Kamati Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti Samia yaridhia Daniel Chongolo kujiuzulu Ukatibu Mkuu

Mama mweupe kichwani....

Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
 
wajaze iliyowazi ili wakawamalize vizuri sana watoa taarifa right?

🤣nimefulahi chana nkulungenzi
 
Wanajitekenya na kujichekesha.....


DAB kawaweza kweli kweli
 
Kujiuzulu kwa mchongo huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Before Makonda no Kashfa after Makonda kashfa why? Sio kwamba Kuna mtu anataka atambe vizuri hapo maana katika hali ya kawaida mwenezi alishawahi kuu juu ya KM akamdharirisha sana sasa ingekuwa rahisi akamtii kwa sasa? Naona kama wamesagiana kunguni hivi.
 
Kwa wale Wabobezi wenzangu wa Psychology ( hasa ile Communication Psychology ) ambayo inajumuisha hadi Body Language ya Mtu bila Kusahau na Eye Contact yake naamini katika hiyo Video Clip mmegundua Mambo makubwa na tata kama Matatu mpaka Matano hivyo naomba sasa tuwasaidie wale ambao hawajagundua lolote.
 
Mwakajumilo tulijua yatamkuta
 
Jaribio la SSH kumfanya Makonda Katibu Mkuu CCM limekwama kwa kura nyingi, imebidi aombe akajifikirie upya aje na mtu mwingine
KUmuweka makonda katibu mkuu ni dharau na kuimalizia CCM yetu rasmi.

Wana CCM wenzangu tukinusuru chama chetu.
 
Mwakajumilo tulijua yatamkuta

CCM hawataki kabisa mtu aliye mwanaCCM ku challenge hoja, kuibua udhaifu, kuwaza mipango inayotoa chachu fikra za mwenyekiti wa chama dola kongwe iboreshwe...

KAMATI YA SIASA MKOA WA MBEYA YATOA KAULI KUTORIDHISHWA NA BAADHI YA MIRADI​

Imewekwa: July 23rd, 2023
Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya imemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Chunya kumpandisha Cheo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mafyeko kutokana na usimamizi mzuri wa ujenzi wa shule mpya inayojengwa katika kata hiyo.

Hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya Mhe. Dkt Stephene Mwakajumilo wakati wa ziara ya kamati ya siasa ya Chama cha mapinduzi kukagua utekelezwaji wa miradi ya maendeleo ndani ya wilaya ya Chunya ikiwa ni usimamizi wa ilani ya chama cha Mapinduzi.

Dkt. Mwakajumilo aliongeza kusema mradi wa ujenzi wa shule mpya Mafyeko kwa asilimia mia moja hauna shida umesimamiwa na kutekelezwa ipasavyo jambo lililopelekea kamati ya siasa kwa pamoja kukubalinana kwamba Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mafyeko ambaye ndiye msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Shule Mpya kupongezwa.

“Injinia msimamizi wa ule mradi amefanya kazi nzuri sana, mkuu wa shule ndio zaidi tumemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri mara baada ya ule ujenzi wa mradi kuisha yule mkuu wa Shule asiwe mkuu wa shule tena apate nafasi nyingine” alisema Dkt Mwakajumilo

Mweyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya Mhe. Dkt Stephene Mwakajumilo pamoja na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wameonyesha kutoridishwa na utekelezaji na usimamizi wa baadhi ya miradi ya maendeleo inayoekelezwa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Chunya.

“Tumekagua miradi nane ndani ya wilaya ya Chunya, tumebaini changamoto baadhi ya maeneo, tuwashauri mkajifunze kwa uongozi wa kata ya Mafyeko jinsi ambavyo mnaweza kusimamia vizuri miradi” aisema Mwakajumilo

Ziara ya kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Mbeya imedumu kwa siku tatu kuanzia tarehe 21-23/7/2023 na imekagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na mradi wa upanuzi wa Hospitali ya wilaya, mradi wa Mitambo ya kuchimbia visima, Mradi wa Maji Matwiga, Ujenzi wa Shule ya msingi Mafyeko kupitia mradi wa Boost, ujenzi wa nyumba ya watumishi 3 in 1 katika shule ya msingi Sipa, ujenzi wa uzio wa Mnada Sipa pamoja na ujenzi wa barabara Sipa
Source : KAMATI YA SIASA MKOA WA MBEYA YAKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI CHUNYA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…