Kama unaingiza faida ya Tsh. 30,000 na kuendelea kwa siku pita hapa

Katika biashara zote zilizotajwa na zitakazotajwa hapa kuna kitu unatakiwa ukitambue na ukielewe

Hutoona biashara yenye link na TRA yani kwa ufupi hizi biashara tunasema zikae local local ili kuepusha

macho/vijicho TRA ukitaka kujiweka ki smart smart unataka kufanya vitu ki professional Asee ndugu yangu

ukifungua ofisi leo humalizi WIKI utawaona wajomba TRA hawa hapa,humalizi wiki utawaona tena wengine wamefata

ki karatasi cha service levy sijui,hujakaa vizuri utamuona bwana AFYA mara paap unashangaa mwaka unaisha wewe ni

unacheza tu rede na serikali,ukiambiwa ofisi iweke in locla way sio kwamba watu hawataki ukae ofisi nzuri La hasha

ila unaepushwa na mkono wa MAGUFULI.

Ujanja wangu wote wa kufata TIN no. na LESENI ilikuaga kwa lengo la kupata LAINI za uwakala zenye MAJINA YANGU

Baada ya kuzipata zile laini TIN NO nikaficha,leseni ficha nipo nadunda na kitambulisho cha MACHINGA

Usije ukajiloga ukaeka mbwembwe ofisi yako jinsi unavyoiremba ndio ukae ukijua TRA nao ndio wanaona Pale pesa ipo.
 
Utakuwa umepatia sana. Chamsingi zingatia sana privacy za wateja wako.

Guest zinaingiza hela nzuri zaidi kwa wateja wa short time kuliko wale wa kulala.
Short time hawatumii umeme mwingi na maji sana, mathalani kama uko kwenye mzunguko wa watu wengi kuna uwezekano chumba kimoja kikahudumia watu mpaka wanne kwa siku moja.

Mchana wateja wengi ni wake za watu na wale ambao hawana nafasi za kutoka majumbani usiku hawa privacy yao inatakiwa kuwa ya hali ya juu sana.
1 usiruhusu ujinga wa mtu kuja kufanya fumanizi
2 usiruhusu mlundikano wa watu wasioeleweka eleweka eneo husika

3 Hakikisha main entry na back door kwa wale wanaotaka strict privacy.

4 Hakikisha una vyumba walau viwili mtu anaweza ingia na asionekane kwa wenye vyumba vingine.
 
mkuu kuwekeza 10m kwenye uber au 7m kwenye bajaji then ukawa unakusanya 20k to 30k kwa siku huo ni udhaifu wa akili labda kama unaendesha mwenyewe, kwa mtaji huo mimi nakusanya zaidi ya 150k mpaka 300k per day kama faida
 
Wewe anzisha tu unaweza ukaanza na vyumba vitatu kisha ukaendeleza taratibu.

Asikwambie mtu chumba kimoja cha guest kinaweza kusomesha mtu mpaka chuo kikuu
 
Asante mkuu kwa ushauri, naufanyia kazi.
Ubarikiwe sana.
 
Ningependa kujua hii biashara ya kukodisha tents na viti kwa ajili ya shughuli mbalimbali,misiba etc

Gharama za kutengeneza hizo tents ama kama zinauzwa zikiwa tayari zinauzwaje?

Walau ziwe tatu zenye uwezo wa ku- accommodate watu 500 au 400 zote kwa pamoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…