Katika ulimwengu wa kishirikina, nguo yako ni wewe

Katika ulimwengu wa kishirikina, nguo yako ni wewe

Amna mkuu, ukistukia mchongo, unajipanga upya muhimu ni kuusoma mchezo, ukitaka kujua unaishije waangalie sana waliokuzunguka utajua tu. Unaweza kujua upo sawa kumbe ni kinyume chake, meditation inasaidia sana
tupe procedure za kufanya meditation
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
So mkuu ukaona mambo yasiwe mengi bora upige para tu kuwakomoa, dah hata mimi hao watu wamecheza na maisha yangu mpaka kidgo nitupwe jera mahala flani nikala nduki kukimbia kesi, kumbe kuna likiumbe hai moja liko behind
ilikuaje mzee?
 
Habari zenu wakuu natumahi mu wazima wa afya.

Leo nimekuja na hili baada ya kuona matukio yakufanana yahusishayo Nguo.

TUKIO LA KWANZA (1):

Kuna jamaa yangu tulifahamiana nae yeye ni ndugu yake na binamu yangu. Yeye ni Upanga Boy (Mzaliwa wa kata ya Upanga wilaya ya Ilala Mkoa wa Dar es Salaam). Back to the story, yeye alikumbwa na tukio (la kishirikina)ambalo lilimfanya awe cha pombe sana, afu michongo sifuri. Ali-turn 40 akiwa home kwao Upanga.

Baada ya jamaa huyo kuwa tatizo katika familia na ukoo kwa muda mrefu. Mwaka 2018 ilikuja bainika kuwa jamaa kalogwa na Shangazi yake wa Singida, Na moja ya " Link " iliyotumika ni nguo (shati) ya jamaa. Jamaa alilitambua shati lake lililopotea siku nyingi akiwa Upanga ila siku hiyo ililiona likiwa Manyoni Singida likiwa limechomwa chomwa sindano, pia likiwa limenyunyuziwa dawa na kufungungwa Power Banks (Ilizi) mbalimbali zenye rangi tofauti tofauti ndani ya chumba ambacho kina giza nene na hakuna mtu uruhusiwa kuingia.

Vyote hivyo vilitosha kuhahakikisha mambo ya jamaa hayaendi, iyo mpaka umauti ulipomkuta 2019 kwenye kilabu kimoja cha pombe maeneo ya vigunguti.

TUKIO LA PILI (2):

Tukio la pili nililisoma humu JamiiForums.

Kuna jamaa yeye ni mzawa na mkazi wa jiji la Dar, Yeye alikuwa ana mpango South Africa.

Alifanya mipango yake kwa siri sana mpaka kufika Mbeya bila familia yake kujua. Kwa bahati mbaya alimtonya ndugu yake hapo Mbeya, Ndugu huyo akawa-informer kwa familia yake ilipo Dar. Mama yake mzazi hakutaka mwanae aende South Africa ivyo ikambidi aende kwa mtaalam amsaidie.

Mtaalam akaagiza Mama Mzazi wa jamaa alete nguzo ya mshikaji afanye mambo. Mtaalam baada ya kukabidhiwa nguo hiyo alifanya mambo kwa ustadi wakutosha.

Uwezi amini bhana yule jamaa ndani ya muda mfupi tu alibadili mawazo "completely" na kurudi kwao Temeke.

Kwako Mshana Jr na wajuvi wengine wenye nyota zenu na mwezi

Tupeni chemistry ya Nguo kwenye ulozi.

Uandishi tuvumiliane tu, amna namna.
[emoji1533][emoji1545][emoji1545][emoji1545]nakuja hapa jioni nikiwa kwenye utulivu mzuri
 
Amna mkuu, ukistukia mchongo, unajipanga upya muhimu ni kuusoma mchezo, ukitaka kujua unaishije waangalie sana waliokuzunguka utajua tu. Unaweza kujua upo sawa kumbe ni kinyume chake, meditation inasaidia sana
Nisaidie namna ya kufanya meditation hiyo unayozungumzia
 
Wengi mnachangia kuonyesha kama story tu,binafsi naona kama ndio napitia hayo muda huu,nipo 40+ ila najionea chenga tu,mke sina mtoto sina,sometimes kama najistukia hivi ila napuuzia,kuna madogo wanazaliwa wanakuwa wanakuwa na maisha yao mi nipo hivi hivi,cha ajabu siishi maisha ya kitajiri wala ya kimasikini yaan sio ya juu wala ya chini,nitaandika hapa hata kujaza kurasa mia,kwa ufupi sielewi,nikipata pesa mi tungi la kutosha,hiyo pesa sasa sijui naipataje ni ngumu kuelewa ila naweza kuanza kitu simple tu kikaniingizia pesa weee baadae nakipotezea
 
Chumvi ina mchango mkubwa sana hapa duniani tena kwenye swala la chakula.

Ila chumvi ni kama aliye wa mwisho japo hana umuhimu mkubwa wa maitaji.

Sijawai sikia uchumi wa nchi au dunia kutikisika kwa ajili ya chumvi!.

Sijawai kusikia serekali wa bunge kuzungumzia chumvi!

Sijawai kusikia maskini kasema kakosa nchunvi hata akiomba hatapewa!

Sijawai kusikia kuna tajiri anayeuza chumvi tu!

Sijawai kuona mtu akinyimwa chumvi labda sukari!

Sijawai kusikia mtu analalamika majumbani kuwa wanamaliza chumvi!

chumvi mbona ni wamwisho
 
oya hizi ishu ni real mzee, sema tu wanga lazima waje wakanushe!

Mi nakumbuka mwaka 2008 kuna bro wetu alizamia machimboni msumbuji kusaka ruby, kila wazee wakituma salamu bro arudi home hataki, basi siku moja dingi mida ya asubuh alikuja na mtaalamu akapika ugali ukachanganywa na maujiuji meusi aliyokuwa anayatoa ndani ya vibuyu na kijiti, na ule ugali ukafunikwa na shati la bro na mtaalamu akasema huu ugali akija mwanao mpe ale, huwezi amini kesho kutwa yake mida ya saa tano usiku bro anaingia nyumbani baada ya miaka sita ya kutokomea huko msumbiji,
Hadi nilimuonea huruma bro[emoji26]amechoka,amekonda mbaya analalamika maisha ya huko magumu na pia akasema juzi yake alipatwa na homa kali na akicheki kufia ugenini ni noma na nauli ya kumrudisha mwanza hana, lakini cha ajabu ilitokea private car inakuja bongo akapata lift hadi moro, moro akadandia fuso mpaka mwanza bila kutumia nauli yeyote...na cha ajabu alivyofika mwanza tu hajui hata ile homa kali ilipotelea wapi, kwa maelezo yake alikuwa anasema alikuwa hadhani kama atafika home mzima, basi bwana mzee akamfunilia ule ugali akagonga kishikaji akalala...lakin baadae mzee alikuja kumchana ukweli jinsi alivyorudishwa home[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Back
Top Bottom