Kamati Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti Samia yaridhia Daniel Chongolo kujiuzulu Ukatibu Mkuu

Kamati Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti Samia yaridhia Daniel Chongolo kujiuzulu Ukatibu Mkuu

Jamaa kishaandika barua ya kujiuzulu na imeletwa kwenu na imepokelewa , mmemkubalia, sasa mnachunguza kitu gani tena?

Hakuna haja ya kupoteza muda kuchunguza yanayojulikana, hivi Kinana akijiuzulu kesho kutwa ( kama tunavyotarajia ) naye atachunguzwa?

Acheni kutupotezea muda, jazeni nafasi zilizoachwa wazi
Mama mweupe kichwani....

Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
 
Jamaa kishaandika barua ya kujiuzulu na imeletwa kwenu na imepokelewa , mmemkubalia, sasa mnachunguza kitu gani tena?

Hakuna haja ya kupoteza muda kuchunguza yanayojulikana, hivi Kinana akijiuzulu kesho kutwa ( kama tunavyotarajia ) naye atachunguzwa?

Acheni kutupotezea muda, jazeni nafasi zilizoachwa wazi
wajaze iliyowazi ili wakawamalize vizuri sana watoa taarifa right?

🤣nimefulahi chana nkulungenzi
 
Jamaa kishaandika barua ya kujiuzulu na imeletwa kwenu na imepokelewa , mmemkubalia, sasa mnachunguza kitu gani tena?

Hakuna haja ya kupoteza muda kuchunguza yanayojulikana, hivi Kinana akijiuzulu kesho kutwa ( kama tunavyotarajia ) naye atachunguzwa?

Acheni kutupotezea muda, jazeni nafasi zilizoachwa wazi
Wanajitekenya na kujichekesha.....


DAB kawaweza kweli kweli
 
Jamaa kishaandika barua ya kujiuzulu na imeletwa kwenu na imepokelewa, mmemkubalia, sasa mnachunguza kitu gani tena?

Hakuna haja ya kupoteza muda kuchunguza yanayojulikana, hivi Kinana akijiuzulu kesho kutwa ( kama tunavyotarajia ) naye atachunguzwa?

Acheni kutupotezea muda, jazeni nafasi zilizoachwa wazi
Kujiuzulu kwa mchongo huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa kilichofanyika leo tarehe 29 Novemba, 2023 Jijini Dar es salaam na kuongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kimeridhia kujiuzulu kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho Comrade Daniel Chongolo

Taarifa ya Katibu wa Itikadi na Uenezi na Mafunzo, Paul Makonda imeeleza walioteuliwa kugombea nafasi ya Uenyekiti kwa mikoa ya Arusha, Mbeya na Mwanza pamoja na Wilaya za Mpanda na Kusini Unguja.


---
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameijulisha Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kupokea barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo, na ameridhia ombi hilo.

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi wa CCM Taifa, Paul Makonda amesema hayo leo Jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa kuhusu Kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa kilichoketi leo Jijini Dar es salaam chini ya Mwenyekiti na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kimejadili hali ya kisiasa ndani ya Chama na nje ya Chama hicho nchini na kimefanya uteuzi wa mwisho wa Wagombea wa nafasi za uongozi ndani ya Chama kwa ngazi ya Mkoa na Wilaya ili kujaza nafasi zilizoachwa wazi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo na uteuzi wa nafasi nyingine.

Pia soma:
- Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo aandika barua ya kujiuzulu

View attachment 2828888View attachment 2828889
Before Makonda no Kashfa after Makonda kashfa why? Sio kwamba Kuna mtu anataka atambe vizuri hapo maana katika hali ya kawaida mwenezi alishawahi kuu juu ya KM akamdharirisha sana sasa ingekuwa rahisi akamtii kwa sasa? Naona kama wamesagiana kunguni hivi.
 
Kwa wale Wabobezi wenzangu wa Psychology ( hasa ile Communication Psychology ) ambayo inajumuisha hadi Body Language ya Mtu bila Kusahau na Eye Contact yake naamini katika hiyo Video Clip mmegundua Mambo makubwa na tata kama Matatu mpaka Matano hivyo naomba sasa tuwasaidie wale ambao hawajagundua lolote.
 
29 November 2023

SABABU ZA KADHAA CCM KUTEUA WAGOMBEA NGAZI ZA WENYEVITI WA MIKOA NA WILAYA

CCM Wilaya ya Kusini Unguja itafanya uchaguzi baada ya kufariki ndugu Mgana Zidi Khamis aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja.



Kutoka wilaya ya Mpanda habari ni kuwa CCM inategemea kumpata mwenyekiti mpya
ccm-mpanda.jpg
Mwenyekiti CCM Wilaya ya Mpanda marehemu Method Mtepa enzi za uhai wake. Picha na Mtandao

Huku CCM wilaya ya Mpanda
Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Ccm wilaya ya Mpanda Bw. Method Mtepa alifariki dunia tarehe 19/09/2023 baada ya kuugua kwa muda mrefu.

IMG-20230530-WA0099.jpg

Picha: Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza ndugu Sixbert Jichagu (katikati) akiwa na mkuu wa mkoa CPA Amos Makala (kushoto), wakati mkuu huyo wa mkoa wa Mwanza,alipofika ofisi za CCM kujitambulisha.

Na kwa uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza, unakuja baada ya mwenyekiti wa mkoa wa Mwanza ndugu Sixbert Jichagu kuteuliwa kuwa DED mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Masasi. Ndugu Sixbert Jichagu alichaguliwa kwa kishindo kikubwa mwezi September 2022 lakini mwenyekiti wa taifa akampangia kituo cha kazi mwaka 2023 kuwa DED halmashauri ya Masasi.

View attachment 2829053
Picha: mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya ndugu Dr. Stephen Mwakajumilo.

Wakati kwa mkoa wa Mbeya, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya ndugu Dr. Stephen Mwakajumilo aliye mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa NEC alileta mtafaruku kwa kuhoji sababu za miradi mingi kusimama baada ya Magufuli kufariki.

Pia mwenyekiti huyo wa CCM mkoa wa Mbeya ndugu Dr. Stephen Mwakajumilo alisema kunahitajika mjadala mpana kuhusu mkataba wa bandari na kuungana mkono wananchi walioomba kupatiwa sababu za, uhalali wa bandari kupewa DP World kwa mkataba ulioolekana kuwa na utata. Msimamo wa ndugu Dr. Stephen Mwakajumilo ukaistua CCM na hata makamu wa rais akasema kuwa wanaCCM hawana utamaduni wa kuhoji waziwazi bila kupitia vikao vya ndani vya CCM kama alivyofanya ndugu Dr. Stephen Mwakajumilo mbele ya vyombo vya habari.

Na mwisho CCM mkoa wa Arusha walimpoteza mwenyekiti wao wa mkoa, Kamishna Mstaafu Zelothe Stephen ambaye alifariki dunia hivi karibuni mwaka 2023.
Mwakajumilo tulijua yatamkuta
 
Jaribio la SSH kumfanya Makonda Katibu Mkuu CCM limekwama kwa kura nyingi, imebidi aombe akajifikirie upya aje na mtu mwingine
KUmuweka makonda katibu mkuu ni dharau na kuimalizia CCM yetu rasmi.

Wana CCM wenzangu tukinusuru chama chetu.
 
Mwakajumilo tulijua yatamkuta

CCM hawataki kabisa mtu aliye mwanaCCM ku challenge hoja, kuibua udhaifu, kuwaza mipango inayotoa chachu fikra za mwenyekiti wa chama dola kongwe iboreshwe...

KAMATI YA SIASA MKOA WA MBEYA YATOA KAULI KUTORIDHISHWA NA BAADHI YA MIRADI​

thumb_1353_800x420_0_0_auto.jpg
Imewekwa: July 23rd, 2023
Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya imemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Chunya kumpandisha Cheo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mafyeko kutokana na usimamizi mzuri wa ujenzi wa shule mpya inayojengwa katika kata hiyo.

Hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya Mhe. Dkt Stephene Mwakajumilo wakati wa ziara ya kamati ya siasa ya Chama cha mapinduzi kukagua utekelezwaji wa miradi ya maendeleo ndani ya wilaya ya Chunya ikiwa ni usimamizi wa ilani ya chama cha Mapinduzi.

Dkt. Mwakajumilo aliongeza kusema mradi wa ujenzi wa shule mpya Mafyeko kwa asilimia mia moja hauna shida umesimamiwa na kutekelezwa ipasavyo jambo lililopelekea kamati ya siasa kwa pamoja kukubalinana kwamba Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mafyeko ambaye ndiye msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Shule Mpya kupongezwa.

“Injinia msimamizi wa ule mradi amefanya kazi nzuri sana, mkuu wa shule ndio zaidi tumemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri mara baada ya ule ujenzi wa mradi kuisha yule mkuu wa Shule asiwe mkuu wa shule tena apate nafasi nyingine” alisema Dkt Mwakajumilo

Mweyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Mhe. Dkt Stephene Mwakajumilo pamoja na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wameonyesha kutoridishwa na utekelezaji na usimamizi wa baadhi ya miradi ya maendeleo inayoekelezwa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Chunya.

“Tumekagua miradi nane ndani ya wilaya ya Chunya, tumebaini changamoto baadhi ya maeneo, tuwashauri mkajifunze kwa uongozi wa kata ya Mafyeko jinsi ambavyo mnaweza kusimamia vizuri miradi” aisema Mwakajumilo

Ziara ya kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mbeya imedumu kwa siku tatu kuanzia tarehe 21-23/7/2023 na imekagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na mradi wa upanuzi wa Hospitali ya wilaya, mradi wa Mitambo ya kuchimbia visima, Mradi wa Maji Matwiga, Ujenzi wa Shule ya msingi Mafyeko kupitia mradi wa Boost, ujenzi wa nyumba ya watumishi 3 in 1 katika shule ya msingi Sipa, ujenzi wa uzio wa Mnada Sipa pamoja na ujenzi wa barabara Sipa
Source : KAMATI YA SIASA MKOA WA MBEYA YAKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI CHUNYA.
 
Back
Top Bottom