Kamati Kuu ya CHADEMA kimewapitisha Freeman Mbowe na Cecil Mwambe kugombea nafasi ya Mwenyekiti Taifa

Kamati Kuu ya CHADEMA kimewapitisha Freeman Mbowe na Cecil Mwambe kugombea nafasi ya Mwenyekiti Taifa

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Sasa ni Rasmi.Kamati Kuu ya CHADEMA katika kikao chao leo cha kikatiba kimewapitisha Freeman Mbowe na Cecil Mwambe kugombea nafasi ya Mwenyekiti Taifa katika uchaguzi utakaofanyika Jumatano Desemba 18.

Katika kuonyesha kukomaa kwa Demokrasia ndani ya chama hicho Kamati Kuu iliwahoji wagombea wote bila upendeleo wowote huku Freeman Mbowe akiachia kwa muda nafasi yake ya Uenyekiti na kukaimiwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee.

Hata hivyo majina yote mawili yatapelekwa katika kikao Cha Baraza Kuu kesho kwa uteuzi wa mwisho na kuidhinishwa rasmi

Freeman Mbowe mwenye ufuasi mkubwa ndani ya chama hicho atakabiliana na mpinzani wake huyo aliyejinasibu kuleta mageuzi makubwa ya kiuongozi na kiutawala ndani ya chama hicho chenye wanachama milioni 6.

Uchaguzi ndani ya chama hicho umegeuka kuwa agenda kuu ya kitaifa kwa sasa kutokana na mvuto wa uchaguzi huo na jinsi unavyoendeshwa kidemokrasia na hivyo kuvuta hisia za watanzania ndani na nje ya nchi.

Kwa siku mbili zilizobaki zitakuwa muhimu kwa wagombea kujinadi na kuomba kura
 
Mshindi wa Uchaguzi huu kati ya hao wawili

atatupa picha ya ushindi wa nani 2020 (URAIS)

onyesheni vitendo vyenu nyie BAVICHA ndio

ntajua hata 2020 mnaweza amua fanya mapinduzi

Ila mkishndwa huu mtihani,2020 na miaka yote hamtokaa mshnde.
 
Cecil Mwambe ametimiza haki yake ya kidemokrasia ila atakayempigia kura eti awe mwenyekiti wa Chadema atakuwa mwehu kwelikweli! Yani wewe ni mwanamchama kweli wa Chadema then unatoka kwako kwenda kumchagua Cecil Mwambe mtu aliyehamia 2015 akitokea CCM awe mwenyekiti! Emb tuache mzaha bwana!
 
December 16, 2019

CHADEMA WAMPITISHA TUNDU LISSU KUGOMBEA/ MBOWE KUCHUANA na CECIL MWAMBE



Kamati ya Uchaguzi wa ndani ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) imetoa majina ya wagombea waliopitishwa kugombea nafasi mbali mbali ndani ya chama hicho ikiwemo nafasi ya mwenyekiti wa chama ambayo waziri mstaafu Fredrick Sumae alitangaza kujitoa na nafasi ya makamu mwenyekiti ambayo pia Saeid Kubenea ameandika barua ya kujitoa kwa kile alichosema kuwa anadhani Tundu Lissu anauwezo mzuri wa kuitumikia nafasi ya umakamu kuliko yeye.
 
Cecil Mwambe anatimiza tu haki yake ya kikatiba, akipigwa chini tusisikie msajili anakurupuka na matamko yake ya ajabu ajabu kuhusu uchaguzi wa CDM, naamini wajumbe wameshaonesha kwa vitendo hawajaribiwi kwenye chaguzi zilizotangulia, sasa sitegemei huu uchaguzi wa mwenyekiti uwe na tofauti yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom