Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda atambulishwa rasmi CCM, atinga kwa bodaboda

Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda atambulishwa rasmi CCM, atinga kwa bodaboda

Katika mapokezi ya Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi, Ndugu Makonda amesema;

"Tangu niteuliwe nimepata nafasi ya kupita katika mitandao kusoma maoni ya baadhi ya watu, wengi wanahamaki na wengi wanabashasha, na katika wengi wanaohamaki wanawaza Makonda ataenda kulipa kisasi.

"Wanawaza makonda ataenda kufanya nini, nimeona na wengina wengine wanaanza kuwataja watu wengine kwamba utaona sasa usiyemtaka kaja, wengine wanasema tumejifunza nini katika jambo lamakonda.... Naomba niseme mbele ya hadhara hii, mgeni rasmi na mbele ya watanzania wapenzi wa chama cha mapinduzi na wakareketwa na mbele za Mungu, mimi sina kisasi na mtoto yoyote.

"Na asiwepo mtu akafirikiri lengo langu ni kumkandamiza, asiwepo mtu yoyote akafikiri wakati nitajitutumua kuonesha mabavu dhidi ya wale waliofikri wamenitenda mabaya, la hasha... naamini Mungu aliwatumia akiniandaa kufanya kazi kubwa zaidi..."
Useme tu ukweli kwamba Ile nguvu aliyokuwa anakupa mwendazake ufanye ulichokuwa unafanya kwa sasa haipo na uwezi kuipata Tena, umeteuliwa kafanye kazi inayokuhusu izo habari za kulipa kisasi ata Kama unataka kulipa itakuwa ngumu kwako kwakuwa huu ni utawala tofauti na ule uliokufanya uwe na kiburi Cha Kila aina, na nafikiri Kama utakuwa na akili sawasawa utakuwa umejifunza jambo wakati wote ambao ulikuwa benchi, sidhani Kama unaweza kurudia ujinga ule na waliokuteua nafikiri watakuwa wamekupa semina elekezi na maonyo ya nini unatakiwa ufanye na miiko ya uongozi wa cheo ulichopewa!
Tunajua lazima Kuna nguvu kubwa imetumika kukupigia debe kurudishwa chamani Sasa kafanye majukumu yako usitoke njia kuu ukawa Kama rafiki yako sabaya!
 
Naona umeanza vibaya kwa kujichetua akili.

Umesahau kwa mkataba mbovu mnauza bandari kwa Mwarabu.

Umesahau Kamanda mwenzangu Lissu alipozunguka nchi nzima kueleza ubovu wa mikataba mibovu ya kifisadi kama huu wa kuuza bandari mlianza kulia na kukumbuka maridhiano?

Lissu akifoka mnalialia kama watoto.

Alafu leo unasema eti sio mpinzani ni mtoa taarifa
Acha uongo wa kitoto.
 
Kijana taratibu..jifunze na urejee kwenye historia yako nyuma.busara inakuhitaji sana la sivyo..

Uongozi bila kutoa lugha za ovyo inawezekana!
 
Makonda ni boya Kama maboya mengine tu Hana jipya. Amewekwa hapo ili kuvutia Sukuma Gang. Lakini bado wataanguka tu.
 
Katika mapokezi ya Katibu Mwenezi, Makonda amesema Tanzania haina chama cha upinzani bali ina watoa taarifa waliojikusanya katika jina la vyama.

Akisema ukimwomna Lissu anaongea si chama kinaongea ni mtu tu anatoa taarifa na wakati mwingine inawezekana taarifa anayoitoa inaweza kuwa imetoka kwenye chanzo ambacho si cha kweli au cha uhakika, lakini kwakuwa ni mtoa taarifa kazi ya chama cha mapinduzi ni kusikiliza taarifa zao, badala ya kushughulika na mtoa taarifa tunashughulika na aliyesababisha hizo taarifa kutoka.

Mfano akisimama kiongozi yoyote wa chama cha kutoa taarifa akatoa taarifa ya kwamba umeme umekatika, jukumu letu kama chama ni kushughulika na anayekata umeme kwa wananchi.
Hotuba ya alie komaa kabisa kisiasa!!
 
Ni usemi ule ule wa kilatini, "La cuta causa Finita" -The decision of the president is Final, don't challenge president decisions

Makonda usiyempenda ndio huyo kaja tena CCM kama Kiongozi wa Itikadi na Uenezi. Maneno mengi yamesemwa juu yake lakini hakuna uthibitisho wa Mahakama juu ya tuhuma.

Maeneo ya Kariakoo hasa makutano ya Mtaa wa Livingstone na Kariakoo mambo ni moto. Ni umati wa madereva bodaboda wakiwa kwenye mapokezi ya Paul Makonda.

Mtaa wa Kariakoo upande wa Lumumba umezibwa kuruhusu umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kumpokea Paul Makonda.

Paul Makonda ni muumini wa siasa za kibabe na nguvu ambazo ndio hitaji kwa sasa kwenye siasa za Tanzania kujibu hoja za upinzani.

Tumeshuhudia operation za CHADEMA wakijitamba na kujisifia lakini majibu ya CCM ni Paul Makonda.

Paul Makonda ni mtu wa propaganda.
Jambazi sugu lililokuwa limejificha kwa aibu ya matendo yake limeibuka tena.
Kama uliwahi kuitizama picha ya Jesus of Nazareti, huyu makonda ni kama Baraba.
Screenshot_20231022-153235~2.jpg
 
Team!
Hii iko very serious na to be frank ni kwamba ili twende vizuri kisiasa lzm tuwe kundi la watu wanaojiheshimu na kuheshimu wengine.

Nasema hivi kwa kuwa wafuasi kibao wa CDM, CUF, NCCR, NLD, Umoja, ACT nk wana kautamaduni walikojenga vichwani ka kutukana, kumkashifu na kudhihaki viongozi wa CCM. Siku zote hudhani kwamba bila kutukana basi chakula hakitapita kooni.

SASA:
Atakayemtukana CDE Paul Makonda kwa namna yoyote ile atakuwa ameitukana CCM na kwa hali hiyo tutamuwajibisha nje na ndani. CDE Paul Makonda sawa na wewe anastahili kushika nafasi yoyote na sifa anazo za kutosha. CCM tumefurahi kwa kuwa ujio wake utainyima CDM usingizi.

Tusilaumiane kwa atayeshupaza shingo.

Ngaika Ndenda
Kakonko.
Kuna wanaume wengine huwa mnatutia aibu
 
Katika mapokezi ya Katibu Mwenezi, Makonda amesema Tanzania haina chama cha upinzani bali ina watoa taarifa waliojikusanya katika jina la vyama.

Akisema ukimwomna Lissu anaongea si chama kinaongea ni mtu tu anatoa taarifa na wakati mwingine inawezekana taarifa anayoitoa inaweza kuwa imetoka kwenye chanzo ambacho si cha kweli au cha uhakika, lakini kwakuwa ni mtoa taarifa kazi ya chama cha mapinduzi ni kusikiliza taarifa zao, badala ya kushughulika na mtoa taarifa tunashughulika na aliyesababisha hizo taarifa kutoka.

Mfano akisimama kiongozi yoyote wa chama cha kutoa taarifa akatoa taarifa ya kwamba umeme umekatika, jukumu letu kama chama ni kushughulika na anayekata umeme kwa wananchi.
Maneno mazito sana hayo.

Mimi miaka mingi sana humu JF nawaita chadomo, Makonda kawaheshimu sana kuwaita watowa taarifa.
 
Back
Top Bottom