Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Kabisa mkuu.
SA inapaswa kufanyia kazi hilo.
Wanaiharibu anchi na reputation yake ni mbovu sana.

Watengeneze kitengo maalumu cha ku deal na hao wahalifu.
Wamalizwe kabisa, hakuna cha mahakamani.
Ukkamatwa kwenye uhalifu hakuna kurudi uraiani ni kwenda mazima.
Kaka wewe tulia. Baada ya mwaka mmoja kuanzia sasa nchi itakuwa salama kuliko wakati mungine wowote uliopita. Waziri wa mambo ya ndani ni kaburu. Aisee huyo jamaa noma. Muulize mtu yoyote aliepo hapa akwambie kinachoendelea.

Kuna misako na operation inayofanyika nchi nzima haswa siku za weekend kuanzia ijumaa kama leo. Mkikutwa wanaume wa3 ndan ya gari au wawili lkn mpo mpo tu mnashushwa na kusachiwa nyinyi na gari lenu. Kijana ukiwa na kibegi kisichoeleweka unasimamishwa na kusachiwa. Kuna baadhi ya maeneo ya hatari kuanzia saa 2 usiku wanatembea wazee wa kuvaa kiraia. Wakikuotea unazurura zurura bila mpango hiyo imekula kwako.

Wale wahamiaji haram, wauza madawa na wahalifu wengine wote kwa sasa wanaishi matumbo joto.
 
Kaka wewe tulia. Baada ya mwaka mmoja kuanzia sasa nchi itakuwa salama kuliko wakati mungine wowote uliopita. Waziri wa mambo ya ndani ni kaburu. Aisee huyo jamaa noma. Muulize mtu yoyote aliepo hapa akwambie kinachoendelea.

Kuna misako na operation inayofanyika nchi nzima haswa siku za weekend kuanzia ijumaa kama leo. Mkikutwa wanaume wa3 ndan ya gari au wawili lkn mpo mpo tu mnashushwa na kusachiwa nyinyi na gari lenu. Kijana ukiwa na kibegi kisichoeleweka unasimamishwa na kusachiwa. Kuna baadhi ya maeneo ya hatari kuanzia saa 2 usiku wanatembea wazee wa kuvaa kiraia. Wakikuotea unazurura zurura bila mpango hiyo imekula kwako.

Wale wahamiaji haram, wauza madawa na wahalifu wengine wote kwa sasa wanaishi matumbo joto.
South Africa ili kuukomesha uhalifu wangefanya operation km aliyofanya raisi wa el Salvador ...inatakiwa wapige msako nchi nzima kukamata wahalifu halafu wanapelekwa kambi maalum yenye mchakamchaka kama jeshini wakaw huko hata miaka mitano wakifundishwa stadi mbalimbali za ufundi wakirudi mtaani watumie ujuzi wao kujiajiri.
 
Kuna group la mabaharia(Sailsman) Facebook admin ni MSANGI. Aisee .........kilasiku MAITI zinatangazwa. Wengi ni bomba au madawa. Inamaana South Africa Kuna Watanzania wengi kuliko Tanzania?
Wahuni nnya wakiona Msangi anawachana na kuwasaidia wanammaind utasikia" anachoresha kiwanja " huyo anayesema anachoreshwa kachoka kuliko kichaaa wa kwenye madampo ya bongo basi tu
 
South Africa ili kuukomesha uhalifu wangefanya operation km aliyofanya raisi wa el Salvador ...inatakiwa wapige msako nchi nzima kukamata wahalifu halafu wanapelekwa kambi maalum yenye mchakamchaka kama jeshini wakaw huko hata miaka mitano wakifundishwa stadi mbalimbali za ufundi wakirudi mtaani watumie ujuzi wao kujiajiri.
Mkuu unajua kila uongozi una stahili yake ya kutawala. Lakini vilevile hiyo style unayosema haiwezi kuwa dawa ya moja kwa moja ya tatizo, ila itasaidia tu kupunguza uhalifu uliokuwepo au uliopo.

Nasema hivyo kwa sababu hata hizo nchi ambazo unazitolea mfano, watu walikuwa wanauwawa kila siku lakini bado watu wanaendelea kuingiza na kuuza madawa. Yani serikali inanyonga hawa kesho wanaibuka wengine, mpaka Marekani, Ulaya na watu wa haki za binadam wakaamua kuingilia kati baada ya kuona kuwa njia inayotumika haimalizi tatizo, sema tu inaongeza vifo vya watu kila siku.

Na hapa mkaburu anaweza kufanya zaidi ya hayo uliyosema. Nafikiri unafaham vizuri historia ya makaburu kwa watu weusi, lakin sasa serikali haipo kwenye mikono yao. Na pia sheria zilizopo sasa haziruhusu hayo kufanyika. Ila hata hivyo kinachofanyika sasa nakuhakikishia kuwa kinaenda kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa, kwani msako uliopo sasa hivi sio wa kitoto na jamaa hana hata miezi mitatu ndan ya ofisi.

Kuna watu watapotezwa kimya kimya bila raia uraiani kujua kinachoendelea. We subiri tu mkuu.
 
Mkuu unajua kila uongozi una stahili yake ya kutawala. Lakini vilevile hiyo style unayosema haiwezi kuwa dawa ya moja kwa moja ya tatizo, ila itasaidia tu kupunguza uhalifu uliokuwepo au uliopo.

Nasema hivyo kwa sababu hata hizo nchi ambazo unazitolea mfano, watu walikuwa wanauwawa kila siku lakini bado watu wanaendelea kuingiza na kuuza madawa. Yani serikali inanyonga hawa kesho wanaibuka wengine, mpaka Marekani, Ulaya na watu wa haki za binadam wakaamua kuingilia kati baada ya kuona kuwa njia inayotumika haimalizi tatizo, sema tu inaongeza vifo vya watu kila siku.

Na hapa mkaburu anaweza kufanya zaidi ya hayo uliyosema. Nafikiri unafaham vizuri historia ya makaburu kwa watu weusi, lakin sasa serikali haipo kwenye mikono yao. Na pia sheria zilizopo sasa haziruhusu hayo kufanyika. Ila hata hivyo kinachofanyika sasa nakuhakikishia kuwa kinaenda kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa, kwani msako uliopo sasa hivi sio wa kitoto na jamaa hana hata miezi mitatu ndan ya ofisi.

Kuna watu watapotezwa kimya kimya bila raia uraiani kujua kinachoendelea. We subiri tu mkuu.
Chief isijekuwa ni nguvu ya soda!! Binafsi south africa ni nchi ambayo ningependa sana kuitembelea ila suala la uhalifu huwa linaniogopesha sana
 
Chief isijekuwa ni nguvu ya soda!! Binafsi south africa ni nchi ambayo ningependa sana kuitembelea ila suala la uhalifu huwa linaniogopesha sana
Kwa hawa weupe wa hapa nnavyowajua mkuu, hapa hakuna cha nguvu ya soda. Huu mziki utaendelea mpaka usalama utatamalaki nchi nzima.

Labda itokee huyu mweupe alieanzisha operation hizi atolewe ktk nafasi yake. Lakini kama ataendelea kuwepo, ujue miaka miwili ijayo hakuna mtu atakaekuwa anatembea hata na kiwembe mfukoni. Trust me mkuu.
 
Huyo hapo pichani. Amezaliwa hapa, amekulia hapa na kila mtu alikuwa anajua kama ni raia wa hapa. Alianza kujiingiza katika mashindano ya urembo na kushinda mataji kadhaa huko nyuma.

Alipopanda mpaka kufika kwenye ngazi za juu na kushinda taji la Miss South Africa. Hapo ndo mziki ulipoanza wa kutaka kujua asili yake. Pilika pilika zikamfikia waziri wa mambo ya ndani. Akaingilia kati kujua kinachoendelea. Ghafla ikajulikana kuwa bint baba yake M'nigeria, na mama ni raia wa msumbiji aliefoji vyeti na kujifanya mzawa. Miss huyo baada ya kugundulika hivyo akavuliwa taji. Na yeye kwa hasira akaenda Nigeria kugombea u miss na akashinda.
Lol wangemuacha tuu😃😃🙃
 
Habari zenu wanaJF wenzangu, ama baada ya salam ningependa kuendelea na mada yangu hapo chini.

Nianze kwa kusema kuwa dunia ina mengi, na kamwe hauwezi kuyajua kama haujaambiwa au kuyaona. Ndio maana waswahili wanamsemo wao unaosema "tembea uyaone". Hii haimaanishi kwamba utembee uyaone magorofa, magari au barabara, bali uone mambo mapya ambayo hapo kabla ya kutembea ulikuwa haujawahi kuyaona au kuyasikia popote.

Sasa leo ningependa nije na mada inayowatahadharisha ndugu zangu wabongo, ili kuwafungua macho na akili ya kujua yale ambayo hapo kabla walikuwa hawajayajua kuhusu South Africa, Dzonga, Afrika borwa, Afrika kusini, bondeni, Kaburu na kila jina linalotambulisha taifa hili.

Ni mambo sita tu ambayo ningependa kukutahadharisha nayo, uyazingatie kabla ya safari. Ila kama kuna mengine ya kuongezea basi wenzangu ambao wako humu pia wataongezea mengine katika comment. Na uzi wangu wa leo unajikita katika mambo yaliopo ndani ya mipaka ya South tu. Kuhusu changamoto zingine za njiani kabla ya kufika South nk, hizo sintozizungumzia kwa sasa. Maana thread za changamoto hizo zipo nyingi na mimi nishawahi kuandika moja.

Tuendelee hapo chini na yale unayotakiwa kuzingatia.

1. Hakikisha una document zote muhimu zinazohitajika safarini. Na kama uliambiwa kuwa gharama ya safari ni laki tatu, basi uandae angalau laki nne, ili moja uiweke pembeni itakusadia mbele ya safari. Kumbuka kuna dharura njiani, dola au rand kupanda nk.

2. Wakati unapanga safari, jitahidi kwanza ujue kingereza. Na kama una kichwa kizito cha kujifunza ngeli, basi upambane ujue hata salam, kuomba kitu au kuaga. South ni nchi inayoongea lugha 11. Ambapo lugha 9 ni za wenyeji na 2 za wazungu. Lakini lugha ya taifa na ambayo inapewa kipaumbele zaidi ni English.

Sasa ukijua English, hata kama hauna elimu ya maaana, uwezekano wa kupata kazi ni mkubwa ukilinganisha na wale ambao hawajui English. Ndomaana wazimbabwe wamedhibiti kazi nyingi na haswa zinazomilikiwa na wazungu, maana wao English kwao ni kama maji na mtungi, halafu wanaongea British safi kuliko waafrika wengine. Kutokujua English kumewanyima watu wengi (haswa kutoka bongo) fursa za kazi, hivyo kusababisha wengine kuamua kufanya deal hatari, halali na zisizo halali ili mradi mtu aishi.

3. Kabla ya kuanza safari hakikisha una address au contacts za wenyeji wako zaidi ya mmoja. Nchi hii kuna watu wengi wameuwawa, wameibiwa, wamekamatwa na kurudishwa nyumbani kwa sababu ya kukimbiwa au kuzimiwa simu na wenyeji wao kabla ya kuingia au baada ya kuingia South. Na hii sio kwa wabongo tu, bali ni nchi zote za East Africa watu wana tabia za kuwaingiza maboya ndugu, jamaa na marafiki zao kwamba waje tu watawapokea na kuwafanyia mpango wa kuishi, lakini ndugu, jamaa au marafiki hao wanapoingia tu mwenyeji huzima simu, hubadili namba nk. Hivyo ukiwa na address au namba za sim zaidi ya 3, itakusaidia ku deal na mwingine baada ya mmoja au wawili wa mwanzo kukuzimia simu.

4. Usiwaze kwamba utafanya kazi fulani tu, bali wewe ujiandae kufanya kazi yoyote (ya halali) kujiingizia kipato. Hili swala la watu kuja huku wakiandaa akili, na saikolojia zao za kichwa kwamba anakuja kufanya kazi fulani tu. Ndio limesababisha baadhi ya wabongo kupoteza mwelekeo wa maisha, na kujikuta wanajitupa katika biashara hatari na zisizokuwa halali.

5. Usilete usela mavi usiokuwa na maana. Vijana wengi waliotaka kuleta usela wa Mbagala, Mburahati, Manzese, Temeke, Tandika nk tumewazika wakiwa bado wadogo. Hii ni kwa sababu huku watu hawana muda wa kukimbizana na mwizi wajichoshe. Ukileta usela mavi, watu wanakutafutia target, wanafumua ubongo, kazi imekwisha. yumbani watu wanarudisha nguo au maiti na kesi hamna. Pia usije kwa lengo la kutafuta na kufanya starehe kupitiliza mpaka ukasahau kilichokuleta. Maana kama starehe hata bongo zipo na umeziacha, kama mademu bongo wapo na umewaacha, kama tungi pia bongo lipo umeliacha. So focus kwa kile kilichokufanya utafute nauli uje. Sio kuendekeza kulewa na chupi za Kaburu utapotea mazima na hakuna mtu atakaekurudisha katika chanel yako tena.

6. Ukifika hapa kama wewe ni mpya usikimbilie kukaa kiti cha mbele katika daladala (tax), hata kama imejaa na imebaki siti moja ya mbele, ni bora usubiri nyingine alafu ndio upande. Hii ni kwa sababu huku majimbo mengi daladala zao hakuna kondakta anaezunguka ndani ya daladala kuomba nauli. So ukisema unakimbilia mbele kukaa na dereva, utashangaa watu wanakusanya hela zote huko nyuma, alaf wanakutupia wewe ndio uhesabu na kama kuna mtu ametoa hela kubwa umrudishie chenji, na ikiwa pungufu uhakikishe waliokupa wanazieneza. Dereva yeye hupokea nauli ambayo imeshahesabiwa tayari na iwe imetimia. Ikipungua hata sh hamsini basi ataanza na wewe uliepokea hela kabla ya kuendelea na waliopo ndani ya gari. Pia asilimia kubwa ya madereva wa hapa wana silaha mbali mbali ndani ya gari zao, kama sio bunduki basi fimbo inayofanana na mkia wa taa. So hela yake isipoenea na wewe ndo New comer (mpya) haujui lugha, basi imekula kwako. Hata ujitetee kwa English yako ya kuunga unga hatokuelewa. Naomba niishie hapa.
Namba sita ni kiboko 😂😂😂
 
Back
Top Bottom