Kama una tabia hizi 10, huwezi kamwe kufanikiwa kwenye maisha

Kama una tabia hizi 10, huwezi kamwe kufanikiwa kwenye maisha

Hata mimi nilitaka kuuliza hivyo hivyo. Tunapojadili mafanikio, tunaongelea nini hasa? Katika muktadha wa Kitanzania ni mpaka uwe tajiri wa aina gani ndiyo uhesabike umefanikiwa?
Mafanikio ni kupata unachotaka na maisha yako kuwa bora mkuu.
Asikudanganye yeyote nje ya hapo.
 
Tajiri anauzaga vitabu jamiiforums?
Mnanishangazaga sana mnapowadharau watu wanaouza vitu.
Hii dunia inaendeshwa na sales people.
Heshimuni sana watu wanaofanya sales, hata kama ni ya kiwango kidogo kiasi gani.
Hata wagunduzi wakubwa wa teknolojia, zimeweza kuwafikia watu baada ya kuuza.
Usidharau kuuza mkuu.
 
Hakuna ugumu wowote kwenye msamiati wa mafanikio.
Labda kama ni academician na unataka tu kucomplicate vitu ili kuonesha kiwango chako cha ujuzi wa mambo.
Lakini dhana ya mafanikio ni rahisi; kupata kile unachotaka sana na maisha yako na ya wengine yakawa bora kupitia wewe kupata hicho.
Iwe ni fedha, cheo, elimu, afya, mahusiano n.k.
Asante kwa maelezo, uwe na wakati mwema.......
 
Nikushauri tu ndugu, kwenye uandishi jaribu kuzungumzia vitu kiuhalisia, usizungumzie nadharia. Hayo uliyoyaandika hapo kila siku yanazungumzwa na motivational speakers hakuna kipya hapo.

Na usipo badilika utapata tabu sana.

Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
 
Ukisoma comments za huu Uzi ndio utajua IQ ya watanzania kwanini iko chini sana.

Kama mtu anashindwa ku-logic na kuwa analytical kwa hizo hoja kumi (10) anaenda kuhoji utajiri wa mleta mada na kuuza vitabu !!! Basi sishangai tunapata Viongozi wanaenda kujenga international airport Chato.


Ili uamini IQ ya watanzania Ni ndogo nimechukua huu Uzi nikamtupia rafik yangu mkoja mkenya Feedback ambazo kanipa ni tofauti na yanayoandikwa humu.


Watanzania tutahidi kuwa analytical. Simaaninishi ni lazima ukabaliane na Uzi ila kuwa na critics zilizojiegemeza kwenye hoja na sio mtu. Kuelekeza critics kwa mtu badala ya hoja hizo 10 ni moja ya dalili uwezo wetu wa kujenga hoja ni mdogo.

Haya ndio Mambo hata kwenye interview allkisimama mtanzania na mkenya tunaishia kuduwaa.
 
Hivyo vitabu vimekuwezesha kumiliki V8 ngapi mpaka sasa au ndio unataka kutuongezea njaa asubuhi asubuhi? Maana raha ya mafanikio tuyaone kwa macho mzee!

Kama bado uko kwenye cycle ya mkono kwenda kinywani nafikiri bado huna viwango vya ku preach namna ya kuwa tajiri! Ujumbe mzuri ni ule unaotekelezeka hata na wewe mtoa ujumbe!

NB: Kwa level ya mafanikio unayozungumzia nafikiri inawahusu akina Bill Gates, Elon Musk, Mark Zuckerberg na wenzao kadhaa ambao wao tu kwa pesa zao wakiamua wanaweza zilisha kaya za Tanzania chips kuku kwa miaka kadhaa bila kuyumba!
Mchokozi sana wewe 😂😂😂.
 
Nikushauri tu ndugu, kwenye uandishi jaribu kuzungumzia vitu kiuhalisia, usizungumzie nadharia. Hayo uliyoyaandika hapo kila siku yanazungumzwa na motivational speakers hakuna kipya hapo.

Na usipo badilika utapata tabu sana.

Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
Wewe kwa hizi akili ndio maana ulitimuliwa kwenu huna tofauti na mifugo


 
Labda ungeainisha ni aina ipi ya Mafanikio unayoyazungumzia. Being Successful it's a perspective statement/ Word. Kila mtu anatafsiri mafanikio yake kutokana na imani yake au desire. Mafanikio hayana Universal meaning...Je kwa mujibu wa mada yako unazungumzia Mafanikio yapi?

-Ndugu zangu Ma-Budha wanaamini Mafanikio ni kufikia Vast spiritual Enlightenment wao wanaita Nirvana
-Kwetu Stoics na Cynics tunaamini mafanikio ni kufanikiwa kutojishikiza katika materials au aina yoyote ya Emotions.
-Wakatoliki tunaamini Mafanikio ni kufa kifo cha utakatifu ili uweze kufika mbele za Bwana.
-Ndugu zangu wachaga wanaamini Mafanikio ni kua na pesa miiiingi sana

Mtoa mada unazungumzia Mafanikio Tangible au non tangible... Spiritualphysical au mentally?
Karibu mkuu,
Mimi ni Mstoa na ninaamini mafanikio ni kufikia uwezo mkubwa ulio ndani yangu na kuiishi misingi mikuu minne ya ustoa ambayo ni;
1. Hekima (wisdom)
Kwa kujifunza yaliyo sahihi na kuyaweka kwenye maisha yangu ili yawe bora zaidi na yawe na manufaa kwa wengine.
2. Haki (justice)
Kuwatendea wengine yaliyo ya haki na kuwa na uadilifu.
3. Ujasiri (courage)
Kuweza kusimamia kilicho sahihi bila kuhofia chochote.
4. Kujidhibiti (moderation)
Kuwa na kiasi kwa kila jambo.
Tofauti ya Ustoa na falsafa nyingine ni ustoa haukuwekei ukomo wa nini unaweza kuwa nacho au huwezi kuwa nacho.
Unaweza kuona Epictetus alitoka kuwa mtumwa mpaka mwalimu wa Falsafa.
Seneca alikuwa tajiri mkubwa wa Roma.
Na Marcus Aurelius alikuwa mtawala wa Roma.
Hivyo kupitia Ustoa, mafanikio ni kuijua asili yako na kuishi kulingana na asili hiyo.

Na hiyo pia ndiyo maana rahisi ya mafanikio kwa yeyote, jua unachotaka sana na pambana kukipata.
Na siyo kuhangaika kuridhisha wengine.
 
Hivyo vitabu vimekuwezesha kumiliki V8 ngapi mpaka sasa au ndio unataka kutuongezea njaa asubuhi asubuhi? Maana raha ya mafanikio tuyaone kwa macho mzee!

Kama bado uko kwenye cycle ya mkono kwenda kinywani nafikiri bado huna viwango vya ku preach namna ya kuwa tajiri! Ujumbe mzuri ni ule unaotekelezeka hata na wewe mtoa ujumbe!

NB: Kwa level ya mafanikio unayozungumzia nafikiri inawahusu akina Bill Gates, Elon Musk, Mark Zuckerberg na wenzao kadhaa ambao wao tu kwa pesa zao wakiamua wanaweza zilisha kaya za Tanzania chips kuku kwa miaka kadhaa bila kuyumba!
Hyu jamaa ni tajiri kwa level za kibongobongo hasa kwa vijana, namjua tokea anaanza harakati zake.na ana miradi tofauti tofauti sio kuuza vitabu pekee yake

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mkuu uzi wako umeelewek vizuri tu ...hapy kwenye kusoma au kujifunza ndo inakuwa kipengele kwa wengi kusoma tunasoma ila mara nyingi udaku ndo unapendwa sana be blessed tukutan kweny watsap..
 
Umenifumbua macho kwa kiasi fulani ila mwishoni hapo ni kama ulikua unaniandaa kwa ajili ya hivo vitabu ulivotaja...japo BIG thanks tutayafanyia kazi.
 
Ukisoma comments za huu Uzi ndio utajua IQ ya watanzania kwanini iko chini sana.

Kama mtu anashindwa ku-logic na kuwa analytical kwa hizo hoja kumi (10) anaenda kuhoji utajiri wa mleta mada na kuuza vitabu !!! Basi sishangai tunapata Viongozi wanaenda kujenga international airport Chato.


Ili uamini IQ ya watanzania Ni ndogo nimechukua huu Uzi nikamtupia rafik yangu mkoja mkenya Feedback ambazo kanipa ni tofauti na yanayoandikwa humu.


Watanzania tutahidi kuwa analytical. Simaaninishi ni lazima ukabaliane na Uzi ila kuwa na critics zilizojiegemeza kwenye hoja na sio mtu. Kuelekeza critics kwa mtu badala ya hoja hizo 10 ni moja ya dalili uwezo wetu wa kujenga hoja ni mdogo.

Haya ndio Mambo hata kwenye interview allkisimama mtanzania na mkenya tunaishia kuduwaa.
Ndio wabongo tulio wengi tulivyo. Negativity imeshakuwa part ya maisha yetu, tena wengine wana heshima kubwa humu jamvini lakini utopolo wanaouandika kwenye huu uzi huwezi kudhania.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Wewe kwa hizi akili ndio maana ulitimuliwa kwenu huna tofauti na mifugo


Kwani ilikuwa ni nyumba ya mama yako ndugu???



Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom