Kampuni inayomiliki Tigo yabadili jina, sasa ni Honora Tanzania

HOME SHOPPING CENTRE walishamiri sana enzi za VASCO DAGAMA; alipoingia JIWE kama Rais kumbadili Kikwete nao wakabadilika na kuitwa jina jipya la GSM!!!!
GSM = Gharib
Home shopping = said

Ni ndugu ila sio kampuni moja, GSM ilikuwepo Zamani tu

Nitakupa mfano wa Biashara ya GSM ni battery za Tiger head, hizi battery zipo toka Nasoma msingi,

Said wa Home shopping alipata majanga akamwagiwa Tindikali hii ili tokea 2013 akashindwa kufocus na biashara akauza kila kitu na kwenda kutibiwa muda mrefu.

Alirudi kipindi cha Magu na kufungua kampuni kibao, in short huyu Said ni mjasiriamali Genious sana, Akileta kitu chake hata kkoo ujue masaa tu kinaishia, ni mtu mwenye Experience na choice nzuri ya Biashara, alianza kidogo kidogo sasa hivi Ana makampuni Makubwa mengi tu, si mtu wa kujionesha.
 
Ni kwamba wawekezaji hupewa miaka 5 ya operation bila kulipa kodi then baada ya huo mda ndonhuanza kulipa kodi. Jamaa wanafanya 3 ama 4 years wanauza kwa madai wamepata hasara. Atakayekuja anaaza tena miaka 5 bure kudadeki
MIC walikuja Tanzania mwaka 1993, na wamekuwa na umiliki huo hadi walipowauzia hao wa Mauritius wanaojiita Honora. Hoja yako haina sense
 
Aliyekwambia ukibadilisha jina la biashara wakwepa kodi nani?
Huwezi windup biashara bila kumalizana na TRA


Kumbe HIMARS ni mbumbumbu wa sheria za kodi kiasi hiki


Kwani si kampuni imenunuliwa na Rostam na wawekezaji wenzake? Mbona sisi Watanzania tunapenda kulalamika hivi? Kampuni zinauzwa na kununuliwa kila siku huo ndo uwekezaji wenyewe.


Wataalamu wetu wa masuala ya kodi, uchumi na uwekezaje mnatuyumbisha kwenye huu uzi. Mpaka sasa nimewasoma wote lakini bado sijajua ni nani yupo sahihi.

Kwanini msilete facts mnabisha na kuchambana tu? Kuna hizo sheria na articles zipo kwanini msituwekee basi tusome hata wenyewe?

Mbona sisi kwenye masuala tuliyobobea huwa tunatoa ufafanuzi usiowachanganya wengine washindwe kujua yupi yupo sawa??
 
🤣🤣Na Salah je?
Yule mwenye benk yake ya ndani kariakoo?
Kuna mdau alileta mada ya kudhulumiwa naye hapo kariakoo
 
Unadhani kuwekeza ni jambo rahisi ?!!!

Hata mahakamani walioweka "plea bargain" si wajinga....[emoji1787]
 
Sheria ndio zimetoa huo mwanya
Mimi nikisikiaga mtu anasema TRA INA sheria legelege huwa namshangaa sana, huenda mtu huyo ni mfanyakazi na hajui lolote kuhusu hii taasisi inayoitwa TRA.

Naweza kuelewa mtu akiniambia tatizo ni rushwa nitskubaliana na wewe.

Kwa msomi TRA ni kikwazo kwa wawekezaji na wafanyabiashara, kama hufanyikazi na TRA huwezi kujuwa hii mamlaka ilivyo chenga.

Kwa Mtanzania wa kawaida ukitaka kufunguwa tu kampuni unaweza kuachana na ndoto hizo kabla hata ya kufunguwa kampuni yenyewe.

Vitu basic kama Tax clearance na VAT registration kwa TRA vikwazo vyake mpaka unashangaa ni kweli Watanzania wanaoambiwa wajiajiri hiyo kauli na kweli au wanawasanifu?

Kuna vijana hawa waliotoka vyuoni ndio wapuuzi kabisa utadhani wamezaliwa Paris kumbe wamezaliwa na kuishi Tanzania mazingira yetu halisi wanayajuwa, lakini wakishavaa vitai vyao vile kama mijusi na visuruwali vya kubana huwa wanaona dunia yote ni yao kumbe lengo kuu la TRA ni kukusanya mapato na siyo kuwakwaza watu wanaokuja kwa hiyari yao kukaa kwenye mfumo, hasa, hasa TRA Ilala ndio maandazi kabisa.
 
Nasikia uso umeungua ndio maana haonekani hadharani
 
Kama nitakuwa nimekuelewa vizuri, yani unachukuwa Mgodi wa makaa ya mawe ambao kwa sasa makaa ni hot cake, halafu baada ya miaka mitatu unaacha? Unauza share?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…