Kanisa la Tanzania linapitia kipindi kigumu sana. Mungu alinusuru

Kanisa la Tanzania linapitia kipindi kigumu sana. Mungu alinusuru

Point no 4, Refer sadaka aloitoa Mungu kumtoa Yesu Kristo, Ibrahimu kumtoa Isaka. Hivyo basi huoni ya kuwa Mungu mwenyewe ndio muanzilishi wa Sadaka???

Sadaka ni divine invitation, Kamsome Kornelio, Dorcas na Daudi.
Sadaka ya Yesu Kristo msalabani (sacrifice) haifanani kamwe na fedha na mali. Huku ni kuudharau msalaba.

Ibrahimu na Isaka ilikuwa unabii wa Kristo msalabani.

Mwanzo 22:2
Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia
.

Kristo ni mwana wa pekee wa Mungu. Huyu ni kwangu mpendwa wangu niliyependezwa naye. Sawa huwezi kusema fedha ni nwanao mpendwa uliyependezwa naye kwa sababu maandiko yamekataza kupenda mali. Habari za kuambiana utoe sadaka inayokuumiza, yaani mali, ni uongo.

Kama matoleo (weweumeita sadaka) ni divine invitation basi tufanyacho ni BRIBING GOD.
 
Ondoa Hapo namba 3 umekosea.Tunaona shule hospitali vyuo n.k vyote hivi vinatoa huduma katika jamii wakati huo mapadre si watu matajiri kama ilivyo kwa wengine na injili inahubiriwa kama kawaida.
Usilolijua...Kuna padre ameangusha ghorofa karibu na kibanda changu
 
Jambo lingine la msingi ndugu zangu katika Bwana..

Tumefika tulipo fika kwasababu hatuakisi upendo.. tunatazama utoaji wa sadaka na kutaka kuwa wakamilifu lakini tukumbuke upendo..
 

Attachments

  • Screenshot_20221029-064458.png
    Screenshot_20221029-064458.png
    26.6 KB · Views: 2
  • Screenshot_20221029-064558.png
    Screenshot_20221029-064558.png
    24 KB · Views: 5
  • Screenshot_20221029-064910.png
    Screenshot_20221029-064910.png
    27.3 KB · Views: 2
Yesu Kristo hakuja kufungua majengo ama taasisi ziitwazo Kanisa. Kimsingi Kanisa ni kusanyiko - congregation - eklesia. Kristo alikuja kutangaza habari njema ya ufalme wa Mungu. Taasisi zilizojiita "Kanisa" ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu, lakini mpango wa Mungu kumtafuta mwanadamu ni kufa na kufufuka kwa Yesu Kristo.

Tumeitwa kuwa ufalme wa makuhani:

Ufunuo wa Yohana 5:9
Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,

Ufunuo wa Yohana 5:10

ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao watamiliki juu ya nchi.

Hawa ni wana wa ufalme wa makuhani kwa Mungu, kutoka dunia yote. Kumbuka Kristo katika mafundisho yake aliongelea agenda moja tu, UFALME WA MUNGU. Ili kuwa raia wa ufalme wa Mungu ni lazima uzaliwe huko, ndio maana ya kuzaliwa mara ya pili. Mungu ni Roho na ufalme wake ni wa kiroho. Huwezi kuwa mwana wa ufalme kwa jinsi ya kimwili bali kwa kuutiisha mwili ni kumfanya Roho atawale. Hili ndio aina ya Kanisa aliloacha Kristo, Kanisa la wamwabuduo halisi.

Makanisa mengi leo hii yapo kimwili tu huku yakijiita wana wa Mungu. Sio kila ajiitaye Mkristo ni mwana wa Mungu, church membership haikufanyi kuwa mwana. Ndio hizo taratibu na sheria nyingi za makanisa. Makanisa ya mali na mafanikio, makanisa yanayolilia milki za dunia. Hayo yanekoma kuwa makanisa ya Mungu aliye hai, ekklesia
Pia udini.. naongea Kila mara hamna dini inayookoa mtu ..Ukristo sio dini, shida inaanza tunapolazimisha Ukristo uwe dini.. lazima ufanye hivi upate majibu, lazima ufanye hivi uwe mtakatifu.. mambo ya kujitakasa takasa
 
Hizi ndio changamoto za kanisa la Tanzania. Tuzidi kumuomba Mungu.

1. Mikutano ya The Big Octoba na The Big Novemba iliyokuwa inahuhubiri kuacha dhambi na kumrudia Kristo imekufa.

2. Mwamposa na Suguye wanauza vifaa vya uponyaji mafuta, maji, keki na vitambaa badala ya kuhubiri watu waache dhambi, pia hawataki kufungua matawi mikoani na kupanda makanisa.

3.RC nao wamechachamaa kwa michango kuanzia kwenye jumuiya hadi Parokiani. Huna hela huzikwi.

4. Mwakasege naye amechachamaa na masomo ya sadaka mwanzo mwisho, mfano semina ya Mbeya (26-30 Oct, 2022) somo ni sadaka tu hakuna kingine.

5. KKKT nao hawaeleweki wachungaji wanaowaiga wapentekosti/walokole ndio wanapata umaarufu mfano Kimaro na Mgogo wale wanaohubiri kilutheriluther hawana chao wala umaarufu.

6. TAG/EAGT hawana wainjilisti wakitaifa kama kina Moses Kulola wamebakia wapigaji tu.

7.Viongozi was dini kugombania mialiko sherehe za kitaifa ili wakalambe asali no aibu.

INAUMA SANA
Umuombe Mungu yupi huyo? You are doomed.
 
Hiyo namba 3, waumini tuko imara sana. Maana michango yote tunayochanga ni kwa ajili ya kulitegemeza Kanisa la Mungu.

Halafu ifikie wakati tuwe wakweli! Hakuna binadamu asiyeishi katika Jumuiya! Sasa kama wewe jumuiya yako ni ya wavuta bangi, inakuwaje tena unataka uzikwe na jumuiya nyingine?
Kanisa ni jumuiya huru, uwe na mchango au usiwe nao, uwe na hela au usiwe nayo, ubaya ulioposasa huku RC tunapeana mpaka risiti za michango ya jumuiya...hizo ni sadaka hapa panaboa sana.
Michango imewaweka pembeni wakristo wasikini!
Michango ndiyo inayompaa tenda za ujenzi na usambazaji wa huduma muhimi nanilii hapa Arusha....
Nasema bila michango bado watu tutatoa kwa moyo....
 
Ondoa Hapo namba 3 umekosea.Tunaona shule hospitali vyuo n.k vyote hivi vinatoa huduma katika jamii wakati huo mapadre si watu matajiri kama ilivyo kwa wengine na injili inahubiriwa kama kawaida.
Kama kuna kitu sintokuja kurudia kutoa ni mchango wa kujenga mradi wa kanisa!! Iwe ni hospitali, shule, hotel, au gesti hausi, SITOI, kkkt arusha ilinipa somo.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Hiyo namba 3, waumini tuko imara sana. Maana michango yote tunayochanga ni kwa ajili ya kulitegemeza Kanisa la Mungu.

Halafu ifikie wakati tuwe wakweli! Hakuna binadamu asiyeishi katika Jumuiya! Sasa kama wewe jumuiya yako ni ya wavuta bangi, inakuwaje tena unataka uzikwe na jumuiya nyingine?
Hiyo namba 3 sio changamoto ya RC kuyumbisha kanisa, amekwepa kusrma changamoto za ukweli, uzinzi wa mapadri na mauaji kanisani tena mauaji ya mapadri ni changamoto kubwa sana huko RC
 
Tumsifu Yesu Kristo Tate Mkuu

Watu wanasahau kwamba makanisa na misikiti inaendeshwa kwa sadaka na kutoa sadaka ni maelekezo ya Mungu bila shurti
RC changamoto yao kubwa kwasasa ni uzinzi wa mapadri, pia mauaji ya mapadri kanisani na hakuna kesi inafikirisha sana
 
Kanisa linapita nyakati ngumu sana. Nyakati hizi sisi akina baba tusiposimama kuijua imani vema na kuongoza familia badala ya kuwaachia wanawake mambo ya imani utaangamiza familia yako kama si leo ni kesho!

Ukristo umevurugwa sana sana! Makanisa mama yaliyokuwa nguzo nayo yanapigwa mawimbi ya nguvu! Walokole ndio wamevurugwa kiasi cha kutisha! Tuliombee Kanisa!
 
Back
Top Bottom