNET CAFE mpk kuanzia MNAZI mmoja
Mm nimetumia internet 1997 dar es salaam. Nikiwa na us robotics modem 56k/sec.
 
Pale maduka mawili kulikuwa na internet Cafe miaka ya 2000 nilikuwa naenda kutuma na kusoma email
 
Mwaka 2009/2010 nilikuwa natumia simu kuingia facebook sasa simu nilikuwa natumia ya sista angu nilivyomrudishia simu yake nikamiss kuperuzi. Siku hiyo nikaenda internet cafe basi nikaingia zangu FB kumbe huyo mzee apita pita kuchungulia alivyoona nipo FB aisee alifoka eti mambo gani hayo ya kihuni huni watoto wa siku hizi sijui mpoje aisee nilinyanyuka nikasepa zangu kimya kimya.
Bila shaka kama bado yupo atagundua alizingua sana.
 
MUHIMU: UZI HUU SIO WA KUKUMBUSHANA COMPUTER GAMES

Binafsi nilianza kwenda Internet cafe 2002, computer zilikuwa zenye visogo 😂 .
View attachment 2648381


Mitanado maarufu kwa hapa bongo ilikuwa ni Marafiki.com na DarHotwire, baadae zikaja Jamboforums (kwa sasa jamiiforums), Hi5, Bongo 5,
View attachment 2654435


tulikuwa tunalipia kwa muda kuanzia nusu saa, Ukilipia wanawasha program ya kuhesabu muda, iliitwa time watcher muda ukiisha inaloki computer, Wajanja walikuja na mbinu za kuruka hiki kiunzi 😂
View attachment 2654432


Speed ilikuwa chini sana, kufungua ukurasa wenye picha unaweza subiri dakika nzima, ukitaka soeed nenda asubuhi sana.
View attachment 2654433


Kuwa na email ilikuwa ndio ujanja wa enzi hizo, Tulichat na kutumiana barua kwa email. katika watu 100 waweza jikuta pekeyako unayo basi unapata ka feeling flani ka v.i.p, email maaarufu ilikuwa hotmail, yahoo na msn.
View attachment 2654431


Enzi hizo tulitumia floppy disk kuhifadhi mafaili, ni kipindi ambacho bado cd na flash hazijawa common.
View attachment 2654434


Enzi hizo websites www.-----.com ilibidi uwe uzitunze kichwani ama uwe na ki diary maalum, Sio kama sasa google imerahisisha sana
View attachment 2654446


Waliokuwa hawana speed ya kutumia keyboard. walijifunza kwa kutumia program inaitwa mavis bacon
View attachment 2654448

///////////////////////////////////////

Hali imebadilika, kwa sasa unaweza kuwa na smartphone au laptop yako unaingia net, Hali haikuwa hivyo kwa miaka ya nyuma kabla ya 2010s, Kipindi hicho ilikuwa ni mwendo wa cafe.

Miaka ya 2007 angalau tulianza kutumia internet kwenye simu za Nokia batani na tovuti maarufu ilikuwa waptrick lakini hizi tobuti bado zilikuwa simple sana, bado tulilazimika kwenda internet cafes kupata mambo kamili,

2010s ndio Modems za kutumia kwenye laptops na simu za kisasa zaidi zenye uwezo mkubwa wa kuperuzi internet zilipoanza kujaa sokoni ndipo wengi tukaacha kwenda internet cafe na hii ikapelekea cafes nyingi kufungwa ama kugeuzwa kuwa stationery.
Ze utamu 2009 ivi hatari
Kulikuwa na Dar talk(something km hivi), kabla ya facebook kulikuwa na Skype.. kulikuwa na BBM MESSENGER ilikuwa kama WhatsApp vile, thanks kwa mchina kuleta hizi simu maana ilikuwa ukidownlpad hata media yenye mb 10 tu inakuandikia 36 years to complete!!😂
Ze utamu 2009 ivi hatari
 
Nakumbuka niliingia kwenye Cafe moja pale Sinza nikalipia mda wa lisaa limoja nilipo kaa kwenye dawati monitor niliiona lakini keyboard sikuwa naiona,nikapanic,sikuweza kumuuliza mhudumu au niliokaa nao jirani nikaogopa wasije wakaniona ni mshamba,ilinigharomu robo saa nzima kuiona ilipo kumbe keyboard ilikuwa imetengenezewa draw nyembamba sana ambayo ukiangalia kwa haraka huwezi igundua kama ipo pale chini ya meza.
 
Bagamoyo kulikuwa na Internet Cafe mitaa ya ADEM, Nilikuwa naenda kuperuzi ngoma kali za mamtoni pamoja na SMS kali za mitongozo kisha nazituma kwa watoto wa kishua mitaa ya mbezi beach.

Bila kusahau kusearch jinsi ya kupata pesa bila kufanya kazi. Ki ukweli internet cafe ilinipa maujanja na nilipiga pesa kwa wale wakuja. Wazungu wa Bagamoyo walinipata vema mzanaki mimi.
Kupata pesa bila kufanya kazi😅😅
 
MUHIMU: UZI HUU SIO WA KUKUMBUSHANA COMPUTER GAMES

Binafsi nilianza kwenda Internet cafe 2002, computer zilikuwa zenye visogo 😂 .
View attachment 2648381


Mitanado maarufu kwa hapa bongo ilikuwa ni Marafiki.com na DarHotwire, baadae zikaja Jamboforums (kwa sasa jamiiforums), Hi5, Bongo 5,
View attachment 2654435


tulikuwa tunalipia kwa muda kuanzia nusu saa, Ukilipia wanawasha program ya kuhesabu muda, iliitwa time watcher muda ukiisha inaloki computer, Wajanja walikuja na mbinu za kuruka hiki kiunzi 😂
View attachment 2654432


Speed ilikuwa chini sana, kufungua ukurasa wenye picha unaweza subiri dakika nzima, ukitaka soeed nenda asubuhi sana.
View attachment 2654433


Kuwa na email ilikuwa ndio ujanja wa enzi hizo, Tulichat na kutumiana barua kwa email. katika watu 100 waweza jikuta pekeyako unayo basi unapata ka feeling flani ka v.i.p, email maaarufu ilikuwa hotmail, yahoo na msn.
View attachment 2654431


Enzi hizo tulitumia floppy disk kuhifadhi mafaili, ni kipindi ambacho bado cd na flash hazijawa common.
View attachment 2654434


Enzi hizo websites www.-----.com ilibidi uwe uzitunze kichwani ama uwe na ki diary maalum, Sio kama sasa google imerahisisha sana
View attachment 2654446


Waliokuwa hawana speed ya kutumia keyboard. walijifunza kwa kutumia program inaitwa mavis bacon
View attachment 2654448

///////////////////////////////////////

Hali imebadilika, kwa sasa unaweza kuwa na smartphone au laptop yako unaingia net, Hali haikuwa hivyo kwa miaka ya nyuma kabla ya 2010s, Kipindi hicho ilikuwa ni mwendo wa cafe.

Miaka ya 2007 angalau tulianza kutumia internet kwenye simu za Nokia batani na tovuti maarufu ilikuwa waptrick lakini hizi tobuti bado zilikuwa simple sana, bado tulilazimika kwenda internet cafes kupata mambo kamili,

2010s ndio Modems za kutumia kwenye laptops na simu za kisasa zaidi zenye uwezo mkubwa wa kuperuzi internet zilipoanza kujaa sokoni ndipo wengi tukaacha kwenda internet cafe na hii ikapelekea cafes nyingi kufungwa ama kugeuzwa kuwa stationery.
Rcl cafe kisutu street walikula sana pesa yangu late 90z
 
Back
Top Bottom