Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

UZI UMEVAMIWA NA MAWINGA KUJA KUHALALISHA WIZI WAO.

ADUI YAKO MUOMBEE NJAAA!!!! NYIE MAWINGA MNAOTAKA KUWIN LIFE KIRAHISI RAHISI TU NENDENI KWA PIDIDDY NDO ANAGAWA HELA BURE.MCHINA ANAKUJA KUWAMALIZA MRUDI VIJIJINI MKAANZE KUJIANDAA NA KILIMO HAKUNA PESA RAHISI. MTAKULA HELA ZA WAJINGA TU!!!!

KWA WAZUNGU AGENT NI MTU MAKINI, MTU SMART ILA BONGO MTU DALALI NI MTU FAILURE ALIYEPOTEZA DIRECTION. NO WONDER INACHUKULIWA NI KAZI YA KUIBIA WATEJA.
 
Vifaa vipi alafu kuna bei huwezi pewa wewe mteja unayekuja mara moja baada ya mwaka zile wanapewa wale wanaokuja kuchukua mzigo mara kwa mara

Mfano kwa hisense sidhan kuna mtu anayemfikia yule mhindi mwenye maduka ya mars yaani bidhaa zote za hisense utazunguka wewe mwisho wa siku utakua recommendede uende kwake na ukipitia kariakoo ni rais kupata bei nzuri
Ok
 
Kwenye comment kuna element za kuongeza cha juu au kumtapeli mtu,unambwato na p diddy sio bure,shughuli ninayofanya inanilipa hadi kuweza kukulisha ww na familia hadi bibi yako shamba huko,acha kushobokea na kuquote ujinga comments za watu usiowajua
Acha use usenge nilikosea kukuquoet
Kiatu kimoja unabargain hakuna tajir anafanya huo ujinga ukimuambia buku atakuambia nakupa 800 nipe vinne au ukienda duka lolote kubwa bei iko pale sio kubargain. Kama ni biashara ya kati mnabargain. Tajir gan ana muda wa kukaa chini nusu saa anaomba kupunguziwa huyo sio tajir jombaa. Ingekuwa biashara za uzalishaji au za kati sawa sio biashara ya mlaji wa mwisho unakuta mtu anakaa dakika 20 apunguziwe buku huku ananunua kiatu kimoja huyo sio tajir mzee. Tajiri ni muda hawanaga muda.
Wewe ni winga tafuta kazi ya kufanya hiyo sio kazi ni utapeli
 
Ww huwezi kumiliki biashara ww ni wingwa bwana. Hiyo ni uongo wewe ni winga.
Na Ubungo mchina akipamalizia hapo mtatia adabu. Unaleta dharau eti nyie mnauzia wageni wa nje. Hivi unataka kusema lile nyomi lote la kariakoo ni la wacongo,Wamalawi na Wazambia. Acheni kujikweza nyie mawinga.

Kwa we Maana kwa maelezo yako ww bado unamindset za kichuuzi hutakuja kuwa mfanyabiashara ww ni mchuuzi for life.
Mkuu mchina akiwepo pale sio sababu ya kushuka bei hapo kwa Kaburu yapo yale kama 40 Johannesburg tu na bado bidhaa zina mawinga Waethiopia sema kupata chimbo halisi ni nzuri zaidi.maana wenye mitaji mikubwa wao mzigo ukifika wanachukua wote Mchina anabaki na Lonya tu ambazo tutafata kununua..
 
Kuna siku nilikuta mashuka tandika bei kitonga,niliyakusanya kama yote,kufika home nilipomuambia Wife bei niliyonunulia,siku ya pili tulirudi wote kuyakusanya tena,tandika ipewe maua yake,kikubwa wangese mawinga wasiende kupaharibu,soko la ilala lilikua zuri sana kwa jeans za mtumba ila now ni ghari mno,jeans za bei rahisi ukiiotea kwa wale wanaotembeza mkononi
Ilala unakuta suruali kali sana inawaka kweli kumbe wahuni wameipaka mafuta ya baiskeli, ukiipiga maji tu utajua mjini sio kuzuri.
 
Ebu nikione! Viatu karume standard bei ni 12,000 kikizidi sana 18,000.
Bongo Dar es Saalam.
1727927387223.png
 
Bro kila mtu ana namna yake ya kutoka so mi binafs ctegemei kuitwa muuza duka milele. Na hata huko madukan huwez kunikuta. Ila nachojaribu kukuambia hicho kitu kipo popote, mi nimekikuta kkoo miaka 25 nyuma na mi kwasasa cfanyi biashara mteja wa mwisho niko kwenye uzalishaji na agent's. Kikubwa life kila mtu ana mkondo wake
Hicho kitu kizuri na ndiyo biashara za Sasa zinavyofanywa.
Ukienda kiwanda Cha bati lazima upitie kwa agent huyu kamabwinga tu.
Mnachotakiwa kufanya ni kutafuta namba ya kuwabana wasizidishe Sana bei na wasifanye utapeli au kuuza vitu vibovu.
Mimi nimejiapiza siwezi kununua tena simu duka flani Kariakoo. Sababu winga aliniuzia simu mbovu nikarudisha akaniletea mbovu Tena. Ubovu wake si wa kuonekana kwa macho Hadi utumie masaa kadhaa.
Zamani nimenunua simu kibao hazikuwa hivyo.
 
Usijisumbue kwenda Kariakoo kununua mzigo ukidhani Kuna bei nafuu
Kariakoo wamejaa wajanja na madalali tu
Unaweza ingia kwenye duka ukamkuta mwenye duka ukamuuliza bei akakuelekeza uongee na vijana wake wakuumize
Nyie watu situka Kariakoo hakufai kabisa, mawinga wameharibu uaminifu.

Matajiri wanauchukulia wateja kama wajinga, wanajua kuwa mtaenda tu.

Sasa naomba niwape machimbo mapya Kwa Dar

1. Kwa wale wa electronics nenda Tegeta pale Kibo complex utapata bei ambayo Kariakoo haipo

Pia nenda Mbagala rangi Tatu utapata electronics zote, kuanzia Tv, simu, cable

2. Nguo nenda Mwenge au Makumbusho

3. Mitumba
Usijaribu kwenda Karume au Ilala tena
Kwa mitumba ya bei nafuu, mabalo za rejareja nenda Tandika, Temeke, Tandale na Mwenge

Kanda ya ziwa, machimbo yapo Katoro

Kwa machimbo mengine, tujaribu ku share.

Ila chonde chonde Kariakoo utaishia kupandiliwa na kupigwa bei ya maana.

Kariakoo nilikuwepo Jana, nikahairisha kuchukua mzigo kisa mawinga
Umaskini na kupenda vitu vya bei chee ni sawa na CCM na wizi wa kura.
 
Shida ni ule usumbufu na uking'ang'anizi wao. Na ile wanakufata kundi kubwa na maneno kibao huku wanakuzongazonga ilhali umeenda kwa hiyari yako na zaidi ya yote unajua duka unaloenda kufanya manunuzi na ukiwaambia bado watataka muongozane dukani ionekane wao ndo wamekupeleka huku wakikutaji bei wao na sio muuzaji.

Wafanyabiashara wajaribu kuyacontrol tu ila sio kuwafukuza, acha vijana wapate chochote.
 
Nilienda kununua generator mwenye duka akaniambia niende kwa winga nikazungumze nae,winga akaniambia bei ni mil 3.5 Mimi nikamwambia Nina mil 2.2 tu sishushi siongezi!
Winga akakomaa akasema nitoe mil 3.3 nikaamua kuondoka.
Ile naondoka tu mwenye duka akanikimbilia akaniambia toa hiyo hiyo mil 2.2
 
Ukosefu wa ajira ndo umeleta hawa inzi saiv nchi hii ukiwa na hela unashindwa kuenjoy kwa kununua vitu vizur kisa hawa inzi wanajiita mawinga hapo kariakoo mm nilitoka bila kununua chochote nikasema hebu nipite na hapo karume yaani balaa la soko la karume kipindi hiko kabla halijaungua lilikuwa mbadala wa kariakoo na hao inzi hawakuwepo.Saiv karume kumejaa vibaka wanaosumbua watu, unakuwa unanunua huku unalinda mali mfukoni maana sio kwa hao nzi waliokuzunguka.Napo pia niliishia kushangaa nikapanda gari nikaondoka🤗.Mjini daslam kumevamiwa vijana wakimaliza chuo hawataki kurudi makwao. Goli moja mawinga 7 au 8 yaani ni viroja🥱

Alafu ni nani aliyewaambia kuwa mm nimetoka nyumbani nakuja mjini alafu ww inzi mmoja unajifanya tour guide( dalali). Nchi imechafuka madalali stendi, madalali masokoni kwenye nyumba na viwanja ndo balaa ni inzi everywhere🥴
Noma sana kuna kipindi nikaenda Keko kununua kitanda ile nafika tu kuna jamaa wawili wakanikaribisha dukani kwao. Nilipotoka walizunguka na mimi maduka yote. Mpaka nikaamua kusepa bila manunuzi
 
Back
Top Bottom