Katibu wa TEC: Maaskofu wanahitaji kuisoma mikataba iliyosainiwa, walipoitwa hawakuambiwa kulikuwa na nini

Katibu wa TEC: Maaskofu wanahitaji kuisoma mikataba iliyosainiwa, walipoitwa hawakuambiwa kulikuwa na nini

Sio kila kinchofanywa serikalini mimi na wewe tukijue, kumbuka kuwa hata hili suala la IGA lilivuja kwa bahati mbaya tu,

Kwako wewe usiyefanya biashara yoyote yenye kutumia bandari ni takataka kwa wenye kutumia bandari hili ni ssuala walilokuwa wakilihitaji kwa miaka mingi.
Unajuaje kwamba sifanyi chochote kinachohusiana na bandari?
Hata kama ingekuwa hivyo, bado ningepinga hujuma kwa nchi ninapoiona mahali popote, siyo lazima inihusu moja kwa moja.
Kinachofanywa na serikali kma ni hujuma kwa nchi, ni lazima tukikatae hata kama kilifanywa gizani kama unavyohimiza wewe.
Wewe ni fisadi mkubwa sana, ndiyo maana unataka mambo ya giza sana.
 
Neno ufisadi ni pana sana na linatumika kwa malengo maalum ya kisiasa. DP World muda wowote anaanza kazi hapo bandarini, kama unaumia sana basi pokea pole maalum.
Nimekueleza mara kadhaa sasa, huyo DP World kuanza kazi hapo bandarini siyo hoja tena, maadam IGA yake ilikufa kibudu.
Mlikotaka kupitishia hujuma zenu kwa nchi hii kulistukiwa. Huyu DP World akija hapo bandarini, hana tofauti yoyote na TICTS aliyeondoka miezi michache iliyopita. Kwa hiyo si tishio tena kama yule wa IGA.
 
Kuwa na mapenzi na nchi kwa mujibu wa Kalamu ni kuwa vipi?. Unaweza kujidanganya kwamba wewe ni mzalendo na ukawa fisadi mwenye kuifilisi nchi kuliko wale mafisadi wenyewe.

Narudia tena kumpa tender DP World ni maamuzi ya CCM yenyewe kabla hata SSH hajateuliwa na Rais JPM awe makamu wake.

Pia ni matakwa ya ushindani wa shoroba [corridor] zilizopo. Tumepewa faida za kijiografia kulinganisha na mataifa mengi ya ukanda huu na tutakuwa wajinga tukikaa tu bila ya sisi kuitumia faida hiyo katika kukuza uchumi wetu.
Jambo ambalo lipo wazi kabisa kati yetu, wewe na mimi ni kwamba wewe maslahi yako yapo DP World, na wala siyo katika ufanisi wa bandari yetu; hili sasa lipo wazi kabisa.

Mimi, sitajali sana, nani anahudumu hapo kwenye bandari yetu na kuleta manufaa makubwa kwa nchi yetu; lakini ningetulia sana moyo wangu kama tungeweza kuwa na viongozi wa kuwasaidia waTanzania wenyewe kuifanikisha kazi hiyo.
Huyu DP World anayekumiliki wewe, alianza shughuli zake mwaka 1999, tu. Siyo muda mrefu sana. Sisi kama nchi, ni lazima nasi tuwe na lengo la kujijengea uwezo wa kufanya mambo ambayo yanaweza kuwa ndani ya uwezo wetu. Kuendesha bandari kwa ufanisi siyo jambo la ajabu sana, kwa nini tutishike kiasi unachofanya wewe tuonekane kutishika.
Na hili silisemei kwa maswala ya bandari peke yake. Tunatakiwa kuchukua hatua za kujijengea uwezo katika kila nyanja ya shughuli zinazofanyika hapa nchini.
Najaribu kunielewa, sihimizi serikali ndiyo ilazimike kuyafanya haya, lakini ni jukumu la serikali kusimamia na kuhimiza uwepo wa hali hii katika jamii yetu.
hatuwezi kuwa nchi ya kutegemea wengine toka nje waje kufanya hata yale tunayoweza kuyafanya sisi.

Uwepo wako hapa jukwaani, tokea mwanzo, ni kupigania DP World tu, na siyo jambo jingine lolote, na wala siyo kampuni nyingine yoyote inayoweza kufanya kazi hapo bandarini kwa ufanisi, hata zaidi ya huyo DP World.

Kwa hiyo nisome vizuri utambue tofauti kubwa sana zilizopo kati yangu na wewe. Kuendelea kwako kuipigania DP World hapa hakutabadili chochote katika utambuzi wangu kwako, kuwa wewe ni mali ya DP World, kwa maslahi unayoyajua mwenyewe.
Kama kweli wewe ni mTanzania, najua utanielewa tu, hata kama hutaweza kubadili msimamo wako.
 
Jambo ambalo lipo wazi kabisa kati yetu, wewe na mimi ni kwamba wewe maslahi yako yapo DP World, na wala siyo katika ufanisi wa bandari yetu; hili sasa lipo wazi kabisa.

Mimi, sitajali sana, nani anahudumu hapo kwenye bandari yetu na kuleta manufaa makubwa kwa nchi yetu; lakini ningetulia sana moyo wangu kama tungeweza kuwa na viongozi wa kuwasaidia waTanzania wenyewe kuifanikisha kazi hiyo.
Huyu DP World anayekumiliki wewe, alianza shughuli zake mwaka 1999, tu. Siyo muda mrefu sana. Sisi kama nchi, ni lazima nasi tuwe na lengo la kujijengea uwezo wa kufanya mambo ambayo yanaweza kuwa ndani ya uwezo wetu. Kuendesha bandari kwa ufanisi siyo jambo la ajabu sana, kwa nini tutishike kiasi unachofanya wewe tuonekane kutishika.
Na hili silisemei kwa maswala ya bandari peke yake. Tunatakiwa kuchukua hatua za kujijengea uwezo katika kila nyanja ya shughuli zinazofanyika hapa nchini.
Najaribu kunielewa, sihimizi serikali ndiyo ilazimike kuyafanya haya, lakini ni jukumu la serikali kusimamia na kuhimiza uwepo wa hali hii katika jamii yetu.
hatuwezi kuwa nchi ya kutegemea wengine toka nje waje kufanya hata yale tunayoweza kuyafanya sisi.

Uwepo wako hapa jukwaani, tokea mwanzo, ni kupigania DP World tu, na siyo jambo jingine lolote, na wala siyo kampuni nyingine yoyote inayoweza kufanya kazi hapo bandarini kwa ufanisi, hata zaidi ya huyo DP World.

Kwa hiyo nisome vizuri utambue tofauti kubwa sana zilizopo kati yangu na wewe. Kuendelea kwako kuipigania DP World hapa hakutabadili chochote katika utambuzi wangu kwako, kuwa wewe ni mali ya DP World, kwa maslahi unayoyajua mwenyewe.
Kama kweli wewe ni mTanzania, najua utanielewa tu, hata kama hutaweza kubadili msimamo wako.
Hapana, napigania maslahi ya Tanzania siku zote. Kumbuka kuwa pale bandarini TICTS wamekaa kwa miaka 22.

Miaka yote hiyo tulikuwa hatufahamu umuhimu wa wazalendo kumiliki mali zao wenyewe?. Hao wazalendo tunaowatetea ndio hawa ambao CAG kila anapotoa report za ukaguzi wanapata ile ambayo ni chafu!. Maana yake wizi na ukosefu wa uzalendo ni sifa yao kuu kuliko nyingine yoyote.

Hawa wazalendo wana uzoefu mbaya wa uendeshaji wa taasisi nyeti yenye hadhi ya TPA, ufisadi wao unakwamisha mipango ya nchi nzima.

Napigania maslahi ya nchi yangu lakini pia nataka kuona ufanisi ukiongezeka pale TPA, sipendi kuona wateja wakikimbia na wanapoondoka wanapeleka sifa mbaya kwa wateja wengine kwamba pale sio mahali pa kupitisha mizigo.

Usidhani wote wanaowapigania DP World wanayo maslahi yao binafsi, hapana, wengi wetu ni wazalendo lakini tunakerwa kuona bandari yetu ikikumbana kila siku na sifa mbaya tu.
 
Narudia tena kumpa tender DP World ni maamuzi ya CCM yenyewe kabla hata SSH hajateuliwa na Rais JPM awe makamu wake.
Unanishangaza kweli kudhani kwamba kuna mtu yeyote anayeweza kuamini kuwa kuna ukweli wowote katika maneno haya uliyoandika hapa. Kuna tatizo fulani katika mfumo wa fikra zako kama huoni disari katika maandishi haya.
Na hata ingekuwa ni kwa nia ya kudanganya, ni mjinga wa namna gani anayeweza kudanganyika na uongo ulio dhahiri kabisa kiasi hiki?
Pia ni matakwa ya ushindani wa shoroba [corridor] zilizopo. Tumepewa faida za kijiografia kulinganisha na mataifa mengi ya ukanda huu na tutakuwa wajinga tukikaa tu bila ya sisi kuitumia faida hiyo katika kukuza uchumi wetu.
Unapewa faida za kijiografia, kama unavyopewa faida za madini na raslimali nyingi nyingine, halafu unakuwa na viongozi wasiokuwa na maono yoyote juu ya raslimali hizo kuinufaisha nchi; badala yake wanagawa tu na kujinufaisha wenyewe, hapo bado unajigamba kuwa na "faida za kijiografia", unabaki tu unaimba maneno hayo hayo kama kasuku!
 
Hapana, napigania maslahi ya Tanzania siku zote. Kumbuka kuwa pale bandarini TICTS wamekaa kwa miaka 22.

Miaka yote hiyo tulikuwa hatufahamu umuhimu wa wazalendo kumiliki mali zao wenyewe?.
Sasa hapa unataka nisifu kitu gani? Kama TICTS kakaa hapo miaka zaidi ya 20 na hatukuweza kujifunza lolote, unadhani hiyo ni furaha kwangu ya kujivunia?
Tafuta maandiko yangu humu kuhusu huyo huyo TICTS utaona kwamba sina lolote la kujivunia juu yake, kama nisivyoona chochote cha kujivunia katika mikataba ya hovyo kabisa iliyohusiana na ujio wa huyu DP World.

Tena inaweza ikawa ni hasara zaidi ikiwa kama kuna lolote atakalofanya DP World kuhusiana na mikataba ile.
TICTS kama ilivyo DP World, wote wanaingia hapo bandarini kwa njama za kihujumu.
 
Miaka yote hiyo tulikuwa hatufahamu umuhimu wa wazalendo kumiliki mali zao wenyewe?. Hao wazalendo tunaowatetea ndio hawa ambao CAG kila anapotoa report za ukaguzi wanapata ile ambayo ni chafu!. Maana yake wizi na ukosefu wa uzalendo ni sifa yao kuu kuliko nyingine yoyote.

Hawa wazalendo wana uzoefu mbaya wa uendeshaji wa taasisi nyeti yenye hadhi ya TPA, ufisadi wao unakwamisha mipango ya nchi nzima.
Unayoyaeleza hapa, ingefaa ukamfikishia Samia, ndiye mwenye jukumu la kuhakikisha kwamba serikali yake na yeye mwenyewe ndio wahujumu wakubwa wa nchi hii.
Nakutuma kwa Samia, kwa sababu ndiye aliyepo sasa, na akishiriki kikamilifu kabisa pamoja na watu kama wewe, kulididimiza taifa hili.
 
Usidhani wote wanaowapigania DP World wanayo maslahi yao binafsi, hapana, wengi wetu ni wazalendo lakini tunakerwa kuona bandari yetu ikikumbana kila siku na sifa mbaya tu
Ninge amini hili, kama ungeona dosari angalau moja tu katika ile IGA. Kinyume chake wewe unaona katika uhai wako wote, hujawahi kuona mkataba mzuri zaidi ya ule.
Ninakudharau sana kwa hilo.
 
Unanishangaza kweli kudhani kwamba kuna mtu yeyote anayeweza kuamini kuwa kuna ukweli wowote katika maneno haya uliyoandika hapa. Kuna tatizo fulani katika mfumo wa fikra zako kama huoni disari katika maandishi haya.
Na hata ingekuwa ni kwa nia ya kudanganya, ni mjinga wa namna gani anayeweza kudanganyika na uongo ulio dhahiri kabisa kiasi hiki?
Unapewa faida za kijiografia, kama unavyopewa faida za madini na raslimali nyingi nyingine, halafu unakuwa na viongozi wasiokuwa na maono yoyote juu ya raslimali hizo kuinufaisha nchi; badala yake wanagawa tu na kujinufaisha wenyewe, hapo bado unajigamba kuwa na "faida za kijiografia", unabaki tu unaimba maneno hayo hayo kama kasuku!
Hakuna anayekulazimisha kuamini lakini ukweli ndio huo, bandari yetu ilihitaji mwekezaji mwenye uzoefu wa uendeshaji kimataifa ili iweze kupambana kiushindani.

Faida za kijiografia kwa maana ya kuhudumiwa nchi saba zinazotuzunguka, kuna suala la corridor za bahari kwa kiswahili zinaitwa shoroba, umepokamata biashara ya shoroba maana yake kiuchumi unakuwa kwenye advantage kulinganisha na mataifa mengine.

Haya masuala yanataka mtu ambaye anaitazama dunia kisasa, nyinyi mlionasa kwenye utandu wa fikra za kijamaa hakuna wa kuwabadilisha, dunia inapita inawaacha na mawazo yenu mgando.
 
Ninge amini hili, kama ungeona dosari angalau moja tu katika ile IGA. Kinyume chake wewe unaona katika uhai wako wote, hujawahi kuona mkataba mzuri zaidi ya ule.
Ninakudharau sana kwa hilo.
Kunidharau kwako hakuondoi ukweli kwamba IGA imeandikwa na mwanasheria mbobezi wa mikataba ya kimataifa, ambaye ameshaiandaa mikataba mingi kama ule na ipo kazini mpaka muda huu.
 
Unayoyaeleza hapa, ingefaa ukamfikishia Samia, ndiye mwenye jukumu la kuhakikisha kwamba serikali yake na yeye mwenyewe ndio wahujumu wakubwa wa nchi hii.
Nakutuma kwa Samia, kwa sababu ndiye aliyepo sasa, na akishiriki kikamilifu kabisa pamoja na watu kama wewe, kulididimiza taifa hili.
Uelewa wako mdogo ndio unakudanganya kwamba Samia alididimiza taifa hili. Alisema tangu anaanza urais kwamba anaifungua nchi, sasa gharama zake ndio hizi haswa kwa sisi wenye mawazo mgando.
 
Sasa hapa unataka nisifu kitu gani? Kama TICTS kakaa hapo miaka zaidi ya 20 na hatukuweza kujifunza lolote, unadhani hiyo ni furaha kwangu ya kujivunia?
Tafuta maandiko yangu humu kuhusu huyo huyo TICTS utaona kwamba sina lolote la kujivunia juu yake, kama nisivyoona chochote cha kujivunia katika mikataba ya hovyo kabisa iliyohusiana na ujio wa huyu DP World.

Tena inaweza ikawa ni hasara zaidi ikiwa kama kuna lolote atakalofanya DP World kuhusiana na mikataba ile.
TICTS kama ilivyo DP World, wote wanaingia hapo bandarini kwa njama za kihujumu.
Kama huna biashara yoyote ya import, export au transit ni lazima usielewe kwa kina faida za ujio wa DP World.
 
Kama huna biashara yoyote ya import, export au transit ni lazima usielewe kwa kina faida za ujio wa DP World.
Sihitaji kuwa na biashara ya aina yoyote kujua mtu fisadi alivyo.
Kwa sasa sina shaka yoyote juu yako kwamba ni mmoja wa adui mkubwa wa nchi yetu kwa wakati huu.
Tutapambana tu na nyinyi.
 
Uelewa wako mdogo ndio unakudanganya kwamba Samia alididimiza taifa hili. Alisema tangu anaanza urais kwamba anaifungua nchi, sasa gharama zake ndio hizi haswa kwa sisi wenye mawazo mgando.
Anawafungulia mafisadi nchi, na tutapambana nao tu hakuna njia nyingineyo.
Haya ni mapambano ambayo hamuwezi kamwe kuyashinda.
 
Kunidharau kwako hakuondoi ukweli kwamba IGA imeandikwa na mwanasheria mbobezi wa mikataba ya kimataifa, ambaye ameshaiandaa mikataba mingi kama ule na ipo kazini mpaka muda huu.
Huyo mwanasheria wako umekwisha tueleza mengi kumhusu, na kumshuhudia kiasi cha utupu alio nao; na yeye tunamdharau kama tunavyokudharau wewe. Nyote msukumo wenu ni ufisadi tu basi..

Kwa mtu mwenye elimu ndogo ya kiwango chako, fisadi yeyote anaweza kukukoga moyo kama anatumia hiyo elimu kukidhi matakwa ya ufisadi.
 
Hakuna anayekulazimisha kuamini lakini ukweli ndio huo, bandari yetu ilihitaji mwekezaji mwenye uzoefu wa uendeshaji kimataifa ili iweze kupambana kiushindani.
Kwani TICTS aliyekaa pale miaka zaidi ya 20 hakuwa na uzoefu?
Wewe unajua DP World tu pekee, kwa sababu ndiye anayekufuga. Kaondoka TICTS aliyewafuga mafisadi, kaingia DP World na kundi lake la mafisadi vile vile.
Faida za kijiografia kwa maana ya kuhudumiwa nchi saba zinazotuzunguka, kuna suala la corridor za bahari kwa kiswahili zinaitwa shoroba, umepokamata biashara ya shoroba maana yake kiuchumi unakuwa kwenye advantage kulinganisha na mataifa mengine.

Haya masuala yanataka mtu ambaye anaitazama dunia kisasa, nyinyi mlionasa kwenye utandu wa fikra za kijamaa hakuna wa kuwabadilisha, dunia inapita inawaacha na mawazo yenu mgando.
Kuna lipi jipya hapa lisilofahamika kwa yeyote.
Unadhani unaweza kuhalalisha uhujumu mnaofanya nyinyi kwa taarifa kama hizi ambazo kila mtu anazifahamu?
 
Kwani TICTS aliyekaa pale miaka zaidi ya 20 hakuwa na uzoefu?
Wewe unajua DP World tu pekee, kwa sababu ndiye anayekufuga. Kaondoka TICTS aliyewafuga mafisadi, kaingia DP World na kundi lake la mafisadi vile vile.
Kuna lipi jipya hapa lisilofahamika kwa yeyote.
Unadhani unaweza kuhalalisha uhujumu mnaofanya nyinyi kwa taarifa kama hizi ambazo kila mtu anazifahamu?
DP World ana mifumo ya kisasa sana ya upakuaji na upakiaji wa makasha melini, hushangai namna alivyopigwa vita mpaka na maaskofu tunaowaheshimu?.

Jiandaeni kufanya biashara kubwa sio kuishi kwa kunyooshea vidole wanasiasa, ni watu wa kuja na kuondoka.
 
Huyo mwanasheria wako umekwisha tueleza mengi kumhusu, na kumshuhudia kiasi cha utupu alio nao; na yeye tunamdharau kama tunavyokudharau wewe. Nyote msukumo wenu ni ufisadi tu basi..

Kwa mtu mwenye elimu ndogo ya kiwango chako, fisadi yeyote anaweza kukukoga moyo kama anatumia hiyo elimu kukidhi matakwa ya ufisadi.
Utabakia na matusi yako meengi na kiburi cha kike, DP World wanaanza kazi hapo bandarini muda sio mrefu ujao.
 
Anawafungulia mafisadi nchi, na tutapambana nao tu hakuna njia nyingineyo.
Haya ni mapambano ambayo hamuwezi kamwe kuyashinda.
Walikuwepo kina Mtikila na wengine wengi tu wenye fikra kama za kwako leo hii wameshalala usingizi wa milele.

Ishi na fikra chanya hizi za kiuanaharakati hazikusaidii chochote.
 
Sihitaji kuwa na biashara ya aina yoyote kujua mtu fisadi alivyo.
Kwa sasa sina shaka yoyote juu yako kwamba ni mmoja wa adui mkubwa wa nchi yetu kwa wakati huu.
Tutapambana tu na nyinyi.
Ubora ule ule wa bandari za UK, India na Belgium ndio unakuja kuwepo katika bandari yetu, nyinyi endeleeni na hayo maneno mengi ya kwenye kanga. Unapoteza muda Kalamu.
 
Back
Top Bottom