Kati ya Polisi na Lissu ni nani wa kuwasaka waliotaka kumuua Lissu??

Kati ya Polisi na Lissu ni nani wa kuwasaka waliotaka kumuua Lissu??

Hakuondoshwa aliondoka. Hivi Dereva umuhimu wake kwenye hili jambo uko kwenye nini ama unazuia nini Polisi kufanya uchunguzi wao? Hivi kati ya Dereva na CCTV iliyong'olewa kwa Kalemani kipi cha muhimu??
Yeye ndio ana taarifa muhimu kwa sababu alijua kuwa kuna gari inawafuatilia
 
Hata ukiibiwa fedha chumbani kwako polisi wanaanza kumuhoji mkeo ndio wanaendelea na wengine!

Very simple
Polisi kuanza kuhoji mkeo na kufanya utafiti wa kuwahoji majirani lilipotokea tukio la kutaka kuua havihusiani. Wao mpaka sasa wameshafanya nini iwe imebakia tu kumhoji Dereva wa Lissu??
 
Polisi kuanza kuhoji mkeo na kufanya utafiti wa kuwahoji majirani lilipotokea tukio la kutaka kuua havihusiani. Wao mpaka sasa wameshafanya nini iwe imebakia tu kumhoji Dereva wa Lissu??
Wewe hujiulizi Kwanini Wote wamerudi isipokuwa dereva wa Lisu tu?
 
Beki 3 wa Lisu na yule wa Tulia ambao kimsingi ndio waliokoa Maisha ya Tundu Lisu wameshatoa Maelezo yao!

Au unataka majirani gani?
Usiwadhalilishe Polisi wetu. Kutokuwepo kwa Dereva wa Lissu hakuwezi kuzuia Polisi werevu kufanya uchunguzi wao. Labda utuambie kuwa Polisi wetu viwango vyao vya kufanya uchunguzi ni vya chini sana.
 
Kwenye mambo ya kihalifu nchi nyingi zimelipa Jeshi la polisi wajibu wa kushughulika na uchunguzi pale uhalifu unapotokea. Kwa Tanzania Polisi kupitia kwa DCI ndiyo wamepewa kazi ya kupeleleza uhalifu unapotokea kupitia kitengo cha CID.

Kwenye Jambo la Lissu ama kwa uzembe ama kwa kukusudia au kwa kuamriwa, Jeshi la Polisi kupitia kwa DCI kwa namna yoyote ile halijaonesha kama lina nia ya kupeleleza nani hasa waliotaka kumuua Lissu. Tangu Lissu ashambuliwe mwaka 2017 leo miaka Sita baadae uwezekano wa kupata ushahidi wa moja kwa moja unakuwa mgumu.

Lakini siku ya tukio kulikuwa kuna kila uwezekano wa kupata ushahidi unaotakiwa kuwatia mbaroni wote waliohusika. Kwanza wale watu walitumia usafiri wa Magari hivyo haikuwa ngumu kupata taarifa zao. Kwa mfano aina ya gari zilizotumika ni lazima tu zilijulikana na kuonekana.

Kwa sababu risasi zilipigwa mchana, ni lazima sauti zilikuwa kubwa hivyo bila ya shaka majirani walitoka kuangalia kuna nini. Hao majirani lazima waliziona gari zilizohusika na aina yake. Majirani hao pia waliona baaada ya tukio gari hizo zilielekea wapi.

Tuliambiwa kwamba Medard Kalemani alikuwa anakaa jengo moja na Lissu. Jee kwa Kalemani kulikuwa hakuna mtu, jee ni kweli kwamba kulikuwa na CCTV na ikaodolewa baada ya tukio. Jee Polisi walipofika kwa Kalemani hakuna waliyemhoji?

Bila ya shaka hao waliotaka kumuua Lissu pia walitumia simu za mkononi, Jee Polisi waliangalia simu zilizopigwa toka kwenye minara ya simu iliyo karibu na tukio lilipotokea, walifanya uchambuzi wa mawasiliano yaliyofanyika toka eneo la tukio masaa miwili kabla ya tukio na dakika chache baada ya tukio?

Baada ya uchambuzi wa mawasiliano hayo walilinganisha namba hizo za simu kabla ya kutumika eneo la tukio zilitumika wapi kabla. Jee hizo namba ziliwasiliana na namba gani nyingine, na hizo namba zinamilikiwa na nani? Lissu ni mwanasiasa, jee Polisi waliangalia mawasiliano ya wanasiasa wa CHADEMA na CCM kabla ya tukio na baada ya tukio walikuwa wamewasiliana na nani na waliwasiliana mara ngapi na kuhusu nini?

Polisi waliwahoji majirani wa Lissu kwa umbali gani na kwa muelekeo upi? Mpaka sasa polisi wanayo maelezo ya watu wangapi waliowahoji toka tukio lilipotokea mpaka sasa. Jee Kuna majirani au marafiki wa Lissu ambaye anatiliwa shaka kutokana na mwenendo wake dhidi ya Lissu?

Polisi mpaka sasa wanao washukiwa wangapi au watu wanaowatilia shaka kuhusika na tukio lile? Hadi hapa ni nani wa kulaumiwa kati ya Polisi na Lissu??
Polisi hawajawahi kujiangaisha na inshu ya Lissu kupigwa risasi, ndo maana chadema ilipoomba wachunguzi kutoka nje ya nchi waje wafanye uchunguzi serikali ilikataa kbs, ilikataa kwa sababu ilihusika kwa 100% ... Order ilitoka kwa raia namba moja,ikatekelezwa na mwanaye mpendwa lkn mwenyezi mungu akasema hafi mtu hapa .. kwahiyo hata hao pimbi wanaomtaka dreva wa Lissu aje kutoa maelezo ni makanjanja tu, walitaka dreva wa Lissu aje ili wamhonge aseme ni chadema ndo walihusika na lile tukio...uzuri kila kilichokuwa kinapangwa na yule raia namba moja wa kipindi kile kulikuwa kinavuja moja kwa moja... hvyo ni tukio la hovyo kuwahi kutokea ambalo kila mwenye akili timamu anajua kbs serikali ilihusika na lile jaribio

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
Very simple!
Wakati mwingine najiuliza ni kwa nini kwenye chama chenu mmejaza "Manipulators" na "Spinning Doctors", Yaani mnataka kila Mtanzania awe "Zombie" kwa faida zenu za kisiasa.

Hivi hao polisi wanaongojea Dereva wa Lissu arudi wangepewa kazi ya kupeleleza lile tukio la Bomu la Oklahoma wangefanyaje? Zama hizi za teknolojia bado kuna mtu mwenye akili timamu anakaa na kuwaambia watu kwamba ameshindwa kupeleleza tukio la Lissu kupigwa Risasi eti kwa kuwa Dereva wa Lissu hayupo!!

Ujinga kabisa huu!!
 
Kwenye mambo ya kihalifu nchi nyingi zimelipa Jeshi la polisi wajibu wa kushughulika na uchunguzi pale uhalifu unapotokea. Kwa Tanzania Polisi kupitia kwa DCI ndiyo wamepewa kazi ya kupeleleza uhalifu unapotokea kupitia kitengo cha CID.

Kwenye Jambo la Lissu ama kwa uzembe ama kwa kukusudia au kwa kuamriwa, Jeshi la Polisi kupitia kwa DCI kwa namna yoyote ile halijaonesha kama lina nia ya kupeleleza nani hasa waliotaka kumuua Lissu. Tangu Lissu ashambuliwe mwaka 2017 leo miaka Sita baadae uwezekano wa kupata ushahidi wa moja kwa moja unakuwa mgumu.

Lakini siku ya tukio kulikuwa kuna kila uwezekano wa kupata ushahidi unaotakiwa kuwatia mbaroni wote waliohusika. Kwanza wale watu walitumia usafiri wa Magari hivyo haikuwa ngumu kupata taarifa zao. Kwa mfano aina ya gari zilizotumika ni lazima tu zilijulikana na kuonekana.

Kwa sababu risasi zilipigwa mchana, ni lazima sauti zilikuwa kubwa hivyo bila ya shaka majirani walitoka kuangalia kuna nini. Hao majirani lazima waliziona gari zilizohusika na aina yake. Majirani hao pia waliona baaada ya tukio gari hizo zilielekea wapi.

Tuliambiwa kwamba Medard Kalemani alikuwa anakaa jengo moja na Lissu. Jee kwa Kalemani kulikuwa hakuna mtu, jee ni kweli kwamba kulikuwa na CCTV na ikaodolewa baada ya tukio. Jee Polisi walipofika kwa Kalemani hakuna waliyemhoji?

Bila ya shaka hao waliotaka kumuua Lissu pia walitumia simu za mkononi, Jee Polisi waliangalia simu zilizopigwa toka kwenye minara ya simu iliyo karibu na tukio lilipotokea, walifanya uchambuzi wa mawasiliano yaliyofanyika toka eneo la tukio masaa miwili kabla ya tukio na dakika chache baada ya tukio?

Baada ya uchambuzi wa mawasiliano hayo walilinganisha namba hizo za simu kabla ya kutumika eneo la tukio zilitumika wapi kabla. Jee hizo namba ziliwasiliana na namba gani nyingine, na hizo namba zinamilikiwa na nani? Lissu ni mwanasiasa, jee Polisi waliangalia mawasiliano ya wanasiasa wa CHADEMA na CCM kabla ya tukio na baada ya tukio walikuwa wamewasiliana na nani na waliwasiliana mara ngapi na kuhusu nini?

Polisi waliwahoji majirani wa Lissu kwa umbali gani na kwa muelekeo upi? Mpaka sasa polisi wanayo maelezo ya watu wangapi waliowahoji toka tukio lilipotokea mpaka sasa. Jee Kuna majirani au marafiki wa Lissu ambaye anatiliwa shaka kutokana na mwenendo wake dhidi ya Lissu?

Polisi mpaka sasa wanao washukiwa wangapi au watu wanaowatilia shaka kuhusika na tukio lile? Hadi hapa ni nani wa kulaumiwa kati ya Polisi na Lissu??

Zama hizo palikuwa na genge la wasiojulikana. Majina haya yalikuja kutajwa kuwa kwenye genge hilo:

Goodluck, Mahita, Jumanne, na yule Mwingine akiwamo.

Sasa kama hiyo ofisi kubwa ndiyo yenye kulisaka kundi hili hili mbona hapo mtihani mkuu?

Kwamba wanajitafutaje wenyewe sasa?

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Back
Top Bottom