Kanisa Katoliki lapoteza Mapadri 25 na Watawa 60 kwa tatizo la upumuaji ndani ya miezi miwili

Kanisa Katoliki lapoteza Mapadri 25 na Watawa 60 kwa tatizo la upumuaji ndani ya miezi miwili

Usidanganye!!! Vifo marekani vilifikia kiwango cha juu Sana kuanzia February kipindi ambacho huyu mshabiki wa LGBT alipoingia madarakani. Ingia mtandao wa worldometer coronavirus live updates kuhakiki hilo. Kipindi chake vifo kila siku vilifikia hadi 3,000!!!

Pitia data tena
 
Kwa nini hatujiulizi - iweje mataifa yaliyo kubali baadhi ya taia wake kufanyiwa majaribio ya chanjo za Oxford, ndio mataifa hayo hayo yaliyo kumbwa na aina mpya hatarishi ya ugonjwa wa COVID-21 - hii inaleta picha gani?

Jana nilishangaa sana nilipo wasikiliza wataalamu wa immunology wa huko Ulaya na Merikani wakisema variant mpya ina uwezo mkubwa wa kukwepa/by pass kinga ya mwili - hivi inaingia akilini kwamba virusi hivi vime mutate tu ili vikwepe kinga ya mwili au kuna wataalamu wenye ajenda zao za siri ndio wame chezea virus hivi ili viwe more virulent - baada ya kuona COVID-19 haiwui Waafrika wengi kama mkewe Bill Gates alivyo tabiria Bara la Afrika kwamba ugonjwa huu ungetuuwa kama nzinge!!

Tukumbuke kwamba mfuko wa Bill Gates na mkewe ndio wanafadhili Big Pharma Companies zinazo zalisha chanjo, wana sayansi wa makampuni hayo wana uwezo mkubwa wa kutekeleza kile mfadhili wao anacho wa-instruct wafanye - moja wapo ikiwa ni kutujia na variant mpya ya virus kama plan "B" kuzitia taharuki ili Serikali zikubali kununua chanjo za Bill Gates fasta, na kwa Afrika zitaingizwa batch za chanjo zenye malengo ya ku depopulate gracefully Bara la Afrika kwa kupitia kuingilia mfumo wa uzazi wa akina mama,pia kuongezea kichocheo cha kinga ya mwili ku-over react na allergies za kawaida tu watuwaaanza
So unfortunate hii ikisemwa na mzungu ndiyo itaonekana ni science, wewe mbuntu basi ni ushirikina....Kuna watu hawasomeki kwanini walipewa akili kwenye vichwa vyao kama hawawezi ku ng'amua vitu simple na direct kama hivi mpaka mzungu aseme...
 


Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Padri Charles Kitima amesema kuwa ndani ya miezi miwili iliyopita zaidi ya mapadri 25, masista na manesi 60 na wenyeviti wawili wa Baraza la Walei wamefariki dunia kwa sababu mbalimbali ikiwemo changamoto ya upumuaji.

Ameongeza kuwa vifo vinaendelea na kuwataka Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari na kuacha mzaha katika katika suala zima la Corona.

Huyu Mungu si hirizi, anataka kila binadamu awajibike na atumie uwezo wake kufikiri. Corona ipo, unaambiwa chukua tahadhari unasema mimi nasali. Mungu wetu anataka watu wawajibike, si kusema tu, tunasali - Ameongeza Padri Charles Kitima

🙏🙏🙏
 
Usimuaibishe mzazi wako. Kwamba unaweza kupiga ban makanisa?. Kweli
Kabisa mkuu! Tunaunga mkono wito wao wa kuchukua thadhali, lakini hii ya kujaribu kutuonesha kama kuna mtu hawajibiki wakati wao wana mamlaka ya kufunga hayo makanisa na kunusuru mapadri wao inashangaza sana.

Shida ni sadaka watatoa wapi?

Yani ningekuwa mimi Magu, ningepiga ban misa kwa miezi 3 tu uone kama hawajaenda kupiga magoti.
 
Mzee ajitathimini sana kwenye hili suala la COVID-19 Vaccine - anaweza kujikuta kabakia peke yake!!
 
Hata watu wote wakikataa, ukweli utabaki kuwa Tanzania tuliponywa na Mungu dhidi ya Corona!! Mungu apishe mbali!! Tanzania tulionja tu harufu ya corona, hata sasa tunasikia harufu tu ya corona....
Amen...May God have mercy on us!
 
Mzee ajitathimini sana kwenye hili suala la COVID-19 Vaccine - anaweza kujikuta kabakia peke yake!!
What is the problem akibaki prke yake?

Kuna jinsi Mungu anaweza mheshimisha kwa utukufu wa jina lake..What if mataifa yote wakichanjwa na bado wakaendelea kufa na corona mpaka wakakubali kuwa hakuna chanjo?

Hufikiri hilo la wao kushindwa unamfikiria tu yeye kushindwa?
After all hakuna mashindano hapo...He is just not accepting everything because all are doing even of they are not certain...So far hakuna certainity kwenye hiyo chanjo yao let him be!
 
Hadi nimemuogopa hyo jamaa.Yaani bado kuna watu wanaamini kuwa bila sayansi tunaweza kuvuka pia.
Do not stoop so low...Science siyo lazima iwe hiyo ya mzungu...Science ni uwezo wa mwanadamu kung'amua what might be a solution to a specific problem ambayo kila mwanadamu amepewa intrinsic capability ya adaptation to any problem ambayo ndiyo science number moja, hizo zingine ni ego tu. It can happen by chance for new facts which after a number of repetition inaweza kuwa repeated....Acheni kudanganya raia...Huko vijijini unadhani hawafanyi science?
 
Msimshirikishe Mwenyezi Mungu kwenye maamuzi yenu nyie CCM. Mungu ametupa weredi wa kutambua na kujikinga na majanga hapa ulimwenguni. Soma kifungu hiki cha Biblia takatifu.

Hosea 4:6​

Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako.
 
Ka

Aiseee sasa Kama Mungu si hirizi kwa nini mapadre na maaskofu katoliki husisitiza watu kumuomba Mungu wakati yeye si hirizi? au kinga au msaada unaoonekana tele wakati wa Mateso yawe ya Corona au vinginevyo?

kanisa katoliki matapeli waumini wanaenda jumapili kufanya nini kanisani kila dominika wakati Mungu sio kinga yao na si hirizi? mkatoliki shituka .ina maana lengo watoe sadaka tu na kuondoka wakati huyo Mungu mnayesema mpe sadaka hana msaada kwao wala sio kinga yao?

Wakatoliki mnapeliwa .Hili tamko alilotoa ni la kipagani Mungu wetu ni kama hirizi ni kinga yetu mateso yasitupate yawe corona au majanga yeyote .Zaburi inatamka wazi kuwa Mungu wetu ni kimbilio na nguvu na msaafa wetu unaoonekana tele wakati wa mateso.Ni kimbilio letu iwe kwenye corona nk ndiye hirizi yetu.

Kwangu mimi Mungu ndiye hirizi yangu
Huna tofauti na wale wasabato wanaotaka kwenda ulaya Bila nauli Wala tiketi..wakidai maombi yatawasafirisha...OMBA SANA MUNGU WAKO JITUME SANA KUFANYA KAZI
 
Kanisa limepoteza Imani hivyo wanavuna walichopanda.

Tunasahau hata wimbi la Kwanza hatukulishinda kwa nguvu zetu.

Petro alianza kuzama majini baada ya kupoteza imani.
Watakao kuelewa tuko wachache sana!

Yaani wimbi la kwanza tumelipita hadi mataifa yakashangaa, jiulize walio omba kuchezea mechi zao hata uwanja wa Taifa wakidai kwao kuna Corona!
 
Du!.. Huyu padri anamlalamikia nani sasa juu ya vifo vya mapadri wenzake na watawa?, Hivi tamko la Serekali la kukiri kuwa UVICO upo Tanzania ndilo lingebatirisha amri ya binadamu kufa ambayo ni ya uhakika kwa asilimia mia? Mimi nadhani angefurahi kuwa watawa na mapadri kwa wingi sana mwaka huu wameitika wito wa muumba wao na kwa kuwa wameishi maisha ya kiroho na kufanya yanayompendeza Mungu kama wanavyowafundisha waumini wao hivi sasa wamekaa mbinguni upande wa wenye haki, anapaswa kumtukuza Mungu kwa hilo na siyo kuingilia mambo ya wanasiasa wanaopinga na kukosoa kila kitu.
 
Ndugu Wanahabari, nadhani ni upuuzi wa kupindukia kuendelea kumsikiliza huyu Musiba, as 1. He is 100% inconsistent, 2. He has no basis for speaking and I am strongly discovering that he is looking for DC, RC, or any position to fill his empty stomach.
Hivi Wa-Tanzania, what is so special with Tanzania to the extent that every country on earth has the bad intention of harming us and not other countries. Musiba's claims are baseless.
 
Sasa ukweli huu niliyo utaja hapo juu ndio unamfanya Rais wetu JPM akatae kuingiza nchini chanjo zenye utata mkubwa
Sasa ni nini kinamzuia Raisi wetu kununua chanjo za covid 19 za laki mbili halafu awape wanasayansi wetu wazichunguze halafu watupe muongozo
Kuliko kupanda jukwaani bila ushahidi wa wanasayansi wetu wa Kitanzania bila utafiti
 
Kosa muhimu walilofanya wakatoliki na madhehebu mengine yote ni kuchelewa kujua na kukemea maovu yaliyoanza kuonekana mwanzo kabisa wa utawala wa Magufuli.

Aliwapumbaza na wakati mwingine kuwapa vitisho wasikemee, na wao wakakaa kimya wakidhani yatakwisha au yatafikia mwisho.
Pengine alijaribu kuchonganisha, dini na dini, kama waislam na wakristo ili pasiwepo na sauti moja ya kukemea mabaya yanayofanyika.

Wao, dini hawakuuona mchezo huu.

Kukaa kimya kwao kulichukuliwa kukubali au kuogopa, kwa hiyo Magufuli akaona mlango wazi wa kufanya lolote bila ya mtu, wapinzani wala dini kusema lolote.

Matokeo yake ndiyo haya sasa hivi.
 
Inasikitisha sana kwa kanisa kutoa kauli kama hii...Hii dini hapa imesimama kama taasisi na wala siyo kuongozi wa kiroho...Kanisa katoliki haliamini katika abortion na wala family planning je hiyo siyo science? Au science inakuwa valid pale ambapo interests zako zimelalia?

Kanisa linashindwa kuelewa ndiyo lililotufikisha hapa baada ya kuwaleta watu wa bara lingine kuchukua ardhi yetu, kuharibu utamaduni wetu, kuleta kila aina ya huzuni na ukoloni ambao leo umeendelea kufumga minyororo....Its just a roman empire in operation...Vueni kanzu vaeni sare za chama acheni kutuvuruga...Yes I said and I repeat...

Kufa kwa kiongozi wa dini kwenye huduma ya kuwaokoa wengine ni ushujaa siyo laana...Mungu na akuhukumu sawa sawa na roho wake wa haki Fr. Kitima...Unaaibisha imani!
Hivi unaelewa unachoandika, au unajipigia pigia tu kujaza maneno yasiyokuwa na maana?

"...abortion na wala family planning, je hiyo siyo science"? Nani kasema ni sayansi au ni sayansi, na inahusu nini na mjadala uliopo hapa.

Andiko lote, hata kama lingeandikwa na mtu aliyekwenda shule, lakini akawa ameliandika baada ya kilevi fulani lisingeweza kuwa mchanganyiko kama hili uliloleta hapa.

Sasa sielewi wewe ni mtu wa aina gani!
 
kufa tutakufa na wengine wataishi,hakuna binadamu anayeweza kuchukua tahadhari ya kifo
 
Tunapotangaza watu wachukue tahadhari kwa sauti ndogo huku hizo tahadhari tukiziponda kwa sauti kubwa ni unafiki.

Zile hatua tulizochukua kipindi Corona imeanza zilisaidia kufanya watu wachukue tahadhari kubwa! Hii handling ya Corona inakwenda kutuvua nguo sasa.
Imenibidi niku'quote' tu kwa haya uliyoandika leo, hata kama sitaongeza la ziada juu yake.

Ahsante.
 
Back
Top Bottom