Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

Nawasalimu wanajukwaa,

Kwanza nianze kwa kuwapongeza Chadema kwa kutumia strategy kali ili " kuwazuga" mashabiki wenu wa mitandaoni ambao wao kazi yao ni kuwapa moyo na siku ya kupiga kura hawaendi kuwapigieni kura.

Hivi ni nani asiyetaka ruzuku ili chama kiendelee kufanya kazi yake? Msitudanganye hapa mliwaruhusu hawa wakina Mama waende wakaape na pia mkaandaa strategy ya kupambana na wanazi wenu wa mitandaoni na kwakweli mmefanikisha.

Kwasasa ni bao moja kwa moja mmesawazisha, wao hawakuenda kuwapigia kura na mlipo waamasisha hawakuitikia wito wenu na nyie mkaamua tusikie ruzuku nendeni mkaape ili kila mtu apambane na lake.

Hongereni sana Chademaa law strategy kali namna hii.
Hongereni wakina Mama kwa ushujaa,
Hongereni Watanzania kwa umoja na mshikamano.
 
Mkuu kuna Trillion 2 zinagombaniwa mjitaidi mzipate.
Karata zenu zote ndo mnazimaliza
 
Wanasema walipata vitisho vya kushambuliwa .
Wakaomba wapewe muda!!

Hivi ni akina mama gani watakiamini tena Chama kisichothamini mchango mkubwa walioutoa wale akina mama?....
Eti uchaguzi ukiisha unaacha makovu! Uchaguzi au uchafuzi! Ushauri wako ni mzuri ukiupeleka Lumumba waanze wao kujitathimini kama wako kwenye raiti traka!!! Ila Mungu ni mkali wameanza wenyewe kuparurana uchaguzi wa meya Arusha ni balaa tupu!
 
Kabisa wamemridhisha kigogo na maria sarungi!
Nawasalimu wanajukwaa,

Kwanza nianze kwa kuwapongeza Chadema kwa kutumia strategy kali ili " kuwazuga" mashabiki wenu wa mitandaoni ambao wao kazi yao ni kuwapa moyo na siku ya kupiga kura hawaendi kuwapigieni kura...
 
Baada ya kusikiliza kile kilichoitwa maamuzi ya kikao cha kamati kuu haya ndiyo nimejionea.

1. Wamevuliwa uanachama wa Chadema kwa sababu hawajatokea kuhojiwa na kamati kuu na siyo sababu ya ubunge wa viti maalum!

2. Wameambiwa wanaweza kuandika barua ya kuomba radhi ili warejeshewe uanachama wao!

3. Ndani ya siku 30 wanaweza kukata rufaa kwa kupinga hukumu ya kamati kuu kwenye baraza kuu la Chadema!

4. Chadema iliwaandikia barua mara mbili kuwabembeleza wafike kuhojiwa na kamati kuu pia kamati kuu ililazimika kubadili eneo la kuwahoji kutoka makao makuu ya chadema hadi kwenye hoteli ya kitalii ili kulinda usalama wao.!

Mtu ambaye ni msaliti unaweza kumbembeleza kwa kumwandikia barua mbili na hadi kuingia gharama za kukodi hoteli ili kumuhoji?

Ni vipi msaliti aruhusiwe kuandika barua ya kuomba radhi tu na atarudishiwa uanachama wake?

Mbona Zito Kabwe na Kitila Mkumbo wakati wanafukuzwa hawakupewa nafasi ya kuomba radhi na kurudishiwa uanachama wao?

Hapa kuna sinema inachezwa na ndani ya siku 30 tutaona matokeo yake, kama mtu alikuwa tayari kutengeneza igizo la kuangushwa na konyagi na kisha kusingizia wasiojulikana, hapa kuna mengi yanakuja.
 
Hongereni CDM kwa kuwa na msimamo hata kama unaumiza vipi, hakuna mtu alie juu ya chama.

Hii ilikuwa ni karata muhimu sana kwenu, mmeicheza vema.
 
Hongereni CDM kwa kuwa na msimamo hata kama unaumiza vipi, hakuna mtu alie juu ya chama.

Hii ilikuwa ni karata muhimu sana kwenu, mmeicheza vema.

Sent from my TECNO-C9 using JamiiForums mobile app
Tumia akili wanawazuga tuu hao ukweli ni kwamba waliwaruhusu, Chairman ni Businessman anaachaje pesaaa.[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Sasa na wao viongozi si wawe wanaandamana peke yao kutuwakilisha kama wanavyotuwakilisha bungeni ?

Au kwenye shida tuwe nao ila kwenye raha na kula viyoyozi bungeni wale peke yao.

Aisee maandamano na migomo ni njia za walio kosa mbinu za ukombozi na kukata tamaa.
Bila hayo Bashir wa Sudan angeondoka?
 
Mbona umepaniki hivyo,au mpango wenu umebuma hivyo inawauma??? Mtavuna mlichopanda!
Hivi nyie Mnawasikiliza akina Mbowe mnafikiri wana nia njema na nchi hii?
Jiukize kwa nini Mnyika hakugombea ubunge?

Kwa nini wagomee viti maalum ?
Hivi unaweza kuumbia umma kuna umuhimu gani wa kuwanyima wale akina mama fursa ya kwenda bungeni kuendeleza mapambano ndani ya bunge ?

Je, wewe binafsi unafaidika nini wale wa kina mama kunyimwa fursa hiyo iliyopo kikatba kwa kuchukua form na kuzikalia ofisini tu bila kuwapa fursa ya kutoa maoni yao kuwa waende au wasiende?

Demokrasia ni pamoja na kuwasikiliza wale waliopinga wazo la kuvunja katiba ya nchi kwa kukataa kupeleka wabunge wa viti maalumu.

SWALI la kujiuliza ni Je, Mbowe ametumia kifungu kipi cha katiba ya nchi kuzuia wabunge waliotakiwa kuteuliwa kikatiba kuingia bungeni!

Je, kuna sheria inayoruhusu Chama cha siasa kuamua mambo yake kinyume na katiba ya nchi!?

Je, ni kifungu kipi cha katiba ya Chadema kinachowapa mamlaka viongozi kuacha kupeleka wabunge wa viti maalumu Bungeni kwa sababu za kizushi kuwa uchaguzi ulivurugwa bila ushahidi wa kutosha zaidi ya kulalamika tu?
Ni lini uchaguzi ulikua huru na haki ?

Kama hakuna sheria wala katiba inayowaruhusu viongozi wa Chama cha siasa kukiuka matakwa ya kikatiba basi Mbowe anapaswa kukamatwa na kuburuzwa mahakamani pamoja na Mnyika na kufungwa jela miaka mia.
 
Hotuba iliyotolewa na mwenyekiti wa chama Freeman aikaeli Mbowe ni hotuba nzuri imenipa nguvu Kubwa kuendelea kukijenga chama. Kamati kuu imewatendea haki wanachama kwani kila mwanachama alisubiri kwa hamu maamuzi ya kamati juu.

Kama kamati kuu ingelifanya kinyume na matarajio ya wanachama hakika chama kingechungulia kaburi, nami nilikuwa nimeahidi kuwa iwapo wasingelifukuzwa ningelijinuga na chama cha ACT, lakini kwa sasa Chama kimeimalika zaidi kuliko kipindi chochote kile,

Kwa maamuzi haya ya kamati kuu ninatamuka kuwa chadema ni chama makini ndio maana CCM wanatumia kila njia ya kukidhoofisha .

Mungu ibariki Chadema,
 
Back
Top Bottom