Siamini kama kuna issue ya maana sana kumhusu Makonda na kile anachokifanya at the moment, mimi binafsi namhurumia kwasababu naamini kabisa hao anaowapa maelekezo nini wafanye, wanamuona kama mdoli tu, wanaweza kuwa wanacheka pembeni
Nasema wanamuona kama mdoli kwasababu nikitazama spidi aliyoanza nayo Makonda, kisha nikatazama aina ya kiongozi tuliyenaye kwa sasa, hasa uwajibikaji, ni vitu viwili tofauti, haviendani kabisa.
Na hiyo tabia ya kiongozi aliyepo, kwa bahati mbaya ndio imechukuliwa na wengi wa wasaidizi wake, hasa mawaziri, ambao nao kwa kiasi kikubwa wanaonekana kufanya kazi kwa mazoea, kama alivyo mama yao, sasa utaanza vipi kuwaamuru watu wa sampuli hii wanaofanana wafanye kile utakacho wewe?
Haiwezekani, Makonda inavyoelekea atapiga kelele kwa sasa kwasababu bado battery zake zinachaji ya kutosha, lakini kwa kadri siku zitavyosogea, naye atajikuta naturally anakuwa neutralised, atafanana nao kwa matendo na hizi mbwembwe zake ndio zitaishia hapo, kwasababu kama ataweza kumsemea kwa mama mtu kama Nape au Mwigulu kisha wakaadhibiwa, never.
- Makonda amezungukwa na maadui wengi, bahati mbaya hajijui.
Hii style yake ilifaa wakati wa Magufuli, na wala sio sasa, anatakiwa akae chini atazame mbinu mpya za kufanya siasa zake, asipokuwa makini kwenye hili, anaweza kujikuta yeye ndie anaondoka kwenye nafasi aliyonayo akawaacha hao anaowapa maagizo, apige hesabu zake vizuri.