Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

UZI UMEVAMIWA NA MAWINGA KUJA KUHALALISHA WIZI WAO.

ADUI YAKO MUOMBEE NJAAA!!!! NYIE MAWINGA MNAOTAKA KUWIN LIFE KIRAHISI RAHISI TU NENDENI KWA PIDIDDY NDO ANAGAWA HELA BURE.MCHINA ANAKUJA KUWAMALIZA MRUDI VIJIJINI MKAANZE KUJIANDAA NA KILIMO HAKUNA PESA RAHISI. MTAKULA HELA ZA WAJINGA TU!!!!

KWA WAZUNGU AGENT NI MTU MAKINI, MTU SMART ILA BONGO MTU DALALI NI MTU FAILURE ALIYEPOTEZA DIRECTION. NO WONDER INACHUKULIWA NI KAZI YA KUIBIA WATEJA.
 
Ok
 
Kwenye comment kuna element za kuongeza cha juu au kumtapeli mtu,unambwato na p diddy sio bure,shughuli ninayofanya inanilipa hadi kuweza kukulisha ww na familia hadi bibi yako shamba huko,acha kushobokea na kuquote ujinga comments za watu usiowajua
Acha use usenge nilikosea kukuquoet
Wewe ni winga tafuta kazi ya kufanya hiyo sio kazi ni utapeli
 
Mkuu mchina akiwepo pale sio sababu ya kushuka bei hapo kwa Kaburu yapo yale kama 40 Johannesburg tu na bado bidhaa zina mawinga Waethiopia sema kupata chimbo halisi ni nzuri zaidi.maana wenye mitaji mikubwa wao mzigo ukifika wanachukua wote Mchina anabaki na Lonya tu ambazo tutafata kununua..
 
Ilala unakuta suruali kali sana inawaka kweli kumbe wahuni wameipaka mafuta ya baiskeli, ukiipiga maji tu utajua mjini sio kuzuri.
 
Hicho kitu kizuri na ndiyo biashara za Sasa zinavyofanywa.
Ukienda kiwanda Cha bati lazima upitie kwa agent huyu kamabwinga tu.
Mnachotakiwa kufanya ni kutafuta namba ya kuwabana wasizidishe Sana bei na wasifanye utapeli au kuuza vitu vibovu.
Mimi nimejiapiza siwezi kununua tena simu duka flani Kariakoo. Sababu winga aliniuzia simu mbovu nikarudisha akaniletea mbovu Tena. Ubovu wake si wa kuonekana kwa macho Hadi utumie masaa kadhaa.
Zamani nimenunua simu kibao hazikuwa hivyo.
 
Umaskini na kupenda vitu vya bei chee ni sawa na CCM na wizi wa kura.
 
Shida ni ule usumbufu na uking'ang'anizi wao. Na ile wanakufata kundi kubwa na maneno kibao huku wanakuzongazonga ilhali umeenda kwa hiyari yako na zaidi ya yote unajua duka unaloenda kufanya manunuzi na ukiwaambia bado watataka muongozane dukani ionekane wao ndo wamekupeleka huku wakikutaji bei wao na sio muuzaji.

Wafanyabiashara wajaribu kuyacontrol tu ila sio kuwafukuza, acha vijana wapate chochote.
 
Nilienda kununua generator mwenye duka akaniambia niende kwa winga nikazungumze nae,winga akaniambia bei ni mil 3.5 Mimi nikamwambia Nina mil 2.2 tu sishushi siongezi!
Winga akakomaa akasema nitoe mil 3.3 nikaamua kuondoka.
Ile naondoka tu mwenye duka akanikimbilia akaniambia toa hiyo hiyo mil 2.2
 
Noma sana kuna kipindi nikaenda Keko kununua kitanda ile nafika tu kuna jamaa wawili wakanikaribisha dukani kwao. Nilipotoka walizunguka na mimi maduka yote. Mpaka nikaamua kusepa bila manunuzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…