Katika ulimwengu wa kishirikina, nguo yako ni wewe

Katika ulimwengu wa kishirikina, nguo yako ni wewe

Amna mkuu, ukistukia mchongo, unajipanga upya muhimu ni kuusoma mchezo, ukitaka kujua unaishije waangalie sana waliokuzunguka utajua tu. Unaweza kujua upo sawa kumbe ni kinyume chake, meditation inasaidia sana
Meditation inafanywa vipi?
 
Wengi mnachangia kuonyesha kama story tu,binafsi naona kama ndio napitia hayo muda huu,nipo 40+ ila najionea chenga tu,mke sina mtoto sina,sometimes kama najistukia hivi ila napuuzia,kuna madogo wanazaliwa wanakuwa wanakuwa na maisha yao mi nipo hivi hivi,cha ajabu siishi maisha ya kitajiri wala ya kimasikini yaan sio ya juu wala ya chini,nitaandika hapa hata kujaza kurasa mia,kwa ufupi sielewi,nikipata pesa mi tungi la kutosha,hiyo pesa sasa sijui naipataje ni ngumu kuelewa ila naweza kuanza kitu simple tu kikaniingizia pesa weee baadae nakipotezea
una demu??? umepanga kuwa mtoto na mtoto ukiwa na umri gani?
 
Habari zenu wakuu natumahi mu wazima wa afya.

Leo nimekuja na hili baada ya kuona matukio yakufanana yahusishayo Nguo.

TUKIO LA KWANZA (1):
Kuna jamaa yangu tulifahamiana nae yeye ni ndugu yake na binamu yangu. Yeye ni Upanga Boy (Mzaliwa wa kata ya Upanga wilaya ya Ilala Mkoa wa Dar es Salaam). Back to the story, yeye alikumbwa na tukio (la kishirikina)ambalo lilimfanya awe cha pombe sana, afu michongo sifuri. Ali-turn 40 akiwa home kwao Upanga.

Baada ya jamaa huyo kuwa tatizo katika familia na ukoo kwa muda mrefu. Mwaka 2018 ilikuja bainika kuwa jamaa kalogwa na Shangazi yake wa Singida, Na moja ya " Link " iliyotumika ni nguo (shati) ya jamaa. Jamaa alilitambua shati lake lililopotea siku nyingi akiwa Upanga ila siku hiyo ililiona likiwa Manyoni Singida likiwa limechomwa chomwa sindano, pia likiwa limenyunyuziwa dawa na kufungungwa Power Banks (Ilizi) mbalimbali zenye rangi tofauti tofauti ndani ya chumba ambacho kina giza nene na hakuna mtu uruhusiwa kuingia.

Vyote hivyo vilitosha kuhahakikisha mambo ya jamaa hayaendi, iyo mpaka umauti ulipomkuta 2019 kwenye kilabu kimoja cha pombe maeneo ya vigunguti.

TUKIO LA PILI (2):
Tukio la pili nililisoma humu JamiiForums.

Kuna jamaa yeye ni mzawa na mkazi wa jiji la Dar, Yeye alikuwa ana mpango South Africa.

Alifanya mipango yake kwa siri sana mpaka kufika Mbeya bila familia yake kujua. Kwa bahati mbaya alimtonya ndugu yake hapo Mbeya, Ndugu huyo akawa-informer kwa familia yake ilipo Dar. Mama yake mzazi hakutaka mwanae aende South Africa ivyo ikambidi aende kwa mtaalam amsaidie.

Mtaalam akaagiza Mama Mzazi wa jamaa alete nguzo ya mshikaji afanye mambo. Mtaalam baada ya kukabidhiwa nguo hiyo alifanya mambo kwa ustadi wakutosha.

Uwezi amini bhana yule jamaa ndani ya muda mfupi tu alibadili mawazo "completely" na kurudi kwao Temeke.

Kwako Mshana Jr na wajuvi wengine wenye nyota zenu na mwezi

Tupeni chemistry ya Nguo kwenye ulozi.

Uandishi tuvumiliane tu, hamna namna.
Nina mada yake kuhusiana na hili nitatafuta link yake
Chochote kinachoitwa chako kisha kikagusana nawe tayari hicho kitu kinakuwa ni wewe kwenye umiliki kiroho..
Wazungu walikuja huku Afrika na kukuta hiyo sayansi kuanzia kuroga kwa kutumia vitu kama nguo mpaka mambo ya laana ... Hawa wakajiongeza na kwenda kufanya utafiti, walichokuja kutoka nacho ndio hiki ambacho leo kinasaidia kumfahamu mhusika halisi kwenye tukio lolote kupitia vinasaba vya DNA
Hawa hawakucheka na kubeza bali walijiongeza .. Unywele wako mmoja unatosha kukutia hatiani kwenye tukio la ujambazi mauaji, asili yako nknk
Kinachofanyika kishirikina ni kutumia vinasaba vilivyoko kwenye vazi lako kuvifunga, kuvizika , kuvitupa chooni, kuvichoma moto ama kuviachia kwenye mkondo wa maji
Hizo njia zote ni mbaya sana kwakuwa hazina rivasi ila huyo jamaa yako yeye nguo iliwekwa chumbani ndio maana yakajulikana haya japo kwa kuchelewa

 
Mimi niliwahi kufanyiwa huo uchawi...kipindi hicho nilikuwa kidato cha tano kule karagwe secondary...yaani shule nzima mimi tu ndio nilikuwa naonekana kituko...ilifikia mpaka mkuu wa shule alinibatiza jina la 'truant boy'....na bado nilikuwa najitahidi kuswali sala tano...ila nilifanikiwa kumaliza kwa mbinde...hata shule niliyohamia watu wote waliokuwa wanasoma combination kama yangu wote walifaulu ila mimi tu ndie nilifeli...UCHAWI UPO
 
Nina boxer moja , shati 6 na kadet 4...najua vizuri nguo zangu sasa sijui huyu demu atanirogea wapi?....Nina kaa uswazi walipo wachawi hizo mishe za kunyoana nywele naziskia sasa Mimi tokea nimehamia huu mtaa ni Bonge la paraa alafu siringi wala nini....

Shabashhhh!
 
Mimi niliwahi kufanyiwa huo uchawi...kipindi hicho nilikuwa kidato cha tano kule karagwe secondary...yaani shule nzima mimi tu ndio nilikuwa naonekana kituko...ilifikia mpaka mkuu wa shule alinibatiza jina la 'truant boy'....na bado nilikuwa najitahidi kuswali sala tano...ila nilifanikiwa kumaliza kwa mbinde...hata shule niliyohamia watu wote waliokuwa wanasoma combination kama yangu wote walifaulu ila mimi tu ndie nilifeli...UCHAWI UPO
Pole sana
 
Back
Top Bottom