Kamuachisha shule binti yangu, kamuoa. Anasema hakuna wa kumfanya lolote Serikali hii

Mbona unaficha namba zenu?
Weka wazi kila kitu kama kweli unataka msaada.
Maana huyo jamaa ni wa kwenda jela tu hamna kitu kingine.

Weka wazi, watu wakipost kwenye blog zao atamrudisha haraka sana.
 
Kwanza tuanzie hapa mtoto anasemaje, ukute ukuni umemkolea na kataka mwenyewe ww unaangaika tulia utakufa kabla ya Siku zako.

Ukimpeleka polisi mtoto akisema mimi nataka utafanya nn, sidhani kama uyo mwamba kamfungia mwanao ndani
 
Umechukua hatua gani zaidi ya kulalamika hapa?

Je umefika Polisi dawati la jinsia?
Je umefika Sengerema kwa Mkuu wa Shule na Afisa Elimu Sekondari kuyaripiti haya na kutoa ushahidi?

Je umefika mtaa anaokaa huyo Mkweo katika ofisi ya Mtaa/Kijiji/Kata kutoa malalamiko haya?
Haya mambo ni madogo yanayopaswa kushughulikiwa katika ngazi ya Kata.
 
Mama kama jamaa ana maisha mazuri mwache tu mtoto wako jifanye kama hujui ,navyomfikiria huyo mtoto wako hana uwezo wa kufika mahali kielimu bora aanze maisha tu na dingii
 
tuhangaike hap kumbe wenyewe wamependana,ila wewe mama hupendi mkwe mzee.
 
Sawa ila tuanze na binti yako, A level ameshajitambua sana tu. Kwanini hakuona umuhimu wa kumaliza masomo yake.

Anyways hapo hakuna mapenzi naye ataachwa anytime anyday na huyo baba atamwaibisha.

Sijui ila pole kwako
 
Namba wamezificha Admins
 
Mie nilifikiri ni Ma Muganyizi, nisingekuelewa
 
Nitumie namba zake PM nidili naye huyo khanithi.
Anasema hakuna wa kumfanya kitu,subiri atajamba cheche very soon!
 
Kidatu cha sita ni mtu mzima huyo kazi iendelee
 
Binti yako ni moja kati ya mabinti wasiojitambua kabisa kweli ameshindwa kujitesa ili aje akusaidie wewe mama ake?....

Form 6 sio mdogo maana tunakutana na form 6 wengine licha ya yote ila wanasoma kwa kujitesa ukiuliza wanasema wanasoma kwaajili ya mama zao why asiwe binti yako......

Pia huyo mzee ni moja kati ya binadamu wa ajabu, hapo mama akisema atumie njia chafu huyo baba akapata matatizo atarudi kwa mama analia apewe msamaha...... kweli dunia ni ngumu sana
 
binti yako yeye anasemaje , ila punguza uongo kidato cha sita wamemaliza mitihani tayari kwahiyo hakuna shule yenye form six! Navyoona huyo binti ameamua kueolewa na huyo mzee baada ya kumaliza mitihani yake
 
mzee acha unyonge wa kijinga. huko hakuna mapanga au mikuki. mvizie malizana naye kimyakimya.
au kachukue mahari upate mkwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…