StudentTeacher
JF-Expert Member
- Jan 30, 2019
- 4,153
- 4,301
Ubatili mtupu na kujilisha upepo.Kwa kweli amekosea kwenye namba 3 eti huna hela huzikwi ??
Ni kuwa kama umejitenga na shughuli za kanisa nao wanakutenga huduma za kanisa
Kuna kutoa sadaka na kutupa sadaka.Mkuu mengine siwezi kuzungumzia..ila suala la sadaka sio option...Watu wanachoma milions kidimbwi + matumizi ya hovyo kwenye sherehe kama bday alafu akiskia kuhusu mchango au sadaka tu hata kutoa 10000 anahisi kama anapigwa..Mahusiano na Mungu sio rahisi kihivyo lazima uinvest..after all ni maamuzi yako pia...Kumtolea Mungu sadaka mtu hataki,kusaidia ndugu,marafiki,familia na wengine ambao ana uwezo wa kusaidia hataki pia sasa mtu huyo anakaa kundi lipi?
Watu wako tayari kuchoma pesa zao kwa mambo ya kidunia lakini hawataki kumrudishia Mungu shukrani na haohao wanategemea Mungu atende miujiza kwenye maisha yao..Its Not Fair at All.
Kweli kabisa mkuuKanisa linapita nyakati ngumu sana. Nyakati hizi sisi akina baba tusiposimama kuijua imani vema na kuongoza familia badala ya kuwaachia wanawake mambo ya imani utaangamiza familia yako kama si leo ni kesho!
Ukristo umevurugwa sana sana! Makanisa mama yaliyokuwa nguzo nayo yanapigwa mawimbi ya nguvu! Walokole ndio wamevurugwa kiasi cha kutisha! Tuliombee Kanisa!
Kuhubiri injili ya kuacha dhambi na kazi ya msalaba na kuyaishi yale tunayoyahubiri kama wahubiri ndio njia pekee ya kweli na uzima.
Vinginevyo hata sadaka tunazotoa au zinazopokelewa makanisani zinaweza kuwa machukizo mbele za muumba.
Maana zipo taratibu za kutoa Sadaka kama agizo lisilo shurti.
Nikuulize wewe, Kabla ya kuwalaumu wengine...Hizi ndio changamoto za kanisa la Tanzania. Tuzidi kumuomba Mungu.
1. Mikutano ya The Big Octoba na The Big Novemba iliyokuwa inahuhubiri kuacha dhambi na kumrudia Kristo imekufa.
2. Mwamposa na Suguye wanauza vifaa vya uponyaji mafuta, maji, keki na vitambaa badala ya kuhubiri watu waache dhambi, pia hawataki kufungua matawi mikoani na kupanda makanisa.
3.RC nao wamechachamaa kwa michango kuanzia kwenye jumuiya hadi Parokiani. Huna hela huzikwi.
4. Mwakasege naye amechachamaa na masomo ya sadaka mwanzo mwisho, mfano semina ya Mbeya (26-30 Oct, 2022) somo ni sadaka tu hakuna kingine.
5. KKKT nao hawaeleweki wachungaji wanaowaiga wapentekosti/walokole ndio wanapata umaarufu mfano Kimaro na Mgogo wale wanaohubiri kilutheriluther hawana chao wala umaarufu.
6. TAG/EAGT hawana wainjilisti wakitaifa kama kina Moses Kulola wamebakia wapigaji tu.
7.Viongozi was dini kugombania mialiko sherehe za kitaifa ili wakalambe asali no aibu.
INAUMA SANA
Hiyo namba 3, waumini tuko imara sana. Maana michango yote tunayochanga ni kwa ajili ya kulitegemeza Kanisa la Mungu.
Halafu ifikie wakati tuwe wakweli! Hakuna binadamu asiyeishi katika Jumuiya! Sasa kama wewe jumuiya yako ni ya wavuta bangi, inakuwaje tena unataka uzikwe na jumuiya nyingine?
Hizi ndio changamoto za kanisa la Tanzania. Tuzidi kumuomba Mungu.
1. Mikutano ya The Big Octoba na The Big Novemba iliyokuwa inahuhubiri kuacha dhambi na kumrudia Kristo imekufa.
2. Mwamposa na Suguye wanauza vifaa vya uponyaji mafuta, maji, keki na vitambaa badala ya kuhubiri watu waache dhambi, pia hawataki kufungua matawi mikoani na kupanda makanisa.
3.RC nao wamechachamaa kwa michango kuanzia kwenye jumuiya hadi Parokiani. Huna hela huzikwi.
4. Mwakasege naye amechachamaa na masomo ya sadaka mwanzo mwisho, mfano semina ya Mbeya (26-30 Oct, 2022) somo ni sadaka tu hakuna kingine.
5. KKKT nao hawaeleweki wachungaji wanaowaiga wapentekosti/walokole ndio wanapata umaarufu mfano Kimaro na Mgogo wale wanaohubiri kilutheriluther hawana chao wala umaarufu.
6. TAG/EAGT hawana wainjilisti wakitaifa kama kina Moses Kulola wamebakia wapigaji tu.
7.Viongozi was dini kugombania mialiko sherehe za kitaifa ili wakalambe asali no aibu.
INAUMA SANA
Hakuna kilicho bora. Tena kutoa sadaka kwa matapeli wanaojiita ni watu wa Mungu ni hatari hata kuliko kuangalia umbea. Kutoa sadaka kwa matapeli ni kuunga mkono kazi ya shetani.Bora utoe sadaka kuliko kununua bando la 5000 kufatilia UMBEA insta na fb
Bora usiache alama yoyote kuliko kuharibu alama zilizokwishawekwa na wakristo wa kweli wa mwanzo. Matapeli wanaojiita viongozi wa dini wamekuwa wengi na hawa kazi yao kubwa imekuwa ni kufuta zile alama ambazo zilikwishawekwa. Wamewakatisha tamaa baadhi ya wakristo baada ya kugundua uovu wao.Nikuulize wewe, Kabla ya kuwalaumu wengine...
Je umeacha alama gani kwenye kazi ya Mungu...?
Watu hawataki kwenda Kanisani, Jumuiya hawaendi, michango hawatoi lakini wanataka wakipatwa na matatizo Kanisa liwasaidie au wakifariki wazikwe na Kanisa.Hiyo namba 3, waumini tuko imara sana. Maana michango yote tunayochanga ni kwa ajili ya kulitegemeza Kanisa la Mungu.
Halafu ifikie wakati tuwe wakweli! Hakuna binadamu asiyeishi katika Jumuiya! Sasa kama wewe jumuiya yako ni ya wavuta bangi, inakuwaje tena unataka uzikwe na jumuiya nyingine?
Haisemwi uende ukatibiwe bure au ukasomeshe mtoto bure!Nikuulize maswali mawili:
1. Unajua ada za shule za RC no sh.ngapi? Una mtoto au ndugu umewahi kumsomesha kwenye hizo shule? Ulilipa sh.ngapi? Ada+michango.
2. Umewahi kutibiwa bure kwenye hospitali za RC mfano Bugando au Tosamaganga Hospital au Peramiho??? Au umewahi kuuguza ndugu yako kwenye hizo hospitali bure?
Seems jamaa siyo Mkatoliki mkuu ameandika kitu asichokuwa na uhakika nacho.Kwa kweli amekosea kwenye namba 3 eti huna hela huzikwi ??
Ni kuwa kama umejitenga na shughuli za kanisa nao wanakutenga huduma za kanisa
Huu ni uzushi na ujinga na Uzindaki wa kiwango Cha juu, hakuna ibada kwenye spiritual world isiyoambatana na sadaka ndo maana kwenye ibada yeyote Ile sadaka ni muhimu ili kufanya upatanisho kwenye spiritualMwakasege naye amechachamaa na masomo ya sadaka mwanzo mwisho, mfano semina ya Mbeya (26-30 Oct, 2022) somo ni sadaka tu hakuna kingine.
Kaandika ujinga mtupuEti mgogo na kimaro wanaiga staili ya wa pentekoste kuhubiri, ungekuwa unajua historia ya injili ungejua muhubiri aliyezaa upentekoste alikuwa Martin Luther mluteri usingeandika ulivyoandika,na ungejua kategori za watumishi wanavyoitwa usingehukumu watumishi kirejareja hivyo wapo watumishi wameitwa kuhubiri uchumi kibiblia kwa hiyo mostly watahubiri katika mlengo huo,n.k
Shule Zina walimu nani atawalipa hospital inahitaji vifaa na madaktari nani atakayewaalipaNikuulize maswali mawili:
1. Unajua ada za shule za RC no sh.ngapi? Una mtoto au ndugu umewahi kumsomesha kwenye hizo shule? Ulilipa sh.ngapi? Ada+michango.
2. Umewahi kutibiwa bure kwenye hospitali za RC mfano Bugando au Tosamaganga Hospital au Peramiho??? Au umewahi kuuguza ndugu yako kwenye hizo hospitali bure?
Watumishi wameitwa kuhubiri uchemi kibiblia? Mbona unatupiga fix jamani? Hao hao watumishi walioitwa kuhubiri uchumi wakitaka gari la kutembea wanaomba mchango kwa waumini na waumini wakitaka gari wanaambiwa waombewe na mhubiri aliyewaomba mchango. Kwa nini yeye mhubiri asiombe gari kwa njia ya maombi?Eti mgogo na kimaro wanaiga staili ya wa pentekoste kuhubiri, ungekuwa unajua historia ya injili ungejua muhubiri aliyezaa upentekoste alikuwa Martin Luther mluteri usingeandika ulivyoandika,na ungejua kategori za watumishi wanavyoitwa usingehukumu watumishi kirejareja hivyo wapo watumishi wameitwa kuhubiri uchumi kibiblia kwa hiyo mostly watahubiri katika mlengo huo,n.k
Hiyo ni kweli kabisa mkuu. Be blessedPia udini.. naongea Kila mara hamna dini inayookoa mtu ..Ukristo sio dini, shida inaanza tunapolazimisha Ukristo uwe dini.. lazima ufanye hivi upate majibu, lazima ufanye hivi uwe mtakatifu.. mambo ya kujitakasa takasa