Kariakoo haina umuhimu kwa uchumi wa nchi kama tunavyo aminishana Bongo lala

Maskini nchi yetu Tanzania. Ndiyo maana wakenya, waganda na wamalawi (kwa sasa) wanakuja Tanzania wanachukua ajira chache zilizopo. Kwa analysis hii! Kajifunze upya hujachelewa. Vijana wetu hawajui hata mchango wa sera na sheria katika kuhamasisha mitaji ya kujenga viwanda nchi mwetu kweli!?!? Ndiyo maana wakipewa uDC tu wanahangaika kupiga vita mila za wazaramo.
 
Hapo wanaotuamisha ni wasomi wetu.Wale wasomi wanaosema Dar inazalisha pesa nyingi huwa najiuliza sana iwapo shule zetu zina faida kweli.

Mazao yanayouzwa nje kama korosho,pamba,mkonge,kahawa,chai,maua,mpunga na Mahindi havilimwi Dar

Madini yanayouzwa nje mf Dhahabu,Tanzanite,Almasi,na mengine hayachimbwi Dar

Mapato ya utalii mengi hayatokani na Dar.
Dar hakuna viwanda vingi vinavyozalisha na kuuza nje ya nchi.

Hapo Dar ni ofisi za wapiga dili wanaodhulumu watu wa bara kwa msaada wa serikali na hivyo kufanya urali wa mzunguko wa pesa kuelemea Dar wakati wazalisha hawaishi Dar.
Wasomi wanafanya uhuni kisha wanaupalilia na kujibarikia na wanachotufanyia hapo Dar
 
Mkuu huu unaitwa UKIRITIMBA umepitwa na wakati dunia ya leo
Hivi unataka kampuni 5 zipewe vibali vya kuagiza ili mradi kariakoo ife?

Angalia jinsi sukari inavyo tutesa kwa ukirimbia kama huo
Kumbuka mafuta yalivyokua yanatutesa kisa waagizaji wachache
Angalia makampuni ya simu yanavyotuchezea akili
Acha soko huria na kusanya kodi yako
 
Sio lazima uelewe kila kitu mkuu
 
Kwa hiyo mko tayari kukandamiza haki za wafanyabiashara kwa kuwa ni Wachache na hawana nguvu

Acheni kiburi Tendendeni haki siku zinakuja
 
Sukari mkuu imeleta shida , kwa sababu kuna watu kama sio huyo msomaali kutumia gep na wenzake kupiga pesa tu ,ukweli lazima usemwe , hata Mpina kaonewa tu, je kwa akili yako nzuri kwa hili la sukari uhamini Tulia hajalamba chochote ,mwenyekiti wa kamati hjalamba chochote, vipi wajumbe wa kamati na hawajalamba chochote ,kwangu roho mtakatifu anasema hapana wamelamba .

Kama nikulisaidia Taifa mkuu hapa palikua penyewe ila ndo hivyo.
Wakata watu makini wanamsaidia ndugu Rais wengine wanaleta uchawa .

Ombi langu uyu ndugu rais amalize miaka hii iliyobakikia apumzike na kula maisha
 
So tushangilie kuwa Dampo?
Mbona unaongea kwa kuwakandamiza wazawa wafanyabiashara bila ya kuwanyooshea vifole watawala ambao ndo wapelelea Hali hii

Unaandika kwa mbwembwe ukiwalaumu wafanyabiadhara lakini ukikwepa kuwapa lawama watawala
Wanao Tunga sera
 
Ningetamani waachwe wafunge hayo maduka yao kadri watakavyo na serikali iweke ulinzi wasibughudhiwe na mtu yeyote na serikali ihakikishe bidhaa zote zinazoingia na kutoka zimelipiwa kodi stahiki ndiyo ziruhusiwe kutoka au kuingia maana nimemsikia mjinga mmoja anadai wao wanaweza kufunga maduka lakini wakaendelea na biashara kama kawaida ila serikali itakosa kodi yaani maana yake watakuwa wakichukua bidhaa kutoka kwenye magodauni yao na kwenda kuziuza sehemu nyingine kimazabe.
Wala wasiwabembeleze halafu tuone mwisho wake utakuwaje.
 
Tuambie wewe una product gani ya ndani ulitusaidia kutengeneza ili tukusaidia tukuamini na kisomo chako cha kukariri
 
Mkisoma zenu huko na kuanza kupokea mishahara inayochelewa mnaandika chochote leo hii mtu unaweza kufikiri na kuandika kuwa Kariakoo sio sehemu ya kukuza Uchumi wa Nchi aisee...ndio maana Karl Peters alikaa na wahuni wenzie kuligawa bara la Afrika na kulitawala..
 
Swali la msingi kabla ya yote, Je, wafanyabiashara wa Kariakoo wanalipa kodi ipasavyo? Mauzo yao yote yanapitia kwenye EFDs machines?

Kama jibu ni hapana, basi serikali inapaswa kuchukua hatua stahiki.
 
Ni dampo lililochangamka.
 
Huu ni uchumi wa dumping sasa haujui hilo🤣 uchumi wa Tanzania unategemea dumping
 
mimi huwa napenda kuongea kwa haki. serikali ni serikali, iwaache watu watoe dukuduku, ila wananchi wanaoachwa kutoa dukuduku pia wafanye hayo kwa amani, tusiumizane. kuhusu kutoa kodi, sisi sote sio mara moja sio mara mbili, tumeshanunua sana bidhaa kariakoo, twafanya hivyo kila wakati, na hakuna asiyejua kuwa kupewa risiti huwa ni option, ulipie ya kupewa efd au ulipie ya kuibia serikali. kama mnakwepa kodi namna hii, natarajia serikali ifanye nini? serikali hiyo ni ya kwetu, sisi ndio tumewaweka, watukusanyie kodi, tupate mapato tuendeshe nchi, sasa kama mnakwepa kodi wakati ninyi wenyewe mmewatuma wakakusanye kodi, mnafikiri nchi itaendeshwaje? barabara, na miundombinu mtajengea nini? tuwe fair sometimes.
 
Mkuu dunia ya leo inaendeshwa na biashara huria na sio ku limit idadi ndogo ya watu kufanya biashara hiyo
Serikali inachopaswa kufanya ni kuweka vigezo vya aina ya bidhaa zinazotakiwa kuingizwa kama ubora nk na sio ku limit idadi ya waingizaji

Ndio maana nakwambia hii shida ya sukari ni kwa sababu vibali wamepewa watu wachache ambao wakiamua wanachezesha michezo yao kutengeneza uhaba na kupata faida maradufu

Angalia mitandao ya simu inavyotufanyia, badala ya kuwa washindani wao wanakaa vikao na kupanga bei sawa ambazo zinawapa faida wao
 
Ni kweli ulichokisema. Tatizo ni kuchangia hoja ukijifanya unaelewa. Bora kuacha tu.
Mkuu watu wengi sana hawaijui Kariakoo kiundani jinsi mzungu wa hela na mapato ulivyo mkubwa, zaidi ya kupita na kuona watu wengi au kwenda kufanya shopping

Ukijua jinsi wa Congo Sudan Zambia, Birundi hadi Sudan nk wanavyokuja kufungasha mizigo kupeleka kwao utashangaa

Unaweza kuiita unavyopenda kwamba ni dumping area lakini huwezi kuondoa ukweli kwamba kuna watu wamelaza mabilioni ya mitaji yao pale, kuna mamilioni ya ajira na kuna mapato ya kodi makubwa sana kuliko mapato ya mikoa zaidi ya asilimia 80 ya mikoa ya Tz

Kuna sababu kwanini kariakoo ni mkoa maalum wa kikodi
Kuna sababu kwanini serikali imetolea macho kariakoo linapokuja swala la kodi kwa kuweka utitiri wa kodi

Shughuli za kiuchumi zinakwenda kwa kutumia fursa mkuu
Hakuna viwanda Tz wanatu wanatumia fursa hiyo kuagiza bidhaa nje

Sasa badala ya kuanza kuona kariakoo sio muhimu kwasababu tu wanadai wamezidishiwa kodi ni vyema basi serikali ikajikita kuhakikisha sera za viwanda vinaanzishwa ku cover bidhaa zinazo agizwa nje badala ya kuwapiga biti hawana umuhimu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…