Kanuni mpya Kikokotoo Inaondoa ubabe wa NSSF. Siasa za Magufuli ziliwabeba waonevu NSSF

Kanuni mpya Kikokotoo Inaondoa ubabe wa NSSF. Siasa za Magufuli ziliwabeba waonevu NSSF

Mshahara wako ni shilingi ngapi mpaka zikife mil 200 ulizochangia ?
Hesabu rahisi, nikifanya kazi kwa miaka 36, ukaitafuta miezi iliyopo ndani yake, ukaitawanya hiyo 200m kwa hiyo miezi, kisha ukaipasua kati, utajua kiasi cha mshahara ninachozungumzia hapo!
 
Ni vile tu haturuhusiwi kutukana humu; kuizngumzia SSRA ambayo day one imeingia kazini ikatengeneza mgogoro mkubwa na wafanyakazi kwa kuondoa fao la kujitoa halafu mtu (hapo kwenye mtu ndio nilitaka kutumia neno baya ) anakuja kuisifia? SSRA imeanzishwa kabla ya Magufuli, uwepo wa SSRA ilikua tatizo kubwa, inakula pesa za mifuko halafu haizalishi, jinga kabisa. Rest in peace mwamba Magufuli, wavivu, wezi, majizi na mafisadi ndio wanao furahia your absence.
 
Kumbuka JPM hakuridhia kikokotoo.
Alitoa miaka 5 kiangaliwe upya.
Mpaka anafariki miaka mitano ilikuwa haijafika.
Kama umefanyiwa uhuni pole.
JPM asilaumiwe kwa hili
Uhuni na siasa kuwadanganya wajinga, kama hakuridhia angekataa kisitumike, kitendo cha kusema miaka mitano kingaliwe wakati huo mifuko ikiendelea kutekeleza maamuzi ya bunge maana yake alipiga siasa ili wananchi wasio elewa kama kawaida mshangilie na kupiga makofi. Na yeye akipata hela ya kufanya miradi yake.
 
Uhuni na siasa kuwadanganya wajinga, kama hakuridhia angekataa kisitumike, kitendo cha kusema miaka mitano kingaliwe wakati huo mifuko ikiendelea kutekeleza maamuzi ya bunge maana yake alipiga siasa ili wananchi wasio elewa kama kawaida mshangilie na kupiga makofi. Na yeye akipata hela ya kufanya miradi yake.
Nimegundua wengi hamuelewi hii mifuko ya hifadhi ya jamii ni nn na hata maana ya hayo mafao.
 
Mwaka 2014 Sheria ya iliyokuwa SSRA ilianza kutumika kulipa mafao na ikasaidia sana kupandisha mafao ya Mfuko wa NSSF na iliyokuwa PPF ambayo ilikuwa inawanyonya kisheenziii wastaafu kabla ya 2014 Julai. Hata baada ya Kanuni hiyo Mfuko wetu wa NSSF uliendelea kuwanyonya wastaafu wengi kwa kigezo eti wale walioingia kabla ya Mwaka 1998 eti walikuwa wakifanyiwa conversion ya michango yao ya kila mwezi kwa wakati huo na kupunguzwa sana.

Kwa mfano, mtu ambaye hata kufikia mwaka 1998 alikwa tarayai kafanya kazi miaka 20 ambayo ni asawa na miezi 240 alikuwa anapunguziwa hiyo miezi hadi kuonekana eti ni miezi isiyozidi 90. Kwa hiyo unakuata mstaafu kapoteza hadi miezi 130 ya utumishi wake katika kulipwa pensheni.

Pamoja na Kanuni hiyo kutaja miezi lakini NSSF wao walikuwa wakiendelea kuwapunja wastaafu kwa kubadili miezi hiyo na kuifanya kuwa michache na imetokea wastaafu wengi sana NSSF wamepoteza pensheni zao kwa sababu ya utaratibu huo wa conversion. Mtu wa NSSF unakuta kafanya kazi miaka mingi lakini pensheni yake unakuta ni kiduchu mno kisa hiyo hiyo conversion formula.

Shangazi yangu alistaafu mwaka 2016 lkn kwa kipindi cha nyuma ya miaka 20 huko kabla ya mwaka 1998 ilichukuliwa miezi 240 na kubadilishwa na kuwa miezi 89 kwa hiyo wakachukua miezi ya kuanzia mwaka Julai 1998 na hiyo miezi 89 na kumlipa pensheni kwa upungufu wa miezi 131 na bila hata aibu tulipofuatilia walikuwa wanakenua kenua meno tu na kutujibu kunya kwa kuwa wakati huo Erio alikuwa anaweza kukaa na kula dinner na Mwendazake Ikulu bila kizuizi chochote.

Nimeangalia Kanuni ya sasa pia haiongelei suala la NSSF kutumia conversion formula lkini kwa kuwa wanafikiri wananchi hatuoni inawezekana kabisa wakaendelea hivyo hivyo kutunyonya kupitia conversion formla.

Rais Samia pls ongelea na hili kwani tambua kuwa wakati mwingine watendaji hawa wa Mifuko wana roho mbaya sana wanasababisha Serikali yako ichukiwe kwa ajili tu ya kufanya makusudi. These people of pension funds are real bad people.
Watu bado wapo kwente koma awahamini kama mama ndio kashika usukani na abiria wanafuraha swala kikotoo mheshimiwa Rais anatakiwa apongezwe kwa nguvu zote, atleast wastaafu kilio chao kimesikika nyie mnaoendelea kuponda endeleeni gari ndio limeshawaka alitarajii kuzima leo wala kesho ..viva samia.
 
Watu bado wapo kwente koma awahamini kama mama ndio kashika usukani na abiria wanafuraha swala kikotoo mheshimiwa Rais anatakiwa apongezwe kwa nguvu zote, atleast wastaafu kilio chao kimesikika nyie mnaoendelea kuponda endeleeni gari ndio limeshawaka alitarajii kuzima leo wala kesho ..viva samia.
Hapo nimeponda nini sasa?
 
Ni vile tu haturuhusiwi kutukana humu; kuizngumzia SSRA ambayo day one imeingia kazini ikatengeneza mgogoro mkubwa na wafanyakazi kwa kuondoa fao la kujitoa halafu mtu (hapo kwenye mtu ndio nilitaka kutumia neno baya ) anakuja kuisifia? SSRA imeanzishwa kabla ya Magufuli, uwepo wa SSRA ilikua tatizo kubwa, inakula pesa za mifuko halafu haizalishi, jinga kabisa. Rest in peace mwamba Magufuli, wavivu, wezi, majizi na mafisadi ndio wanao furahia your absence.
Mhhh Tanzania ina wajinga wengi sana sana!
 
Fao la kujitoa na lirudishwe...
Hili la muhimu aisee, NSSF walinitesa maana mie contract iliisha nikauchuna miezi kadhaa ndio nikaenda kufungua yaani kufika pale wakaja na issue za fao la kukosa ajira (33% ya salary for 6 months) yaani nilitaka kuanguka ukizingatia nilikaa miezi 6 mambo yalivyoanza kuwa tight nikaenda...nikapigwa miezi 2 tena mbele ndo wakaanza kuingiza hiyo hela yao kila mwezi kwa miezi 6. Ilivyoisha mzigo ukakata nikaanza kupambana nilipwe zote nikaambiwa yaani mpaka miezi 18 iishe tangu nilipolipwa mafao ya kukosa (nikapoa kabisa)

Ilibidi nibaki kuhesabu miezi maana barua hawajibu, ukiingia twitter mpaka facebook hawajibu labda kama unatoa pongezi ndio utajibiwa, yaani juzi kati miezi kadhaa iliyopita ndio nikalipwa (nilicho experience hiyo issue yao haifanyi kazi)
 
Mifuko ya hifadhi za jamii inapata faida kubwa sana,kutokana na uwekezaji wa michango ya wanachama kwenye Treasury Bond na rasilimali zisizo hamishika Kama majengo,madaraja, hostel,na nyumba nk.
Lakini mifuko ya hifadhi za jamii, wakati wa kikokotoa mafao hususani NSSF wanachukua jumla ya michango ya mwanachama kama alivyochangua kwa kipindi chake cha utumishi wake bila kuhuisha na faida iliyopatikana kutokana na uwekezaji wa michango yake au mfumuko wa bei.
Mfuko wa PSSSF wao wanachukua michango ya miezi mitatu ya mwisho, kufanyia kikokotoo Cha mafao ya mtumishi kwa miaka yote ya utumishi wake.

Ushauri

1). Serikali iangalie uwezekano wa kuhuisha mafao ya kila mwezi kwa Wastaafu wa zamani,to take into inflation rate and super profit accruing from membership contribution invested in various ventures.
2). Kwa kuwa NSSF walishaanza kuwalipa Wastaafu 25% malipo ya mkupuo,Ni vema kwa wahanga wa kikokotoo hicho wafanyiwe mapitio na kulipwa stahiki zao.
3). Serikali itoe kanuni kwa NSSF kutumia michango inayotokana na mshahara ya mwisho (Kama wanavyofanya PSSSF) kikokotoa mafao ya wanachama wao.
4). NSSF Iwe inatoa mchanganuo wa mafao ya Wastaafu,kwa maana sasa hivi, imekuwa siri hata mstaafu mwenyewe hapewe.Ni Sheria ya Siri ni kati ya Mteja na taasisi,kwa nini mteja asipewe nakala ya namna mfuko ulivyofikia malipo ya mkupuo na ya kila mwezi.
 
Kumbuka JPM hakuridhia kikokotoo.
Alitoa miaka 5 kiangaliwe upya.
Mpaka anafariki miaka mitano ilikuwa haijafika.
Kama umefanyiwa uhuni pole.
JPM asilaumiwe kwa hili
Mkuu hauko sahihi. Sheria ya kubadilisha kikotoo ilipelekwa na kupitishwa bungeni na Jennistèr Mhagama wakati wa JPM. Sheria hii ililalamikiwa sana na wadau na hasa Bungeni. Mbunge wa Kigoma (marehemu kwa sasa) alillamika sana na alisema namnukuu " sheria hii inaenda kuumiza wastaafu".
Ilivyoanza kutumika ndiyo vilio vikaanza hapo JPM akasema kiangaliwe upya, watu wakashangilia wasijue kuwa bila kubadilisha sheria Yale ni maneno tu hayana nguvu ya kisheria. Sawa hivi wastaafu wengi wanategemea wakienda kudai pension yap wanakutana na kikotoo cha JPM kwa sababu mifuko inafuata shèria na siyo maneno.
 
Hapo ni uonevu tu bora mtu apewe mafao yake yote atajua mwenyewe na maisha yake maana serikali haina guarantee ya maisha ya mtu kusema eti umlipe pension kila mwez utajuaje miaka aliyobakiza kuishi baada ya kustaafu..?
Waliopitisha hayo mambo hawajafanya fair mtu apewe chake basi kwan hata akizitumia vibaya wao wanaumia nn..
 
Mifuko ya hifadhi za jamii inapata faida kubwa sana,kutokana na uwekezaji wa michango ya wanachama kwenye Treasury Bond na rasilimali zisizo hamishika Kama majengo,madaraja, hostel,na nyumba nk.
Lakini mifuko ya hifadhi za jamii, wakati wa kikokotoa mafao hususani NSSF wanachukua jumla ya michango ya mwanachama kama alivyochangua kwa kipindi chake cha utumishi wake bila kuhuisha na faida iliyopatikana kutokana na uwekezaji wa michango yake au mfumuko wa bei.
Mfuko wa PSSSF wao wanachukua michango ya miezi mitatu ya mwisho, kufanyia kikokotoo Cha mafao ya mtumishi kwa miaka yote ya utumishi wake.

Ushauri

1). Serikali iangalie uwezekano wa kuhuisha mafao ya kila mwezi kwa Wastaafu wa zamani,to take into inflation rate and super profit accruing from membership contribution invested in various ventures.
2). Kwa kuwa NSSF walishaanza kuwalipa Wastaafu 25% malipo ya mkupuo,Ni vema kwa wahanga wa kikokotoo hicho wafanyiwe mapitio na kulipwa stahiki zao.
3). Serikali itoe kanuni kwa NSSF kutumia michango inayotokana na mshahara ya mwisho (Kama wanavyofanya PSSSF) kikokotoa mafao ya wanachama wao.
4). NSSF Iwe inatoa mchanganuo wa mafao ya Wastaafu,kwa maana sasa hivi, imekuwa siri hata mstaafu mwenyewe hapewe.Ni Sheria ya Siri ni kati ya Mteja na taasisi,kwa nini mteja asipewe nakala ya namna mfuko ulivyofikia malipo ya mkupuo na ya kila mwezi.
Kwa sasa wanatumia fomula mpya!
 
Back
Top Bottom