Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

Bro hujui how things work. Biashara zote dunian zinafanyika online na wakat mwingine huwez kuwa na watu wote online so unakuta una mawinga kama 50 kila mtu ana wafuasi elfu 4 tuseme na wanakuja dukan kupiga picha kuposti so ndani ya nusu saa kila Winga anakuja huyu anataka pcs 30 huyu kumi huyu 20 na wanakuja kuchukua mizigo kupelekea wateja huko walipo so yeye anapata cha juu na wewe unapata chochote kitu. Ndivyo mfumo wa biashara ulivyo dunian lazima awepo mtu wa kati anaerahisisha kazi zako ziaende. Kwa mtu ambae amesafir anajua hasa viwandani. Biashara ni agent mzee. Na hiyo ya dukan kusubirishwa ni kawaida kkoo mi tangu naanza biashara vijana wanafanya hivyo miaka hiyo we umestuka leo na hata wagen wanajua. Kwa mfano mimi biashara yangu ni groups za whatsp za wateja wangu kutoka congo zambia Zimbabwe kenya malawi Rwanda Burundi comoro msumbiji nk. So mzigo ukitoka natoa sampo store narusha kwenye whatsp kila mtu anaweka order humo humo kutoka hizo nchi na wanaingiza mizigo kwenye account yako unawatumia mizigo yao. Simpo mzee life ishabadilika kaka. Mimi naweza kuuza mizigo nikiwa hukuhuku china ikawafuata wateja walipo na wakaniingizia mpunga wangu kwenye account tu. So usikariri maisha mzee pinduka maisha na yenyewe yanavyopinduka waache wenye kibarua cha kulaumu walaumu kila mtu apigane vita vyake. Ukiona umestuka ujue kuna mwingine ni mtaji, biashara ni mchezo wa sanaa kuna wakati unafungwa na kuna wakat unafunga.
Mkuu, uchuuzi wa kitapeli si mzuri. Kwa eneo kama Kariakoo hauoni impact kwa haraka sababu watu ni wengi na kila siku kuna watu wapya wa kutapeliwa ila si jambo zuri kibiashara.

Unaweza kuwa na duka lako, ukawa na bei elekezi kwa mawinga wako wanaowaleta wateja hapo dukani. Utauza mno maana hutategemea wapitaji wapya bali wapya na wanaopita na kurudi.

Kwa wale wanaopost online na wanawapelekea wateja sawa ila kwa hawa wanaokuja na mteja dukani jitahidi uwe na bei elekezi kwa wateja wako.
 
Usijisumbue kwenda kariakoo kununua mzigo ukidhani Kuna bei nafuu
Kariakoo wamejaa wajanja na madalali tu
Unaweza ingia kwenye duka ukamkuta mwenye duka ukamuuliza bei akakuelekeza uongee na vijana wake wakuumize
Nyie watu situka Kariakoo hakufai kabisa, mawinga wameharibu uaminifu
Matajiri wanauchukulia wateja kama wajinga, wanajua kuwa mtaenda tu
Sasa naomba niwape machimbo mapya Kwa Dar

1. Kwa wale wa electronics nenda Tegeta pale Kibo complex utapata bei ambayo Kariakoo haipo

Pia nenda Mbagala rangi Tatu utapata electronics zote, kuanzia Tv, simu, cable

2. Nguo nenda Mwenge au Makumbusho

3. Mitumba
Usijaribu kwenda Karume au Ilala tena
Kwa mitumba ya bei nafuu, mabalo za rejareja nenda Tandika, Temeke, Tandale na Mwenge

Kanda ya ziwa, machimbo yapo Katoro

Kwa machimbo mengine, tujaribu ku share.
Ila chonde chonde kariakoo utaishia kupandiliwa na kupigwa bei ya maana
Kariakoo nilikuwepo Jana, nikahairisha kuchukua mzigo kisa mawinga
Kuuliza sio ujinga then wafanyabiashara wananufaika kitu gani na hao mawinga? Au ni roho nzuri tu, yaani nifungue duka kwa pesa zangu alafu mimpe nafasi dalali apange bei ili nae apate ulaji alinisaidia mtaji?
 
Usijisumbue kwenda kariakoo kununua mzigo ukidhani Kuna bei nafuu
Kariakoo wamejaa wajanja na madalali tu
Unaweza ingia kwenye duka ukamkuta mwenye duka ukamuuliza bei akakuelekeza uongee na vijana wake wakuumize
Nyie watu situka Kariakoo hakufai kabisa, mawinga wameharibu uaminifu
Matajiri wanauchukulia wateja kama wajinga, wanajua kuwa mtaenda tu
Sasa naomba niwape machimbo mapya Kwa Dar

1. Kwa wale wa electronics nenda Tegeta pale Kibo complex utapata bei ambayo Kariakoo haipo

Pia nenda Mbagala rangi Tatu utapata electronics zote, kuanzia Tv, simu, cable

2. Nguo nenda Mwenge au Makumbusho

3. Mitumba
Usijaribu kwenda Karume au Ilala tena
Kwa mitumba ya bei nafuu, mabalo za rejareja nenda Tandika, Temeke, Tandale na Mwenge

Kanda ya ziwa, machimbo yapo Katoro

Kwa machimbo mengine, tujaribu ku share.
Ila chonde chonde kariakoo utaishia kupandiliwa na kupigwa bei ya maana
Kariakoo nilikuwepo Jana, nikahairisha kuchukua mzigo kisa mawinga
Namba 3 uko sawa
Ila namba mbili umeharibu Makumbusho wahuni sana sishauri ukununue vitu makumbusho😅
 
Back
Top Bottom