Katika ulimwengu wa kutafuta pesa kudhulumiwa kawaida sana

Ina maana harufu ya kuoza haikuweza kugumdulika hadi mwaka ukakatika?
 
Trial and Error

Ktk utafutaj kujilipua na kulipuliwa n hatua.
 
Unazungumzia tukio la sharifshamba???
 
Kuzulumiwa ni kawaida ila siyo suala la kuzoea..unafika mahala unakua mjanja na wewe
 
Kipande cha songas pale ubungo wizi huo ni maarufu sana,walikuuzia wap hiyo sabun???
Dodoma.

Mchuchu aliniona natumia simu ya batani ya TECNO T484 akaipenda, nikamwambia tulia nitakununulia.

Siku za mbele katika mizunguko yangu Town nikasimamishwa na msela yuko smart tu, akaniambia ana shida kuna matatizo yametokea, anauza simu yake ya TECNO T528 (jamii ya T484), nikaona yes!, ntaenda kumspraizi mchumba, nikainunua, akanifungia kwenye mfuko.

Niko njiani narudi nikaamua kuikagua kwa furaha, hamadi!!, mche wa sabuni!!, nguvu zikaniishia, ikabidi nikae barabarani pembeni ya lami nusu saa nzima akili ikae sawa. Nilijiona bonge la mjinga. Mchumba sijamwambia hiyo ishu mpaka leo, nimemnunulia mpya dukani.

Nikikumbuka nilivyotapeliwa kiboya wakati mimi mwenyewe mtoto wa mjini roho inaniuma sana.
 
Bugurun kuna bar ina nyumba ya wagen inaitwa kituri kuna msukuma asiyejulikana ktk eneo lile alichukua chumba na kukaa siku kadhaa haijulikan alipata vp kiunganish kat yake na matapel wa bugurun pandia lkn aliwapa oda kubwa ya simu zilizotumika anazihitaj.
Baada ya siku kadhaa wale matapeli wa pandia walimletea yule msukuma simu nying tu tofaut tofaut walimkuta akiwa chumban kavaa boksa na fulana baada ya kukubaliana bei msukuma akatoa shart inabid waandikishiane akaingiza mkono ktk fuko la lambo ambalo lipo pembezon mwa kitanda baada ya kwakwachu ndan ya ule mfuko akatoa buku jipyaaaaa akampa mmoja wao aende akanunue peni na daftar,baada ya peni na daftar kuletwa akawaambia huku akiwa kazikumbatia zile simu kwa vile yy yupo peke ngoja aende kumwita muhudum awe shahid wake na hiyo ndio ikawa mara ya mwisho yule msukuma kuonekana ktk mazingira yale.
Jamaa baada ya kukaa muda mrefu mule ndan ilibid wachungulie ndan ya lile fuko ambalo lilitoka buku baada ya kwakwachu za muda mfup wakakuta kondom km zote wakatoka fasta nje kumuulizia wakaambiwa jamaa alipanda boda na kuondoka zake mpaka hapo wale matapel wakaona tushapigwa tayar.
 
Baada ya kumsapraiz mchumba ukafanyiwa ww sapraiz
 
Wote wa mjini, hata darasani mtihani ufaulu hutofautiana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…