Kati mamba, simba na chatu yupi mrahisi kuokoka tukikutana naye?

Kati mamba, simba na chatu yupi mrahisi kuokoka tukikutana naye?

Kila mnyama ana weekness yake chatu mbio hana, mamba nchi kavu mgambo tu hana jipya, simba ukimwangalia directly machoni ana aibu kama unamtongoza si ajabu akaanza kutafuna vidole na kuvunja vijiti ila ombea usikutane na nyegele ni mpaka akukague we ni jinsia gani
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]jamani
 
si mnasema mamba akiwa nchi kavu ni mchumba

sasa mkute anaatamia mayai yake ndio utajua hujui
Mnyama yeyote anasehemu yake ya kujidai hutoboi, simba ukimkuta polini ni tofauti na ukikutana nae mtaani, hata wewe ukiwa ugenini kujiamini kunapungua kama ukiwa nyumbani. Ila mamba usimchukulie poa mzee waliokaa visiwani wananielewa.
 
Naombeni mniambie mimi sijawahi kukutana na mamba wala chatu ila nahitaji kujua je ukikutana na Hao Wanyama.

Assume una upanga mkali yupi ukipambana naye Shambani huko ng'anya yake sio ndogo.

Yaani yupi ukijiingiza kwenye mfumo wake wa mtego pambano lake atakuzidi kirahisi na yupi mwepesi kumshinda.
bora simba kuliko chatu na mamba. chatu ni hatari kupita watu mnavyodhani, akifanikiwa kukukamata tu hata uwe na nguvu gani hutoki, anakubana mbavu muda si mrefu umeshanyooka. mamba ana nguvu kwenye maji za ajabu, na ule mdomo akiufumba baada ya kukung'ata, hata jeki inahangaika kuufunua. ndizo nguvu Mungu aliwaumba nazo. simba ni hatari ila ana akili, huwa anajihami pia, unaweza walau kusavaivu.

lakini hatari kuliko vyote tunavyojadili ni dhambi, Mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele kwa Yesu Kristo Bwana wetu. mauti inayoongelewa hapa ni hii ya mwili kufa, na baada ya hapo, mauti ya kutengwa na Mungu na kuunguzwa moto milele na milele. bora uuliwe na hawa wanyama ukaenda uzimani, kuliko kuuliwa na hawa na zaidi ya hapo ukaenda motoni. Neema ya Mungu imefunuliwa kwetu nayo yatufundisha kukataa mabaya, ukiona unapumua, unaongea, una afya, jua ni Neema ya Mungu, anakuvuta pengine utabadilika, Mungu anakupenda mno kuliko unavyoelewa, ameshaona hatari iliyoko mbele yako, hatari ya moto wa milele, hatari ya kifo cha kidunia pia, na anakupa nafasi pengine uokoke ili ukifa ufe katika Bwana na ukiishi uishi katika Bwana. Mpe Yesu maisha yako leo, uone kama hautabadilika, Okoka leo, kwasababu hujui lini utakata pumzi.
 
Hao wote utaokoka hatari ukutane na nyati jike aliyepoteza ndama

Utatamani ardhi ikumeze

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo kuna dogo alikua na babaake anamfundisha uwindaji.
Wakamtwanga risasi guruneti wakamjeruhi begani.
E bana Nyati alirudi nao mpk kambini mpk gari
walisahau maana ilikua ni mbio tu,
Na nyati akawepo hapo Nje anawangoja.
Huyo Dogo toka siku hiyo ikawa ni kilio tu.
Hataki chochote zaidi ya kurudi kwao.
Tukamrudisha Airport atimke.
 
Mnyama yeyote anasehemu yake ya kujidai hutoboi, simba ukimkuta polini ni tofauti na ukikutana nae mtaani, hata wewe ukiwa ugenini kujiamini kunapungua kama ukiwa nyumbani. Ila mamba usimchukulie poa mzee waliokaa visiwani wananielewa.
tunakuelewa vizuri mnooo

Mamba ni habari nyingine
 
Back
Top Bottom