Katibu Wizara ya Nishati Felchesmi Mramba: Umeme unaokuja kutoka Ethiopia utakuwa na hasara lakini hiyo hasara haituhusu

Katibu Wizara ya Nishati Felchesmi Mramba: Umeme unaokuja kutoka Ethiopia utakuwa na hasara lakini hiyo hasara haituhusu

Walau huyu Katibu Mkuu Mramba namwelewa.

Nilitaka kuanzisha mada nzito hasa kuwa Raisi awavurumishe wataalamu wa Tanesco waende Ethiopia wakajifunze kuwa wao kwa nini kilomita zote hizo toka Ethiopia umeme haupotei njiani na kuwapa loss ila wetu kilomita nyingi unapotea na kuipa Tanesco mabilioni ya hasara

Argument ya katibu mkuu ina make sense naikubali Ruksa kanunueni kwa muono wangu huo umeme wa Ethiopia

Katibu mkuu Mramba nimekuelewa
Sidhani kama umemuelewa.

Umeambiwa hasara ipo japo haituhusu sisi. Kwa maana hiyo suala la upotevu wa umeme njiani lipo hata kwa hao Ethiopia.

Sasa kama hasara ipo kwa Ethiopia basi hakuna faida ya wataalam wa Tanesco kwenda kujifunza huko Ethiopia kama ulivyopendekeza.
 
Wanatangaza wao, mjadala wanaanzisha wao wenyewe na kujijibu wenyewe tena.
Nchi ina vituko hii
 
Hio ni bei gani kwa Tshs ? 0.077 !!! Na kwanini tunazalisha kwa gharama zaidi wakati tuna vyanzo lukuki na Bwawa likiisha ni kwamba overheads zinapungua hivyo gharama ya uzalishaji kupungua ?

Kuliko kuendelea kununua nje hata zikipanda na kuwa dola 5 kwanini wasiwaze long term kuhakikisha umeme unafika kila kona ya Tanzania kwa gharama nafuu ?

Shida tunawaza leo na sio kesho waliotangulia kila mtu angewaza leo yake sisi tungekuta hio miundombinu ? Hio 0.077 badi ni gharama kubwa na inatoka kwenye Kodi zetu inabidi tuwaze sisi ndio tuanze kupeleka excess huko na kupata hizo 0.077 after all tuna vyanzo vingi kuliko wao...; Leo hii tunanunua LPG ili tupikie kwanini tusitumie huo umeme kwa kupikia kwa walio karibu na grid ili hio excess ya kununua LPG ndio tukanunue huo umeme wa so called bei rahisi ?

Na hii excess ya kwetu tunaiuza kwa kiasi gani ? Hiki Chama kishakuwa Chama cha Madalali
 
Sidhani kama umemuelewa.

Umeambiwa hasara ipo japo haituhusu sisi. Kwa maana hiyo suala la upotevu wa umeme njiani lipo hata kwa hao Ethiopia.
Rudia kusoma nilichoandika

Mtu kuuza kwa loss bidhaa zake kitu cha kawaida ili mtu aambulie chochote

Ethiopia kusafirisha umeme kilomita zote hizo wanapata loss kubwa lakini wako tayari kutuuzia kwa bei nafuu na hiyo loss yao walau wapunguze loss

Ndio maana ufafanuzi wa katibu mkuu Mramba kasema hiyo loss yao haituhusu sisi tunaangalia bei nafuu wanatuuzia

Wewe ndio una kichwa kigumu kuelewa nilichoandika

Rudia kusoma nilichoandika
 
Hii nchi Yaani unaweza ukajikaza kabisa usichangie chochote kwa ajili yako, lkn ukakuta Jambo likakukereketa kweli hahahaa!
 
Wakuu,

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba amesema uamuzi wa Tanzania kuchukua umeme Ethiopia ni kitu chenye faida na si hasara kama watu wanavyodhani.

Mramba amesema ni faida kwa kuwa baadhi ya vyanzo vya umeme hapa nchini vinazalisha uniti moja kwa bei kubwa kuliko bei ambayo umeme huo utanunuliwa kutoka Ethiopia.

"Huo umeme wa Ethiopia tunanunua kwa senti za Marekani 0.077 lakini tuna vyanzo vingi ambavyo vinazalisha kwa gharama ya juu zaidi, hivyo hii ni nafuu kwetu," amesema na kuongeza umeme utaonunuliwa Ethiopia ni Megawati 100 tu.

Amesema umeme unaopelekwa mikoa ya Kaskazini unapotea kwa kiwango cha megawati 17 ambazo zinatosha kuhudumia Mkoa wa Songwe (unaotumia Mega 14) na zaidi.


"Hata huo wetu unaokuja kutoka Ethiopia utakuwa na hasara lakini hiyo hasara haituhusu, sisi tunanunulia mpakani Namanga, lakini tukipeleka sisi (umeme) tunatumia gharama kubwa," amesema Mramba.
Ameongeza kuwa "wachumi na wataalamu wote waliofanya tathmini juu ya jambo hilo waliona ni faida kubwa kuliko hasara"


Aidha, Mramba alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia ununuzi wa umeme huo na kuongeza kuwa ufafanuzi uliotolewa na Msemaji wa Serikali baada kuibuka kwa mjadala huo uko sahihi.

"Maelezo ya msemaji wa Serikali yako sawa, hayana dosari," amesema Mramba na kuongeza kuwa suala la mauziano ya umeme ya nchi na nchi ni la kawaida na mpaka sasa Tanzania inauza na kununua umeme kutoka mataifa tofauti zaidi ya matatu.

Source: Mwananchi
Kama namwelewa sana KM Mramba. Ufafanuzi usiokuwa na utata wa mhandisi🙏🙏🙏
 
Kwa hiyo transmission costs za kuutoa Ethiopia hadi Namanga watazibeba wakenya halafu watawauzia nyie bei chee kutoka kwao.

Kwamba waethiopia wanazalisha umeme wao kwa gharama ndogo kuliko sisi huku wote vyanzo ni HEP tena sisi ujenzi ni latest!

Au teknolojia tuliyotumia akina Manyuzi wametupiga ni ya 1940s?
Mitambo ni mipya ila nyaya za zamani, nisawa na kununua gari jipya ukalipitisha barabara mbovu, bora ukodi bolt tu
 
Sijui kichwani mwetu ni viazi na ndo maana tunadharaulika kiivo
 
Elimu Elimu Elimu... TANESCO endeleeni kutoa elimu huku tukijaribu kuwaelewa... kabla hatujakata tamaa kuelewa. Topic ngumuuuuu
 
Tunalipa kodi,wao ndiyo wanapanga wazitumiaje.
Tukazane kulipa kodi.
 
Back
Top Bottom