Kati ya Polisi na Lissu ni nani wa kuwasaka waliotaka kumuua Lissu??

Kati ya Polisi na Lissu ni nani wa kuwasaka waliotaka kumuua Lissu??

Kwenye mambo ya kihalifu nchi nyingi zimelipa Jeshi la polisi wajibu wa kushughulika na uchunguzi pale uhalifu unapotokea. Kwa Tanzania Polisi kupitia kwa DCI ndiyo wamepewa kazi ya kupeleleza uhalifu unapotokea kupitia kitengo cha CID.

Kwenye Jambo la Lissu ama kwa uzembe ama kwa kukusudia au kwa kuamriwa, Jeshi la Polisi kupitia kwa DCI kwa namna yoyote ile halijaonesha kama lina nia ya kupeleleza nani hasa waliotaka kumuua Lissu. Tangu Lissu ashambuliwe mwaka 2017 leo miaka Sita baadae uwezekano wa kupata ushahidi wa moja kwa moja unakuwa mgumu.

Lakini siku ya tukio kulikuwa kuna kila uwezekano wa kupata ushahidi unaotakiwa kuwatia mbaroni wote waliohusika. Kwanza wale watu walitumia usafiri wa Magari hivyo haikuwa ngumu kupata taarifa zao. Kwa mfano aina ya gari zilizotumika ni lazima tu zilijulikana na kuonekana.

Kwa sababu risasi zilipigwa mchana, ni lazima sauti zilikuwa kubwa hivyo bila ya shaka majirani walitoka kuangalia kuna nini. Hao majirani lazima waliziona gari zilizohusika na aina yake. Majirani hao pia waliona baaada ya tukio gari hizo zilielekea wapi.

Tuliambiwa kwamba Medard Kalemani alikuwa anakaa jengo moja na Lissu. Jee kwa Kalemani kulikuwa hakuna mtu, jee ni kweli kwamba kulikuwa na CCTV na ikaodolewa baada ya tukio. Jee Polisi walipofika kwa Kalemani hakuna waliyemhoji?

Bila ya shaka hao waliotaka kumuua Lissu pia walitumia simu za mkononi, Jee Polisi waliangalia simu zilizopigwa toka kwenye minara ya simu iliyo karibu na tukio lilipotokea, walifanya uchambuzi wa mawasiliano yaliyofanyika toka eneo la tukio masaa miwili kabla ya tukio na dakika chache baada ya tukio?

Baada ya uchambuzi wa mawasiliano hayo walilinganisha namba hizo za simu kabla ya kutumika eneo la tukio zilitumika wapi kabla. Jee hizo namba ziliwasiliana na namba gani nyingine, na hizo namba zinamilikiwa na nani? Lissu ni mwanasiasa, jee Polisi waliangalia mawasiliano ya wanasiasa wa CHADEMA na CCM kabla ya tukio na baada ya tukio walikuwa wamewasiliana na nani na waliwasiliana mara ngapi na kuhusu nini?

Polisi waliwahoji majirani wa Lissu kwa umbali gani na kwa muelekeo upi? Mpaka sasa polisi wanayo maelezo ya watu wangapi waliowahoji toka tukio lilipotokea mpaka sasa. Jee Kuna majirani au marafiki wa Lissu ambaye anatiliwa shaka kutokana na mwenendo wake dhidi ya Lissu?

Polisi mpaka sasa wanao washukiwa wangapi au watu wanaowatilia shaka kuhusika na tukio lile? Hadi hapa ni nani wa kulaumiwa kati ya Polisi na Lissu??
Wewe si Polisi haya mambo huyajui bora ungekaa kimya. Kwa miiko ya Kipolisi, na ndiyo ukweli, shahidi mzuri ni yule aliyewaona kwa macho wao huita eyewitness. Kuna mtu mmoja aliwaona mchana kweupe kama ulivyosema, mtu huyo anaitwa tundulissu. Kwa nini hajaenda Polisi, badala ya kuwatukana? Kulikuwa na shahidi mwingine, eyewitness, dereva wake tundulissu naye kawaona kwa macho yake, na ni askari. Kafichwa na CHADEMA (nasikia yuko kafungiwa chumbani pale Ufipa). Finally, hakuna hadi leo aliyelalamika, kwani tundulissu hana ndugu? Hana mke? Umetaja CCTV, nani alizing'oa? Saa ngapi? Kumbuka hakuna aliyejua kuwa tundulissu ataenda lunch siku hiyo, aliyezing'oa kwani alijuaje?

Umetaja majirani, sawa kabisa: Watanzania tunashiriki harusi, iddi, kipaimara, Christmas, mazishi, nk. Mbona hawakujitokeza hata mmoja? Jiulize, au labda tundulissu hana ushirikiano? Si unajua alivyo mshari na matusi, labda wamemtenga? Pia unajua alivyo majivuno, labda majirani kawachosha? Au labda yeye huwaga haendagi kwenye misiba ya jirani?

Kwa basic mathematics, 2+2=4. Ni wazi kuwa tundulissu na CHADEMA walijua kila kitu kilichotokea, haja yao ilikuwa kuitia aibu serkali na kuifitinisha na raia. Wewe uliona wapi risasi za SMG ziingie moyoni au tumboni halafu mtu asife? Hii ilipangwa ila hawakutegemea ataumia kiasi hicho, lakini wanaogopa kusema. Ila tukumbuke Dr Mollel aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA jimbo la Sanya Juu, afisa wao mwandamizi, aliyoboa kuwa alishambuliwa na CHADEMA. Hata Dr Slaa unakumbuka alikataa kwenda kumslamu au kumpa pole kwa sababu ana dukuduku lake. Let CHADEMA come clean on this, our Police are very busy please.
 
Wewe si Polisi haya mambo huyajui bora ungekaa kimya. Kwa miiko ya Kipolisi, na ndiyo ukweli, shahidi mzuri ni yule aliyewaona kwa macho wao huita eyewitness.
Kwanza umeandika mambo meengi yasiyohusiana na hii mada kasoro hili moja. Kuwa eneo la tukio siyo sifa ya kuwa "Eyewiteness" kwa kuwa ili uweze kuona ni lazima ubongo wako utoke kwenye kuangalia kwenda kwenye kuona. Ndiyo maana unaweza kumuangalia mtu lakini usimuone.

Yaani kwenye Mazingira yale ulitaka Dereva wa Lissu awe na uwezo wa kuona waliomshambulia Lissu kuliko CCTV? Yaani CHADEMA wasio chombo cha kufanya upelelezi unataka kuwatwisha jambo lisilowahusu? Hivi kama Lissu alikuwa hana mahusiano na majirani zake inazuia vipi polisi kuwahoji hao majirani?

gabby-giffords-interview.jpg

Unamuona huyu dada, anaitwa Gabby Gilford, alikuwa ni Mbunge kwenye Bunge la Marekani na alipigwa Risasi iliyopenya toka upande mmoja wa sikio kwenda sikio jingine. Leo Gabby yupo hai akiwa na akili timamu.

Unashangaa vipi Lissu kuwa hai!!??
 
Wewe si Polisi haya mambo huyajui bora ungekaa kimya. Kwa miiko ya Kipolisi, na ndiyo ukweli, shahidi mzuri ni yule aliyewaona kwa macho wao huita eyewitness. Kuna mtu mmoja aliwaona mchana kweupe kama ulivyosema, mtu huyo anaitwa tundulissu. Kwa nini hajaenda Polisi, badala ya kuwatukana? Kulikuwa na shahidi mwingine, eyewitness, dereva wake tundulissu naye kawaona kwa macho yake, na ni askari. Kafichwa na CHADEMA (nasikia yuko kafungiwa chumbani pale Ufipa). Finally, hakuna hadi leo aliyelalamika, kwani tundulissu hana ndugu? Hana mke? Umetaja CCTV, nani alizing'oa? Saa ngapi? Kumbuka hakuna aliyejua kuwa tundulissu ataenda lunch siku hiyo, aliyezing'oa kwani alijuaje?

Umetaja majirani, sawa kabisa: Watanzania tunashiriki harusi, iddi, kipaimara, Christmas, mazishi, nk. Mbona hawakujitokeza hata mmoja? Jiulize, au labda tundulissu hana ushirikiano? Si unajua alivyo mshari na matusi, labda wamemtenga? Pia unajua alivyo majivuno, labda majirani kawachosha? Au labda yeye huwaga haendagi kwenye misiba ya jirani?

Kwa basic mathematics, 2+2=4. Ni wazi kuwa tundulissu na CHADEMA walijua kila kitu kilichotokea, haja yao ilikuwa kuitia aibu serkali na kuifitinisha na raia. Wewe uliona wapi risasi za SMG ziingie moyoni au tumboni halafu mtu asife? Hii ilipangwa ila hawakutegemea ataumia kiasi hicho, lakini wanaogopa kusema. Ila tukumbuke Dr Mollel aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA jimbo la Sanya Juu, afisa wao mwandamizi, aliyoboa kuwa alishambuliwa na CHADEMA. Hata Dr Slaa unakumbuka alikataa kwenda kumslamu au kumpa pole kwa sababu ana dukuduku lake. Let CHADEMA come clean on this, our Police are very busy please.
Utopolo mtupu, yaani inaonekana ww ni mmoja wa wale waliomshambulia mhe Lissu

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
Wewe si Polisi haya mambo huyajui bora ungekaa kimya. Kwa miiko ya Kipolisi, na ndiyo ukweli, shahidi mzuri ni yule aliyewaona kwa macho wao huita eyewitness. Kuna mtu mmoja aliwaona mchana kweupe kama ulivyosema, mtu huyo anaitwa tundulissu. Kwa nini hajaenda Polisi, badala ya kuwatukana? Kulikuwa na shahidi mwingine, eyewitness, dereva wake tundulissu naye kawaona kwa macho yake, na ni askari. Kafichwa na CHADEMA (nasikia yuko kafungiwa chumbani pale Ufipa). Finally, hakuna hadi leo aliyelalamika, kwani tundulissu hana ndugu? Hana mke? Umetaja CCTV, nani alizing'oa? Saa ngapi? Kumbuka hakuna aliyejua kuwa tundulissu ataenda lunch siku hiyo, aliyezing'oa kwani alijuaje?

Umetaja majirani, sawa kabisa: Watanzania tunashiriki harusi, iddi, kipaimara, Christmas, mazishi, nk. Mbona hawakujitokeza hata mmoja? Jiulize, au labda tundulissu hana ushirikiano? Si unajua alivyo mshari na matusi, labda wamemtenga? Pia unajua alivyo majivuno, labda majirani kawachosha? Au labda yeye huwaga haendagi kwenye misiba ya jirani?

Kwa basic mathematics, 2+2=4. Ni wazi kuwa tundulissu na CHADEMA walijua kila kitu kilichotokea, haja yao ilikuwa kuitia aibu serkali na kuifitinisha na raia. Wewe uliona wapi risasi za SMG ziingie moyoni au tumboni halafu mtu asife? Hii ilipangwa ila hawakutegemea ataumia kiasi hicho, lakini wanaogopa kusema. Ila tukumbuke Dr Mollel aliyekuwa Mbunge wa CHADEMA jimbo la Sanya Juu, afisa wao mwandamizi, aliyoboa kuwa alishambuliwa na CHADEMA. Hata Dr Slaa unakumbuka alikataa kwenda kumslamu au kumpa pole kwa sababu ana dukuduku lake. Let CHADEMA come clean on this, our Police are very busy please.

Ndugu policeman:

1. Hukuwaongelea polisi waliopaswa kuwa getini kuwakagua wote wenye kuingia kwenye Ile compound ya viongozi area D.

2. Hukuwaongelea polisi Dodoma, ambao taarifa yao ya awali ilisema walizipata CCTV recordings husika za tukio.

3. Umejisahaulisha kuwa CCTV ziling'olewa baada ya tukio.

4. Umejisahaulisha pia kuwa upelelezi ulipaswa kufanyika na kuwapata wahalifu hata kama Lissu na Dereva wote wangalikuwa marehemu.

5. Umejisahaulisha pia kuwa hata kama Chadema, Lissu au driver walihusika upelelezi ulipaswa kuonyesha hayo na kuwakamata wahusika wote.

Kwani mna kipi cha kuficha kwenye hili sekeseke ndugu?

Au ni Ile habari kubwa kuwa mwenye lake jambo alikuwa ni yule mwenye ule mhimili uliokuwa umejichimbia zaidi?
 
Lisu anaogopa nini kumleta dereva wake?
Nini dereva, kwa nini yeye mwenyewe Lissu hawamuhoji? Ushahidi wa dereva na ushahidi wa CCTV cameras footages upi ni wa uhakika zaidi? Polisi waliopaswa kuwa zamu na mabosi wao wanaopanga zamu za lindo kwa nini hawakuhojiwa? Kwa nini hata Jiwe mpenda sifa hakuwahi hata 'kuwapiga' chini mabosi wa polisi Dodoma au hata IGP manake alikuwa maridadi kwa misifa.
Vipi wazo la Mbowe la kushirikisha FBI au MI6 ya Scotland Yard mbona polisi walilikataa wakidai kila kitu kipo ndani ya uwezo wao, kumbe ilikuwa ni danganya toto hawakuwa wakitaka upelelezi ufanyike.
Mambo ya ajabu baada ya shambulio:
-Kuzuia watu wasimuombee Lissu.
-Kuzuia T-shirts zenye maandishi ya 'Get well soon Lissu'
-Kufura kwa subwoofer Ndugai kwamba imekuwa Lissu kapelekwa kutiwa Nairobi(obviously angebaki wangemmalizia hospitali) na wakadai ni mtoro asilipwe chochote wala asigharamiwe matibabu.

La muhimu kuliko yote - Footages za CCTV cameras ziibuliwe kokote zilikofichwa tujionee shambulio lilivyofanyika na si kupewa story za watu za kuungaunga au kuwatia watu kwenye pressure(brutal interrogations) mpaka wakiri hata mambo ya uongo, a picture speaks thousand words.
 
Kwenye mambo ya kihalifu nchi nyingi zimelipa Jeshi la polisi wajibu wa kushughulika na uchunguzi pale uhalifu unapotokea. Kwa Tanzania Polisi kupitia kwa DCI ndiyo wamepewa kazi ya kupeleleza uhalifu unapotokea kupitia kitengo cha CID.

Kwenye Jambo la Lissu ama kwa uzembe ama kwa kukusudia au kwa kuamriwa, Jeshi la Polisi kupitia kwa DCI kwa namna yoyote ile halijaonesha kama lina nia ya kupeleleza nani hasa waliotaka kumuua Lissu. Tangu Lissu ashambuliwe mwaka 2017 leo miaka Sita baadae uwezekano wa kupata ushahidi wa moja kwa moja unakuwa mgumu.

Lakini siku ya tukio kulikuwa kuna kila uwezekano wa kupata ushahidi unaotakiwa kuwatia mbaroni wote waliohusika. Kwanza wale watu walitumia usafiri wa Magari hivyo haikuwa ngumu kupata taarifa zao. Kwa mfano aina ya gari zilizotumika ni lazima tu zilijulikana na kuonekana.

Kwa sababu risasi zilipigwa mchana, ni lazima sauti zilikuwa kubwa hivyo bila ya shaka majirani walitoka kuangalia kuna nini. Hao majirani lazima waliziona gari zilizohusika na aina yake. Majirani hao pia waliona baaada ya tukio gari hizo zilielekea wapi.

Tuliambiwa kwamba Medard Kalemani alikuwa anakaa jengo moja na Lissu. Jee kwa Kalemani kulikuwa hakuna mtu, jee ni kweli kwamba kulikuwa na CCTV na ikaodolewa baada ya tukio. Jee Polisi walipofika kwa Kalemani hakuna waliyemhoji?

Bila ya shaka hao waliotaka kumuua Lissu pia walitumia simu za mkononi, Jee Polisi waliangalia simu zilizopigwa toka kwenye minara ya simu iliyo karibu na tukio lilipotokea, walifanya uchambuzi wa mawasiliano yaliyofanyika toka eneo la tukio masaa miwili kabla ya tukio na dakika chache baada ya tukio?

Baada ya uchambuzi wa mawasiliano hayo walilinganisha namba hizo za simu kabla ya kutumika eneo la tukio zilitumika wapi kabla. Jee hizo namba ziliwasiliana na namba gani nyingine, na hizo namba zinamilikiwa na nani? Lissu ni mwanasiasa, jee Polisi waliangalia mawasiliano ya wanasiasa wa CHADEMA na CCM kabla ya tukio na baada ya tukio walikuwa wamewasiliana na nani na waliwasiliana mara ngapi na kuhusu nini?

Polisi waliwahoji majirani wa Lissu kwa umbali gani na kwa muelekeo upi? Mpaka sasa polisi wanayo maelezo ya watu wangapi waliowahoji toka tukio lilipotokea mpaka sasa. Jee Kuna majirani au marafiki wa Lissu ambaye anatiliwa shaka kutokana na mwenendo wake dhidi ya Lissu?

Polisi mpaka sasa wanao washukiwa wangapi au watu wanaowatilia shaka kuhusika na tukio lile? Hadi hapa ni nani wa kulaumiwa kati ya Polisi na Lissu??
We jamaa mbona una maswali magumu kiasi hicho?
 
Hitller hakuna nayejua kwamba aliuwawa au alijiua mwenyewe kwenye Tindikali.....mfano wa hovyoo huu.Lissu dereva wake yupo na yeye yupo watajwe tu.
Yule Muhutu mwenzako Jiwe ndiye alikuwa muhusika namba moja(hii ni kwa mujibu wa Lissu mwenyewe na ameongea live kwenye vyombo vya habari) na mpaka leo si polisi wala uongozi wa serikali waliokanusha, wanatamani lile tukio lisahaulike lakini halitosahaulika na litakuwa likiibuliwa mara kwa mara mpaka majibu yapatikane.
 
Polisi hawajawahi kujiangaisha na inshu ya Lissu kupigwa risasi, ndo maana chadema ilipoomba wachunguzi kutoka nje ya nchi waje wafanye uchunguzi serikali ilikataa kbs, ilikataa kwa sababu ilihusika kwa 100% ... Order ilitoka kwa raia namba moja,ikatekelezwa na mwanaye mpendwa lkn mwenyezi mungu akasema hafi mtu hapa .. kwahiyo hata hao pimbi wanaomtaka dreva wa Lissu aje kutoa maelezo ni makanjanja tu, walitaka dreva wa Lissu aje ili wamhonge aseme ni chadema ndo walihusika na lile tukio...uzuri kila kilichokuwa kinapangwa na yule raia namba moja wa kipindi kile kulikuwa kinavuja moja kwa moja... hvyo ni tukio la hovyo kuwahi kutokea ambalo kila mwenye akili timamu anajua kbs serikali ilihusika na lile jaribio

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
Lissu angekufa kwenye lile shambulio moja kwa moja kesi angepachikwa Mbowe, sasa ilikuja kuwawia vigumu kufanya hivyo kwa kuwa Lissu yuko hai na ujinga huo angeupigia kelele sana hasa kwenye vyombo vya habari vya kimataifa.
 
Nini dereva kwa nini yeye asihojiwe? Ushahidi wa dereva na ushahidi wa CCTV cameras footages upi ni wa uhakika zaidi? Polisi waliopaswa kuwa zamu na mabosi wao wanaopanga zamu za lindo kwa nini hawakuhojiwa? Kwa nini hata Jiwe mpenda sifa hakuwahi hata 'kuwapiga' chini mabosi wa polisi Dodoma au hata IGP manake alikuwa maridadi kwa misifa.
Vipi wazo la Mbowe la kushirikisha FBI au MI6 ya Scotland Yard mbona polisi walilikataa wakidai kila kitu kipo ndani ya uwezo wao, kumbe ilikuwa ni danganya toto hawakuwa wakitaka upelelezi ufanyike.
Mambo ya ajabu baada ya shambulio:
-Kuzuia watu wasimuombee Lissu.
-Kuzuia T-shirts zenye maandishi ya 'Get well soon Lissu'
-Kufura kwa subwoofer Ndugai kwamba imekuwa Lissu kapelekwa kutiwa Nairobi(obviously angebaki wangemmalizia hospitali) na wakadai ni mtoro asilipwe chochote wala asigharamiwe matibabu.

La muhimu kuliko yote - Footages za CCTV cameras ziibuliwe kokote zilikofichwa tujionee shambulio lilivyofanyika na si kupewa story za watu za kuungaunga au kuwatia watu kwenye pressure(brutal interrogations) mpaka wakiri hata mambo ya uongo, a picture speaks thousand words.
Achana nae huyu ni mmoja wa wahusika!!
 
Yule Muhutu mwenzako Jiwe ndiye alikuwa muhusika namba moja(hii ni kwa mujibu wa Lissu mwenyewe na ameongea live kwenye vyombo vya habari) na mpaka leo si polisi wala uongozi wa serikali waliokanusha, wanatamani lile tukio lisahaulike lakini halitosahaulika na litakuwa likiibuliwa mara kwa mara mpaka majibu yapatikane.
Wewe utakuwa unakipele kinakuwasha huko matakoni,unawezaje kunishadadia hivyo kama nilishakununua wala sikukulipa?,husiniharibie mfungo plz.
 
Back
Top Bottom