Kama ulihisi UVCCM Simiyu ni kiboko, hebu angalia hawa UVCCM Mkoa wa Mara wakigawana rushwa hadharani

Ndo tutegemee uchaguzi huru na haki kwa msingi huu?
 
Mkuu unajuaje kama hiyo ni rushwa na wala si posho za mkutano?
Kama nilivyosema awali nimefuatilia kwanza ndio nikaipost, hakuna posho ya aina yoyote iliyotolewa siku hiyo ya uchaguzi.
 
Alafu mbona kama wanagawana elfu kumikumi au ishirini ishirini hivi...hela mbuzi kabisa.
 
Ishu sio kuandamana bali unaandamana kwa ajili ya nini??

Sidhani kama sisi ni waoga kiasi hicho ila nadhani ni kukosa ajenda ya pamoja ya kutufanya tuandamane.
Baadhi yetu ukosefu wa kitu fulani ni fursa kwa wengine, hivyo wanatamani kiendelee kuadimika wafanye biashara. Na bahati mbaya zaidi unakuta hicho kitu kinawanufaisha watu wengi mno hivyo kua na unafiki ndani yake harakati zikianza.

Mfano ishu ya maji, walalamikaji ni waishio mijini ambapo maji yalikua yakipatikana lakini mikoa mingine maji sio tatizo kabisa mfano Mbeya, hivyo mtu wa Mbeya kulalamikia maji sio rahisi coz hajui ugumu wa kuyapata.

Mfumuko wa bei, wafanyabiashara wengi wananufaika na hiki kitu japo kwa nje wanalaumu ila deep down wanafaidi sana baadhi yao.

Tatizo tunakosa hiyo sababu ya kuwatoa watu majumbani, labda ule uchaguzi wa 2015, kama chadema ingeamua mbwai na iwe mbwa watu wangejitoa coz ilikua ishu inayojumuisha watu wengi mno.

Uchaguzi wa 2020 asngetoka mtu, tayari watu maslahi waliyaweka mbele.
 
na waliopo pichani tunawajua kwa sura na majina yao aibu hizi huku kwetu Mara hazikuwepo
 
na waliopo pichani tunawajua kwa sura na majina yao aibu hizi huku kwetu Mara hazikuwepo
Nafikiria chama kitachukua hatua stahiki kwa haya yaliyojitokeza, mtoa rushwa na hao mnaowafahamu waliopo pichani
 
Hii ilitosha Kwa Chama makini kufuta uchaguzi wote.

Halafu ktk haya yakiendelea Eti Kuna watu wanataka tumtetee mkt kuwa "Anaupiga mwingi'' eti'
 
Hii ilitosha Kwa Chama makini kufuta uchaguzi wote.

Halafu ktk haya yakiendelea Eti Kuna watu wanataka tumtetee mkt kuwa "Anaupiga mwingi'' eti'
Ni kweli chama makini hakiwezi kuruhusu haya. Ukisema ukweli unaonekana umeisaliti nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…