Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda atambulishwa rasmi CCM, atinga kwa bodaboda

Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda atambulishwa rasmi CCM, atinga kwa bodaboda

Sasa unakuta m Swahili, kipato chair, hakifiki hata 2000 kwa siku, na yeye anaandsmana kumshangilia bashite!
Unaruhusu utumiwe na majizi, Yao yananeemeka, wewe unakufa njaa!
 
Sasa unakuta m Swahili, kipato chair, hakifiki hata 2000 kwa siku, na yeye anaandsmana kumshangilia bashite!
Unaruhusu utumiwe na majizi, Yao yananeemeka, wewe unakufa njaa!
Vipi na wake wanaotumika na vyama vya upinzani kuandamana kuna faida yoyote wanapata
 
Kuanzia Saa Tatu (3) Kamili pale Ofisi Ndogo Lumumba Mwamba na Kiboko ya Wapinzani wote Tanzania hasa CHADEMA na ACT Wazalendo Ndugu Paul Makonda (Katibu Mwenezi na Itikadi CCM Taifa) atakuwa anatambulishwa kuanza Kazi ya Kuwanyoosha na Kuwaadabisha Wapinzani wote nchini Tanzania.

Hakika mtamkoma....!!

====

Makonda atinga na bodaboda, umati wampokea Dar​

View attachment 2793632
Na Tuzo Mapunda

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda amewasili Ofisi ndogo ya makao makuu ya chama hicho yaliyopo Lumumba akiwa kwenye Msafara wa bodaboda na kupokewa na umati wa wafuasi na viongozi wa chama na Serikali.

Makonda amewasili akiwa amepakizwa kwenye bodaboda kwa kile kilichodaiwa kuwa alishindwa kuja na gari yake kutokana na msongamano wa magari na umati wa watu uliojitokeza kwenye eneo la ofisi hiyo.

Makonda amewasili kwenye ofisi hizo nsaa 4:30 asubuhi na kuingia moja kwa moja kwenye ofisi za chama hicho kwenda kuwasalimia viongozi mbalimbali waliojitokeza kumlaki akiwemo Sophia Mjema aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miezi tisa.

Makonda aliyeteuliwa kwenye nafasi hiyo Oktoba 22 mwaka huu, baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa dakika 10 alitoka na kwenda kwenye ukumbi wa kukabidhiwa ofisi na mtangulizi wake kabla ya kuongea na vyombo vya habari.

Baada ya kuingia kwenye ukumbi huo, mkuu wa utawala wa chama hicho, Marko Mhanga alikuwa wa kwanza kuongea kwa kuwakaribisha viongozi na wanachama waliojitokeza kisha kutambulisha viongozi wa vitengo mbalimbali ndani ya chama hicho.

Baada ya kumaliza utambulisho huo, Marko alimkaribisha Sophia Mjema kuendelea na shughuli ya kumkabidhi ofisi Makonda aliyefanya kazi serikali kwa awamu ya tano kwa kushika nafasi tofauti na mara ya mwisho akihudumu kwenye nafasi ya ukuu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Katika tukio hilo, Sophia amesema kitengo hicho ni moyo unaotegemewa na chama hicho kuhakikisha katika chaguzi zinazokuja kinapata ushindi wa kishindo.

"Nimehudumu kwenye nafasi hii kwa kipindi cha miezi tisa nilikabidhiwa kijiti na Shaka Hamdu Shaka na juzi Oktoba 22 Chama kilifanya uteuzi na leo nakukabidhi wewe, tunaimani kubwa utatimiza azma ya chama chetu," amesema.

Amesema anafahamu kwa kuwa wote kwa muda mrefu walikuwa huko serikalini lakini amekuja kukitumikia chama ambacho shabaha yake ni kuendelea kushika dola.

"Una timu kubwa ya kushirikiana nayo, nawaomba watumishi ninaowaacha mpeni ushirikiano dhabiti katika muendelezo wa kukijenga chama chetu," amesema.

Makonda baada ya kukabidhiwa vitendea kazi alitumia dakika nne kuzungumza akianza kwa kumshukuru mtangulizi wake Sophia huku akieleza ni miongoni mwa viongozi waliomfundisha kazi akiwa mtumishi serikali.

"Kwa bahati nzuri nimekuja kukitumikia chama na wewe unanikabidhi tena kijiti kijiti hiki asante sana, kikubwa nashukuru bado naendelea kwenye ulingo wa siasa kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan kwenye nafasi nyingine," amesema.

"Sina maneno mengi nasema asante sana kwa kuwa mtumishi wa wengi, ni matumaini yangu mlango ambao Mungu ameufungua atanipa hekima, busara na uvumilivu na kukitumikia chama kwa uadilifu, uaminifu na mafanikio makubwa, ili nisimuabishe Mungu wala Rais aliyeniamini na kuniteua katika nafasi hii," amesema.

Ametumia fursa hiyo kuwaomba watumishi wenzake wa chama hicho kumpatia ushirikiano kumuelekeza na kumshauri.

"Duniani kote watu wanaishi kwa taarifa na taarifa zinafanya maamuzi ukiwa na chanzo kibovu utafanya maamuzi mabovu, lakini ukiwa na chanzo kizuri utafanya maamuzi sahihi wakati wote," amesema.

Amesema ni matumaini yake atapatiwa ushauri mzuri utakaosaidia ujenzi wa chama hicho ili kiendelee kupata mashiko kwa wananchi.

Makonda amkumbusha Sophia kutowasahau wajane

Amemtakia Sophia kila la kheri kwenye majukumu yake mapya, huku akimweleza kutokuwasahau wajane maana nao ni miongoni mwa kundi maalumu.

"Wewe mwenyewe umekuwa shahidi tumewapigania nilipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na sasa wewe umepata nafasi hiyo utakuwa kiungo muhimu na mimi nitakuwa na kukumbusha ujane kama sehemu ya kundi maalumu," amesema.

Baada ya mazungumzo hayo viongozi hao waliondoka kwenye ukumbi huo kuelekea kwenye ofisi za CCM, mkoa ambako sherehe za kumkaribisha kiongozi huyo zilikuwa zimeandaliwa.
View attachment 2793619
ELIMU ni nyenzo muhimu sanaa Tanzania tumebarikiwa rasilimali watu ma million Kwa mamilion kulikua Kuna haja Gani ya kumrudisha Paul makonda (Daud Bashite) kwenye chama kama spoke man wa chama Cha mapinduzi....

Wapo wanao sema kua Paul makonda ni mshirikina wa kiwango Cha juu sanaa kiasi kwamba Huwa anatumiwa na viongozi wake kuwasaidia mambo mengi yaende inavyo takikana Mimi nilisikia yakisemwa ivyo......

Ni lini kama taifa tutaacha siasa za kujimwambafy na kujipa mabavu nimemsikia Paul akijigamba kua Tanzania hakuna vyama vya upinzani bali ni vikundi vya watu wenye maslah binafsi.....

Kama taifa tunaenda mbele au tunarudi nyuma 🤨🤨🤨🤨
 
Mh. Makonda Katibu wa Uenezi na Itikadi wa Chama cha Mapinduzi, kiongozi mwenye nyota ya pekee inayong'ara nchini anatarajiwa kupokelewa Leo kwenye ofisi ya CCM, Lumumba, Dar Es Salaam.

Siku ya Leo tarehe 26 Oktoba 2023

Kila la kheri Mheshimiwa, kutoka kwa mwana JF Mimi. Natumaini siku moja nitakutana nawe uso kwa uso kwa mara ya kwanza.

Makonda Oyeeee

Kazi iendelee...
Umesahau kuweka namba ya simu ili muonane uso kwa uso.
 
Wanalialia tu
Watanzania wengi tuna changamoto kubwa ya kufikiri sana.
Makonda hana tofauti na Musiba au Sabaya. Nguvu ulizoziona kwao nyakati zile Hazina tofauti na kifaa cha umeme kinachoitwa MOTA, hata iwe kubwa kiasi gani utendaji wake unategemea na umeme kutoka kwenye chanzo/ transformer. Ambayo nayo hupokea nguvu kutoka chanzo kingine I.e.generator. Makonda alipata umaarufu tena wa aibu siku alipomshambulia Mzee Warioba kwenye kongamano la katiba Ubungo, na viongozi wasio na haya walikiona kitendo hicho ni cha kishujaa wakamzawadia ukuu wa Wilaya.
Huko kwenye ukuu wa Wilaya hakuwa na jipya zaidi ya kelele za hovyo hovyo tu, kwa sababu anajua kucheza na akili za viongozi wasiojiamini akalamba ukuu wa mkoa awamu ya Tano.
Ni mkuu wa mkoa pekee aliyepewa ulinzi kuliko wote, na huyo huyo aliyempa ulinzi, baadaye akamuacha kwenye mataa alipojitosa kwenye uchaguzi wa ubunge akiamini yeye ni maarufu sana. Wakristo wanaosoma biblia,Iko hadithi ya punda aliyembeba Yesu.Yerusalemu kuelekea hekaluni, na Yesu alishangiliwa sana na bahati mbaya inawezekana punda alidhani anashangiliwa yeye na bahati mbaya wako watanzania akili zao ni kama za huyo punda, kwamba Makonda alifokea marpc.. kwenye mikutano walifikiri ana nguvu hizo, anasema siye wabara tusije Dar bila kuoga wanajua mwamba amesema, ukweli mchungu sana ni huzuni sana kuamini hao watu wapo mpaka awamu hii na wengine wamo humu. Kweli ndio maana ni afadhali ya mjinga akielimika hataitwa mjinga tena,lakini tunao wapumbavu ambao hata ufanye nini hawatabadilika labda aliyewaketa duniani aingilie kati.
Kwamba tunasahau huyo huyo aliyempandisha mabega ndiye aliyemshusha mpaka anaondoka duniani, Makonda alikuwa mtaani.
Awamu ya tano wengi walikuwa kama MOTA kubwa, Ally Hapi, huyu Rc wa dar, hata yule mbunge wa Arusha sasa hivi. Nguvu yao ilitokea ikulu na ndio sababu Chalamila wa Mbeya siyo Chalamila wa Mwanza au Kagera. Ni Makonda huyu huyu aliyesavabisha Nape apoteze uwaziri, ni Makonda huyu huyu aliyemwita Ridhiwani Kikwete ajieleze kuhusu biashara ya dawa za kulevya.
Sasa mnaosema huyu ni kiboko cha Chadema, hampaswi kulaumiwa, maana unafiki ni moja ya sifa kubwa ya ccm.
Hivi huyu ataondoa shida ya umeme! Ajira!kuungua kwa masoko!! Haswa Kariakoo!!
Makonda wa sasa hana tofauti na MOTA ya 1.5Kw. labda mama huyu amrudishie like genge lake la gizani.
 
Makonda Mungu akupe hekima usijaribu kulipa kisasi!! Mazingira ya kazi yako yatakuwa magumu sana!! Huku Gwajima, huku Nape, huku Kinana!! Umewekwa hapo kuimarisha timu mama kuelekea 2025!! Hilo usilisahau!! Vinginevyo mtumbuo utakuhusu!!
 
"Niseme tu kuanzia leo Oktoba 26, 2023, Taifa hili halina chama cha upinzani bali lina vyama vya watoa taarifa, na sisi kama chama tawala tutafanyia kazi taarifa zao kwa sababu ni chachu ya ujenzi si tu wa demokrasia bali wa maendeleo katika Taifa letu."

1698321618962.jpg
 
🔴#Live: MAPOKEZI-MAKONDA AANDIKA HISTORIA DAR ATUPA KOMBORA ZITO KWA FREEMAN MBOWE

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Paul Makonda a.k. a “BABA KEAGAN” amesema tangu ateuliwe kuna Watu wamehamaki wengi wao wakiwaza kuwa Makonda ataenda kulipa kisasi huku wengine wakiwataja baadhi ya Watu na kuwaambia ‘Utaona sasa usiyemtaka kaja’, ambapo Makonda amesema hajaja kulipa kisasi kwa yeyote.

Akiongea leo Jijini Dar es salaam baada ya kupokelewa na Viongozi na Wanachama wa CCM, Makonda amesema “Tangu niteuliwe nimepata nafasi ya kupitapita kwenye mitandao, nimesoma maoni ya baadhi ya Watu, wengi wanahamaki na wengi wana bashasha lakini wanaohamaki wengi wao wanawaza Makonda ataenda kulipa kisasi, nimeona na wengine wanaanza kuwataja Watu wengine kwamba ‘Utaona sasa usiyemtaka kaja’, naomba niseme Mimi sina kisasi kwa Mtu yoyote, na asiwepo Mtu yoyote yule akafikiri lengo langu ni kumkandamiza, au nitajitutumua kuonesha mabavu dhidi ya wale waliofikiri wamenitenda mabaya”

“Mnaohisi kuna jambo halikuwa sawa Mimi naelewa Mungu aliwatumia kunisaidia kumjua Mungu zaidi, naamini Mungu aliwatumia ili kuniandaa kwa kazi kubwa zaidi msiwe na hofu, naomba ushirikiano na umoja wenu na wala Dkt. Samia hajaniteua kuja kuhangaika na mambo ya Makonda bali uenezi wa CCM na wala Dkt. Samia na Kamati Kuu haikukaa kwenye kikao kumtafuta Mtu wa kwenda kulipa kisasi, walimtafuta Mtu atakayeongeza nguvu katika kujenga imani ya Watanzania kwenye CCM”

Katika moja kati ya mazungumzo yake Bwana Makonda amesema ameongea na Rais wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA apewe kibali cha kuruka angani na Helkopter kuendelea na mikutano ya hadhara na kama ameishiwa mafuta amepewa kibali rasmi cha kujaza mafuta kwa ajili ya helkopter anayotumia.

“Naomba kuchukua nafasi hii kuiagiza Serikali inayohusikamna Mamlaka ya Vibali, kama ni watu wa Anga nawaelekeza mpeni Mbowe kibali aruke na Helkopter na kama hana mafuta nimeongea na Dkt.Samia, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi amesema atamchangia, Akiruka angani tutamfata, akienda nchi kavu tutamfata, akiingia kwenye boat tutamfata atapigwa kila kona”

Mbali na hayo Mnec huyo ameingia katika ofisi ndogo za Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam (Lumumba)na Pikipiki za kubeba abiria maarufu kama “Bodaboda”.

Mamia ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi wamejitokeza kwa wingikumlaki Makonda licha ya eneo la Ofisi za Ccm kuwa dogo kutokana na watu kufurika.

Mwisho Paul Makonda amesema ameongea na Rais Samia kumtembelea Rais wa Zanzibar Dkt.Hissein Ali Mwinyi pamoja na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili wakamwambie wanahitaji Mwenezi wa aina gani kwa sababu hajawahi kuwa Mwenezi mahali popote.
Credit by Mimi Mwenyewe.
 
Kuanzia Saa Tatu (3) Kamili pale Ofisi Ndogo Lumumba Mwamba na Kiboko ya Wapinzani wote Tanzania hasa CHADEMA na ACT Wazalendo Ndugu Paul Makonda (Katibu Mwenezi na Itikadi CCM Taifa) atakuwa anatambulishwa kuanza Kazi ya Kuwanyoosha na Kuwaadabisha Wapinzani wote nchini Tanzania.

Hakika mtamkoma....!!

====

Makonda atinga na bodaboda, umati wampokea Dar​

View attachment 2793632
Na Tuzo Mapunda

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Itikadi na Uenezi CCM, Paul Makonda amewasili Ofisi ndogo ya makao makuu ya chama hicho yaliyopo Lumumba akiwa kwenye Msafara wa bodaboda na kupokewa na umati wa wafuasi na viongozi wa chama na Serikali.

Makonda amewasili akiwa amepakizwa kwenye bodaboda kwa kile kilichodaiwa kuwa alishindwa kuja na gari yake kutokana na msongamano wa magari na umati wa watu uliojitokeza kwenye eneo la ofisi hiyo.

Makonda amewasili kwenye ofisi hizo nsaa 4:30 asubuhi na kuingia moja kwa moja kwenye ofisi za chama hicho kwenda kuwasalimia viongozi mbalimbali waliojitokeza kumlaki akiwemo Sophia Mjema aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miezi tisa.

Makonda aliyeteuliwa kwenye nafasi hiyo Oktoba 22 mwaka huu, baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa dakika 10 alitoka na kwenda kwenye ukumbi wa kukabidhiwa ofisi na mtangulizi wake kabla ya kuongea na vyombo vya habari.

Baada ya kuingia kwenye ukumbi huo, mkuu wa utawala wa chama hicho, Marko Mhanga alikuwa wa kwanza kuongea kwa kuwakaribisha viongozi na wanachama waliojitokeza kisha kutambulisha viongozi wa vitengo mbalimbali ndani ya chama hicho.

Baada ya kumaliza utambulisho huo, Marko alimkaribisha Sophia Mjema kuendelea na shughuli ya kumkabidhi ofisi Makonda aliyefanya kazi serikali kwa awamu ya tano kwa kushika nafasi tofauti na mara ya mwisho akihudumu kwenye nafasi ya ukuu wa mkoa wa Dar es Salaam.

Katika tukio hilo, Sophia amesema kitengo hicho ni moyo unaotegemewa na chama hicho kuhakikisha katika chaguzi zinazokuja kinapata ushindi wa kishindo.

"Nimehudumu kwenye nafasi hii kwa kipindi cha miezi tisa nilikabidhiwa kijiti na Shaka Hamdu Shaka na juzi Oktoba 22 Chama kilifanya uteuzi na leo nakukabidhi wewe, tunaimani kubwa utatimiza azma ya chama chetu," amesema.

Amesema anafahamu kwa kuwa wote kwa muda mrefu walikuwa huko serikalini lakini amekuja kukitumikia chama ambacho shabaha yake ni kuendelea kushika dola.

"Una timu kubwa ya kushirikiana nayo, nawaomba watumishi ninaowaacha mpeni ushirikiano dhabiti katika muendelezo wa kukijenga chama chetu," amesema.

Makonda baada ya kukabidhiwa vitendea kazi alitumia dakika nne kuzungumza akianza kwa kumshukuru mtangulizi wake Sophia huku akieleza ni miongoni mwa viongozi waliomfundisha kazi akiwa mtumishi serikali.

"Kwa bahati nzuri nimekuja kukitumikia chama na wewe unanikabidhi tena kijiti kijiti hiki asante sana, kikubwa nashukuru bado naendelea kwenye ulingo wa siasa kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan kwenye nafasi nyingine," amesema.

"Sina maneno mengi nasema asante sana kwa kuwa mtumishi wa wengi, ni matumaini yangu mlango ambao Mungu ameufungua atanipa hekima, busara na uvumilivu na kukitumikia chama kwa uadilifu, uaminifu na mafanikio makubwa, ili nisimuabishe Mungu wala Rais aliyeniamini na kuniteua katika nafasi hii," amesema.

Ametumia fursa hiyo kuwaomba watumishi wenzake wa chama hicho kumpatia ushirikiano kumuelekeza na kumshauri.

"Duniani kote watu wanaishi kwa taarifa na taarifa zinafanya maamuzi ukiwa na chanzo kibovu utafanya maamuzi mabovu, lakini ukiwa na chanzo kizuri utafanya maamuzi sahihi wakati wote," amesema.

Amesema ni matumaini yake atapatiwa ushauri mzuri utakaosaidia ujenzi wa chama hicho ili kiendelee kupata mashiko kwa wananchi.

Makonda amkumbusha Sophia kutowasahau wajane

Amemtakia Sophia kila la kheri kwenye majukumu yake mapya, huku akimweleza kutokuwasahau wajane maana nao ni miongoni mwa kundi maalumu.

"Wewe mwenyewe umekuwa shahidi tumewapigania nilipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na sasa wewe umepata nafasi hiyo utakuwa kiungo muhimu na mimi nitakuwa na kukumbusha ujane kama sehemu ya kundi maalumu," amesema.

Baada ya mazungumzo hayo viongozi hao waliondoka kwenye ukumbi huo kuelekea kwenye ofisi za CCM, mkoa ambako sherehe za kumkaribisha kiongozi huyo zilikuwa zimeandaliwa.
View attachment 2793619
Failing State! Badala ya kupambana na Ripoti ya CAG na mchwa walioiba trilions mnapambana na Mbowe aliyekulia ushuani wakai mimi na wewe tukiwa tunalala nyumba moja na mifugo huko kolomije?
 
Umesahau kuweka namba ya simu ili muonane uso kwa uso.

Eeeeh
Siku moja yaja.. kuna siku nilikuwa nimekuja Dar kutoka huku mkoani.. nikaenda kukutana na friends restaurant moja Oysterbay.. nafika tu wananiambia nimepishana nae.. wakanionyesha alipokuwa amekaa anaongea na watu fulani nao walikuwa wanaondoka.

Ningemfata kwa kweli.. kumsalimia..

Labda atanitumia inbox humu niende ofisini kumsalimia 😅😅😅
 
Back
Top Bottom