Kampuni Kutoka China Kujenga Daraja la Dar- Zanzibar

Kampuni Kutoka China Kujenga Daraja la Dar- Zanzibar

Hata kulijadili hili ni ujinga sana, hata haiingii akilini, tuna changamoto nyingi sana zinahitaji utatuzi.

Anga na maji vinatosha!!
 
Upembuzi yakinifu ni hatua muhimu sana kabla ya kufanya uwekezaji. Kuna wakati tulinunua boti ya kufanya safari za Dar Bagamoyo bila upembuzi yakinifu, bila shaka tunajua hasara tuliyopata.
Safi 2050 daraja itaanza kujengwa nguzo ya kwanza bagamoyo!
 
hahahaha, ni kipaumbele chetu kwasasa?.

hakuna maeneo mengine yanayohitaji quick investment na short time return kwasasa?

Kwanini asitafutwe muwekezaji na kuingia parnership na serikali tuchimbe chuma cha Liganga na Mchuchuma kwa haraka ili bei ya chuma ipungue, then tutafute kampuni with partner na watanzania wakajenga plant kwaajili ya kutengeneza electric cars na huku tunaweka nguvu kubwa ya kuchimba graphite pale Lindi vs mass production batteries plant kule kusini?

Mkuu kwani hawajui...hii mipango inahitaji mwamba jasiri...mwenye uthubutu...Mundele anatisha anakupa proposal hupangui..unaitikia tu..Yes sir na iwe hivyo..
 
Serikali imeanza mazungumzo na Kampuni ya China Overseas Engineering Group Company (COVEC) ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika ujenzi wa daraja litakalo unganisha Tanzania Bara na Zanzibar.

Naibu Waziri wa Uchukuzi Godfrey Kasekenya amesema bungeni leo Aprili 28, 2023 kuwa Mazungumzo hayo yameanza Machi 11, 2023 na yalihusisha wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Ujenzi kwa upande wa Tanzania Bara na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa upande wa Zanzibar.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mwantum Dau Haji aliyetaka kujua mpango wa serikali kujenga daraja hilo, Naibu Waziri Kasekenya amesema bado mazungumzo yanaendelea na serikali inakusudia kujiridhisha na teknolojia zinazotumika katika ujenzi wa madaraja makubwa kabla ya kuanza ujenzi.

“Daraja hili litajengwa kwa kushirikiana na sekta binafsi kwa utaratibu wa PPP (Public-Private Partnership),” amesisitiza Kasekenya.

#HabarileoUPDATES
View attachment 2602214
Mods unganisha huu uzi tayari Kuna Uzi humu uko page ya 5
 
 
Serikali imeanza mazungumzo na Kampuni ya China Overseas Engineering Group Company (COVEC) ambayo imeonesha nia ya kuwekeza katika ujenzi wa daraja litakalo unganisha Tanzania Bara na Zanzibar.

Naibu Waziri wa Uchukuzi Godfrey Kasekenya amesema bungeni leo Aprili 28, 2023 kuwa Mazungumzo hayo yameanza Machi 11, 2023 na yalihusisha wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Ujenzi kwa upande wa Tanzania Bara na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa upande wa Zanzibar.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mwantum Dau Haji aliyetaka kujua mpango wa serikali kujenga daraja hilo, Naibu Waziri Kasekenya amesema bado mazungumzo yanaendelea na serikali inakusudia kujiridhisha na teknolojia zinazotumika katika ujenzi wa madaraja makubwa kabla ya kuanza ujenzi.

“Daraja hili litajengwa kwa kushirikiana na sekta binafsi kwa utaratibu wa PPP (Public-Private Partnership),” amesisitiza Kasekenya.

#HabarileoUPDATES
View attachment 2602214

Payback period yake ni muda gani? Account rate return inasemaje ili kujua iyo Capital Expenditure itakuwa na faida zipi? Feasibility na Appraisal zake zimekaaje? Sio tu mtu anatoa majibu kiholela afu nawe unabeba unayaleta kwenye hii platform aisee
 
Kampuni ya China Overseas Engineering Group imeonesha Nia ya kujenga Daraja la km 40 Kati ya Dar na Zanzibar,Naibu Waziri Kasekenya amesema Bungeni..

My Take
Kama Daraja hili litajengwa linaweza kutumia nusu ya gharama za Kujenga SGR.

Swali Je Tunalihitaji Kwa Sasa?



Mimi ninaunga Mkono Serikali kuunda Daraja litakalo unganisha Dar na Zanzibar ni maendeleo makubwa tutapata wageni wengi kuja kutembelea na tutapata pesa za kigeni nyingi kwa ajili ya hilo daraja la Dar to Unguja wanaopinga wache wapinge hawapendi maendeleo ya nchi yetu. Ona Video wenzetu wazungu wanavyo endelea kutengeneza madaraja yanayopita juu ya bahari na chini ya bahari. Sisi tunapinga paipo an limu yoyote ile.

The Insane Scale of Europe’s New Mega-Tunnel​



Türkiye to open world’s longest and tallest suspension bridge in Canakkale​



World's longest sea bridge - BBC News​



How the world's longest underwater tunnel was built - Alex Gendler​



Inside The World’s First Undersea Roundabout​



Eurasia Tunnel: Tunnel beneath Bosphorus is now in business​



The Longest Bridge In The World​


 
Daraja la nini? Jamani, tuna mambo makubwa mno ya kufanya, daraja la nini?
 
Mradi usiokuwa na tija kabisaaaa!.
Kwa kuwa unajengwa kwa mpango wa PPP, hauna tabu yoyote, kila jambo linalofanyika ni endeleo kwa taifa letu, chochote cha kujenga iwe kiwanda au lolote lile ni MAENDELEO.
#stop ignorant!
 
Payback period yake ni muda gani? Account rate return inasemaje ili kujua iyo Capital Expenditure itakuwa na faida zipi? Feasibility na Appraisal zake zimekaaje? Sio tu mtu anatoa majibu kiholela afu nawe unabeba unayaleta kwenye hii platform aisee
Wewe upinde umetokea wapi? Haya maswali unamuuliza Nani? Sometimes kama hujui kitu kaa kimya lofa wewe..
Heading inasema "kampuni ya China yaonesha nia" unauliza feasibility wakati kilakitu bado hakijakaa sawa?
 
hahahaha, ni kipaumbele chetu kwasasa?.

hakuna maeneo mengine yanayohitaji quick investment na short time return kwasasa?

Kwanini asitafutwe muwekezaji na kuingia parnership na serikali tuchimbe chuma cha Liganga na Mchuchuma kwa haraka ili bei ya chuma ipungue, then tutafute kampuni with partner na watanzania wakajenga plant kwaajili ya kutengeneza electric cars na huku tunaweka nguvu kubwa ya kuchimba graphite pale Lindi vs mass production batteries plant kule kusini?
Tuna hayo mawazo kaka we acha tu.
 
Zanzibar ina hela gani za kujenga daraja wakati bajeti ya nchi nzima ya Zanzibar 2022/2023 ilikuwa Tsh trill. 2.5 kwanza itaweka dhamana ipi kuchukua mkopo wa bank labda kama alivyowahi kusema J.k kuwa walichonacho ni virungu vya polisi tu.
True Zanzibar ukitoa watalii hakuna cha maaana.
 
Mimi ninaunga Mkono Serikali kuunda Daraja litakalo unganisha Dar na Zanzibar ni maendeleo makubwa tutapata wageni wengi kuja kutembelea na tutapata pesa za kigeni nyingi kwa ajili ya hilo daraja la Dar to Unguja wanaopinga wache wapinge hawapendi maendeleo ya nchi yetu. Ona Video wenzetu wazungu wanavyo endelea kutengeneza madaraja yanayopita juu ya bahari na chini ya bahari. Sisi tunapinga paipo an limu yoyote ile.

The Insane Scale of Europe’s New Mega-Tunnel​



Türkiye to open world’s longest and tallest suspension bridge in Canakkale​



World's longest sea bridge - BBC News​



How the world's longest underwater tunnel was built - Alex Gendler​



Inside The World’s First Undersea Roundabout​



Eurasia Tunnel: Tunnel beneath Bosphorus is now in business​



The Longest Bridge In The World​


Naomba unisaidie! Ni faida gani Watanzania bara watazipata kutokana na daraja hilo tofauti na sasa?
 
Sina wasi wasi hili daraja ni ndoto tu halitajengwa katika karne hii. Wachilia mbali mambo ya gharama eneo linapotaka kujengwa litahitaji mipango mikubwa sana. Ikitajwa kujengwa baina ya Dar es salaam na Zanzibar lazima daraja hilo litaingia./Litatokea maeneo ya mpakani baina ya dAR na Bagamoyo sijui ni Bunju au wapi pale.Eneo hilo bado lina mawimbi makali ya bahari na bahari inapochafuka ndio kazi zaidi. Hilo daraja itabidi liwe pana ili kutoa njia za uokozi na si njia mbili tu.Tuseme kumetokea kimbunga cha ghafla na gari ziko katikati ya daraja.Lazima ziwe na njia ya kukatisha safari na kurudi ilikotoka.Haitowezekana gari ikishaelelekea Zanzibar basi iwe ni kwenda tu.Hii siku ikitokea athari hiyo ya hali mbaya basi tutapoteza watu wengi baharini.
 
Back
Top Bottom